Elections 2010 Maandamano- uchaguzi tanzania jumamosi nov 6washington dc 2010, 10:am (white house)

shilanona

Member
Oct 31, 2010
55
22
Ndugu Watanzania ambao tunaoshi maeneo ya Washington DC, tunawatangazia wote kwamba tutafanya mandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu, 2010 na namna shughuli ya kuhesabu kura za uchaguzi zilivyofanywa na Tume ya Uchaguzi wa Tanzania ambao uligubikwa na wizi na udanganyifu wa hali ya juu katika sehemu na maeneo mbalimbali nchini Tanzania. Kwa kuwa State Department imetoa ridhaa ya maandamano haya ya amani, tunawaomba Watanzania, wanayoipenda Tanzania, sehemu yoyote walipo hapa Washington DC, Maryland, Virginia na Pennsylvania wajitokeze kwa wingi, wake kwa waume, watoto na kumbuka kuja na bendera, mabango, ngoma, zeze na vinubi, Tshirts ili message ifike kwa Presedent Obama.

Tunawaomba watanzania wote waishio Marekani mujitokeze kwa wingi katika kupinga matendo hayo ya ubadhilifu nchini kwetu. Kwa wale ambao wanataka kujitokeza wasiliana nasi kwa: #202 367 2761 # 301 655 6577 # 224 628 8279
 
Mkuu,

Itakuwa busara ukiwawekea watu hapa hicho kibali maana wengi wataona siyo mchezo tena ila ni kweli.

Angalieni tu hawa CCM wa Ughaubuni maana wao CCM mbele, Taifa la Tanzania their A**.
 
good luck guys, thats what i call patriotism; really this will count a lot for what you did for your country ingawa hamkuweza kuvote to me this is equivalent to 1.25 votes:smile:
 
Sina maneno ya kuelezea furaha yangu na umakini wa maamuzi yenu. Mungu kesha bariki ndiyo maana hata kibali mmepata. Wajulisheni Marekani na ulimwengu kuwa wengi wetu Tanzania tunaamini juu ya nguvu ya demokrasia ya kweli. Baadhi ya nchi ikiwemo marekani wana makengeza na umuhimu wa demokrasia Tanzania. God bless you keep us informed
 
Sina maneno ya kuelezea furaha yangu na umakini wa maamuzi yenu. Mungu kesha bariki ndiyo maana hata kibali mmepata. Wajulisheni Marekani na ulimwengu kuwa wengi wetu Tanzania tunaamini juu ya nguvu ya demokrasia ya kweli. Baadhi ya nchi ikiwemo marekani wana makengeza na umuhimu wa demokrasia Tanzania. God bless you keep us informed

Obama will be leaving for India tonight.
He won't be in town.
 
Ndugu Watanzania ambao tunaoshi maeneo ya Washington DC, tunawatangazia wote kwamba tutafanya mandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu, 2010 na namna shughuli ya kuhesabu kura za uchaguzi zilivyofanywa na Tume ya Uchaguzi wa Tanzania ambao uligubikwa na wizi na udanganyifu wa hali ya juu katika sehemu na maeneo mbalimbali nchini Tanzania. Kwa kuwa State Department imetoa ridhaa ya maandamano haya ya amani, tunawaomba Watanzania, wanayoipenda Tanzania, sehemu yoyote walipo hapa Washington DC, Maryland, Virginia na Pennsylvania wajitokeze kwa wingi, wake kwa waume, watoto na kumbuka kuja na bendera, mabango, ngoma, zeze na vinubi, Tshirts ili message ifike kwa Presedent Obama.

Tunawaomba watanzania wote waishio Marekani mujitokeze kwa wingi katika kupinga matendo hayo ya ubadhilifu nchini kwetu. Kwa wale ambao wanataka kujitokeza wasiliana nasi kwa: #202 367 2761 # 301 655 6577 # 224 628 8279
Hongereni sana kwani munawakilisha kilio cha wengi. Tanzania haitaendelea kusifiwa tena wakati viongozi wake wanaingia madarakani kwa wizi wa kura. Ulimwengu lazima ujulishwe hilo.
 
goodlucky mnaandamana kwa waelewa manake huku maandamano hayaruhusiwi labda ya kumpongeza kikwete watendaji wa serikali tunawalipa kwa kodi zetu lakini hawatutumikii sisi wananchi ambao kimsingi ndio tuliowaajiri wanabaki kumlamba miguu kikwete ambaye naye tumempa ajira kama wao inashangaza lakini ndiyo hali halisi hapa bongo :A S angry:
 
Watumwa wakubwa nyie, Oboma ndio baba yenu? Tz ni nchi huru aichaguliwi rais na Marekani. Mimi niko Washngton na si shiriki kwenye upuuzi wenu.
 
Watumwa wakubwa nyie, Oboma ndio baba yenu? Tz ni nchi huru aichaguliwi rais na Marekani. Mimi niko Washngton na si shiriki kwenye upuuzi wenu.
Unajulikana wewe:doh: kwa kuwa unajikomba upate vyeo vya ukoo kwa Kiwete wetu wa CCM. Kumbuka wewe si wa ukoo wa Wasambaa (Makamba), Mkuchika, Wasomali wala Wakwere. Utaishia kujikomba tu!!!:A S angry:
 
U r guyz are so Brave...At 1st I thought u guys are all CCM after reading there is a CCM branch in USA with HQ in Washington DC.........Keep it up.....May be we can do the same back home......we are still wtn 4 Dr. Slaa
 
Mimi nakataa Kikwete siyo chaguo la Watanzania

1. Sikumpigia kura yangu. Ndugu zangu wa karibu na marafiki zangu wengi hawakuwa wakimtaka na walikiri kutompigia kura
2. Kachaguliwa na Watanzania 5,276,827 (Zikiwepo na kura za maluani - uchakachuaji) kati ya Watanzania zaidi ya Milioni 40
3 Wananchi waliojiandikisha zaidi ya 11,511,020 ambao ni asilimia 57.16% hawakupiga kupiga kura kutokana na either kuhofia kura zao kuchakachuliwa au mfumo mbovu uliowekwa ili kupunguza kura za wapinzani mfano, kuzuia raia kupiga kura ya raisi sehemu yoyote ya nchi wakati anachaguliwa raisi wa nchi nzima au kufunga vyuo vya elimu ya juu na mashule.
4. Kachaguliwa na wananchi wengi walio vijijini kutokana na uelewa mdogo.
5. Amesaidiwa sana na vyombo vya ulinzi na usalama na taasisi za serikali vikiwemo vyombo vya habari vya serikali kufanikisha matakwa yake na familia yake
6. Katumia gharama kubwa sana katika kampeni (Mabango kutoka Canada, magari ya kifahari nk. wakati Watanzania wanaishi maisha ya dhiki kubwa
7. Ahadi zake ni nyingi na amezitoa nje ya Ilani kama alivyothibitisha meneja wa kampeni zake na yeye mwenyewe alisema nyingine zilikuwa za papo hapo.
8. Miaka mingine mitano ya Wadanganyika kudharaulika na kunyanyaswa na mafisadi wakati president akijikomba kwa wale Nyerere aliosema - nanukuu "Mijitu hii lengo wao ni kututawala, kwa nini tunawaongezea uwezo wa kututawala?'' mwisho wa kunukuu

Waliopiga kura 8,626,283 = 42.84%

Kura zilizoharibika = 2.64%

Mgawanyo wa kura ni hivi:

APPT: 96,933 = 1.12%
CCM: 5,276,827 = 61.17%
CHADEMA: 2,271,941 = 26.34%
CUF: 695,667 = 8.06%
NCCR: 26,388 = 0.31%
TLP: 17,482 = 0.20%
UPDP: 13,176 = 0.15%
 
Back
Top Bottom