Maamuzi ya Kamati Kuu CHADEMA Yana walakini, tutafakari tena.

Daniel Anderson

JF-Expert Member
Aug 7, 2011
872
141
Ndugu zangu, watanzania wenzangu,

Kwa takriban mwezi sasa unapita huku wingu la kisiasa hapa nchini likiwa limegubikwa na mijadala kuhusu siasa za chama kikuu cha upinzani (CHADEMA). Ilianza mivutano kuhusu maamuzi ya mwenyekiti wa PAC ndugu Zitto kuwataka makatibu wakuu wa vyama kujieleza ni kwa nini hawajawasilisha ukaguzi wa vyama vyao kwa mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali kwa ukaguzi kama sheria yetu inavyotaka.

Miongoni mwa waathirika wa maamuzi haya kilikuwa ni chama chake mwenyewe cha CHADEMA na hivyo kufanya matamko mengi juu ya uamuzi huu, tena chama chake kikitoa matamko karibu kila siku kumpinga mwanachama wao huyu.

Zikaanza kuibuka shutuma na vioja vingi vya ajabu kabisa katika historia ya siasa zetu hapa nchini, ambapo hadharani kabisa, Mbunge Godbless Lema alijitokeza kuwasha moto wa migogoro kwa kuupinga msimamo wa chama kuhusu posho. Akahalalisha kile wanachadema tulichokiona ni haramu tangu baada ya uchaguzi mkuu wa 2010 (posho za kukaa kwa wabunge) kwa kumwita Zitto ni mnafiki na anayeudanganya umma wa watanzania. Hapa hatukujiuliza ni nani mnafiki kati ya Zito aliye walk the talk au aliyegoma na kupokea kimyakimya?

Kwa nini Lema ametumia nguvu kubwa kwa Zitto badala ya kuhoji maamuzi ya KUB kurejesha gari alilikataa mwanzo, tena kimya kimya bila kutoa sababu zenye mashiko za kumfanya afanye hivyo? Kwani kwa kufanya vile KUB alijitofautisha vipi na hawa CCM tunao waparua kila siku kuwa ni wanafiki? Anyway, sijadili suala la KUB, ila mazingira na maamuzi ya CC juu ya Zitto & Co.

Ni kweli Zitto ni msaliti? Mbona kwenye kamati kuu alijibu hoja zote mlizozitoa juu yake na hakuna kosa lililoonekana juu yake? Kama ni walaka ambao amekiri haujui kabisa, ambao ni kweli unamtaja kwamba atahusishwa (bt hakuhusishwa up to the point) kwa nini ahukumiwe kwa kuonekana tu kuwa unamlenga japo hajashiriki? Hebu tuambieni tena na tena ili tuwaelewe lakini vinginevyo, tunavunjika sana moyo sisi wanachama.

Elezeni Zitto has amefanya nini. Ile ripoti ya siri si mliikataa wenyewe? Si mlisema hamuhusiani nayo? Kwa kweli ingekuwa ni ile ripoti basi hata mimi ningeunga mkono na wala si hii ya pili ambayo haina uhalisia hata kidogo.

Kamati kuu hebu tuambieni, mbona mnajichanganya kuhusu hata huu waraka wenyewe? Si mlisema ndo huu mliouweka mtandaoni? Mbona bada ya mijadala na kuonekana hauna tatizo mgkageuka na kusema upo mwingine? Mbona hata Mwigamba kakiri kuwa huu ndio wenyewe? Au mnafikiri hatuwezi kuhoji maamuzi ya kamati kuu?

Kwa nini mgogoro na Zitto uwe sasa na si wakati mwingine? Kwa nini tunapoelekea uchaguzi na si kabla? Kwa nini ripoti ya siri ambayo, kwangu ningeipa nafasi zaidi katika maamuzi, iwe leo tunapoelekea uchaguzi? Kwa nini tunaweka mazingira ya Mbowe kutawala daima? Mbona hata shutuma dhidi yake tunazipuuza? Kwa nini hatukuamua vinginevyo dhidi yake kwa kashfa ya kukiuzia chama magari mabovu? Kwa nini tuli'mute' alipobainika kuwa na jumba la kifahari Dubai?

Mbona hatujahoji iweje naye kwake jimboni upinzani hauna nguvu hata ukilinganisha na iringa mjini? Kwa nini chama kinaenda kwa matukio na si agenda ya chama? Kwa nini amekuwa akiongoza chama kwa mfumo wa matamko na kulaani?

Ukweli ni kuwa tunahitaji mabadiliko ndani ya chama tena mapema iwezekanavyo. Umepita ule wakati wa kwenda na fikra na matamaanio ya mwenyekiti badala ya mahitaji ya chama. Chama ni cha watanzania wote si Mbowe pekee ndiye mwenye hati miliki ya kuwa mwenyekiti daima.

Tunahitaji msukumo mpya wa kutuwezesha kujiimarisha vijijini zaidi. Hizi porojo tulizonazo za nyuma ya keyboard zinatudanganya. Tembelea Matombo hadi Kisaki uone kazi ilivyo kubwa. Nenda Engusero hadi Pori kwa pori uone watu walivyo na kiu ya mabadiliko. Nenda Matwiga, Mafyeko, Lupa, Makongorosi na Chunya kwa ujumla uone haja kubwa ya mabadiliko ilivyokubwa miongoni mwa watanzania wa kule.

Siyo sifa kufukuzana kila kukicha tena kwa apparent reasons kama zinazotolewa na uongozo sasa. Nasema hivi, hata kama mkiamua kumfukuza Zitto, mjue wapo wengine watakaokuja kuwa na misimamo thabiti ya kuenenda kwa kadiri ya maneno yao kama Zitto alivyo. Mtawaita wasaliti kwa kuwa na msimamo sahihi wa kuyapeleka mambo ndani ya chama, lakini chama ni cha wanachama wote.

Nawapa challenge tu, itisheni leo baraza kuu muone kama hakutakuwa na ngumi kwa sababu ya maamuzi yenu haya.
 
Very illogical arguments. Mistari miiingi tena ya kurudia rudia

wewe unataka kurudisha watu walikokwisha long time, tayari maamuzi yashafanyika kwa taratibu za chama kadiri ya sheria na kanuni inayosimamiwa na katiba yao.

wewe unayetaka kutuambia kwambwa ni kwa sababu ya sijui mahesabu ya chama bla bla, wao chadema hawakutoa hizo kama ndio sababu za kufikia maamuzi yao.

endelea kuota ndugu lakini kwa faida yako tu, acha kujadili personality, individuals, jikite kwenye misingi ya masuala.

someone said humu humu JF 'uhuru ulio na woga ni utumwa, lakini pia uhuru usio na nidhamu ni uwendawazimu, sijui original source but chadema wamesimamia hilo neno hapo juu

jumapili njema
 
Umeshaambiwa kuna chadema family na Halisi ,cdm halisi ni ZZK tafakari!!
 
Yap, nimekubali uchambuz wako, kuna mambo mengi yana msukumo wa nafas ya uenyekiti na ugombea urais 2015.

Next time yale mambo muhimu yawekee alama kidogo, kama namba hiv na short summary. mana watu wengi humu siku hiz hawasomi uchambuz mrefu..
 
Straight to the point, asante sana ndugu kwa kuhoji maswali ya msingi. japo Mbowe yupo tayari kutumia mbinu zote ili aendelee kuwa Mwenyekiti bahati mbaya anakiua Chama.
Hiki ni kizazi chenye kuhoji, huwezi kujinadi kuiondoa CCM iliyokosa dira, wakati wewe binafsi unafanya mambo ya hovyohovyo kabisa.
Itamfaa nini Mbowe kuongoza chama kilichogawanyika?, ni nini ufahari wa kubomoa kazi yako Mwenyewe?

Injustice anywhere is an injustice everywhere. Ni lazima wananchi wote wanachama wa vyama, na wasio wanachama tupinge udhalimu huu, CHAMA KISICHOWATENDEA HAKI WANACHAMA WAKE HAKINA HAKI YA KUEXIST.

Mbowe, Unaogopa nini?, Huwezi kushinda uenyekiti kwa hoja?. Je sikio likikuuma dawa yake ni kulikata?, Jicho likikuuma dawa yake ni Kuling'oa?. UMEMUONEA MH ZITTO , NA WEWE DHAMIRA YAKO INAJUA, NA HUTAKUWA MWENYE AMANI MOYONI MPAKA UMTENDEE HAKI MH ZITTO NA WANACHAMA WENGINE. JITAFAKARI NDUGU
 
Very illogical arguments. Mistari miiingi tena ya kurudia rudia

wewe unataka kurudisha watu walikokwisha long time, tayari maamuzi yashafanyika kwa taratibu za chama kadiri ya sheria na kanuni inayosimamiwa na katiba yao.

wewe unayetaka kutuambia kwambwa ni kwa sababu ya sijui mahesabu ya chama bla bla, wao chadema hawakutoa hizo kama ndio sababu za kufikia maamuzi yao.

endelea kuota ndugu lakini kwa faida yako tu, acha kujadili personality, individuals, jikite kwenye misingi ya masuala.

someone said humu humu JF 'uhuru ulio na woga ni utumwa, lakini pia uhuru usio na nidhamu ni uwendawazimu, sijui original source but chadema wamesimamia hilo neno hapo juu

jumapili njema
Mkuu hebu tuweke hisia pembeni na tujikite kwenye uhalisia. Nimesema kuwa ule waraka hauna justification ya kufikia maamuzi yale, zaidi ni woga wa uchaguzi ndania ya chama tu. Mwenyekiti hataki kupingwa, na sisi kama wanachama hatutaki demokrasia ya kichina. tunataka ushindani sahihi utakaoweka nafasi kwa kila mtu kugombea nafasi ndania ya chama, provided ana meet vigezo vilivyowekwa, si kuteuana ambako mwenyekiti anataka. Hakuna sababu ya kumvua Zitto nafasi zake, kama zipo ziseme usiishie kusema ni bla bla.
 
nashauri zzk aachane na cdm na kuanzisha chama kipya
Hapana, kufanya hivyo ni kuendelea kuimarisha misingi ya CCM na kufanya kazi ya kuwatoa iwe ngumu zaidi. Hakuna sababu ya yeye kutoka ila abaki ndani ya chama na kamati kuu iangalie upya maamuzi yake.
 
Straight to the point, asante sana ndugu kwa kuhoji maswali ya msingi. japo Mbowe yupo tayari kutumia mbinu zote ili aendelee kuwa Mwenyekiti bahati mbaya anakiua Chama.
Hiki ni kizazi chenye kuhoji, huwezi kujinadi kuiondoa CCM iliyokosa dira, wakati wewe binafsi unafanya mambo ya hovyohovyo kabisa.
Itamfaa nini Mbowe kuongoza chama kilichogawanyika?, ni nini ufahari wa kubomoa kazi yako Mwenyewe?

Injustice anywhere is an injustice everywhere. Ni lazima wananchi wote wanachama wa vyama, na wasio wanachama tupinge udhalimu huu, CHAMA KISICHOWATENDEA HAKI WANACHAMA WAKE HAKINA HAKI YA KUEXIST.

Mbowe, Unaogopa nini?, Huwezi kushinda uenyekiti kwa hoja?. Je sikio likikuuma dawa yake ni kulikata?, Jicho likikuuma dawa yake ni Kuling'oa?. UMEMUONEA MH ZITTO , NA WEWE DHAMIRA YAKO INAJUA, NA HUTAKUWA MWENYE AMANI MOYONI MPAKA UMTENDEE HAKI MH ZITTO NA WANACHAMA WENGINE. JITAFAKARI NDUGU
Hapo umenena mkuu. Huu ni ukweli utakaokinusuru chama, vinginevyo hali ni mbaya kuliko projections zao
 
Umeshaambiwa kuna chadema family na Halisi ,cdm halisi ni ZZK tafakari!!
Hakuna hizo chadema unazozisema, ipo moja tu ila ni wakati wa kuijenga na tuziache politics za ajabu ajabu zinazofanywa na uongozi. Sitarajii kuwa mikutano ya Dr. Slaa itapokewa kwa nguvu tulizozoea. tunakoenda hata Kinena atakuwa na watu kwenye mikutano yake ikilinganishwa na Dr. Slaa
 
hakuna hizo chadema unazozisema, ipo moja tu ila ni wakati wa kuijenga na tuziache politics za ajabu ajabu zinazofanywa na uongozi. Sitarajii kuwa mikutano ya dr. Slaa itapokewa kwa nguvu tulizozoea. Tunakoenda hata kinena atakuwa na watu kwenye mikutano yake ikilinganishwa na dr. Slaa

mkuu una mtazamo makini ubarikiwe,lakini angalia wasije wakakumwagia tindikali
 
Back
Top Bottom