Maandalizi ya Kiusalama ya Ziara ya Obama Tanzania (na Afrika kwa Ujumla)

Mzalendo_Mwandamizi

JF-Expert Member
Dec 12, 2007
1,117
4,764
296obamaAFRICA.jpg




Washington- Rais Obama atapokwenda Afrika Kusini mwa Sahara mwezi huu, taasisi zenye jukumu la usalama wake hazifanyi lelemama.

Mamia wa mashushushu wa Kikosi cha Ulinzi wa Rais wa Marekani (US Secret Service) watasambazwa katika maeneo ya usalama huko Senegal, Afrika ya Kusini na Tanzania. Manowari ya Jeshi la Vita la Marekani inayotumika kubeba ndege za kivita au nyambizi, ikiwa na matabibu waliokamilika, itakuwa imeegeshwa pwani kwa ajili ya dharura.

Ndege za kijeshi za kubeba mizigo zitasafirisha magari 56, ikiwa ni pamoja na 'limousines' 14 na magari ya mizigo matatu yote yakiwa na makasaha ya vioo visivyopenya risasi vitakavyowekwa katika madirisha ya hoteli atakazofikia Obama na familia yake. Ndege za kivita zitakuwa 'zikizurura' angani kwa zamu, kuwezesha ulinzi wa masaa 24 katika 'anga ya Rais' ili ziweze kuchukua hatua pindi ndege ya adui itakapoingilia kati.

Maandalizi haya mhsusi ya kiusalama-ambayo yataigharimu Serikali ya Marekani makumi ya mailioni ya dola- yapo kwenye nyaraka ya siri iliyopatikana kwa gazeti hili (la Washington Post). Wakati maandalizi hayo yanaendana na mengineyo katika safari nyingine, nyaraka husika inatoa picha ya jitihada za hali ya juu katika kumlinda Amiri Jeshi Mkuu wa wa majeshi ya Marekani anapokuwa ziarani nje ya nchi hiyo.

Safari yoyote ya Rais, kama za wiki hii huko Ireland ya Kaskazini na Ujerumani, ni zina changamoto na gaharama kubwa kilojistiki.Lakini safari hii ya Afrika inakuwa ngumu zaidi kutokana na sababu mbalimbali, na inaweza kuwa yenye gharama zaidi kuliko zote katika utawala wa Obama, kwa mujibu wa watu walio karibu na maandalizi hayo.

Familia ya Obama inatarajiwa kutembelea nchi hizo tatu kuanzia June 26 hadi Julai 3 ambapo maafisa wa Marekani ndio watakaokuwa na jukumu la kuhudumia takriban kila kitu, badala ya kutegemea hudma za polisi, jeshi na hospitali katika nchi wenyeji.

Rais Obama na mkewe pia WALIPANGA KUFANYA ZIARA KWENYE MBUGA ZA WANYAMA ('SAFARI' kwa Kiingereza), ambayo ingehitaji kikosi cha kupambana na mashambulizi dhidi ya Rais kubeba silaha maalum zenye risasi maalum za kumudu kuwaangamiza duma, simba na wanyama wengine hatariu wa mwituni endapo wangekuwa tishio, kwa mujibu wa nyaraka hiyo

Lakini maafisa walisema Alhamisi kuwa ZIARA HIYO (YA MBUGANI) IMEAHIRISHWA [ NA HII NDIO SABABU ILIYOPELEKEA UZUSHI WA BAADHI YA MABLOGA KUWA ZIARA YA OBAMA KUJA TANZANIA IMEFUTWA] na badala yake imeandaliwa ziara ya kutembelea Kisiwa cha Robben pembezoni mwa pwani ya Cape Town, Afrika Kusini, ambapo Nelson Mandela alifungwa kama mfungwa wa kisiasa.

Gazeti hili lilipowauliza maafisa wa Ikulu ya Marekani (White House) kuhusu ZIARA YA MBUGANI ('safari') mapema mwezi huu,walisema hawajafikia uamuzi wa mwisho kuhusu suala hilo.Afisa mmoja wa Ikulu hiyo alieleza Alhamisi kuwa kufutwa kwa ziara hiyo ya mbugani hakukuhusiana na udadisi uliofanywa na gazeti hili hapo awali.

"Hatuna nyenzo zisizo na ukomo kufanikisha safari ya Rais, na tumeipa kipaumbele ziara ya Kisiwa cha Robben badala ya ziara ya MASAA MAWILI mbugani nchini Tanzania," alieleza msemaji Josh Earnest. "Kwa bahati mbaya, hatuwezi kufanya mambo yote mawili." [HEBU ANGALIA HAPA JINSI BLOGA HUSIKA ALIVYOCHAPIA SENTENSI HIYO NA HATA JINA LA MSEMAJI HUYO WA IKULU]

Nyaraka za ndani za kiutawala zilizosambazwa mwezi April zilionyesha kuwa familia ya Obama ilipanga kufanya ziarazote mbili- ya mbugani na kisiwani, kwa mujibu wa mtu anayefahamu maandalizi hayo.

Marais wa zamani, Bill Clinton na George W. Bush pia waliwahi kufanya ziara za mataifa mbalimbali ya Afrika, ambazo zilihitaji maandalizi magumu kama haya. Bush alikwenda mwaka 2003 na 2008, akiambatana na mkewe katika safari zote hizo. Mabinti wawili wa Bush pia walisafiri naye katika ziara ya kwanza, ambayo ilijumuisha 'safari' kwenye hifadhi ya wanyama katika mpaka wa Botswana na Afrika Kusini.

"Hata katika nchi zilizoendela za Ulaya ya Magharibi, kiwango cha huduma kinachohitajika kwa ajili ya ziara ya rais ni cha hali ya juu," alisema Steve Atkiss, ambaye alikuwa mwandaaji wa ziara akiwa msaidizi maalum wa hudma kwa Bush. "Kadri unavykwenda mbali zaidi, katika maendeo yenye maendeleo duni, kwa hakika ni changamoto ya kilojistiki."

Ikulu ya Marekani na Mashushushu wa Secret Service wamekataa kuzungumzia mipango ya kiusalama, na wasiaidizi wa kiutawala wametahadharisha kuwa maandalizi ya safari ya rais hayajahitimishwa.

Safari za nje za Obama zinakuja wakati taasisi za serikali, ikiwa pamoja na Secret Service, zinapambana na kukata matumizi kwa lazima. Walizni hao wa Rais walilazimika kukata dola milioni 84 katika bajeti yao ya mwaka huu, na mwaka huu Idara hiyo ilifuta ziara za wageni kutembelea Ikulu ya Marekani (kiutalii) ili kuokoa dola 74,000 kwa wiki ambazo ni gharama za watumishi kufanya kazi nje ya muda (overtime).

Taarifa nyingi kuhusu ziara za Rais nje ya nchi hufanywa siri kwa sababu za kiusalama wa taifa, na kuna ufahamu kidogo tu kwa umma kuhusu gharama za jumla. Ripoti kutoka Ofisi ya Uwajibikaji wa Serikali ilionyesha kuwa ziara ya Clinton barani Afrika mwaka 1998 alipozuru nchi sita iliigharimu Serikali ya Marekani angalau dola miloni 42.7.Kiwango hicho kilitumika zaidi na Jeshi, ambalo lilifanya safari 98 kusafirisha watendaji na magari,na kuandaa maendeo ya dharura za kimatibu katika nchi tano.

Kiwango hicho hakikujumuisha gharama za Secret Service ambazo zinachukuliwa kama siri.

Ziara ya Obama inaweza kugharimu kati ya dola milioni 60 hadi milioni 100 kwa kuzingatia gharama za safari za nyuma barani Afrika. Nyaraka ya Secret Service kuhusu ziara hiyo,ambayo ilionwa na gazeti hii, iliyowasilishwa na mtu anayeguswa na gharama za ziara hiyo, haikuonyesha Idara hiyo itatumia kiasi gani cha fedha.

"Miundombinu inayoambatana na ziara za Rais zipo nje ya uwezo wetu," alisema Ben Rhodes, Naibu Mshauri wa Usalama wa taifa wa Obama katika mawasiliano ya kimkakati. "Mahitaji ya kiusalama hayapangiw na Ikulu, hupangwa na Secret Service."

Maafisa wa zamani na wa sasa wa usalama wa serikali waliohusika na ziara za rais walibainisha kuwa watendaji wa Ikulu nao husaidia katika kuainisha mahitaji hayo, kwani hupanga sehemu za kutembelea na mipaka yake. Secret Service na Jeshi hufuatilia maandalizi hayo ya ziara yaliyowasilishwa kwao kwa kutaja mahitaji ya kiusalama.

Maafisa wa Ikulu ya Marekani wamesema kuwa dhamira ya ziara hiyo imekuwepo kitambo sasa, na itakuwa ya kwanza kwa Obama kama Rais kutembelea Afrika Kusini mwa Sahara licha ya 'kusimama' kwa masaa 22 nhini Ghana kwa msaa 22. Demokrasia changa zilizomo kwenye ratiba ya ziara hiyo ni washirika muhimu wa kiusalama katika eneo hilo, Rhodes alisema.

Obama atafanya mikutano na kila kiongozi wa nchi atakayotembela kwa minajili ya kujenga ushirikiano bora wa kiuchumi katika wakati huu ambapo China inawekeza vya kutosha barani Afrika. Pia atapigia mstari programu za afya, ikiwa ni pamoja na mapambano dhidi ya Ukimwi.

Mke wa Rais, ambaye alitembelea Afrika Kusini na Botswana bila ya mumewe mwaka 2011, atashiriki kwenye baadhi ya amtukio katika ziara hiyo. Hilo pia ni changamoto la kilojistiki kwa vile naye atahitaji maandalizi tofauti ya kiusalama kuhusu walinzi na magari, kwa mujibu wa nyaraka hiyo.

Msemaji wa Secret Service, Ed Donovan, alikataa kuzungumzia maandalizi ya ziara hiyo. "Siku zote huwa tunatoa kiwango stahili cha ulinzi kutengeneza mazingira salama," alisema.

Kwa mujibu wa nyaraka ya Secret Service, Obama atakaa siku moja Dakar, Senegal, siku mbili Johannesburg,Afrika Kusini, na siku moja Dar es Salaam, Tanzania.

KATI YA MAGARI 56 KWA AJILI YA ZIARA HIYO NI 'LIMOUSINES' KWA AJILI YA RAIA NA MKEWE , GARI MAALUM LA MAWASILIANO YA SIMU NA VIDEO, GARI LA KUZUWIA MAWASILANO YA RADIO KUZUNGUKA GARI LA RAIS, GARI LILILOJITOSHELEZA LA WA WAGONJWA (ambulance) AMBALO LINAMUDU MAABUKIZI YA KIBAIOLOJIA NA KIKEMIKALI NA GARI LA VIFAA VYA MIONZI YA X-RAY

Mashushushu wa Secret Service husafirisha magari kama hayo, pamoja na vioo vya kuzuwia risasi, katika ziara nyingi, ikiwa ni pamoja na zile za ndani ya Marekani, msemaji wa Ikulu alieleza. Lakini kwa vile kuna nchi tatu zinazohusika katika ziara hiyo, kunahitajika seti tatu za maandalizi hayo,kwa sababu hakuna muda wa kutosha wa kuhamisha vifaa, kwa mujibu wa nyaraka hiyo.

Mashushushu 100 wanahitajika kama 'waangalizi' - kumudu maeneo ya kumzunguka Rais- katika kila mji atakaozuru. 66 wanahitajika kumpokea Obama jijini Dar es Salaam. Kabla 'safari' ya Mbuga ya Taifa ya Mikumi haijaahirishwa wiki iliyopita, ziada ya mashushushu 35 ilijumuishwa kwenye maandalizi hayo ili kumlinda Rais, mkewe na mabinti zao wawili, kwa mujibu wa nyaraka hiyo.

Kadhalika, kati ya mashushushu 80 hadi 100 watasafiri na kufanya kazi kwa shifti kwa masaa 24, kwa ajili ya ulinzi wa Obama na familia yake, vikosi vya kupambana na mashambulizi (counterassault teams) na waandaaji wa lojistiki.

Nyaraka hiyo ya maandalizi ya ziara haionyeshi idadi ya mashushushu watakaohusika na ziara hiyo, japo baadhi watafanya kazi katika kituo zaidi ya kimoja.

Maafisa walisema Secret Service haitaki ziara ya Rais pasipo kituo cha hali ya juu cha jirani cha kukabili maradhi. Kitengo cha utabibu cha Ikulu hufanya maamuzi kuhusu hospitali gani Rais awapo ziarani nje ya nchi kinakidhi viwango, kwa kufanya ziara kwenye nchi husika, maafisa walieleza.

Katika nchi zinazoendelea, Jeshi la Majini la Marekani huweka 'hospitali inayoelea' kwenye manowari ya kubeba ndege au nyambizi, jirani.

"Hivi ndivyo inavyohitajika kuilinda taasisi ya urais wa Marekani," alisema Atkiss kuhusu mahitaji husika, "pasi kujali nani ni rais."

NIMEITAFSIRI HABARI HII KAMA ILIVYO KATIKA GAZETI LA WASHINGTON POST

 
Kwa mlolongo huu ina maana Rais wa Marekani hawezi kutembelea nchi kam Zambia ua Ethiopia ambazo hazina bahari ya kuweza kuegesha manowari yao.Kumbe ndio maana Rais wao hatembei ovyo kama walivyo maris wa Kiafrika ambao kila baada ya wiki huenda London, Washington au Brussels.

Thanks Mr Chahali.
 
1. Kwan wazungu wengine wanaoenda mbugani kutembea wanabeba snippers wasiliwe na wanyama?
2. Obama anakuja kufanya nini hasa? Utalii? Ziara ya kiuchumi?
 
Malimwengu! ninaogopa huko baadaye inaweza kuwa kasumba kwa viongozi wetu wanaweza hitaji gharama hizi hata watakapofanya ziara za namna hii huko Tandahimba au Arusha kisa hakuna amani, Mungu aepushe mbali, Obama bora usije
 
Very interesting hapa akija wang'oa kucha wetu wa Tiss watawekwa kando kabisa hata Fastjet atalindwa na hao secret service
 
Kwa mlolongo huu ina maana Rais wa Marekani hawezi kutembelea nchi kam Zambia ua Ethiopia ambazo hazina bahari ya kuweza kuegesha manowari yao.Kumbe ndio maana Rais wao hatembei ovyo kama walivyo maris wa Kiafrika ambao kila baada ya wiki huenda London, Washington au Brussels.

Thanks Mr Chahali.
Za JK ni za low cost but due to the frequency the overall cost equals Obama
 
Kwa mlolongo huu ina maana Rais wa Marekani hawezi kutembelea nchi kam Zambia ua Ethiopia ambazo hazina bahari ya kuweza kuegesha manowari yao.Kumbe ndio maana Rais wao hatembei ovyo kama walivyo maris wa Kiafrika ambao kila baada ya wiki huenda London, Washington au Brussels.

Thanks Mr Chahali.

Viongozi wetu wa Kiafrica hawana thamani kwasababu ya ufisadi wao na uzururaji wao ng'ambo kila siku so wala hawahitaji ulinzi
 
duh! Hawa majamaa bana ni noma ila ni kweli hakuna hospitali yenye hadhi ya obama hapa bongo??hahaha
 
Hii ndio USA taifa lenye nguvu duniani ziara yao ya siku moja bajeti ya wizara yetu kwa mwaka mzima!
 
Mgeni njoo wenyeji tupone. Au kinyume chake Mgeni njoo wenyeji tukome
 
Daaaa kwa hiyo wale wachomoa kucha za watu TISS watakuwa hawana kazi hiyo siku au sio??kweli Marekani taifa kubwa...

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
duu hu ugeni sasa kero, anakuja kutalii na vifaa vya kijeshi kama anakwenda kuipiga North Korea
 
Back
Top Bottom