Maandamano na migomo ya Misri na Tunisia yalianzaje anzaje?

Ndibalema

JF-Expert Member
Apr 26, 2008
10,956
4,648
Wana Jf, naandika hili nikiwa na nia ya dhati kabisa ya kutaka kujua for just in case wakuu.

Hivi Wamisri na Watunisia walianza anza vipi mpaka wakaandamana na kuanzisha harakati za kuziondoa serikali zao madarakani.

Simaanishi kuwa nahitaji kujua chanzo, laa!
Nataka kujua wali'organize vp mpaka maandamano mgomo ukapewa support na. Raia wengi tena kwa muda mfupi tuu.

Kingine, Serikali zao ziliamua ku'block mawasiliano yote ya ndani na nje ya nchi lakini still waandamanaji wanaonekana wana ushirikiano kana kwamba wana mawasiliano.

Jamani mwenye kujua anijuze,
Yaliandikwa matangazo magazetini, matangazo na wito wa kuandamana ulitangazwa ktk televisheni na redio stesheni au ilikuwaje kuwaje?
 
DSC_4539.JPG chinga1.jpg

Tunisia ilianza hivi kuna yule jamaa Mohamed Bouazizi (mmachinga wa Tunisia) alichukuliwa vitu vyake na Mgambo/askari na baada ya kutosikilizwa na gavana wa huko aliamua kujipiga kiberiti...then maandamano ya kumsapoti yaliendelea mpaka Ben Ali akakimbia Saudia Arabis
 
mgambonew.gif
.Yaani kwa kifupi manyanyaso ambayo hawa jamaa wanayapata wakati wanatafuta senti ya kula faida zao kwa siku hazikifi hata elfu 2....mgambo wanawanyanyasa .....sasa kule tunisia Bouazizi kuonyesha amechukia na manyanyaso aliamua kujipiga kiberiti
 
Kwa hapa kwetu, ikitokea machinga kaijpiga kiberiti kwa sababu ya manyanyaso ya mgambo, kuna yeyote atakayejitokeza kumsuport au mwili wake utakuwa umegeuka majivu for nothing!!
Wengine watakebehi "aah ni ukosefu wa elimu tuu"

Na Misri je, walianzaje?
 
Back
Top Bottom