Salim Said na Elias Msuya
KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) maalim Seif Sharif Hamad, amesema ukandamizaji na uporaji wa haki za wananchi unaoendelea kisiwani Zanzibar sasa basi.
Maalim Seif alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaamu na kusisitiza kuwa watatumia nguvu ya umma kuhakikisha kwamba, wanaishinda dola kandamizaji iliyo chini ya CCM.
Hamad alisema hayo akiwa makao makuu ya chama hicho, Buguruni jijini Dar es Salaam wakati akitoa msimamo wa chama chake kuhusiana na vurugu zinazoendelea Pemba katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura kisiwani humo.
Kutokana na vurugu hizo tayari nyumba sita za mawakala wa CUF zimechomwa moto, huku baadhi yao wakijeruhiwa kutokana na mabomu ya kutoa machozi na kuwamwagia maji yenye kemikali ya kuwasha.
Hamad alisema chama chake kinawapongeza wananchi hao kwa msimamo thabiti wa kukataa kudhulumiwa haki zao zinazoporwa kupitia chaguzi kuu tangu mwaka 1995.
Tunajua wanapatishwa mateso makubwa na watawala madhalimu wasiojali raia wao, lakini hiyo ndiyo gharama ya kudai haki. Hivyo tunawapongeza na kutoa wito kwamba, wasichoke wala kuyumba katika kutetea haki hizo, alisema Hamad na kuongeza:
Umefika mwisho kwa watawala wakandamizaji wa CCM, tunasema ukandamizaji na uporwaji wa haki za wananchi wa Zanzibar sasa basi na tunawahakikishia kwamba nguvu ya umma itashinda dola kandamizaji.
Hatua tunayoipita sasa pia wamepita wananchi wa nchi nyingine waliokandamizwa na kunyimwa haki zao, lakini hawakukata tamaa na mwishowe walishinda.
Aliahidi kwamba, viongozi wa chama hicho kwa kushirikiana na wananchi wapenda haki na demokrasia wa visiwa vya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla wataushinda udhalimu huo tu.
Maalim alisisitiza kwamba, vurugu zote zinazotokea Zanzibar zinasababishwa na njama ovu za CCM na serikali zake kuwazuia wananchi wengi wenye sifa kutoandikishwa katika daftari la kudumu la wapigakura kwa lengo la kupunguza kura za upinzani katika uchaguzi mkuu.
Sambamba na hilo njama hizo zinahusisha kuwanyima haki wapigakura halali 175,000 kisiwani Pemba na kujaza watu wasio na sifa kwa idadi hiyohiyo, ambao ni pamoja na watu maalum wanaotoka sehemu mbalimbali za Tanzania, maarufu kwa jina la Janjaweed kwa ajili ya kuongeza kura za CCM, alisema na kuongeza:
Njama hizi hazitosaidia chochote zaidi ya kuifanya hali kuwa mbaya zaidi na ni vyema serikali za CCM zikajifunza kutokana na matendo kama hayo yaliyofanywa huko nyuma.
Hamad alidai zaidi kuwa njama hizo zinatekelezwa kwa pamoja na Idara ya Vitambulisho vya Mzanzibari Mkazi (Zan ID) na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na kuratibiwa na Idara ya Usalama wa Taifa.
Katika njama hizo wanawatumia maofisa wa ngazi za juu ambao ni pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Zan ID, Mohammed Juma Ame na watendaji wa sekretarieti ya ZEC wakiongozwa na Mkurugenzi wake Salum Kassim Ali, alidai Hamad.
Hata hivyo, Salum Kassim alipoulizwa na gazeti hili alisema hiyo ni haki ya kidemokrasia ya Hamad kusema anachotaka na kuongeza kuwa ingekuwa bora angetoa mifano na kuthibitisha madai yake hayo.
Mimi ni mtendaji wa ZEC na nafanya kazi kwa mujibu wa sheria na kanuni zake na hakuna hata siku moja niliyoambiwa labda nimekiuka sheria, taratibu au kanuni za taasisi yangu katika utendaji, alisema Kassim na kuongeza:
Maalim angekuwa specific(wazi) na kutoa ushahidi katika tuhuma zake mimi ningejibu, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote hadi hapo atakapotoa uthibitisho wa madai yake na kwa kifupi nasema madai yake yote ni uongo mtupu.
Pia Kassim alikataa kwamba yeye ni afisa wa usalama wa taifa na kuongeza kwamba, hayo ni madai tu ambayo hata yeye anaweza kuibuka na kutoa madai yoyote kwa maalim Seif.
Hamad alisema CUF inalaani vikali vitisho kwa wananchi na waandishi wa habari, matumizi makubwa ya nguvu kubwa ya kijeshi dhidi ya raia na kitendo cha utawala kuingilia mamlaka na utendaji wa tume ya uchaguzi.
Tunawataka wakuu wa mikoa, wilaya, mkurugenzi wa Idara ya Zan ID na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi kuacha kuingilia shughuli za ZEC na ZEC nao wakatae kuingiliwa katika shughuli zao, alisema.
Wakati huo huo, Maalim Seif alisema ameshtushwa na kauli za Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)aliyotoa alipokuwa akifafanua kuhusu mabaki ya vitambulisho vya kupigia kura vilivyookotwa na viongozi wa chama hicho baada ya kuchomwa moto katika Bohari Kuu ya Taifa hivi karibuni.
Namshangaa sana Kiravu (Rajab). Kwanini atoe kauli za kishabiki kama kiongozi wa chama cha siasa? Kauli kama hizo zinatakiwa kutolewa na viongozi wa vyama vya siasa hasa CCM. Yeye ni kiongozi wa chama gani? Kwa mtindo huo tutaiaminije Tume ya Taifa ya Uchaguzi?" alihoji.
Niliwahi kusema siku moja tuuogopeni mwanadaamu akichoka kudhulumiwa huwa hajali litamtokea nini yaani huwa anabadilika na kuwa mnyama. Naona viongozi wetu watafute suluhu ya hili jambo ama sivyo Pemba na Zanzibar patatokea maafa.
KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) maalim Seif Sharif Hamad, amesema ukandamizaji na uporaji wa haki za wananchi unaoendelea kisiwani Zanzibar sasa basi.
Maalim Seif alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaamu na kusisitiza kuwa watatumia nguvu ya umma kuhakikisha kwamba, wanaishinda dola kandamizaji iliyo chini ya CCM.
Hamad alisema hayo akiwa makao makuu ya chama hicho, Buguruni jijini Dar es Salaam wakati akitoa msimamo wa chama chake kuhusiana na vurugu zinazoendelea Pemba katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura kisiwani humo.
Kutokana na vurugu hizo tayari nyumba sita za mawakala wa CUF zimechomwa moto, huku baadhi yao wakijeruhiwa kutokana na mabomu ya kutoa machozi na kuwamwagia maji yenye kemikali ya kuwasha.
Hamad alisema chama chake kinawapongeza wananchi hao kwa msimamo thabiti wa kukataa kudhulumiwa haki zao zinazoporwa kupitia chaguzi kuu tangu mwaka 1995.
Tunajua wanapatishwa mateso makubwa na watawala madhalimu wasiojali raia wao, lakini hiyo ndiyo gharama ya kudai haki. Hivyo tunawapongeza na kutoa wito kwamba, wasichoke wala kuyumba katika kutetea haki hizo, alisema Hamad na kuongeza:
Umefika mwisho kwa watawala wakandamizaji wa CCM, tunasema ukandamizaji na uporwaji wa haki za wananchi wa Zanzibar sasa basi na tunawahakikishia kwamba nguvu ya umma itashinda dola kandamizaji.
Hatua tunayoipita sasa pia wamepita wananchi wa nchi nyingine waliokandamizwa na kunyimwa haki zao, lakini hawakukata tamaa na mwishowe walishinda.
Aliahidi kwamba, viongozi wa chama hicho kwa kushirikiana na wananchi wapenda haki na demokrasia wa visiwa vya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla wataushinda udhalimu huo tu.
Maalim alisisitiza kwamba, vurugu zote zinazotokea Zanzibar zinasababishwa na njama ovu za CCM na serikali zake kuwazuia wananchi wengi wenye sifa kutoandikishwa katika daftari la kudumu la wapigakura kwa lengo la kupunguza kura za upinzani katika uchaguzi mkuu.
Sambamba na hilo njama hizo zinahusisha kuwanyima haki wapigakura halali 175,000 kisiwani Pemba na kujaza watu wasio na sifa kwa idadi hiyohiyo, ambao ni pamoja na watu maalum wanaotoka sehemu mbalimbali za Tanzania, maarufu kwa jina la Janjaweed kwa ajili ya kuongeza kura za CCM, alisema na kuongeza:
Njama hizi hazitosaidia chochote zaidi ya kuifanya hali kuwa mbaya zaidi na ni vyema serikali za CCM zikajifunza kutokana na matendo kama hayo yaliyofanywa huko nyuma.
Hamad alidai zaidi kuwa njama hizo zinatekelezwa kwa pamoja na Idara ya Vitambulisho vya Mzanzibari Mkazi (Zan ID) na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na kuratibiwa na Idara ya Usalama wa Taifa.
Katika njama hizo wanawatumia maofisa wa ngazi za juu ambao ni pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Zan ID, Mohammed Juma Ame na watendaji wa sekretarieti ya ZEC wakiongozwa na Mkurugenzi wake Salum Kassim Ali, alidai Hamad.
Hata hivyo, Salum Kassim alipoulizwa na gazeti hili alisema hiyo ni haki ya kidemokrasia ya Hamad kusema anachotaka na kuongeza kuwa ingekuwa bora angetoa mifano na kuthibitisha madai yake hayo.
Mimi ni mtendaji wa ZEC na nafanya kazi kwa mujibu wa sheria na kanuni zake na hakuna hata siku moja niliyoambiwa labda nimekiuka sheria, taratibu au kanuni za taasisi yangu katika utendaji, alisema Kassim na kuongeza:
Maalim angekuwa specific(wazi) na kutoa ushahidi katika tuhuma zake mimi ningejibu, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote hadi hapo atakapotoa uthibitisho wa madai yake na kwa kifupi nasema madai yake yote ni uongo mtupu.
Pia Kassim alikataa kwamba yeye ni afisa wa usalama wa taifa na kuongeza kwamba, hayo ni madai tu ambayo hata yeye anaweza kuibuka na kutoa madai yoyote kwa maalim Seif.
Hamad alisema CUF inalaani vikali vitisho kwa wananchi na waandishi wa habari, matumizi makubwa ya nguvu kubwa ya kijeshi dhidi ya raia na kitendo cha utawala kuingilia mamlaka na utendaji wa tume ya uchaguzi.
Tunawataka wakuu wa mikoa, wilaya, mkurugenzi wa Idara ya Zan ID na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi kuacha kuingilia shughuli za ZEC na ZEC nao wakatae kuingiliwa katika shughuli zao, alisema.
Wakati huo huo, Maalim Seif alisema ameshtushwa na kauli za Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)aliyotoa alipokuwa akifafanua kuhusu mabaki ya vitambulisho vya kupigia kura vilivyookotwa na viongozi wa chama hicho baada ya kuchomwa moto katika Bohari Kuu ya Taifa hivi karibuni.
Namshangaa sana Kiravu (Rajab). Kwanini atoe kauli za kishabiki kama kiongozi wa chama cha siasa? Kauli kama hizo zinatakiwa kutolewa na viongozi wa vyama vya siasa hasa CCM. Yeye ni kiongozi wa chama gani? Kwa mtindo huo tutaiaminije Tume ya Taifa ya Uchaguzi?" alihoji.
Niliwahi kusema siku moja tuuogopeni mwanadaamu akichoka kudhulumiwa huwa hajali litamtokea nini yaani huwa anabadilika na kuwa mnyama. Naona viongozi wetu watafute suluhu ya hili jambo ama sivyo Pemba na Zanzibar patatokea maafa.