Maandalizi ya sikukuu: Vyakula bei juu!

abdulahsaf

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
858
130
[h=1]Maandalizi ya sikukuu bei juu[/h]
bei+chakula.jpg


Na Haika Kimaro na Mbuke Samweli


Posted Alhamisi,Decemba13 2012 saa 22:43 PM
Kwa ufupi
Bei ya maharage zimepanda kutoka Sh1,600 kwa kilo hadi kufikia Sh2,100, mchele umepanda kutoka Sh1,800 kwa kilo hadi kufikia Sh2,400, unga wa ngano umepanda kutoka Sh1,200 kwa kilo hadi kufikia Sh 1,500 kwa kilo



MAANDALIZI ya sikukuu za mwisho wa mwaka zimeingia dosari baada ya bei ya bidhaa za chakula kupanda kwa kiwango cha juu nchini.Mwanachi limefanikiwa kufanya uchunguzi na kugundua bei za vyakula zimepanda kwa kiasi kikubwa wakati huu wa kuelekeakatika sikukuu na kusababisha usumbufu kwa baadhi ya wananchi.


Bei ya bidhaa kama unga wa sembe umepanda kutoka Sh1,000 kwa kilo hadi kufikia Sh1,400 kwa kilo tofauti na awali huku wafanyabiashara hao wakijitetea kupanda kwa bidhaa hizokunatokana na msimu wa sikukuu.


Bei ya maharage zimepanda kutoka Sh1,600 kwa kilo hadi kufikia Sh2,100, mchele umepanda kutoka Sh1,800 kwa kilo hadi kufikia Sh2,400, unga wa ngano umepanda kutoka Sh1,200 kwa kilo hadi kufikia Sh 1,500 kwa kilo.


Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti wafanyabiashara wa soko la nafaka jijini Dar es Salaam, walisema kuwa hali hiyo inachangiwa na tabia ya kuwepo kwa baadhi ya wafanyabiashara kuwa na tabia ya kupandisha bei ya vitu hasa pale inapofikia msimu wa sikukuu.


Joshua John ,mfanyabiashara katika soko la Tandale, alisema kuwa kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa na tabia ya kupandisha bei kila inapofika msimu wa sikukuu kwa sababu zao binafsi hata kama nafaka hazijapanda kwa sababu wameshazoea kuwa ndicho kipindi kizuri cha kuvuna pesa kutoka kwa wateja.


Nao wateja waliokuwepo sokoni hapo, Jackline Shoo alidai kusikitishwa na tabia ya wafanyabiashara hao kuwa na tabia ya kupandisha bei kiholela hususani wakati wa sikukuu hali inayowafanya wabadili ratiba za matumizi ya pesa ili waweze kujikimu kimaisha na familia zao.


“Sijui kwa nini hawa wafanyabiashara wanakuwa na tabia ya kupandisha bei za bidhaa hususani wakati wa sikukuu hali inayotulazimu tubadili matumizi ya pesa ili tuweze kujikimu na familia zetu” alisema Shoo


Hata hivyo baadhi ya wateja wanaopata huduma sokoni hapo wameitaka mamlaka husika ambayo ni wizara ya biashara na viwanda kusimamia na kufuatilia tatizo hilo kwa umakini kwani kitendo hicho kinawakosesha amani kila inapofika misimu ya sikukuu
 
maandalizi ya sikukuu bei juu

bei+chakula.jpg


na haika kimaro na mbuke samweli


posted alhamisi,decemba13 2012 saa 22:43 pm
kwa ufupi
bei ya maharage zimepanda kutoka sh1,600 kwa kilo hadi kufikia sh2,100, mchele umepanda kutoka sh1,800 kwa kilo hadi kufikia sh2,400, unga wa ngano umepanda kutoka sh1,200 kwa kilo hadi kufikia sh 1,500 kwa kilo



maandalizi ya sikukuu za mwisho wa mwaka zimeingia dosari baada ya bei ya bidhaa za chakula kupanda kwa kiwango cha juu nchini.mwanachi limefanikiwa kufanya uchunguzi na kugundua bei za vyakula zimepanda kwa kiasi kikubwa wakati huu wa kuelekeakatika sikukuu na kusababisha usumbufu kwa baadhi ya wananchi.


Bei ya bidhaa kama unga wa sembe umepanda kutoka sh1,000 kwa kilo hadi kufikia sh1,400 kwa kilo tofauti na awali huku wafanyabiashara hao wakijitetea kupanda kwa bidhaa hizokunatokana na msimu wa sikukuu.


Bei ya maharage zimepanda kutoka sh1,600 kwa kilo hadi kufikia sh2,100, mchele umepanda kutoka sh1,800 kwa kilo hadi kufikia sh2,400, unga wa ngano umepanda kutoka sh1,200 kwa kilo hadi kufikia sh 1,500 kwa kilo.


Wakizungumza na mwananchi kwa nyakati tofauti wafanyabiashara wa soko la nafaka jijini dar es salaam, walisema kuwa hali hiyo inachangiwa na tabia ya kuwepo kwa baadhi ya wafanyabiashara kuwa na tabia ya kupandisha bei ya vitu hasa pale inapofikia msimu wa sikukuu.


Joshua john ,mfanyabiashara katika soko la tandale, alisema kuwa kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa na tabia ya kupandisha bei kila inapofika msimu wa sikukuu kwa sababu zao binafsi hata kama nafaka hazijapanda kwa sababu wameshazoea kuwa ndicho kipindi kizuri cha kuvuna pesa kutoka kwa wateja.


Nao wateja waliokuwepo sokoni hapo, jackline shoo alidai kusikitishwa na tabia ya wafanyabiashara hao kuwa na tabia ya kupandisha bei kiholela hususani wakati wa sikukuu hali inayowafanya wabadili ratiba za matumizi ya pesa ili waweze kujikimu kimaisha na familia zao.


“sijui kwa nini hawa wafanyabiashara wanakuwa na tabia ya kupandisha bei za bidhaa hususani wakati wa sikukuu hali inayotulazimu tubadili matumizi ya pesa ili tuweze kujikimu na familia zetu” alisema shoo


hata hivyo baadhi ya wateja wanaopata huduma sokoni hapo wameitaka mamlaka husika ambayo ni wizara ya biashara na viwanda kusimamia na kufuatilia tatizo hilo kwa umakini kwani kitendo hicho kinawakosesha amani kila inapofika misimu ya sikukuu



jee tutavuka kweli watanzania kama hali ni hii na huku wananchi hatuna ajira, afya mbovu, huduma za jamii zote rushwa kwanza ndio uhudumiwe .jee kweli tunakula madunda ya nchi yetu au wenye meno ndio wenye kufaidika.

Kuongoza tena ccm kipindi cha miaka 10 basi watanzania wote tutakuwa mahututi, chabure kwa ccm ni t-shart na magwanda tu.
 
Back
Top Bottom