Ukiona mkeo anakwambia mtoe mimba kwasababu iliingia bahati mbaya ,ujue hana uhakika kama mimba ni yako mchunguze vizuri anachepuka.
Kuna jirani yangu aliambiwa hivyo na mkewe wakatoa, mwaka mmoja baadaye ikaingia nyingine bibie akijua ni ya mumewe kumbe akajaza akazaliwa mtoto anafanana sana na jirani yake.
 
Wakuu habari!

Jambo hili nimelivalia njuga na naona matunda yake yanaanza kuonekana, nafikiri nikiendelea hivi kwa mfululizo wa miaka mitano kwa kiasi kikubwa jamii itarudi kwenye mstari.

Moja ya matokeo chanya katika nyuzi zangu za ubikra ni kuwa wale walioolewa bila ya bikra na wale ambao bado hawajaolewa na hawana bikra wanapiga kelele wakitapa tapa, wengi wamekuja Pm wakiniomba niache. Ujumbe wangu ni huu; Asiyefunzwa na Mama yake hufunzwa na ulimwengu. Mandhali Jokajeusi nipo mada hizi zitaendelea mpaka nitakapoondoka duniani. Hivyo wale wanaaoumia nawapa pole kwa sababu huu ni mwanzo tuu.

Madhara ya Makuu ya kuoa mwanamke asiye na bikra, Kijana usiyeoa soma kwa umakini ukitumia akili zaidi ya hisia zako.

1. MTALAKA HATONGOZWI
Kabla hujaoa mwanamke asiye na bikra kaa ukijua kabisa mtalaka hatongozwi, popote pale duniani. Pia kumbuka awali ni awali hakuna awali mbovu. Pia kumbuka, Mavi ya kale hayanuki. Hivyo mwanamke anapokuwa tayari alishakuwa kwenye mahusiano na wanaume huko nyuma ya kimapenzi kisha wakaachana kwa sababu abc kisha wewe ukampata akakuambia ameachana na ma-ex wake jua kuwa anakudanganya, kuachana labda kama wamekufa lakini kama wapo hai hesabu umeumia ndugu yangu.
Nina ushahidi usio na shaka kuhusu jambo hili na hata humu JF kila siku tunasikia malalamiko ya wanawake kurudiana na ma-ex wao au kufumaniwa nao. Hiyo ni kawaida sana, na mara zote mimi siwalaumu wanawake kwa kufanya hivyo kwani hiyo ndio asili. Mtalaka hatongozwi.

Usipokubali maneno yangu na ukashindwa kujifunza kwa yanayotokea kwa wenzako basi subiri wewe ndio uwe funzo na mfano kama walivyo wabishi wengine.

2. KUBAMBIKIZIWA MIMBA
Wanawake wengi wasio na bikra wamewaingiza wanaume katika magonjwa makuu kwa kuwabambikizia watoto wasio wao. Hata ule utafiti usemao kuwa 60% ya wanaume wanalea watoto wasio wao unalandana(correlation) na idadi ya wanaume waliooa wanawake wasio na bikra.
Kuna uwezekano wa kuingia kwenye mahusiano na mwanamke mwenye mimba changa ikiwa tuu ulimkuta hana bikra, mifano ipo ya kutosha hata huku mitaani achilia mbali watu maarufu kama vile Muna Love na Casto Dickson Vs Baba patrick, Mama Diamond na Babab Ricardo Vs Mzee Abdul, na wanawake kukubambikizia mtoto hawaoni shida kwa sababu tayari wameshakuona wewe ni maandazi, tayari umejidharau, yaani uache kuoa mtoto mbichi uchukue used alafu wakuheshimu. Hiyo hakuna mwanamke wa hivyo.

Usijedhani ukimuoa mwanamke asiye na bikra na single mother ataona umemuonea huruma kwa kumsitiri, yeye atakachojua kuwa uzuri wake ndio sababu umedata naye, hivyo suala la kuonewa huruma hilo sahau, na ndio maana wao wakifanya matukio yao kwako wala hawatakujali kuwa uliwastiri. Nafikiri mifano mnayo hata huko mitaani.
Hivyo kuoa mwanamke asiye na bikra kuna uwezekano mkubwa wa kubambikiziwa mtoto achilia mbali kuchetiwa ambapo ni costant

3. WATOTO KUWA NA TABIA ZA AJABU AJABU
Ukioa mwanamke asiye na bikra na malaya, sio ajabu watoto wako wakawa na vitabia vya ajabu ajabu yaani mchanganyiko kulingana na idadi ya wanaume waliolala na mke wako. Angalia wanawake wengi ambao ni malaya kisha angalia tabia za watoto waliowazaa. Watoto wamenajisiwa. Mtoto akipimwa DNA ni wakwako lakini tabia zipo mbali sana na wewe na ukoo wenu na ukoo wa mama yake. Hii ni kutokana na kuwa mwanamke anapolala na wanaume tofauti tofauti hujinajisi na kujipa maroho machafu kwani tendo lenyewe ni chafu.
Kama unabisha jaribu sumu kwa kuonja. Waliooa wananielewa zaidi kwani wanayaona hayo kwa macho yao.

4. WATOTO KUUNGANA NA MAMA YAO.
Ukioa mwanamke asiye na bikra ni rahisi sana kwa watoto kumsikiliza Mama kuliko kukusikiliza wewe Baba, au ni rahisi sana kwa watoto wako kumsikiiza Baba mwingine kuliko kukusikiliza wewe. Hii ni kutokana na kuwa tayari wewe sio namba moja, wewe sio kichwa tena bali mkia. Unapoambiwa Baba ni kichwa cha nyumba wanamaanisha Namba moja, yaani Baba ndio mwenye maamuzi, mwanzo, na ndio maana popote pale kichwa ndio hutangulia, sasa kama kwa mkeo hukutangulia kumjua unafikiri utakuwaje kichwa kwake au namba moja kwake. Wakati mwingine wapo wanawake wachache wema wanaojitahidi kuwa wema licha ya kuolewa bila ya bikra lakini bado nature inawavuta kufanya mabaya.

Zamani Baba alikuwa ndio nguzo ya familia kwa sababu nyingi mno, watoto walikuwa wanamsikiliza Baba, hii ni kutokana na kuwa wamama wengi waliolewa wakiwa na bikra. Lakini tangu wanawake waanze kuolewa bila bikra siku hizi Baba sio lolote tena, na ndio maana ongezeko la watoto wasemao nani kama Mama ni kubwa, na sababu nimeshaieleza.
Kama unabisha jaribu sumu uone.
Baba kama unataka heshima sikiliza ninachokuambia, ukijifanya unajua na unaheshimiwa kisa sasa unanguvu subiri miaka 60 huko utakumbuka maneno ya Jokajeusi.

5. KUOA MAMA WA WAFU
Kuoa mwanamke asiye na bikra kunaweza kupelekea kuoa mama wa wafu, unaoa mwanamke aliyetoa mimba nyingi nawe huwezi kulijua hilo na huna uhakika, Lakini ukioa mwanamke bikra unaoa mke unayejua ni msafi na aliyejitunza. Tayari unaoa mwanamke ambaye anakesi ya mauaji na laana ambayo huijui, ni bora ungekuwa unaijua hii itakusaidia kumlilia Mungu amsamehe na awasamehe, jambo moja la kuzingatia ni kuwa kuomba msamaha kwa makosa makubwa hakuombwi kwa kusema tusamehe makosa yetu, hiyo ni sala ya jumla ambayo watu huomba wakiwa kwenye halaiki, Jokajeusi nashauri, mwanamke kama umetoa mimba ni vyema umjulishe mumeo mtarajiwa ili muweke mambo sawa, sio umuingize Mwanaume wa watu kwenye mikosi na mabalaa bila ya yeye kujua.

6. MWANAMKE ASIYE NA BIKRA SIO MKEO BALI MSHIRIKA.
Kuna tofauti kubwa kati ya mke na mshirika wa maisha. Mke ni sehemu yako yaani ni ubavu wako, mshirika sio sehemu yako bali mmeamua kushirikiana katika maisha. Mke hukupenda wewe na familia yenu, naye ni sehemu ya ukoo wenu. Lakini mshirika sio sehemu ya ukoo wenu kwanza huwaza kuwapa faida wazazi wake zaidi. Siku hizi wanaume wengi wanaoa wanawake wasio na bikra na ndio maana hao washirika wao hupendelea makwao kwani sio mwili mmoja na waume zao. Mwanaume mwenye mke anaouwezo wa kumwambia mke wake kuwa asienda kwenye msiba hata wa mama yake(mama wa mke) na mke wake akamtii, lakini mwanaume aliyeoa mshirika wa maisha hana uwezo wa kumzuia mshirika wake asiende kwenye msiba wa mama yake(mama wa mshirika).
Kwa kifupi mume anakuwa anamamlaka kwa mke wake na sio kwa mshirika. Kumbuka mshirika ni mwanamke aliyeolewa bila ya bikra, na bikra aliiotoa kwa makusudi kabisa.
Mke ukishamuoa hawazi tena nyumbani alipozaliwa mpaka mume mwenyewe umkumbushe kwamba aende kusalimia, lakini mshirika kwa mwaka huenda nyumbani mara mbili mpaka mara tatu.
Hapa hoja kubwa ni kuwa huwezi mtawala mwanamke ambaye sio mkeo, mkeo lazima akusikilize kwa chochote kile Lakini ukiona mwanamke unayeishi naye hakusikilizi jua sababu ni hiyo hapo juu, hukuoa akiwa bikra.

Waliooa wananielewa, sumu aionjwi

7. UMILIKI
Ukioa mwanamke asiye na bikra, cha mwanaume ni cha wote na cha mwanamke ni chake mwenyewe. Watu wanasema wanawake ni wabinafsi, mimi nawaambiaga kuwa mwanamke sio mbinafsi mpaka pale atakapoolewa bila ya kuwa na bikra. Wanawake wengi walioolewa bila bikra ni wabinafsi kupitiliza. Hii ni tofauti na mwanamke aliyeolewa na bikra yake, ambaye chake ni cha wote na cha kwako ni chawote. Mkeo(aliyeolewa bikra) anajua kuwa yeye ni mali yako na kila kitu anachomiliki yeye. Mkeo yaani uliyemuoa bikra anapenda umlinde yaani umchunge kwani anajua yeye ni malkia, yeye ni wathamani, lakini mwanamke ambaye hajaolewa akiwa na bikra hapendi umchunge, umlinde wala kumfuatilia, wana msemo wao wanasema mwanamke hachungwi, msemo huo sio wa mke bali mshirika. Hata humu JF wapo na wanajijua.
Mkeo uliyemuoa bikra hata watoto atakuambia watoto wako wanasumbua, au wanashida abc, au hata ukiwaadhibu atakuambia utawaua wanao Mume wangu. Lakini ambaye hajaolewa bikra ni kawaida kusikia wakisema muache mwanangu.

8. SIRI YA MTOTO
Mwanaume ukishaoa mwanamke asiye na bikra basi jua siri ya mtoto niwa nani anaijua Huyo mshirika wako. Ndio maana siku hizi mpaka sheria zinatungwa kuwa Baba ni mlezi sio mzazi. Kwani wanawake wengi wameolewa wakiwa bikra.

Siku hizi ndoa ni ndoano kwa sababu wanaume wengi wanaoa wanawake wasio na bikra. Mpaka wengine wanaogopa na kuiona ndoa haina maana.
Lakini ndoa ni sehemu tamu,yenye raha ikiwa utaoa mwanamke mwenye bikra. Vijana ndoa ni tamu kama utapata mke wako na sio mshirika wako.

Nitaendelea kuwafunza vijana hivi hivi mpaka wenye akili watakaponielewa.

Jokajeusi
Hizi mada zako zinagusa pabaya sana,sio wanandoa wengi wataipenda,ila kuna fundisho pia kwa wasio na ndoa...
 
Hizi mada zako zinagusa pabaya sana,sio wanandoa wengi wataipenda,ila kuna fundisho pia kwa wasio na ndoa...
Mimi nimeoa, ingawa sikuoa bikra, lkn ukweli ni kwamba bikra inaleta heshima zaidi kwa mwanamke, na ni usafi na utakatifu wa kizazi utakachozaa. Kuoa mke bikra ni bora zaidi lakini mwanaume pia akiwa bikra ni bora mara zaidi. Ndoa ya watu wawili ambao wote hawajawahi kufanya ngono, ni ndoa tamu sana na yenye upendo wa kweli %
 
Mimi nimeoa, ingawa sikuoa bikra, lkn ukweli ni kwamba bikra inaleta heshima zaidi kwa mwanamke, na ni usafi na utakatifu wa kizazi utakachozaa. Kuoa mke bikra ni bora zaidi lakini mwanaume pia akiwa bikra ni bora mara zaidi. Ndoa ya watu wawili ambao wote hawajawahi kufanya ngono, ni ndoa tamu sana na yenye upendo wa kweli %
Waambie hao
 
Ombi kwa mara ya pili.

Dear future husband usije ukaifahamu jamiiforums.

Huku mtaani kwetu kuna mama aliolewa na Bikra yake, uwa ananiambia D siijui mbo.o tofauti na ya baba Xx lakini huyu mwanaume sijui nimfanyie yapi atulie. Mume wake ni kicheche mbaya, skirt mpya isiingie mtaani anatupia ndoano. Hana heshima kwa mke wake hata kidogo.

Ona huyo kajitunza ila kaja kupata galasa, bikra ina heshima sawa lkn sio guarantee ya utulivu ndani ya ndoa. Sitaki kuamini kama kuna wake waliolewa bila bikra then sio waaminifu kwa ndoa zao. Hata hao mabikira siku wakishawishika wakaonja nje na kunogewa yatakuwa Yale yale tu.

Nikirepot kutokea pande za kaskazini ni mimi mjumbe kutokea chama cha wanawake un'virgin Tunakwambia hivi utulivu tunao kwenye mahusiano yetu, imagine aliyenibikiri ameshatangulia mbele ya haki nabaki vipi sasa huku duniani? Unataka tuishi maisha ya kijane kama wahindi? Hii tamaduni kwetu huku haipo ni lazima tu nitakuwa na mahusiano mengine.

Nimeandika sana. Lol
Unagangaika Nini?.... Kama mwanaume akiamua kuoa..hizi mada Wala Haziwezi mtoa kwenye mstaari wake..

Usiwe na hofu Wala usihangaika....
Mungu anajua sisi Ni wakosefu na Bado anatubariki ....So don't mind KABISA.
.
.Maneno ya Huyu yawezekana yakawa na ukweli...lakini Yasikusumbue
 
Haha
Sihangaiki kwa chochote, I only dance according to the Post's tune.
Unagangaika Nini?.... Kama mwanaume akiamua kuoa..hizi mada Wala Haziwezi mtoa kwenye mstaari wake..

Usiwe na hofu Wala usihangaika....
Mungu anajua sisi Ni wakosefu na Bado anatubariki ....So don't mind KABISA.
.
.Maneno ya Huyu yawezekana yakawa na ukweli...lakini Yasikusumbue
 
Utakuwa na tatizo la akili hujijui unahitaji tiba, daily bikra, single mother I think you need healing in ur heart mi mada kumi kumi na yote hyo unaanzisha kujifariji na ujiponye nafsi yako . Hongera kwa kutoa sumu moyoni na hivi twatumia fake I'd
Nilipofungua tu nikaanza kutafuta reply yako.😀😀
 
Mkuuu..Hii ishafika comment 100
Anzisha nyingine.... ya Bikra.

Leo weekend sisi wakucomment tupo
 
Haha
Sihangaiki kwa chochote, I only dance according to the Post's tune.
Umecomplain Sana ...nimeona hii the second time.
What has passed yalishapita...hayatajirudia

What matters Ni future yako how you Choose to live with your husband kwa heshima ..

Hawa Wanaume Wanaamini usafi Ni was mwanamke pekeee.....

Huyu Mwamba kukisifia Uzinifu wake ...Inashangaza Akili zetu zilivyo.
 
Unagangaika Nini?.... Kama mwanaume akiamua kuoa..hizi mada Wala Haziwezi mtoa kwenye mstaari wake..

Usiwe na hofu Wala usihangaika....
Mungu anajua sisi Ni wakosefu na Bado anatubariki ....So don't mind KABISA.
.
.Maneno ya Huyu yawezekana yakawa na ukweli...lakini Yasikusumbue
Sio yawezekana yakawa na ukweli bali ni ya ukweli. Ingawa sote tuna baraka zetu toka kwa Mwenyezi MUNGU lkn tambua kuwa walio wasafi wanazo baraka zaidi hata juu ya kizazi chao
 
Sio yawezekana yakawa na ukweli bali ni ya ukweli. Ingawa sote tuna baraka zetu toka kwa Mwenyezi MUNGU lkn tambua kuwa walio wasafi wanazo baraka zaidi hata juu ya kizazi chao
Nikweli...kabisa lakini Usafi huu Kama Mungu atakavyo...Ni wa mwanamke pekeee?..
 
Mungu anavyose Msikurubie Zinaaa ....Namaanisha Wanaume wazini sanaaaa...alafu Waoe bikra wapate Vizazi vyema?...

Mtume Muhammad hakuoa Bikra..bi hadija...Je kizazi chake Ni kichafu..?

Mwenyezi Mungu anatutaka tuombe Atupe watoto walio pious ...TUMUOMBE Atupe wake na Waume wake walio wema..

Na Huyu Huyu Mungu anasema mzinifu awe na mzinifu mwenzake..

Lakini watu wanataka kumjua Mungu kwenye maswala ya kugegeda tu... ukiamua kumjua Mungu na kumfuata fuata yote aelekezayo.....

Mnasema wanawake wanajaa makanisani Kutafuta Mungu awape awaume...JE HILI NI KOSA?...Huko kanisani wanatakiwa waende watakatifu?
 
Nikweli Mungu anatutaka tuwe wasafi... Lakini je usafi wa bikra ya mkeo Ni kwa Ajili yake..na Mungu wake..Wewe binafsi unaishije maisha yako je maisha yako yanampendeza Mungu......

Kujisifia kuwa Nimetomba Sana wanawake wasio bikra Ila nimeoa Bikra kutoka kwa Mungu..Tena nikafanya nae kabla kunihakikishia ndo nikao...hayo Maneno yanaongelewa na anae mjua Mungu...


Tuache unafiki wakujifanya tunamjua Mungu Sana..ilhali hata nusu hatufiki...

Sijaandika haya Kwa Kusema BIKRA NO MBAYA...HAPANA
 
Nikweli...kabisa lakini Usafi huu Kama Mungu atakavyo...Ni wa mwanamke pekeee?..
Hapana, usafi huu unapaswa kuwa kwa wote, mwanaume na mwanamke. Ni bahati mbaya hakuna namna ya kuthibitisha usafi wa mwanaume. Mwanamke akiwa msafi basi walau familia inakuwa safi angalau kwa asilimia 50.
 
42 Reactions
Reply
Back
Top Bottom