Maandalizi ya halaiki kwa ajili ya sherehe za kuzima mwenge yaliigharimu serikali kiasi cha shilingi milioni mia moja (mil 100). Pamoja na kugharimu kiasi hicho cha fedha ni dhahiri kuwa wanafunzi walioshiriki walikosa kushiriki kikamilifu katika masomo yoa. Cha kujiuliza ni; Je, matumizi makubwa kama hayo katika shughuli kama hiyo yana tija kwa taifa na wanafunzi ikizingatiwa kuwa ni wanafunzi hao hao kila siku tunasikia kilio cha madawati na huku serikali ikidai haina pesa!Source: Star TV, taarifa ya habari saa 2.