Zanzibar 2020 Maalim Seif Sharif Hamad unataka kutugawa Watanzania kwa faida ya nani?

.......Lakini zaidi ya nusu ya Wazanzibari wanaishi bara na wanavitega uchumi bara,na hilo linaweza kuwa kikwazo cha kuvunja Muungano,labda utabuniwa ushirikiano wa kindugu bila nchi hizo mbili kuingilia mambo ya nchi nyingine.
Hilo wala siyo shida.. mbona wahindi Wana vitega uchumi vingi Tanzania, na hakuna muungano kati ya Tz na India?
 
Hilo wala siyo shida.. mbona wahindi Wana vitega uchumi vingi Tanzania, na hakuna muungano kati ya Tz na India?
Mimi staki kumungunya maneno,tukivunja muungano kwa jazba,usishangae wakaja watu na visasi kuwa wazenj wote rudi kwenu.
Mimi nimeona General Idd Amin alivyowafukuza zaidi ya 70,000 wahindi Uganda.

Pia nimeona Kenya mara kunapokuwepo msuguano wa kisiasa kati ya Tanzania na Kenya,mara nyingi watanzania waliopo Kenya watakamatwa ,kupigwa na kuharibiwa mali zao.

Hii ni tabia yetu.
 
Muungano haujawahi kuenziwa kama unavyotaka tuamini. Ni wa kulazimishana tokea mapinduzi yake, kuna ushahidi wa kutosha wa Nyerere kuleta majeshi kupindua serekali ya Zanzibar na baadae kumtishia Karume lazima akubali muungano.

Haujawahi kuenziwa muungano huu, si na wazee wala sie vijana. Na sababu ya msingi ya sisi wazanzibari kuukataa sio ubaguzi, ni sababu ya kiuchumi. Umedhoofisha kila sekta ya uchumi wa visiwa vya Zanzibar na kuwatia watu ufukara.
 
Hitaji la siku nyingi la Wazanzibari waliokuwa wengi ni kulivua na hatimaye kuondokana na koti la muungano. Huu ndio ukweli wenyewe, ni sisi Watanganyika ndio ambao hasa tunauhitaji kwa udi na uvumba.
Jamani Matajiri wa pemba na wengine wa ZNZ watawekeza kwenye soko gani , na hizi nyumba zao zilizoko huku bara itakuwaje??
 
Umeandika upuuzi, yule anayesema hapa sitaleta maji mkichagua tofauti na chama changu huyo ndiyo anahubiri umoja na kusema watatumia dola kubaki madarakani ndiyo umoja? shame on you
Ungemuongeza na lingine hawa hawana aibu kbs. Hakuna kauli mbaya kama ya ubaguzi eti sileti maji au sileti umeme. Hizi siasa za ajabu sana.
 
Bara ubaguzi nje nje!
Ukichagua upinzani no maendeleo.
Maalim kamatia hapo hapo.
Usikubali Ukhanithi.
 
“Mimi sioni tabu kumwambia (Magufuli) tugawane mbao”. Haya ni maneno aliyoyatamka Mgombea wa Urais Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad akiwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika eneo la Mkele, Mjini Magharibi visiwani Zanzibar.

Kauli hiyo ameitoa sambamba na kauli zingine nyingi ambazo zinaonesha dhamira ya dhati ya Maalim Seif Sharif Hamad kuvunja Muungano endapo tu atachaguliwa kuwa Rais katika Visiwa hivyo.

Ameendelea kusema hata kama Rais Magufuli atachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania basi atamwambia Rais Magufuli abaki na Tanganyika na yeye (Maalim Seif) Zanzibar. Hii ni kauli inayoashiria wazi kuwa Mgombea huyu hana nia njema na Muungano ambao umedumu na kuenziwa na Marais wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi Zanzibar, kwa takribani miaka 56 tangu uasisisiwe na Waasisi wake, Hayati Mzee Abeid Aman Karume na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mnamo Aprili 26, 1964.

Tunapenda kumkumbsha Maalim Seif na Chama cha ACT Wazalendo kuwa dhambi ya ubaguzi mnayotaka kuitekeleza haitawaacha salama watanzania kwani itaathiri maisha ya watanzania wa pande zote ambao kwa miaka yote wameishi na kufanya shughuli zao za kiuchumi na kijamii mahali popote bila kubaguliwa wala kubughudhiwa.

Uimara na utulivu wa Muungano huu ambao ni mkongwe zaidi barani Afrika, umekuwa wa kutolewa mfano na kuzifanya nchi nyingi kuunda umoja ikiwemo Jumuiya ya Ulaya, Jumuiya ya Afrika Mashari na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), kuzitajakwa uchache.

Ni rai yetu kwa Wazanzibari na watanzania kwa ujumla, kuwakataa viongozi wa aina ya Maalim Seif ambae hata hajaingia madarakni anaanza kuonesha wazi wazi kuwagawa watanzania. Tuchague kiongozi kutoka Chama kitakachowaunganisha watanzania na kuwapa uhuru wa kufanya shughuli zao mahali popote bila kubaguliwa wala kubughudhiwa kwa ajili ya ustawi wa maisha yao.
Kama muungano ulikuwa wa hiari, kwa nini uwashikie watu bunduki kulazimisha waendelee na ambacho hawakitaki tena?
 
Kwa faida ya Wazanzibari. Wazanzibari hawautaki Muungano na kama mnabisha, jaribuni kura ya maoni muone matokeo yake. Hata Watanganyika walio wengi hawautaki Muungano, maana hawaoni faida yake kwa mwananchi.

Anaeutakia mema Muungano hawezi kuzuia miradi ya Zanzibar. JMT imekataa kujenga Bandari Zanzibar, yule Mkuu wa mkoa wa Zanzibar zoba nae hana la kusema, Mafuta na Gesi mnataka kuyachukua wakati madini yenu hamtaki tugawane, Mkuu wa mkoa wa Zanzibar na Juj wa Majuj (Balozi Seif Sura Mbaya Ally Iddi) wake wameufyata, mpaka leo hamna kinachoendelea!

Muungano hautakiwi na Wazanzibari! Kila mmoja achukue mbao zake tu na kama mbuzi tu ale kutokana na urefu wa kamba yake. CCM imebaki kununualia watu mafuta na kugawa flana waende mikutanoni :D
 
Anayetugawa ni yule anayesema usinichagulie huyu maana mtajuta sitowaletea maji!
 
Kwa namna ipi?
Nchi ndogo yenye mafuta na gesi asilia,utalii,bahari kwa uvuvi ,uchukuzi na kilimo cha mwani,kilimo cha mazao ya karafuu nk.Ni rahisi kujiongoza na kupiga hatua haraka zaidi kuliko kwenye muungano.
Wakiweza kuboresha sekta ya utalii kutoka watalii laki sita kwa mwaka kwa sasa hadi milioni 2 tu,ukiongezea na uchimbaji wa mafuta na gesi ni wazi nchi hii ndogo yenye watu million 2 itakuwa nchi tajiri kuliko nchi yoyote katika Afrika Mashariki.
 
Nchi ndogo yenye mafuta na gesi asilia,utalii,bahari kwa uvuvi ,uchukuzi na kilimo cha mwani,kilimo cha mazao ya karafuu nk.Ni rahisi kujiongoza na kupiga hatua haraka zaidi kuliko kwenye muungano.
Wakiweza kuboresha sekta ya utalii kutoka watalii laki sita kwa mwaka kwa sasa hadi milioni 2 tu,ukiongezea na uchimbaji wa mafuta na gesi ni wazi nchi hii ndogo yenye watu million 2 itakuwa nchi tajiri kuliko nchi yoyote katika Afrika Mashariki.
Kwasasa ni nani anawazuia kufanya hicho unachosema?, Kuna yeyeote mwenye maamuzi juu ya hayo asiye mzanzibar?
 
Maalim Seif ndio alivyo. Ni mchochezi na mnafiki tangu enzi zake CCM.
Bila huu muungano angeweza kuzunguka bara kwa uhuru hadi watoto wake wakasoma huku?
 
Kila mwaka mnaleta majeshi yenu mnabaka na kuuwa Kisha mnatuita sisi ndugu zenu
 
Kwasasa ni nani anawazuia kufanya hicho unachosema?, Kuna yeyeote mwenye maamuzi juu ya hayo asiye mzanzibar?
Katika Muungano kuna mipaka yake.Kwamfano majeshi ni sharti la Muungano, majeshi yana gharama kubwa.Zanzibar akiwa nje ya Muungano anaweza kupata ulinzi kutoka baadhi ya mataifa makubwa bila yeye kugharimia kitu,labda taifa kubwa wao kugharimia ustawishaji wa Zanzibar.
 
Maalim Seif ndio alivyo. Ni mchochezi na mnafiki tangu enzi zake CCM.
Bila huu muungano angeweza kuzunguka bara kwa uhuru hadi watoto wake wakasoma huku?
Wakenya wangapi wanazunguka huko jee mumeungana nao nyinyi ni WAKOLONI WEUSI hamna lolote mumezoea kunywa damu za wazanzibar
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom