Maana ya Wapinzani wataleta Vita ndio hii hapa.

STEIN

JF-Expert Member
Aug 29, 2010
1,770
553
Ndugu zangu wanaJF, Imekuwa ni wimbo/jadi kwa CCM kipindi cha uchaguzi kuhubiri eti wapinzani wakichukua nchi wataleta Vita, Udini, Watavuruga amani iliyoko nchini. Je ni kweli kwamba wapinzani wataleta haya ambayo CCM wanayahubiri? HAPANA.

Mimi kwa upande wangu naamini hakuna chama cha upinzani kitakacholeta ugomvi wa aina yeyote kwani viongozi wa Upinzani wana utashi wa kisiasa kama ambavyo tumeona wakati wa kampeni na baada ya uchaguzi wa mwaka huu.

Ni jambo la kushangaza kuona CCM na serikali yake wamekuwa na desturi ya kuwalazimisha waTZ kuwa na ugomvi usio na msingi wowote hata pale ambapo wananchi kwa hiari yao wamemchagua kiongozi fulani imekuwa ni desturi kwa CCM kuwalazimisha watawaliwe na fisadi wanayemtaka. Hi ilionekana wakati wa kampeni na kutangangaza matokeo pale wanapopeleka askari kwa ajili ya kuwapiga wananchi ili wamtangaze mgombea wao aliyeshindwa.
Mfano hayo yalitaka kutoke mwanza, ubungo, kawe, karatu, arusha, mbeya, musoma etc.

Lakini CCM wakaenda mbali zaidi kwa kufanya hujuma na kutofuata utaratibu katika uchaguzi wa Mameya na wenyeviti wa halimashari, tumeona Zengwe likitokea mwanza, arusha, mbeya mjini, moshi, kigoma, ukerewe, mbulu hii yote ikiwa ni kuhakikisha madiwani wa CDM wasishiriki mchakato wa kuchagua mwenyeki/Meya wao. Hii ni dalili za kuwataka hata watu ambao hawataki fujo unawalazimisha kufanya vurugu na hatimaye kuleta uvunjifu wa amani. Huwezi kumpiga mbunge aliyechaguliwa na wananchi mpaka anazimia halafu unasema unadumisha amani hata siku moja hii haikubaliki.

Nafikiri wananchi sasa wataelewa kuwa wanaoleta vurugu, umaskini, ujinga ufisadi nchi sasa wako hadharani na dawa yao ni kuwang'oa wote, wakibakia ni wachache mno kiasi kwamba hawawezi kufanya kitu kama ambavyo Karatu na moshi wamefanya. Ni kuwaondoa wote.

MUNGI IBARIKI TZ NA WATU W
AKE.
 
Umenikumbusha miaka ya 94 uchaguzi wa serikali za mitaa, kule kijijini kwetu Endamarariek kampeni ilikuwa kwamba tusiwachague wapinzani, maana mkiwachagua Tanzania itakuwa kama Rwanda na Burundi.
 
Hapana, siku hizi wengi tumesoma na tv, radio, magazeti kwa sana, wamechemshaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Freedom is coming TOMORROW!!! Freedom is around the conner!!! The day is coming when we shall break all the CCM chains and shackles around us!!! ALUTA CONTINUA!!!!!
 
Naungana na Jf kuendelea kukemea hayo ambayo CCM imekuwa inayafanya kwa maslahi ya chama hicho. Ni aibu kubwa sana na viongozi wake wa juu kuyatamka. Watanzania sasa hatudnganyikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!
 
TUNALAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAANI UDIKITETA HUU WA CCM NI KAMA NILIVYOMJIBU MWANAJF AITWAYE MUYA ALIYEKUWA AKITETEA KUPIGWA KWA LEMA HUU NI UDIKITETA NA UNYANYASAJI WA HALI YA JUU TANGU NIZALIWE SIJAWAHI KUSIKIA MBUNGE WA CCM AMEPIGWA HATA KOFI NA POLISI -KUMPIGA LEMA NI SAWA NA KUWAPIGA WANANCHI WALIOMCHAGUA LEMA YAANI UNAMSHA HASIRA KWA HAO WATANZANIA.MIMI NINAAMINI WEWE MUYA NDIO NEGATIVE MINDED PERSON WITH VERY LITTLE THINKING -TRY TO OPEN UP YOUR THINKING CAPACITY -AND THINK OUTSIDE THE BOX, TALK THE FACTS
1. ccm walizimisha mbunge wa viti maalum kupitia tanga apigie kura ccm eti kisa mwenyekiti mkoa arusha -hii ni kuvunja sheria au? jibu unalo
2. Mkurugenzi anatakiwa kuendesha kikao cha madiwani cha kuchagua meya na naibu wake baada ya idadi ya wajumbe kufika ukiondoa wajumbe yaani madiwani wa chadema 2/3 haipo nani kavunja sheria wewe muya????? jibu unalo
3. Hon. Lema aliwambia waliitisha kikao hicho wakati wametoa barua ya semina bila kuwajulisha chadema wapi kuna haki???
4. Police kazi yao ni kulinda amani raia na mali zake kwakuwa mheshimiwa Lema alikuwa anahoji utaratibu na ccm kwenda kumwita OCD amutoe Lema kwenye kikao na hivyo OCD kutumia Polisi hiyo ni haki? Tuambie wewe muya unajua sheria
5. Tangu uzaliwe ni lini ulisikia mbunge wa ccm kapigwa hata kofi na polisi zaidi ya mgombea mbunge wa shinyanga kumpiga mtama OCD kule Maswa je angekuwa Shibuda ndio kampiga OCD ingekuwaje?? hiii inasikitisha saana.
6. Kwa ujumla CCM sasa inaonesha waziwazi sura yake halisi ya sasa na kwa vyovyote vile inachochea hasira na vurugu ipo siku tutasema vinginevyo harafu wewe muya sijui utatwambia lini -kipofu mkubwa au fisadi mkubwa wewe.
7. Mapolisi wa namna hii ipo siku nguvu ya umma itawaangukia ndio watapata adabu na fundisho
8. Ninaamini IGP hana uwezo wa kufanya lolote kwa ccm kupigwa kwa lema ni agizo la serikali kupitia mkurugenzi arusha mjini aliyekuwa akitekeleza amri ya aliyemtea kuhakikisha kwa kumwaga damu au vingenevyo chadema haiongozi jiji -yana mwisho haya
 
CCM inatumia sana mtaji wa wajinga kutawala Tz.Nionavyo mimi asilimia 90 ya wanainchi Tz ni majuha hivyo CCM ambacho nakitafsili kama Chama Cha Majuha,Mafisadi,Majizi,Majahili,Majangiri,Machizi,Mazembevu,Milafi,Mifunza,Mashetani hiyo ni M. Na hiyo amani wanayosema wapinzani wataipoteza waionyeshe ipo wapi mi kwa akili yangu niliyo nayo sija iona hiyo amani ipo wapi haswa. Wananchi kila siku taabu tu kama ufisadi,rushwa,mtu anaishi chini ya dola moja,hakuna fulsa za wasomi kujiajiri, foleni barabarani,usafiri duni wa umma na mengine mengi.CCM ni jini linatunyonya watanzania hivyo tuwakemee na kuwakataa.KUONGOZWA NA CCM NI SAWA NA KUMKABIDHI NCHI TAHIRA. NI AFADHARI WIZI WALIOUFANYA WAKOLONI KULIKO HUU UPUUZI WA CHAMA CCM. Hiki ni kinyesi cha mtu na si chama. Kinaniumiza sana na huwa naomba Mungu awachukue kwa mauti maana wanatugharimu sana.
 
Umenikumbusha miaka ya 94 uchaguzi wa serikali za mitaa, kule kijijini kwetu Endamarariek kampeni ilikuwa kwamba tusiwachague wapinzani, maana mkiwachagua Tanzania itakuwa kama Rwanda na Burundi.

Mkuu mungi Hayo yalihubiriwa sana na kama unakumbuka ha DR. Slaa alipata wakti mgumu sana kuwa shawishi watu, lakini hatimaye watu wa KRT wakmuelewa na kumpa ubunge.

Sasa kazi yetu ni moja kuwaonyesha kwamba CCM ndio wakuleta vita maana hawataki kuondoka madarakani kidemocrasia.

I hate mafisa and their CCM

Peoples power
 
CCM inatumia sana mtaji wa wajinga kutawala Tz.Nionavyo mimi asilimia 90 ya wanainchi Tz ni majuha hivyo CCM ambacho nakitafsili kama Chama Cha Majuha,Mafisadi,Majizi,Majahili,Majangiri,Machizi,Mazembevu,Milafi,Mifunza,Mashetani hiyo ni M. Na hiyo amani wanayosema wapinzani wataipoteza waionyeshe ipo wapi mi kwa akili yangu niliyo nayo sija iona hiyo amani ipo wapi haswa. Wananchi kila siku taabu tu kama ufisadi,rushwa,mtu anaishi chini ya dola moja,hakuna fulsa za wasomi kujiajiri, foleni barabarani,usafiri duni wa umma na mengine mengi.CCM ni jini linatunyonya watanzania hivyo tuwakemee na kuwakataa.KUONGOZWA NA CCM NI SAWA NA KUMKABIDHI NCHI TAHIRA. NI AFADHARI WIZI WALIOUFANYA WAKOLONI KULIKO HUU UPUUZI WA CHAMA CCM. Hiki ni kinyesi cha mtu na si chama. Kinaniumiza sana na huwa naomba Mungu awachukue kwa mauti maana wanatugharimu sana.

Good thing ni kwamba waTZ are no longer wajinga maana hata wao wameishiwa mbinu za kuiba kura badala yake wanatumia Nguvu kama Arusha walishazidikwa kete na CDM, Tukiunge mkono.

Na issue ya kuwazika sasa ni katiba mpya.

Peoples power.
 
Chonde chonde watawala wetu SISI M someni alama za nyakati watanzania wanawasoma!!!!!!!!!!!!!!!! Kama mliona kilichotokea Mwanza kuweni macho...Hii si nchi ya kuchezea kama gololi...wananchi wa sasa si wa kudanganya kama ..watoto!!!!! msongo wa mawazo na hasira umewajaa watu poleple moshi unafuka!!!1 msianze kupuliza huo Moshi wandugu oooohooo!
KILA MWANANCHI ANA HAKI.....sisiem haiko juu ya sheria....OLE OLE OLE SISI M!!!! OLE OLE OLE MAFISADI.....KIFO chenu kipo karibu
 
Mzee hapo kwenye wino mwekundu umenikuna sana!!

Ndugu zangu wanaJF, Imekuwa ni wimbo/jadi kwa CCM kipindi cha uchaguzi kuhubiri eti wapinzani wakichukua nchi wataleta Vita, Udini, Watavuruga amani iliyoko nchini. Je ni kweli kwamba wapinzani wataleta haya ambayo CCM wanayahubiri? HAPANA.

Mimi kwa upande wangu naamini hakuna chama cha upinzani kitakacholeta ugomvi wa aina yeyote kwani viongozi wa Upinzani wana utashi wa kisiasa kama ambavyo tumeona wakati wa kampeni na baada ya uchaguzi wa mwaka huu.

Ni jambo la kushangaza kuona CCM na serikali yake wamekuwa na desturi ya kuwalazimisha waTZ kuwa na ugomvi usio na msingi wowote hata pale ambapo wananchi kwa hiari yao wamemchagua kiongozi fulani imekuwa ni desturi kwa CCM kuwalazimisha watawaliwe na fisadi wanayemtaka. Hi ilionekana wakati wa kampeni na kutangangaza matokeo pale wanapopeleka askari kwa ajili ya kuwapiga wananchi ili wamtangaze mgombea wao aliyeshindwa.
Mfano hayo yalitaka kutoke mwanza, ubungo, kawe, karatu, arusha, mbeya, musoma etc.

Lakini CCM wakaenda mbali zaidi kwa kufanya hujuma na kutofuata utaratibu katika uchaguzi wa Mameya na wenyeviti wa halimashari, tumeona Zengwe likitokea mwanza, arusha, mbeya mjini, moshi, kigoma, ukerewe, mbulu hii yote ikiwa ni kuhakikisha madiwani wa CDM wasishiriki mchakato wa kuchagua mwenyeki/Meya wao. Hii ni dalili za kuwataka hata watu ambao hawataki fujo unawalazimisha kufanya vurugu na hatimaye kuleta uvunjifu wa amani. Huwezi kumpiga mbunge aliyechaguliwa na wananchi mpaka anazimia halafu unasema unadumisha amani hata siku moja hii haikubaliki.

Nafikiri wananchi sasa wataelewa kuwa wanaoleta vurugu, umaskini, ujinga ufisadi nchi sasa wako hadharani na dawa yao ni kuwang'oa wote, wakibakia ni wachache mno kiasi kwamba hawawezi kufanya kitu kama ambavyo Karatu na moshi wamefanya. Ni kuwaondoa wote.

MUNGI IBARIKI TZ NA WATU W
AKE.
 
Nimeikumbukia hii tread kwani, leo tunashuhudia maana ya upinzani kuleta vita, Mnamo tarehe 5, January waTZ tumehakikisha jinsi gani ccm walivyo wabaya hadi Diwani wa CCM na aliyekuwa naibu meya FEKI wametupa proof ya nilichokiandika wakati ule.

Peoples power lazima ifanye kazi sasa na milele.
 
Naamini kabisa sasa mnaelewa kuwa kuiondoa CCM Zanzibar sio kurudisha uarabu au kurudisha utumwa ,nilijua mambo yakizidi mtaelewa na mtaweza kutambua pumba na mchele.
 
Back
Top Bottom