MSEZA MKULU
JF-Expert Member
- Jul 22, 2011
- 3,752
- 5,494
Mwaka 1929 nje kidogo ya mji wa beijing kwenye mapango ya milima kuligunduliwa fuvu na mifupa ambayo inasadikika kuwa ya binadamu wa kwanza. Kila mwaka sehemu hii hutembelewa na watalii zaidi ya 150,000. Researchers wa kichina wanafanya juu chini kuhakikisha wanatafuta kigezo ili ionekane mtu wa kwanza aliishi china.
SIASA ILIYOJIFICHA NYUMA YA MIFUPA HIYO
Wachina wengi hawaamini kuwa mtu wa kwanza alikuwa afrika kwa mujibu wa historia tena Arusha. Wanataka kila kitu kitoke china.Utafiti wa kisayansi unaonyesha karibu asilimia 97 ya Vinasaba vyao orgin yake in afrika.
Kumeibuka vuguvugu kubwa asia kuanza kufukua mifupa na mafuvu ili tu angalau ijulikane mtu wa kwanza aliishi Asia hata kama sio china. Archeologist wetu wanayo nafasi ya kuilinda na kuitetea hiyo tunu Adimu kabisa Ulimwenguni iliyopo Olduvai Gorge kabla jamaa hawajafanya mapinduzi ya kitalii.