Maamuzi ya Spika, muovu hawezi kuwa na ujasiri wa kumwadhibu muovu mwingine

Leo habari iliyo juu ni uamuzi wa spika Tulia Ackson wa kuwaruhusu Halima na wenzake kuendelea kuwa wabunge licha ya kutokuwa wanachama wa chama chochote cha siasa, jambo ambalo ni kinyume na matakwa ya katiba yetu.

Spika Tulia anasema, hawezi kuwaondolea ubunge wabunge waliovuliwa uwanachama wa chama cha siasa kwa sababu wabunge waliovuliwa uwanachama wa CHADEMA, wamefungua kesi mahakamani kupinga kufutwa kwao uwanachama! Ni sababu ya kushangaza, ni sababu ya kipuuzi na kinafiki kwa sababu mfumo wa sheria haufanyi kazi namna hiyo.

Leo hii, hata ukifukuzwa kazi na muajiri wako kimakosa, huwezi kuendelea kuwa mfanyakazi eti kwa sababu tu umefungua kesi. Kama anayoyasema Tulia, ndiyo mifumo ya kesi ingekuwa inafanya kazi namna hiyo, basi mambo yangekuwa hovyo sana.

Siku zote, hukumu ya mwanzo huendelea kusimama mpaka siku kitakapopatikana chombo cha juu zaidi chenye mamlaka ya kisheria au kikatiba kuweza kutengua uamuzi wa awali.

Anachosema Tulia, ni dhihirisho la unafiki mkubwa uliopo nchini mwetu. Sheria hazina maana, bali zinapindishwa ili kutekeleza matakwa ya watu fulani.

Utawala wa awamu ya 5 haukutaka demokrasia, lakini baadaye baada ya kuona kuwa utakosa pesa ya Jumuia ya Madola, wakalazimisha, kwa kutengeneza upinzani bandia Bungeni.

Lakini tuwe wakweli, ndani ya Bunge hili bandia, nani ana ujasiru wa kumwadhibu mwingine? Karibia wabunge wote, pamoja na spika, waliopo huko Bungeni, ni zao la uovu mkubwa, uchafu, na takataka za kila aina zilizotendwa mwaka 2020 wakati wa utawala dhalimu wa kipindi cha giza.

Ubunge wa kupewa wa akina Halima una tofauti gani na ule wa kupewa wa Spika, na wengine wengi ambao wapo Bungeni? Hawa wabunge pamoja na huyu Spika, ambao wote walipachikwa na marehemu bila ya ridhaa ya wananchi, wana uhalali gani wa kuwaondoa akina Halima kwenye Bunge hili fake wakati nao wamefika hapo kwa namna ile ile ambayo akina Halima walifika?

Akina Halima walipelekwa pale na jiwe, huyo spika, naye kapelekwa pale na jiwe, ni nini kinachowafanya akina Halima wawe batili, halafu akina Katambi waliopata kura 3 kwenye kura za maoni dhidi ya Masele aliyepata kura 360 za wajumbe, lakini Jiwe likamviringisha mpaka kwenye unaibu Waziri?

Tufahamu tu kuwa akina Halima, ni waovu kama wenzao wengi waliojazana kwenye hilo jumba. Tunasubiria embe chini ya mchongoma.
Unaleta siasa sio sheria.
Sheria za kazi sio sawa na siasa. Kule kazini wanaangalia uwezekano muajiri kuathirika ikiwa muajiriwa atamhujumu..
Lakini wameweka fidia kubwa sana ikithibitika kuwa kulikuwa na makosa ktk kumfukuza pia wameweka fidia pesa aliyostahili kuwa amelipwa na atakayolipwa mpaka mwisho wa mkataba au kurudishwa kazini pia kuna fidia ya defamation ambayo kiwango chake ni kikubwa sana
Defamation kwa mwanasiasa hailipiki atakuambia mimi nilikuwa nataka niwe Raisi ningepata pension ya Urais wewe umeharibu carrier yangu nilipe fidia. Je chama kitaweza kuwalipa?
 
Kumbuka wale sio wabunge wa kupigiwa kura.

Wabunge wa kuteuliwa wanaenda pale kwa mapendekezo ya chama.

Sasa hawa chama kupitia vikao halali vimekataa kuwahi kupeleka majina.

Hatua zaidi ikachukuliwa kuwavua uanachama.

Utawala bora, bunge lingeandika barua kwa chama kupata uthibitisho.
Lakin kwa vile ni Chadema wanaona kama wanakikomo chama.

Kwa akili zao mbovu,mfumo mzima wa utawala bora unanajisiwa.

Unaleta siasa sio sheria.
Sheria za kazi sio sawa na siasa. Kule kazini wanaangalia uwezekano muajiri kuathirika ikiwa muajiriwa atamhujumu..
Lakini wameweka fidia kubwa sana ikithibitika kuwa kulikuwa na makosa ktk kumfukuza pia wameweka fidia pesa aliyostahili kuwa amelipwa na atakayolipwa mpaka mwisho wa mkataba au kurudishwa kazini pia kuna fidia ya defamation ambayo kiwango chake ni kikubwa sana
Defamation kwa mwanasiasa hailipiki atakuambia mimi nilikuwa nataka niwe Raisi ningepata pension ya Urais wewe umeharibu carrier yangu nilipe fidia. Je chama kitaweza kuwalipa?
 
Mpaka Sasa kinachoendelea Ni uvunjaji wa katiba na Sheria, tangu lini ukihukumiwa kwenda jela, ukakata rufaa unatolewa bila hukumu kusikilizwa? Hili bunge limepoteza dira Bora livunjwe tu
 
Mkuu chukua kadi ya ccm kama huna, una akili sana kama wao
Mkuu ni kweli mimi kadi ya kijani sina,nilikuwa CDM asilimia mia moja,tangu kamanda Mbowe alipotoa ushauri kwa mh.Rais watu wote walazimishwe kuchanjwa chanjo ya corona nikaona kumbe 'Nyani ni wale wale,nimebadilishiwa msitu''

Kiukweli mpaka hapo mimi nailaum CDM kwa walichokifanya kwa akina Mdee,kwa sasa bunge lipo live
tunakosa hoja mahususi za wamama hawa machachali kwa sababu mtu yeyote mwenye akili timamu huwezi kupigana
vita pande mbili,utapigwa.Wameamua kujikalia kimya mpaka wanaowaita COVID 19 wanyamaze kwanza ndo waendelee na kupambana na kijani.
 
Mpaka Sasa kinachoendelea Ni uvunjaji wa katiba na Sheria, tangu lini ukihukumiwa kwenda jela, ukakata rufaa unatolewa bila hukumu kusikilizwa? Hili bunge limepoteza dira Bora livunjwe tu
Mkuu unamaanisha,mtu akikupeleka polisi ukawekwa ndani afu jamaa zako wakaja kukuwekea mdhamana
ukitolewa ndani huruhusiwi kurudi nyumbani kwako ( Yaani uraiani ulipokuwa mwanzoni)?
Kama jibu ni unaruhusiwa, hali kadhalika wabunge hawa,Chadema iliwatuhumu kupata ubunge kwa njia isiyo halali,na kwa bahati mbaya imechukua sheria mkononi.
Jambo ambalo ni kinyiume cha sheria,

Kwa Vipi? Hawa wanawake wanadai walienda bungeni kwa baraka zote za CDM,
Na CDM inasema haijawapa baraka bali walifoji nyaraka
Kufoji nyaraka ni kosa la jinai,CDM ilitakiwa kuwafungulia mashitaka ili mahakama iwahukumu kwa koosa la kufoji.
kitendo cha wao kufanya kazi ya mahakama kuwahukumu na kuwapa adhabu ya kuwavua ubunge ni kinyume cha sheria.

Kuna hoja ya wingi wa kula za wajumbe waliopiga kura ili wavuliwe uanachama,
Binafsi mimi naona hiyo siyo hoja,maana uhalifu ni uhalifu bila kujali waliotenda uhalifu ni wengi kiasi gani.
Mfano mzuri ni wale wanaoua na kuchoma vibaka,bila kujali wingi wao,wakikamatwa
wanakutwa na kosa la kuchukua sheria mikononi mwao.

Na katika hili Wajumbe wa CDM wamejichukulia sheria mikononi bila kufikisha kesi mahakamani.
 
Leo habari iliyo juu ni uamuzi wa spika Tulia Ackson wa kuwaruhusu Halima na wenzake kuendelea kuwa wabunge licha ya kutokuwa wanachama wa chama chochote cha siasa, jambo ambalo ni kinyume na matakwa ya katiba yetu.

Spika Tulia anasema, hawezi kuwaondolea ubunge wabunge waliovuliwa uwanachama wa chama cha siasa kwa sababu wabunge waliovuliwa uwanachama wa CHADEMA, wamefungua kesi mahakamani kupinga kufutwa kwao uwanachama! Ni sababu ya kushangaza, ni sababu ya kipuuzi na kinafiki kwa sababu mfumo wa sheria haufanyi kazi namna hiyo.

Leo hii, hata ukifukuzwa kazi na muajiri wako kimakosa, huwezi kuendelea kuwa mfanyakazi eti kwa sababu tu umefungua kesi. Kama anayoyasema Tulia, ndiyo mifumo ya kesi ingekuwa inafanya kazi namna hiyo, basi mambo yangekuwa hovyo sana.

Siku zote, hukumu ya mwanzo huendelea kusimama mpaka siku kitakapopatikana chombo cha juu zaidi chenye mamlaka ya kisheria au kikatiba kuweza kutengua uamuzi wa awali.

Anachosema Tulia, ni dhihirisho la unafiki mkubwa uliopo nchini mwetu. Sheria hazina maana, bali zinapindishwa ili kutekeleza matakwa ya watu fulani.

Utawala wa awamu ya 5 haukutaka demokrasia, lakini baadaye baada ya kuona kuwa utakosa pesa ya Jumuia ya Madola, wakalazimisha, kwa kutengeneza upinzani bandia Bungeni.

Lakini tuwe wakweli, ndani ya Bunge hili bandia, nani ana ujasiru wa kumwadhibu mwingine? Karibia wabunge wote, pamoja na spika, waliopo huko Bungeni, ni zao la uovu mkubwa, uchafu, na takataka za kila aina zilizotendwa mwaka 2020 wakati wa utawala dhalimu wa kipindi cha giza.

Ubunge wa kupewa wa akina Halima una tofauti gani na ule wa kupewa wa Spika, na wengine wengi ambao wapo Bungeni? Hawa wabunge pamoja na huyu Spika, ambao wote walipachikwa na marehemu bila ya ridhaa ya wananchi, wana uhalali gani wa kuwaondoa akina Halima kwenye Bunge hili fake wakati nao wamefika hapo kwa namna ile ile ambayo akina Halima walifika?

Akina Halima walipelekwa pale na jiwe, huyo spika, naye kapelekwa pale na jiwe, ni nini kinachowafanya akina Halima wawe batili, halafu akina Katambi waliopata kura 3 kwenye kura za maoni dhidi ya Masele aliyepata kura 360 za wajumbe, lakini Jiwe likamviringisha mpaka kwenye unaibu Waziri?

Tufahamu tu kuwa akina Halima, ni waovu kama wenzao wengi waliojazana kwenye hilo jumba. Tunasubiria embe chini ya mchongoma.
Huu ndiyo ukweli
 
Kumbuka wale sio wabunge wa kupigiwa kura.

Wabunge wa kuteuliwa wanaenda pale kwa mapendekezo ya chama.

Sasa hawa chama kupitia vikao halali vimekataa kuwahi kupeleka majina.

Hatua zaidi ikachukuliwa kuwavua uanachama.

Utawala bora, bunge lingeandika barua kwa chama kupata uthibitisho.
Lakin kwa vile ni Chadema wanaona kama wanakikomo chama.

Kwa akili zao mbovu,mfumo mzima wa utawala bora unanajisiwa.
Mkuu unachanganya mambo.
1. Kama chama kinakataa kupeleka majina hii ni kesi nyingine. Kwanza uelewe Spika au Bunge halihusiki na kesi ya hivi. Kwa sababu Spika anapelekewa jina tu anaambiwa fulani ni Mbunge wa Bunge lako muapishe awe Mbunge(NI AMRI KIKATIBA).. na hana mamlaka ya kuhoji uhalali wake.... japokuwa Mtu mwingine yeyote anaweza kuhoji KWA KUFUNGUA KESI MAHAKAMANI kama vile tu kesi zinazofunguliwa kupinga ushindi wa mbunge fulani aliyetangazwa na NEC.
Hivyo, Kesi hii kimsingi ni kesi ya Tume ya Uchaguzi NEC, kwani tume ndio iliwateua na kumuagiza Spika awapokee kama Wabunge. Swali hapa ni;
Kama tume iliwateua wabunge ambao hawajapendekezwa na chama walipata wapi majina?
Kwa nini CDM hawajaishtaki Tume kwa kuteua Wabunge ambao haijawapendekeza?
Au kuitaka NEC ieleze imepata wapi hayo majina.? (Natambua CDM iliwahi kuomba nyaraka kwa tume lakini ilikaa kisiasa zaidi walipaswa kwenda mahakamni na mahakama ndio iagize tume walete nyaraka husika).
Kwa suala hili CDM walimchafua na kumsingizia sana Spika Ndugai. Kwangu mimi niliona kama ulaghai wa kisiasa uliokuwa unafanywa na Chama.


2. Kufukuzwa COVID 19.
Kwamba Chadema imeacha kushughulika na NEC na imeamua kuwaadhibu walioteuliwa.. sawa;
Hapa pekee kuna walakini..
Jee Covid19 walijiteua?
Nani alipeleka majina yao NEC?
Kama kuna afisa alipeleka majina NEC ni nani?
Ofisa huyo alikuwa na mamlaka hayo kwa mujibu wa Chama?
Ni nani huyo na amechukuliwa hatua gani?
Au Walifoji nyaraka?
Kama walifoji nyaraka kwa nini wasipelekwe mahakamani kwa kufoji wafungwe na Ubunge wao UFE automatically?
Wakifungwa wanapoteza nyadhifa zote chamani na ubunge bila kusumvuka na uanachama wao.

Sijui kama vikao vya kamati kuu na Baraza kuu waliangalia haya. Wameamua kuchukua shortcut kuwafukuza. Sasa covid 19 wameenda mahakamani kuulizia uhalali wa kufukuzwa kwao. Hii ni fursa kwetu tusiojua ukweli kujua kinachoendelea
Ni tume waliwaingiza kibabe
Ni kina Mdee walifoji na kuwadanganya tume na kuwasaliti Chadema?
Kuna kiongozi aliwasaidia ndani ya Chadema na wanatuchezea shere!! na hatimae tujue walifukuzwa kihalali?
Je ubunge wao ni halali au sio halali?

Kama hakuna faulo ndani ya Chama basi chadema walipaswa kufurahia sana hawa kina Mdee kwenda mahakamani kwani kufanya hivyo ni kuweka ukweli Hadharani.. Kuiumbua tume na serikali kwa ujumla na kuonyesha usaliti wa kina Mdee.
 
. Kama anayoyasema Tulia, ndiyo mifumo ya kesi ingekuwa inafanya kazi namna hiyo, basi mambo yangekuwa hovyo sana.
Inashangaza kweli, kipindi Lema kavuliwa ubunge na kwenda mahakamani, alibakia nje ya Bunge mpaka kesi ilipomalizika.

Wabunge wa CUF walipovuliwa ubunge wote waliondolewa bungeni japo walikuwa wamekwenda mahakamani kupinga hilo.

Sheria za hii nchi ni kwa ajili ya watu fulani tu.
 
Hizo double standards zinazofanywa na Bunge letu ni za nini?

Hivi wale wabunge wa viti maalum wa CUF, si mliwafukuza ubunge, mara tu Mwenyekiti wenu, Profesa Lipumba alipowapa taarifa kuwa keshawavua uanachama wao?

Hivi kwa nini, huyu Spika Tulia, tunayeaminishwa kuwa ana PhD ya sheria, aamue kuisigina waziwazi Katiba ya nchi, ambayo ndiyo supreme ya sheria zote za nchi hii?🥺
Mkuu mystery, nafikiri lile la wabunge 8 wa CUF lilikuwa kosa kubwa sana, alilofanya spika Ndugai. Nafikiri kosa lile halipaswi kuwa msingi wa maamuzi ya hawa 19 wa
CHADEMA! Kwa sababu tunapenda haki, tukubali kwamba hawa waruke ruke kote, mwisho watatulia kama maarage ya Mbeya!
Sitetei maamuzi ya spika, lakini nafikiri uamuzi kama huu ndo ulipaswa kufanywa hata wakati wa wabunge 8 wa CUF! Sisi CHADEMA tusikubali njia ya mkato, mchakato wote ufanyike, watoke kihalali!
 
unafukuzwa kazi leo,unaiambia hazina usinitoe kwenye payroll nitakata rufaa kesho. Daaa!I dont neee sex my government fu#$$cks me everyday
 
Mkuu ni kweli mimi kadi ya kijani sina,nilikuwa CDM asilimia mia moja,tangu kamanda Mbowe alipotoa ushauri kwa mh.Rais watu wote walazimishwe kuchanjwa chanjo ya corona nikaona kumbe 'Nyani ni wale wale,nimebadilishiwa msitu''

Kiukweli mpaka hapo mimi nailaum CDM kwa walichokifanya kwa akina Mdee,kwa sasa bunge lipo live
tunakosa hoja mahususi za wamama hawa machachali kwa sababu mtu yeyote mwenye akili timamu huwezi kupigana
vita pande mbili,utapigwa.Wameamua kujikalia kimya mpaka wanaowaita COVID 19 wanyamaze kwanza ndo waendelee na kupambana na kijani.
Basi mkuu hamia huko, mimi nakutakia kila la heri
 
Back
Top Bottom