Maandamano makubwa ya Kihistoria kufanyika nchini Venezuela leo Februari 2, 2019

Chaliifrancisco

JF-Expert Member
Jan 17, 2015
23,489
70,277
Maandamano makubwa yanatarajiwa kufanyika nchini Venezuela baadae hii leo katika harakati za kumataka raisi wa nchi hiyo Nicolas Maduro kujiuzulu. Harakati hizo zinachochewa na Juan Guaido ambaye wiki iliyopita alijitangaza kuwa ndie kiongozi halali wa nchi hiyo.



January 23 takribani watu millioni moja waliandamana mitaani nchini Venezuela, kuitikia wito wa Juan Guaido, wakimtaka raisi Maduro ajiuzulu.

Guaidó anaungwa mkono na mataifa mengi ya Latin America, Marekani na Ulaya. Maandamano ya leo February 2 yanatarajiwa kuwa makubwa zaidi kuliko yale ya January 23.

Raisi Maduro kwa upande wake anaungwa mkono na jeshi la nchi hiyo pamoja na Urusi, China na Uturuki na mpaka sasa inapoandikwa makala hii bado yupo madarakani.

Inakadiriwa kuwa asilimia zaidi ya 80 ya wananchi hawamuungi mkono raisi huyo na wanamtaka ajiuzulu. Nchi jirani nazo zimeathirika kutokana na hali mbaya nchini Venezuela ambapo inakadiriwa watu zaidi ya million tatu wameikimbia nchi hiyo kutokana na hali mbaya ya kiuchumi na kijamii iliyoikumba nchi hiyo toka enzi za utawala wa Hugo Chávez.

Mataifa ya Ulaya na Marekani kwa upande wao wanaathirika na hali ilivyo Venezuela kutokana na kushindwa kuthibiti uzalishaji wa dawa za kulevya kutokana na rushwa iliyokithiri.


As world leaders pile in for Mr Maduro or against him, they are battling over an important idea which has lately fallen out of favour: that when a leader pillages his state, oppresses his people and subverts the rule of law, it is everybody’s business.

My take

Utawala wa kimabavu na uonevu hautaweza kulifikisha taifa lolote sehemu salama hasa katika zama hizi. Mwenye masikio na asikie na mwenye macho haambiwi tazama.

https://edition-m.cnn.com/2019/02/01/americas/venezuela-guaido-maduro/index.html?r=https://www.google.com/


The battle for Venezuela’s future


Credit: The Economist
CNN
 

Attachments

  • 20190202_LDD001_0.jpg
    20190202_LDD001_0.jpg
    10.8 KB · Views: 30
Obama aliiharibu libya na dunia inashuhudia watu wakizama baharini kwenda Italy.

Trump anaiharibu Venezuela.

UN imebaki kubung'aa tu
Hii crisis haijaanza leo chief ipo tokea 2010. Tokea kwenye utawala wa Hugo Chavez, kipindi chote hicho wameshindwa kupata suluhu zaidi tu ameingia 'Chavez mdogo' in Maduro.
 
Umesema utawala wa mabavu hauwezi kulifikisha taifa lolote sehemu salama!

Unajua chimbuko la matatizo ya Venezuela?

Unauziwa propaganda za West na kwa sababu ya ujinga unazinunua bila hata kutumia common sense.

Yes, Rais Maduro sio maraika lakini nchi za west zinamvisha sura ya kishetani ili ziweze kupata raslimali adhimu ya mafuta kwa bure au gharama ya karibu na bure.

Mind you, Venezuela ni nchi inaongoza duniani kwa wingi wa akiba ya mafuta.
 
Umesema utawala wa mabavu hauwezi kulifikisha taifa lolote sehemu salama!

Unajua chimbuko la matatizo ya Venezuela?

Unauziwa propaganda za West na kwa sababu ya ujinga unazinunua bila hata kutumia common sense.

Yes, Rais Maduro sio maraika lakini nchi za west zinamvisha sura ya kishetani ili ziweze kupata raslimali adhimu ya mafuta kwa bure au gharama ya karibu na bure.

Mind you, Venezuela ni nchi inaongoza duniani kwa wingi wa akiba ya mafuta.
In a November 2016 survey by Datincorp, Venezuelans living in urban areas were asked which entity was responsible for the crisis, with 59% stating that President Chávez (25%), President Maduro (19%) and chavismo (15%) were the causes, while 16% blamed the opposition (10%), entrepreneurs (4%) and the United States (2%)

Haya ni maoni ya wa Venezuela, need i say more?
 
Kuelekea maendeleo ya kweli, ni lazima system iflash kila uchafu naturally au kwa kutumia nguvu.

Ni lazima watu wafe, wenzetu walioendelea wamepata maendeleo yao ya sasa kwa jasho na damu.

Hakuna maendeleo yoyote duniani yalihowahi letwa kwa KAULI za kitapeli- MKURABITA, KILIMO KWANZA, ARI MPYA NGUVU MPYA KASI ZAIDI, HAPA KAZI TU. NCHI YA VIWANDA. Maendeleo huletwa na mapinduzi ya Jambo husika, na ukisikia kulikuwa na mapinduzi ya viwanda huko ulaya ujue wanaume walimaanisha, walitafutwa watu wakawekwa mahali wa design na kutengeneza mitambo kwa gharama yoyote ile. Sio ubabaishaji wa kuunga mkono juhudi za Rais, wakati kichwani huna chochote cha kusaidia nchi yako

Yanayotokea Venezuela hata hapa yanakuja, and the stage is already set by the government.(serikali imeonesha kwa kauli na vitendo kuwa ili ukitaka kufanikisha Jambo ni lazima uendoe kikwazo kilichopo mbele yako kwa gharama yoyote ile, huu mwangwi ni lazima utarudi kwa wananchi nao wataamua ili wapate haki, viongozi wanaowataka ni lazima wawaondoe walioko madarakani kwa njia yoyote ile) Hawa viongozi ambao hawajui kutumia njia rahisi kubadili rasilimali za nchi ziweze kuwasaidia wananchi, ni muda muafaka sasa kuwa flashed na system.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umesema utawala wa mabavu hauwezi kulifikisha taifa lolote sehemu salama!

Unajua chimbuko la matatizo ya Venezuela?

Unauziwa propaganda za West na kwa sababu ya ujinga unazinunua bila hata kutumia common sense.

Yes, Rais Maduro sio maraika lakini nchi za west zinamvisha sura ya kishetani ili ziweze kupata raslimali adhimu ya mafuta kwa bure au gharama ya karibu na bure.

Mind you, Venezuela ni nchi inaongoza duniani kwa wingi wa akiba ya mafuta.
Inakadiriwa kuwa asilimia zaidi ya 80 ya wananchi hawamuungi mkono raisi huyo na wanamtaka ajiuzulu.
 
Umesema utawala wa mabavu hauwezi kulifikisha taifa lolote sehemu salama!

Unajua chimbuko la matatizo ya Venezuela?

Unauziwa propaganda za West na kwa sababu ya ujinga unazinunua bila hata kutumia common sense.

Yes, Rais Maduro sio maraika lakini nchi za west zinamvisha sura ya kishetani ili ziweze kupata raslimali adhimu ya mafuta kwa bure au gharama ya karibu na bure.

Mind you, Venezuela ni nchi inaongoza duniani kwa wingi wa akiba ya mafuta.
Unajua tofauti ya utawala wa mabavu na utawala unaotanguliza maslahi ya wananchi mbele kwa kulinda rasilimali za nchi? Au unafikiri ili kiongozi aweze kulinda rasilimali za nchi ni lazima uongozi wake uwe wa mabavu?

Hakuna wananchi wajinga ambao wataona wamepata kiongozi anayelinda rasilimali za nchi alafu waandamane kumkataa, ukiona wananchi wanaandamana kumkataa kiongozi alafu huyo kiongozi anajitapa kwamba analinda rasilimali za nchi ni kwamba wananchi wameshapima na kuona kwamba ni bora hizo rasilimali zipotee ila waishi maisha ya uhuru na amani, pengine hata hizo rasilimali zinanufaisha kikundi kidogo cha watu.

80% ya wananchi kumkataa kiongozi sio kitu kidogo
 
Unajua tofauti ya utawala wa mabavu na utawala unaotanguliza maslahi ya wananchi mbele kwa kulinda rasilimali za nchi? Au unafikiri ili kiongozi aweze kulinda rasilimali za nchi ni lazima uongozi wake uwe wa mabavu?

Hakuna wananchi wajinga ambao wataona wamepata kiongozi anayelinda rasilimali za nchi alafu waandamane kumkataa, ukiona wananchi wanaandamana kumkataa kiongozi alafu huyo kiongozi anajitapa kwamba analinda rasilimali za nchi ni kwamba wananchi wameshapima na kuona kwamba ni bora hizo rasilimali zipotee ila waishi maisha ya uhuru na amani, pengine hata hizo rasilimali zinanufaisha kikundi kidogo cha watu.

80% ya wananchi kumkataa kiongozi sio kitu kidogo
Wanachoshindwa kuelewa ni kuwa matatizo yote huwa yanaanza kidogo kidogo. Ikifikia hatua ya kuwa nchi inakosa stability alafu kukawa na intervention kutoka kwa mataifa mengine lawama watatupiwa walio intervene.

Ajabu
 
Maandamano makubwa yanatarajiwa kufanyika nchini Venezuela baadae hii leo katika harakati za kumataka raisi wa nchi hiyo Nicolas Maduro kujiuzulu. Harakati hizo zinachochewa na Juan Guaido ambaye wiki iliyopita alijitangaza kuwa ndie kiongozi halali wa nchi hiyo.



January 23 takribani watu millioni moja waliandamana mitaani nchini Venezuela, kuitikia wito wa Juan Guaido, wakimtaka raisi Maduro ajiuzulu.

Guaidó anaungwa mkono na mataifa mengi ya Latin America, Marekani na Ulaya. Maandamano ya leo February 2 yanatarajiwa kuwa makubwa zaidi kuliko yale ya January 23.

Raisi Maduro kwa upande wake anaungwa mkono na jeshi la nchi hiyo pamoja na Urusi, China na Uturuki na mpaka sasa inapoandikwa makala hii bado yupo madarakani.

Inakadiriwa kuwa asilimia zaidi ya 80 ya wananchi hawamuungi mkono raisi huyo na wanamtaka ajiuzulu. Nchi jirani nazo zimeathirika kutokana na hali mbaya nchini Venezuela ambapo inakadiriwa watu zaidi ya million tatu wameikimbia nchi hiyo kutokana na hali mbaya ya kiuchumi na kijamii iliyoikumba nchi hiyo toka enzi za utawala wa Hugo Chávez.

Mataifa ya Ulaya na Marekani kwa upande wao wanaathirika na hali ilivyo Venezuela kutokana na kushindwa kuthibiti uzalishaji wa dawa za kulevya kutokana na rushwa iliyokithiri.


As world leaders pile in for Mr Maduro or against him, they are battling over an important idea which has lately fallen out of favour: that when a leader pillages his state, oppresses his people and subverts the rule of law, it is everybody’s business.

My take

Utawala wa kimabavu na uonevu hautaweza kulifikisha taifa lolote sehemu salama hasa katika zama hizi. Mwenye masikio na asikie na mwenye macho haambiwi tazama.

https://edition-m.cnn.com/2019/02/01/americas/venezuela-guaido-maduro/index.html?r=https://www.google.com/


The battle for Venezuela’s future


Credit: The Economist
CNN
Venezuela wana reserve kubwa duniani ya oil na gas...hii ndo sababu kubwa... Wakijidanganya kupata democracy ya USA watailipa kwa oil na gas.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakwambia maduro hachomoki! In desperation anawauzia saudi arabia maelfu ya tani za dhahabu akiba ya taifa. Maduro must go.
 
Umesema utawala wa mabavu hauwezi kulifikisha taifa lolote sehemu salama!

Unajua chimbuko la matatizo ya Venezuela?

Unauziwa propaganda za West na kwa sababu ya ujinga unazinunua bila hata kutumia common sense.

Yes, Rais Maduro sio maraika lakini nchi za west zinamvisha sura ya kishetani ili ziweze kupata raslimali adhimu ya mafuta kwa bure au gharama ya karibu na bure.

Mind you, Venezuela ni nchi inaongoza duniani kwa wingi wa akiba ya mafuta.
jaribu kuweka facts unapojibu,acha jazba,Pia jifunze kuandika.MALAIKA NA SIO Maraika
 
Aibu mamilioni ya wananchi kuikimbia nchi kutokana na kuanguka uchumi chanzo uongozi hovyo. Maduro's, Bashir's must go.
Kama hauna kadi ya kijani ya kimarekani (I am told, by holding that card, you have to defend the US stance at all cost otherwise...) basi haujui chanzo halisi cha matatizo ya Venezuela.
 
Back
Top Bottom