Maamuzi ya Bunge kuwafungia wabunge kuhudhuria vikao ni ukiukwaji wa KATIBA

Wajibu wa kujenga nidhamu bungeni ni wa wote; Kiti na wabunge. Kama uko huru kifikra ni rahisi kuona kwamba siku ya tukio Kiti chenyewe kiliandaa mazingira ya kutokea kwa kilichotokea. Kwa kadri ya mambo yalivyokuwa Kiti ambacho kinajua wajibu wake kisingeenda kujificha kwenye Kanuni bali kingemsikiliza Mnyika na kuahidi kufuatilia ili kujua ni nani aliyemtolea tusi la kwamba yeye ni "mwizi", basi. Na mambo yangeendelea kama kawaida! Nadhani Prof. Shivji aliposema Bunge halipaswi kuendeshwa kama darasa la wanafunzi alikuwa sahihi. Kiti kinataka kuliendesha Bunge kama vile darasa, tena nadhani la chekechea!

Mnyika alipewa nafasi na Ndugai kuomba mwongozo kuhusiana na mchango wa Lusinde,ipitie upya hoja ya Mnyika ujiridhishe kuwa alichokuwa anazungumza ndicho alichoomba,akakumbushwa.Akapuuza,akaambiuwa umeeleweka keti Lusinde aendelee na hoja yake akagoma ungekuwa spika ungeruhusu mgomo wa Mnyika uendelee?

Tukubaliane kwa manufaa ya kuhitimisha hoja Ndugai tuseme alikosea akaamrisha Mnyika atolewe nje,je ilikuwa busara wah. Wabunge wawili wanawake kutaka kupigana na askari ili Mnyika asitolewe nje.

Askari wa bunge wangekuwa wavuta bangi wakaamua kuwaonyesha kuwa wana nguvu kuliko wah.wawili wale nini kingetokea?

Je ni busara kwa mh.Mbunge anapohisi kuonewa au nduguye kuonea kujitetea kwa kutumia nguvu zake na siyo akili zake? ndicho tunachotak kufundisha watotot wetu?
 
Mnyika alipewa nafasi na Ndugai kuomba mwongozo kuhusiana na mchango wa Lusinde,ipitie upya hoja ya Mnyika ujiridhishe kuwa alichokuwa anazungumza ndicho alichoomba,akakumbushwa.Akapuuza,akaambiuwa umeeleweka keti Lusinde aendelee na hoja yake akagoma ungekuwa spika ungeruhusu mgomo wa Mnyika uendelee?

Tukubaliane kwa manufaa ya kuhitimisha hoja Ndugai tuseme alikosea akaamrisha Mnyika atolewe nje,je ilikuwa busara wah. Wabunge wawili wanawake kutaka kupigana na askari ili Mnyika asitolewe nje.

Askari wa bunge wangekuwa wavuta bangi wakaamua kuwaonyesha kuwa wana nguvu kuliko wah.wawili wale nini kingetokea?

Je ni busara kwa mh.Mbunge anapohisi kuonewa au nduguye kuonea kujitetea kwa kutumia nguvu zake na siyo akili zake? ndicho tunachotak kufundisha watotot wetu?
Unatakiwa uelewe kwamba. Kiti kilianza kwa kuwagombanisha Lusinde na Mnyika, kama ambavyo wachungaji wa ng'ombe hugombanisha ng'ombe madume wanapokuwa malishoni. Mpaka kwenye hatua hii unayoisema hali ilikuwa imeishachafuka bungeni. Mnyika hakuta kukaa kwa sababu alitaka apewe suluhisho la "kutukanwa" kwake.

Ndio maana nakuambia, Kiti makini, chenye uweledi na kinachozingatia hiyo unayoiita "nidhamu" kingeona kuwa, chenyewe kimesababisha kuchafuka kwa hali ya hewa, hivyo kisingejifanya kiziwi kwamba hakikusikia tusi aliloloporomoshewa Mnyika, na hata kingekuwa hakikusikia kweli, kwa kutambua kuwa hali ya hewa imeishafuka, kingemtuliza Mnyika kwa kumwambia kuwa kitachunguza kuona ni nani amemtukana na hatua zitachukuliwa, basi!

Kwa namna ambavyo Kiti kiliamrisha wale askari kwenda kumtoa nje Mnyika, ilitarajiwa Mnyika asite kwanza kwa kuwa kama nilivyoeleza mazingira ambayo Kiti kilikuwa kimeyaandaa yalileta tafsiri ya wazi kwamba Mnyika au wapinzani wanaonewa. Mtu anayehisi ameonewa halafu unamletea askari polisi, tena kwa lugha iliyotumiwa na Kiti, haishangazi kuona anasita na kubaki anashangaa kama ilivyotokea kwa Mnyika.

Unajitetea kwa akili kama unakabiliana na wanaotumia akili. Kule bungeni akili zimewekwa pembeni, bali uhuni na ubabe ndio umepewa nafasi. Na inafanyika hivi kwa kuwa hata viongozi wa Bunge wanajua kuna watu nje ya Bunge wanaweza kusapoti uhuni wanaoufanya.

Mwisho, wewe mwenyewe jiulize kama Bunge linataka kufundisha nini watoto wetu. Na kabla ya kujiuliza upanue kidogo fikra zako ili tafakuri yako izame kwenye muktadha mzima wa uendeshaji wa shughuli za Bunge; mfano, Kiti kinapovunja kanuni za Bunge kwa kuwapa "vifungo" wabunge ambavyo havipo katika kanuni, bila Kamati kuwasikiliza na bila Bunge kuwasikiliza, kinawafundisha nini vijana wadogo ambao wanatamani siku moja wawe Kiti?
 
Wewe hujaona matusi ya bingwa wenu wa matusi Kibajaj?

Hivi nyinyi wanaccm mkoje?

Mna macho lakini hamuoni, mna masikio lakini hamsikii.....

Hebu tujikumbushe chanzo cha vurugu lote lililotokea hadi kusababisha Ndugai atoe maamuzi ya kipuuzi kabisa kama yale.

Mbunge Lusinde alikuwa akichangia bajeti ya wizara ya Nishati na Madini na kuwaita wapinzani ni watetezi wa wezi wa madini yetu!

Hivi katika uhalisia ni nani hasa mtetezi mkubwa wa wezi wa madini ni wabunge wa upinzani au wabunge wa CCM?

Tujikumbushe kidogo, hicho kilio cha kuibiwa madini ni kilio cha muda mrefu ambacho wapinzani wamekuwa wakikitoa, lakini wamekuwa wakipuuzwa na kukejeliwa na wabunge wa CCM kwa kuitwa ni wazushi........

Mbaya zaidi wakati Mnyika anachangia kwa kutoa taarifa kuwa wabunge wa upinzani hawatetei wezi, akaibuka Mbunge wa CCM Show....nzaaa akawasha mic na kumuita Mbunge Mnyika mwizi!

Alichokiomba Mnyika kwa Spika ni utaratibu wa kawaida kabisa wa kanuni za Bunge letu, aidha Mbunge huyo aliyewasha mic afute kauli yake au athibitishe wizi wa Mnyika.....

Cha kushangaza kupita kiasi ni maamuzi ya Spika kwa kusema kwa kuwa hiyo kauli ya Mnyika kuitwa mwizi haijaingia kwenye Hansard yeye hawezi kulishughulika suala hilo!

Huyo Ndugai anaongoza Bunge kwa upendeleo wa hali ya juu kwa wabunge wenzake wa CCM....

Yaani tayari keshasahau kuwa hapo siku za nyuma liliwahi kutokea tukio kama hilo kwa Mbunge Mdee kumuita yeye fa.....laaa na yeye Ndugai akataka hiyo issue iwe treated utadhani Mdee kafanya kosa la jinai kubwa utadhani kaua mtu!

Hakika kwa kitendo cha Spika Ndugai kuinitiate akina Mdee na Bulaya wafungiwe kuingia vikao vya Bunge kwa mwaka mzima amevunja hata kanuni za Bunge lake analoliongoza, kwa kuwa kanuni za Bunge zimeweka 'maximum penalty' ya kosa lolote Bungeni kupewa adhabu isiyozidi vikao vya siku 20 pekee.

Kwa namna Ndugai anavyoliongoza Bunge letu, amepoteza kabisa sifa za kuongoza Bunge letu na anapaswa ang'olewe kwenye nafasi hiyo na arudi nyumbani kwake Kongwa ili akafanye kazi aliyoizoea, ya kuwachapa bakora 'mabulai' wenzie, kama alivyomchapa yule mgombea mwenzie wa CCM mwaka 2015 hadi yule 'Bulai' mwenzie akazirai na nusura akate roho!
we kilaza unachangia au unahubiri maana umeandika mistari mingi kuliko mchokoza mada mbaya zaidi pumba tupu.
 
Back
Top Bottom