Maamuzi ya Bunge kuwafungia wabunge kuhudhuria vikao ni ukiukwaji wa KATIBA

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,422
911,172
Haki ya wabunge kuhudhuria vikao na kuwawakilisha wananchi wa majimbo yao ni ya kikatiba na kanuni feki za Bunge zinazolipa Bunge mamlaka ya kuwasimamisha wabunge kutekeleza majukumu yao ya kikatiba zinakiuka katiba ambayo wabunge hawa waliapa kuilinda na kuitetea Katiba husika!

Bunge halipo juu ya katiba na ndiyo maana wabunge wote huapa kabla ya kuanza shughuli za Bunge ya kuwa wataitii katiba ambayo hakuna mahali ndani ya katiba hiyo wamepewa mamlaka ya kuwasimamisha wabunge na kuwapora wananchi wanaowawakilisha haki yao ya kikatiba ya uwakilishi.

Tusipokuwa waangalifu itafikia wakati Bunge linamsimamisha Mbunge kwa miaka mitano na kuwapora wananchi wa jimbo husika haki yao ya kikatiba ya kuwakilishwa kwa kipindi chote cha uwakilishi.

Adhabu za kikanuni za Bunge hazina mamlaka ya kupora wananchi haki zao za kikatiba kama kuwakilishwa.

Kama Mbunge kavunja kanuni Bunge linaweza kumpa faini ili aathirike Mbunge mwenyewe bila kuathiri haki ya kuwakilishwa ya wananchi wa jimbo lake.


Spika Job Ndugai kuwaadhibu askari walioheshimu haki za binadamu pia linatia aibu si kwake tu bali kwa Bunge zima na taifa kwa ujumla.


images.jpg
images%281%29.jpg
images%282%29.jpg
 
Haki ya wabunge kuhudhuria vikao na kuwawakilisha wananchi wa majimbo yao ni ya kikatiba na kanuni feki za Bunge zinazolipa Bunge mamlaka ya kuwasimamisha wabunge kutekeleza majukumu yao ya kikatiba ni kuikiuka katiba walioapa kuilinda na kuitetea!

Bunge halipo juu ya katiba na ndiyo maana huapa kabla ya kuanza shughuli za Bunge ya kuwa wataitii katiba ambayo hakuna mahali ndani ya katiba hiyo wamepewa mamlaka ya kuwasimamisha wabunge na kuwapora wananchi wanaowawakilisha haki yao ya kikatiba ya uwakilishi.

Tusipokuwa waangalifu itafikia wakati Bunge linamsimamisha Mbunge kwa miaka mitano na kuwapora wananchi wa jimbo husika haki yao ya kikatiba ya kuwakilishwa.

Kama Mbunge kavunja kanuni Bunge linaweza kumpa faini ili aathirike Mbunge mwenyewe bila kuathiri haki ya kuwakilishwa ya wananchi wa jimbo lake.


Spika Job Ndugai kuwaadhibu askari walioheshimu haki za binadamu pia linatia aibu si kwake tu bali kwa Bunge zima na taifa kwa ujumla.


View attachment 520010View attachment 520011View attachment 520012

Nikiangalia kwa umakini kabisa vurugu yote ya ijumaa ilipangwa kwenye vikao vya CCM ili ile bajeti ipite.!Tatizo wapinzani walidhani CCM wako pamoja nao kwenye issue za raslimali za Taifa kumbe hakuna kitu.

Inatia shaka na hasira pale wabunge 300 wa CCM wanaposhabikia mchanga aka Makinikia na kuacha minara ya dhahabu inayoporwa na hao akina Kalemani.

Ninawashangaa wanachama wa CCM wanaoona lakini wanajifanya hawaoni.Ninawashangaa wasomi wanaoambiwa ati wanaPhD kuacha huu uovu wa Ndugai ukawa kigezo cha kuzika issue nzima ya madini na mikataba mibovu halafu tunaambiwa ti Rais ana nia njema na madini,sijui lakini siyo kwa style hii
 
Haki ya wabunge kuhudhuria vikao na kuwawakilisha wananchi wa majimbo yao ni ya kikatiba na kanuni feki za Bunge zinazolipa Bunge mamlaka ya kuwasimamisha wabunge kutekeleza majukumu yao ya kikatiba zinakiuka katiba wabunge hawa waliapa kuilinda na kuitetea Katiba husika!

Bunge halipo juu ya katiba na ndiyo maana huapa kabla ya kuanza shughuli za Bunge ya kuwa wataitii katiba ambayo hakuna mahali ndani ya katiba hiyo wamepewa mamlaka ya kuwasimamisha wabunge na kuwapora wananchi wanaowawakilisha haki yao ya kikatiba ya uwakilishi.

Tusipokuwa waangalifu itafikia wakati Bunge linamsimamisha Mbunge kwa miaka mitano na kuwapora wananchi wa jimbo husika haki yao ya kikatiba ya kuwakilishwa.

Kama Mbunge kavunja kanuni Bunge linaweza kumpa faini ili aathirike Mbunge mwenyewe bila kuathiri haki ya kuwakilishwa ya wananchi wa jimbo lake.


Spika Job Ndugai kuwaadhibu askari walioheshimu haki za binadamu pia linatia aibu si kwake tu bali kwa Bunge zima na taifa kwa ujumla.


View attachment 520010View attachment 520011View attachment 520012
Una hoja but you have a missed a point kwa kutoa conclusion.

Hoja yako umeinyima haki ya kudadavuliwa na wajuvi wa sheria na katiba kwa hoja yoyote inayokinzana na conclusion yako inaweza kuzua malumbano yasiyokuwa na tija.

BTW una nafasi ya kuirekebisha kwa kufanya editing ambayo itaifanya iwe hoja chokonozi badala ya hoja inayohukumu.
 
Nikiangalia kwa umakini kabisa vurugu yote ya ijumaa ilipangwa kwenye vikao vya CCM ili ile bajeti ipite.!Tatizo wapinzani walidhani CCM wako pamoja nao kwenye issue za raslimali za Taifa kumbe hakuna kitu.

Inatia shaka na hasira pale wabunge 300 wa CCM wanaposhabikia mchanga aka Makinikia na kuacha minara ya dhahabu inayoporwa na hao akina Kalemani.

Ninawashangaa wanachama wa CCM wanaoona lakini wanajifanya hawaoni.Ninawashangaa wasomi wanaoambiwa ati wanaPhD kuacha huu uovu wa Ndugai ukawa kigezo cha kuzika issue nzima ya madini na mikataba mibovu halafu tunaambiwa ti Rais ana nia njema na madini,sijui lakini siyo kwa style hii
Anayekemea mapungufu ya sheria na mikataba ni mzalendo siyo mtetezi wa wezi kama wabunge wa CCM wanavyodai.

Pili, kumtafuta mchawi kwa kuunda kamati feki kama ile ya Prof. Mruma ni kukiuka mikataba ambayo imeweka kifungu cha msuluhishi kwa minajili ya kutatua migogoro.

Anayetetea ukiukwaji tajwa yeye ndiye mtetezi wa wezi wa mali za umma.
 
Una hoja but you have a missed a point kwa kutoa conclusion.

Hoja yako umeinyima haki ya kudadavuliwa na wajuvi wa sheria na katiba kwa hoja yoyote inayokinzana na conclusion yako inaweza kuzua malumbano yasiyokuwa na tija.

BTW una nafasi ya kuirekebisha kwa kufanya editing ambayo itaifanya iwe hoja chokonozi badala ya hoja inayohukumu.
Bila kuhitimisha nitakuwa sijajitendea haki na wala wewe sijakutendea haki.

Lengo langu siyo kuamsha udadisi au kuchokoza mada bali kuonyesha mapungufu ya kanuni za Bunge kwenye eneo husika
 
Bunge halina mamlaka ya kuwapora wananchi wa majimbo husika haki yao ya kikatiba ya kuwakilishwa.

Mvuta bangi aadhibiwe yeye binafsi bila kuathiri haki za wapigakura za kuwakilishwa
kanye urudi kitandani ulale mambo ya sheria na katiba yaache hujui kitu.
 
Kwa hili Raisi wa TLS Mhe. Lissu chama chenu kisipoonyesha njia basi acheni zile mbembwe zingine baada ya hapa.
Hatutetei maovu lakini haki kwa wote ionekane imetendeka. Yaliyowakuwa Mnyika,Mdee na Bulaya ni defense yao ndiyo imegeuzwa kuwa Kosa.
Pili haki ya wapiga kura kuporwa haiko sawa Kikatiba. Kanuni ya Bunge iko kinyume na Katiba ya Nchi .

Adhabu kama kuwanyima Posho na marupurupu mengine ndiyo sahihi na si kuwakilisha waliowapeleka Bungeni.
 
Anayekemea mapungufu ya sheria na mikataba ni mzalendo siyo mtetezi wa wezi kama wabunge wa CCM wanavyodai.

Pili, kumtafuta mchawi kwa kuunda kamati feki kama ile ya Prof. Mruma ni kukiuka mikataba ambayo imeweka kifungu cha msuluhishi kwa minajili ya kutatua migogoro.

Anayetetea ukiukwaji tajwa yeye ndiye mtetezi wa wezi wa mali za umma.

Issue kubwa hapo ni kwamba CCM inajaribu kumficha KAlemani kwenye MAOVU ya mikataba na miswada mibovu kwa maana ndiyo sababu ya kuwepo kwake.

Kama kweli CCM wangekuwa wazalendo wasingepigia makelele makombo wakati wageni wanachukua chakula chote,halafu tunakuwa kama mazuzu kupigia makofi RAIS anayetaka tujadili makombo ya madini.Aibu kwa TAIFA masikini kama letu kupigia makofi ati RAIS ana uchungu sana kuona tunanyimwa asilimia kubw akwenye makombo ya chakula.Upumbavu wa hali ya juu kabisa wa hili bunge letu
 
Tuwekee kipengele mahsusi cha katiba kilichovunjwa

Nenda ukapigie makofi Makombo kule bungeni.Badala ya kuhoji haki za msingi za madini yetu MINARA/MICHE ya dhahabu uanpiga kelele kwenye makombo aibu jingalao,toka huko hatuhitaji makombo watanzania,madini mali yetu tunatakiwa tupigie kelele MICHE ya dhahabu.
 
Haki ya wabunge kuhudhuria vikao na kuwawakilisha wananchi wa majimbo yao ni ya kikatiba na kanuni feki za Bunge zinazolipa Bunge mamlaka ya kuwasimamisha wabunge kutekeleza majukumu yao ya kikatiba zinakiuka katiba ambayo wabunge hawa waliapa kuilinda na kuitetea Katiba husika!

Bunge halipo juu ya katiba na ndiyo maana wabunge wote huapa kabla ya kuanza shughuli za Bunge ya kuwa wataitii katiba ambayo hakuna mahali ndani ya katiba hiyo wamepewa mamlaka ya kuwasimamisha wabunge na kuwapora wananchi wanaowawakilisha haki yao ya kikatiba ya uwakilishi.

Tusipokuwa waangalifu itafikia wakati Bunge linamsimamisha Mbunge kwa miaka mitano na kuwapora wananchi wa jimbo husika haki yao ya kikatiba ya kuwakilishwa kwa kipindi chote cha uwakilishi.

Adhabu za kikanuni za Bunge hazina mamlaka ya kupora wananchi haki zao za kikatiba kama kuwakilishwa.

Kama Mbunge kavunja kanuni Bunge linaweza kumpa faini ili aathirike Mbunge mwenyewe bila kuathiri haki ya kuwakilishwa ya wananchi wa jimbo lake.


Spika Job Ndugai kuwaadhibu askari walioheshimu haki za binadamu pia linatia aibu si kwake tu bali kwa Bunge zima na taifa kwa ujumla.


View attachment 520010View attachment 520011View attachment 520012



Kuwafungia wabunge watumiaji madawa ya kulevya si kosa, sema tu aliwaonea huruma maana ilibidi awahukumu wanyongwe ili kuwa fundisho kwa wabunge wengine. Madawa ya kulevya si peremende.
 
Bahati nzuri katiba inatambua kwamba kuna kanuni na sheria nyingine ndio maana huwa inasema "BILA KUATHIRI KANUNI NA SHERIA ZINGINE ZA NCHI" Kwa maana hiyo hakuna katiba iliyokiukwa.
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom