Habari za wana-magamba kuandaa vijana kwa ugaidi wa kisiasa hazijaanza leo. Nape anabaraguza tu, anapopinga kuwepo njama na mikakati hiyo. Ushahidi wa kuthibitisha hoja za mafunzo ya ugaidi wa aina hiyo ambao sasa umekua na kufikia kiwango cha kukaribia au kufanana na 'al shabab' au 'al qaida' ni mojawapo ya mahojiano na kijana mmoja aliyeamua kuokoka '(kuzaliwa mara ya pili)katika kipindi cha "This is my Story" kilichorushwa na ATN miezi ya nyuma. Kijana huyo alidai kwamba alifuatwa na kuombwa kujiunga na vijana wa chama cha magamba huko kilosa. Vijana hao walifundishwa kuhujumu matokeo ya kura wakati wa uchaguzi wa siku za nyuma.
Kwa kuwa kila mwaka wa uchaguzi chama hiki kina kawaida ya kufundisha vijana kadhaa kwa kila wilaya wa kufanya hujuma katika upigaji kura na matokeo; na kwa sasa yamkini mafunzo yao yameboreshwa sana hadi kuwa ya kigaidi. kwa hiyo,kufikia sasa kuna jeshi kubwa kabisa la vijana hawa chini ya chama hiki.
Wasi wetu, jeshi hili linaweza kutumiwa na ye yote kufanya cho chote, po pote, wakati wo wote ili mradi wahakikishiwe "MSHIKO" unaovutia. Kwa hiyo, ni kundi hatari hata kwa wana-magamba wenyewe. Hili ni suala la wakati tu, litatokea sio baadaye sana wala si karibu sana.Kila lisemwalo lipo ama..........
Kwa kuwa kila mwaka wa uchaguzi chama hiki kina kawaida ya kufundisha vijana kadhaa kwa kila wilaya wa kufanya hujuma katika upigaji kura na matokeo; na kwa sasa yamkini mafunzo yao yameboreshwa sana hadi kuwa ya kigaidi. kwa hiyo,kufikia sasa kuna jeshi kubwa kabisa la vijana hawa chini ya chama hiki.
Wasi wetu, jeshi hili linaweza kutumiwa na ye yote kufanya cho chote, po pote, wakati wo wote ili mradi wahakikishiwe "MSHIKO" unaovutia. Kwa hiyo, ni kundi hatari hata kwa wana-magamba wenyewe. Hili ni suala la wakati tu, litatokea sio baadaye sana wala si karibu sana.Kila lisemwalo lipo ama..........