Maalim Seif ni rehma kwa wazanzibari, hatukaniki na hafedheheki

Kakke

JF-Expert Member
Dec 4, 2010
1,883
1,482
Imeandikwa na Ahmed Omar Khamis


  • Akina Borafya ni simba walioshindwa kula nyama mbugani watakula buchani?


Kwa kauli yake Nyerere alikuwa akiumia kichwa sana na kukosa usingizi kutokana na kuwepo kwa nchi iitwayo Zanzibar pembeni ya nchi yake ya Tanganyika. Alitamka wazi wazi kwamba alitamani Zanzibar aididimize katika Bahari ya Hindi kama angeweza. Hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kulitekeleza hilo bila shaka lakini ambacho Nyerere alikusudia ni kuiondoa Zanzibar katika ramani ya dunia na aidhibiti kwa kuiweka ndani ya viganja vya mikono yake, ndani ya mamlaka yake, amri yake, uendeshaji wake, aipe atakacho na ainyime atakacho. Nyerere alianzisha vyema mradi wake huu kwa kulitumia vuguvugu la ukabila katika zama za kupigania uhuru lililoanzishwa na wakoloni kwa kulifanya mtaji wa kuwasambaratisha wazanzibari na kuwagawa mafungu ili azma yake itimie.

Nyerere alilichukua kundi moja la wazanzibari na kulipa maarifa ya Pan Africanism kwamba kila mwenye ngozi nyeusi na mwenye asili yake kutokea bara ndie muafrika wa kweli, mzawa na mwenye haki za kiafrika zitokanazo na ardhi ya Afrika, kinyume chake na mwengine yeyote ni mgeni Afrika na ni mgeni hivyo hivyo kwa Zanzibar ambayo ni sehemu ya Afrika. Alilihamasisha kundi hilo kuwadharau na kuwaona wenzao kuwa hawana sifa ya kuwa wazanzibari. Kupitia fitna hizo wazanzibari wakachinjana na kuuana mara kadhaa wenyewe kwa wenyewe, wazawa wa visiwa hivi (badala ya wakoloni wao) katika zama za kupigania uhuru na mapinduzi ya 1964.

Nyerere alikamilisha mradi wake wa kuiweka Zanzibar katika mikono yake kupitia muungano wa kijanja wa 1964. Kupitia muungano huo Nyerere aliyajengea rasmi misingi ya kisheria isiyo na mipaka na hojiwa mamlaka yake ya kuidhibiti Zanzibar. Hivyo basi enzi ya wazanzibari kunyanyasika kupitia kitanzi cha muungano ikaanzia hapo. Uimara wa muungano ulitegemea sana migawanyiko ya wazanzibari. Utawala wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tokea mwaka 1964 ulijaribu kwa nguvu zote kumzuia kila mtu mwenye mwenye asili ya kisiwa cha Pemba kushika nyadhifa za juu za serikali hiyo kwa shutma kwamba eti wapemba wananasibika na wapinga mapinduzi ya 1964. Nyerere alihakikisha anailinda na kuisimamia kwa nguvu zake zote misimamo hii ya wanamapinduzi ili aweze kujenga ridhaa ya mamlaka yake kwa Zanzibar kwa watawala wanamapinduzi wa Zanzibar.

Firauni alifanya vituko vingi duniani vya kufuru hadi kufikia kujiita Mungu. Mungu alimpelekea habari Firauni kwamba atazaliwa mtoto wa kiume ambae atakua nabii na ataleta nuru na ukombozi kwa watu wa Israel. Baada ya kupata habari hizo Firauni hakuruhusu uhai wa mtoto yoyote wa kiume aliyezaliwa akifahamu kwamba ndie adui kwa utawala wake. Aliweza kuwaangamiza watoto wachanga wote wa kiume waliozaliwa ili kuunusuru utawala wake. Jambo la kushangaza ni jinsi Nabii Mussa (mtoto wa kiume) alivyolelewa na kukulia ndani ya kasri ya Firauni. Hii ni kwa sababu Nabii Mussa ni rehma kutoka kwa Mungu, hivyo Firauni na wasaidizi wake hawakuwa na uwezo wa kumuangamiza. Nabii Mussa alikuwa yuko chini ya nusura ya Mungu ambayo bila shaka inashinda nguvu za wote ambao wangetamani kumdhuru.

Maalim Seif hakuwahi kutamani kuwa mwanasiasa wala kuwa kiongozi tokea utoto wake, ujana wake na hata alipokuwa mwanafunzi ijapokuwa kipaji cha uongozi kilionekana kwake mapema mno. Hakuwahi kuwaza kama angekuwa kiongozi siku moja. Hii ina maana uongozi haikuwa tunu yake wala ndoto yake. Tunaweza kusema uongozi kwa Maalim Seif ni rehma kwa wazanzibari kutoka kwa Mungu ili aje awakomboe kutokana na utawala uliojengewa misingi imara kwa muda mrefu ya ubaguzi, chuki, farka, unyanyasaji, ukandamizaji na maonevu kadhaa wa kadhaa. Maalim Seif ameletwa kuja kuwaunganisha wazanzibari waliogawanywa tokea miaka ya 1950 na kuwafanya waonane kwamba wao ni ndugu wa damu. Maalim Seif amekuja kuwaunganisha wazanzibari kudai nchi yao iliyopotea kupitia mungano wa 1964 na kuirejesha ndani ya mamlaka yao ili waweze kujiamulia mambo yao yote kijamii, kisiasa na kiuchumi na hivyo wapate kuifaidi keki ya taifa lao tukufu.

Hivyo basi majemedari wa mapinduzi hawakuweza kuizuia rehema ya Mungu na hivyo hawakuwa na nguvu za kuiepusha rehma ya Mungu isimpeleke Maalim Seif ikulu ya serikali yenye misingi ya kimapinduzi. Katika makala hii tutaeleza japo kwa ufupi jinsi umuhimu wa Maalim Seif ulivyo kwa wazanzibari. Viongozi wote wengine wanazuka, wanakuwa maarufu na kupotea lakini sivyo kwa Maalim Seif ambae nyota yake inazidi kung'ara kila siku zikienda. Jambo hili linawatahayarisha na kuwaiaibisha wale wenye mawazo ya akina Borafya wanaodhani ipo siku wanaweza wakamtusi Maali Seif akatukanika, wakamfedhehi akafedheheka, wakamkejeli akakejelika na wakamdharau akadharaulika.

Katika mwaka 1975 Maalim Seif akiwa katika kazi yake ya uwalimu hapo katika chuo cha uwalimu Beit raas (sasa SUZA) alipokea taarifa kwamba anahitajika na Rais Aboud Jumbe. Alishangaa sana kusikia wito wa Rais kwani hakutarajia kabisa kama angejulikana au kuhitajika na Rais siku moja. Baada ya kuwasili ikulu, Rais Aboud Jumbe alimwambia Maalim Seif kwamba kuanzia siku hiyo atafanya kazi katika ofisi yake kama katibu msaidizi maalum (special assistant) wa Rais. Hivyo ndivo rehema ya Mungu ilivyomfikisha Maalim Seif ikulu ya Zanzibar ndani ya zama za revolutionary justice. Hakuota, hakuwaza, hakujisogeza wala hakuomba.

Katika mwaka 1977 Rais Aboud Jumbe aliamua kufanya mabadiliko ya baraza la mapinduzi. Kupitia mabadiliko hayo alimtangaza Maalim Seif pamoja na wenzake kuwa ni mawaziri wapya wateule wa SMZ yeye akiwa ni waziri wa elimu. Kufuatia mabadiliko hayo serikali ya Aboud Jumbe ikapata nuru. Ilitoa unafuu mkubwa kwa wananchi ukilinganisha na utawala wa Karume uliotangulia. Baada ya mapinduzi wanafunzi hawakuweza kuendelea na maomo kwa mujibu wauwezo wao wa kupasi mitihani bali ilikuwa kwa kuzingatia makabila ya baba zao. Utaratibu uliotumika uliruhusu waafrika asilimia themanini (80%), waarabu asilimia kumi na tano (15%), wahindi asilimia nne (4%) na wakomoro asilimia moja (1%) kuendelea na masomo. Baada ya kuwa waziri Maalim Seif alimshauri Jumbe kuubadilisha utaratibu huo na badala yake wanafunzi wachaguliwekuendelea na masomo kwa uwezo wao wa kupasi mitihani na sio makabila yao. Jumbe na Seif walifanikiwa kufanya hivyo japokuwa walipambana na upinzani mkali wa Seif Bakari na Natepe (Burgess 2009).

Sambamba na hili Maalim Seif alifanya jitihada ya kuwatafutia wanafunzi wa kizanzibari nafasi maalum za kujiunga na chuo kikuu cha Dar-es-Salaam hata kama kiwango chao cha kufaulu kilikuwa chini ukilinganisha na wanafunzi wa Tanzania bara kwa sababu kwamba Zanzibar inatoa kiwango kidogo cha wanafunzi wanaokwenda katika elimu ya juu ukilinganisha na Tanzania bara na kwa kuzingatia kwamba elimu ya juu ni suala la muungano. Maalim Seif pia alimshauri Jumbe nafasi za elimu ya juu baina ya wanafunzi wa Pemba na Unguja iwe kwa uwiano wa asilimia 40 – Pemba na asilimia 60 – Unguja. Kabla ya hapo kulikuwa na kiwango kikubwa cha ubaguzi katika kuchagua wanafunzi wa kujiunga na vyuo vikuu baina ya Unguja na Pemba kukiwa na upendeleo mkubwa kwa kisiwa cha Unguja ili kujenga chuki baina ya watu wa Unguja na Pemba. Hata hivyo kutokana na asilimia kubwa (60) ya nafasi za Unguja, wanafunzi kutoka Unguja hawakuweza kujaza nafasi zao na hivyo nafasi hizo kukamilishwa na wanafunzi kutoka Pemba (Burgess 2009).

maalim-seif-564x423.jpg

Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Malim Seif Sharif Hamad

Baada ya Rais Aboud Jumbe kulazimishwa kujiuzulu, Rais mpya Ali Hassan Mwinyi aliingia madarakani. Mwinyi alimteua Maalim Seif kuwa waziri kiongozi wa serikali yake. Chini ya ushauri mzuri wa Maalim Seif Zanzibar ilizidi kupata neema katika Utawala wa Mwinyi. Zanzibar ilirudisha matumizi ya paspoti ili kudhibiti uingiaji holela wa watu na hivyo basi mambo mengi ya udhia kama vile ujambazi, uhalifu, madawa ya kulevya na maradhi ya kuambukiza yaliweza kudhibitiwa. Upigaji watu kiholela na kuwaweka ndani mambo ambayo yalikuwa yakifanywa na Youth League katika awamu zilizotangulia yaliondoshwa. Serikali mpya pia ikawashawishi vijana kusoma na kupatiwa nafasi za masomo nje ya nchi. Halkadhalika vijana wasomi wakashawishiwa kuomba nafasi za uongozi serikali bila ya kuzingatia makabila ya baba zao au mahusiano ya baba zao na u-hizbu, u-Afro au ukomred kabla ilivyokuwa kabla (Burgess 2009). Halkadhalika Mwinyi na Maalim Seif walianzisha katiba mpya ya mwaka 1984 iliyoruhusu utawala wa sheria na mipaka ya madaraka kwa mihimili ya dola ambayo iliandikwa na mwanasheria mkuu wa serikali wa wakati huo ambe ni waziri wa katiba na sheria wa sasa, Abuu Bakar Khamis Bakar. Pia walianzisha mfumo mpya wa mahakama za kisheria na kufutilia mbali mahakama za wananchi zilizoanzishwa na Karume ambazo zilikuwa zikiendeshwa kinyume na misingi ya sheria na haki. Haki za binaadamu katika katiba ya Zanzibar zililingana zaidi na zile za umoja wa mataifa kuliko zile zilizokuwemo katika katiba ya Jamhuri ya muungano.

Kwa kweli serikali ya Mwinyi na Maalim Seif pamoja na kudumu kwa muda mfupi sana iliweza kuleta mabadiliko mengi. Mabadiliko mengine yalikuwa ni pamoja na uhuru wa wananchi kutoa maoni yao. Mambo mengi ambayo kwa njia moja au nyingine yalionekana kuwa ni ya kubana haki za raia ambayo yalikuja mara baada ya Mapinduzi yalibadilishwa katika wakati huo. Vizuizi vingi vya kufaidi uhuru na haki za kiraia viliondolewa. Vyombo vya habari vya Serikali vilitakiwa kuanzisha vipindi maalum vya kuwapa nafasi wananchi kutoa maoni yao juu ya uendeshaji wa nchi yao. Vipindi kama ‘Zanzibar ni Njema' katika Radio ya Zanzibar na ‘Jicho' katika Televisheni ya Zanzibar (TVZ) vilivyotoa fursa kwa Wazanzibari kutoa maoni yao kuhusu uendeshaji na utendaji wa Serikali yao vilianzishwa katika kipindi hicho.

Lakini kubwa zaidi katika utawala wa Mwinyi na Maalim Seif ilikuwa ni kuruhusiwa biashara huria, yaani ‘Trade Liberalisation' hatua ambayo ilipelekea ghafla kubadilika kwa hali za maisha ya watu na kuimarika kwa uchumi na pato la taifa. Jambo hili lilimchukiza sana Nyerere kwani ni kinyume na siasa yake ya ujamaa lakini Mwinyi na Seif walimjibu Nyerere kuwa "tunataka kuuimarisha ujamaa kwa kutumia mfumo huria". Majibu hayo yalimpoza Nyerere. Uhaba mkubwa wa chakula uliokuwepo kabla ulimalizika na umasikini ukapungua makali yake kwa kiwango kikubwa. Wafanya biashara kutoka nchi za jirani kama Kenya na Tanzania bara wakawa wanakuja Zanzibar kutafuta bidhaa. Maisha ya watu yakaboreka na neema kutanda. Hapo ndipo Mwinyi alipozaa msemo wake maarufu, Zanzibar ni njema atakae aje na baadae msemo huu ukawa miongoni mwa maneno ya hekima.

Baada ya kifo cha Edward Sokoine, Nyerere alimteua Salim Ahmed Salim kuwa waziri mkuu mpya. Hivyo basi Salim Ahmed Salim kwa upande wa Jamhuri ya muungano alitarajiwa sana kuwa mrithi wa kiti cha urais baada ya kustaafu Nyerere. Kwa upande wa Zanzibar nako Maalim Seif alitarajiwa sana kurithi kiti cha urais baada ya Mwinyi kumaliza muda wake. Upepo huo wa lisiasa haukuwa ukiwapungia vyema wanamapinduzi wa Zanzibar. Hivyo basi wanamapinduzi hawakupendelea mabadiliko hayo kutokea na walifanya kila wawezalo kuubalisha upepo huo wa kisiasa ili Salim Ahmed Salim kwa upande wa Jamhuri ya Muungano na Maalim Seif kwa upande wa Zanzibar wasiweze kuwa marais wanaofuatia. Kosa la Maalim Seif lilikuwa ni upemba wake wakati Salim Ahmed alikuwa na makosa matatu. Kosa la kwanza ni uarabu, kosa la pili ni upemba kama Maalim Seif na kosa la tatu ni mwanachama wa zamani wa ZNP. Ijapokuwa Nyerere na Mwinyi walimuona Salim ndiye anaefaa zaidi kuwa raisi wa Jamhuri ya muungano lakini alipigwa vita na wanamapinduzi.

Nyerere kwa kuwatii wanamapinduzi akasitisha azma ya kumteua Salim na badala yake kumteua Mwinyi kuwa rais Mpya wa Jamhuri ya muungano. Kwa upande wa Zanzibar majina matatu ya Idri Abdul-wakil, Maalim Seif na Salmin Amour ndio yaliojadiliwa na NEC kuteua mmoja wao kuwa rais mpya baada ya Mwinyi kupelekwa katika kiti cha urais wa Jamhuri ya Muungano. Mzee Idris alikuwa wa mwanzo kuomba jina lake liondoshwe kutokana na uzee. Maalim Seif alikuwa kijana na alijulikana zaidi katika chama, katika NEC na wananchi wa Unguja na Pemba hivyo kulikuwa na kila aina ya uwezekano wa kushinda kura nyingi kulinganisha na Idris Abdul-wakil. NEC ilishangazwa sana kutangazwa ushindi wa Idris Abdulwakil. Hapana shaka wanamapinduzi waliingilia kati suala hilo na kumfanya Nyerere kuchakachua matokeo ya kura ili kumpinga Maalim Seif na Kumpitisha Idris. Hapa ndipo wakati mgumu kwa siasa za Zanzibar baada ya kuzaliwa CCM ulipoanza. Wazanzibari hawakufurahia Mwinyi kupelekwa bara wala hawakufurahishwa na uteuzi wa Idris na kuachwa Maalim Seif kwa kuwa Idris hakujulikana vyema na wazanzibari. Takriban asilimia 80 ya wananchi wa Pemba na asilimia 63 ya wanachi wa Mkoa wa Mjini maghrib Unguja walimpigia Idris kura ya "hapana" na hivyo kuzua mtafaruku mkubwa wa kisiasa. Baada ya wimbi la kukataliwa Idris kutanda Zanzibar na hivyo siasa za CCM kuwa ngumu mno Nyerere alimshauri Idris kumteua Maalim Seif kuwa waziri kiongozi.

Hata uteuzi huo wa waziri kiongozi haukuwafurahisha wanamapinduzi. Wao walitaka waziri kiongozi awe Salmin Amour. Hivyo basi wakazidisha na kuendeleza chuki na vita vyao dhidi ya Maalim Seif. Kila aina ya shutma na visingizio wakavitoa ili kumpotezea umaarufu Maalim Seif ndani ya chama na ndani ya Serikali. Moja ya shutma zilizowahi kutolewa ni kuwadharau, kuwavunjia heshima na kuwadhalilisha wanamapinduzi, akina Seif Bakari. Shutma nyengine ni kutaka kurejesha usultani Zanzibar. Katika kipindi hichi kuliimarika mahusiano ya kidiplomasia baina ya Zanzibar na falme za kiarabu. Wanamapinduzi wakatumia fursa hiyo kutoa shutma kwamba Maalim Seif ana mipango wa kurejedisha utawala wa kisultani Zanzibar. Katika ziara moja ya Maalim Seif nchini Oman katika jitihada zake za kuiletea neema Zanzibar, Sultan Qabous alisema wazi kwamba ana kila sababu ya kuisaidia Zanzibar kwa kiwango kikubwa kwa kuwa ni wasomi wa kizanzibari ndio walioijenga Oman bila ya serikali ya Oman kuchangia chochote katika elimu zao (Burgess 2009). Maalim Seif na Qabous kupitia ziara hiyo waliahidiana mambo mengi ya maendeleo kwa Zanzibar kama vile ujenzi wa viwanja vya ndege, kutanua miradi ya maji na ujenzi wa barabara. Ahadi zote hizo zilibezwa, kupuuzwa na kuzuiliwa utekelezaji wake na wanamapinduzi.

Tuhuma nyengine dhidi ya Maalim Seif ni kuwapendelea wapemba. Maalim Seif alituhumiwa kuwapendelea wapemba kwa ushauri wake wa mgao wa huduma na mipango ya maendeleo kwa asilimia 60- Unguja na 40 – Pemba. Baada ya tuhuma kadhaa wa kadhaa kushindikana kutumika kama sababu na visingizio vya kumtoa Maalim Seif katika wadhifa wake ikatumika shutuma ya kufanya upinzani ndani ya chama. Kupokonywa Maalim Seif uwaziri kiongozi kukawadia na habari zikazagaa kila upande. Mrithi wa nafasi Maalim Seif iliamuliwa kuwa Dr Omar Ali Juma ili kuwatuliza wapemba baada ya kitendo cha kutolea Maalim Seif. Hata hivyo Dr Omar aliposikia habari hizo haraka alifiki kwa Maalim Seif na kumwambia kwamba kuna habari kwamba unataka kutolewakatika nafasi yako na baadae nafasi nipewe mimi lakini mimi sitokubali nikijua ni kuwagawa wazanzibari na kujenga fitna. Tarehe 18 Januari mwaka 1988 Seif Sharif akapokonywa wadhifa wa uwaziri kiongozi na Dr Omar Ali Juma akachaguliwa kuwa waziri mkuu mpya huku Dr Omar Ali Juma akifurahia na wala hakukataa kama alivyoahidi kabla.

Baada ya kitendo cha Maalim Seif kufukuzwa Zanzibar haikuwa shuwari. Mengi yalizungumzwa, chama cha CCM kulaaniwa na kukataliwa, Nyerere kuonekana ndie anaewagawa wazanzibari na Muungano kushutumiwa. Matukio hayo yalimkera sana Nyerere na ndipo alipolazimika kumfukuza Maalim Seif kabisa katika chama ili akose jukwaa la kufanyia siasa. Kikao cha NEC kilichofuatia kilijadili tuhuma dhidi ya Maalim Seif na wenzake saba tuhuma dhidi ya Seif na wote walitakiwa kujiuzulu nafasi zao katika chama ambapo baada ya wote kugoma kufanya hivyo Nyerere akatamka mbele ya wajumbe wa NEC "kama mmegoma kujiuzulu kwa nafasi niliyonayo nimekufukuzeni nyote katika chama". Maalim seif na wenzake walifukuzwa katika chama siku ya mwezi 27 Ramadhani, kwa mujibu wa waislamu ni usiku wenye uwezekano mkubwa wa kupatikana lailatul-qadr.

Baada ya Maalim Seif kutolewa serikalini na kufukuzwa katika chama wazanzibari wakaghadhibika mno. Watu makundi kwa makundi wakarudisha kadi za chama na wengine kuzichana. Wengine walitengeneza sanamu za Nyerere hususan huko Pemba na kuziharibu hadharani kuonyesha hasira zao. Mara tu Maalim Seif alipowasili kisiwani Pemba kutokea Dodoma makundi kwa makundi ya watu walikuwa wakikusanyika wakiwa na hamu na shauku ya kuzungumza nae. Nchi ilipooza na siasa za chama cha mapinduzi Zanzibar zikakwama. Nyerere akahisi kwamba hata kuwa nje ya chama na serikali Maalim Seif ataendelea kuwa tishio kwa nchi na chama hivyo tuhuma kadhaa zikabuniwa ili kumtia gerezani. Serikali ilijaribu kwanza kutaka kumshtaki Maalim Seif kwa madai kuiba nyaraka za serikali lakini baada ya kushindwa kuthibitisha walimshtaki kwa kosa la kuitisha mikutano haramu. Seif alifungwa jela kwa kipindi cha miezi 30 kuanzia mwezi wa Mei 1989 hadi mwezi wa Novemba mwaka 1991. Jitihada mbali mbali zikachukuliwa za kidiplomasia, shirika la Amnesty International na wasomi kudai Seif Sharif atolewe jela. Baada ya hapo akatolewa pamoja na masharti na vikwazo vingi. Pamoja na yote hayo bado Maalim Seif aliapa kutimiza ahadi yake ya kuwatetea wazanzibari kama alivyoahidi.

….itaendelea
 
Maalim ni mwana political scientist aliebobea sio mpiga kelele ni mwenye ni mwenye mtazamo endelevu juu ya wananchi.ni mtanzani pekee aliyeweza kujibizana na nyerere face to face.ana uchungu na zanzibar pamoja na wazanzibar pia.it could be better to call him father of isles.mungu ibariki zanzibar na watu wake.ameen
 
Maalim ni mwana political scientist aliebobea sio mpiga kelele ni mwenye ni mwenye mtazamo endelevu juu ya wananchi.ni mtanzani pekee aliyeweza kujibizana na nyerere face to face.ana uchungu na zanzibar pamoja na wazanzibar pia.it could be better to call him father of isles.mungu ibariki zanzibar na watu wake.ameen

Kumbe mnatamani hiyo title? I didn't know that. By the way, what are the requirements to qualify for the title? Lets learn from others - India, USA, Argentine, etc. There are fathers of nations and not of isles, villages, or shehias.
 
Sioni rehema kwenye maalim seif zaidi ya kibaraka wa CCM aliyewasaliti wananchi baada ya kuwaponza wakamwaga damu. Namuona mtu mwenye uchu wa madaraka anayeweza kuzimwa kwa kuhongwa cheo chochote mradi yeye na familia yake washibishe matumbo yao. Sioni rehma zaidi ya nakma kama tutampiga darubini vizuri jamaa huyu. Mwandishi wa makala huenda katumwa au kaamua kujituma.
 
kwa kweli kwa historia ya upinzani zanzibar, maalim seif , hamad rashid na juma duni haji wana mchango mkubwa sio wa wakuwabeza hata kidogo.Ishu ni kuangalia wameteleza wapi pengine.
 
Zanzibar is a dead side of the country.Maalim pamoja na kuwa kibarakaw a Qaboos bado anaitwa majina matamu hivi?Wazanzibar watakuja juta sana kwa tabia zao hizi za kuangalia kribu palipo na jema na kuangalia mbali ili wakamilishe mabaya.

Seems that unafiki dhambi wanayoishutumu sana ndio inawatafuna wazazibar sasa na baadaye.Wamekuwa ktk Muungano kinafiki sana.Sasa wote wanaanza jitenga rudi ktk utumwa.Mleta maada kaandika mengi sana ila kasahau on yaliyo wazi ktk alichoandika.

-Nyerere alijua Zanzibara imeshazama na kinachoendelea ni kujaribu shikilia kichwa ili kila jitihada za kuipoa zikifanyika basi kichwa kitokeze na pua kupa hewa kidogo.Nyerere alijua kuwa hawezi kuw amkorofi dhidi yao ili kuwaweka sawa, pia hawezi wastaarabisha, alijua pale ni kitovu cha matatizo na Bara hawatakuwa na ujanja zaidi ya kuwajibika iokoa.Hakuwa na kauli nyingine zaidi ya kusema kuwa angetamani kingekuwa mbalia baharini ili kisimhusu wala wahusu watanzania.Mimi pia ninge/na ninafikiri hivyo pia.
 
kwa kweli kwa historia ya upinzani zanzibar, maalim seif , hamad rashid na juma duni haji wana mchango mkubwa sio wa wakuwabeza hata kidogo.Ishu ni kuangalia wameteleza wapi pengine.

Kumbe Maalim anafanana na Mussa !
 
Ww uliyeandika hapa ni Mpemba Uandishi wako tu unadhihirisha, Mpemba yeyote hawezi kusema bila kumtaja nyerere kama maneno yangekuwa yanafufua basi huyu nyerere angefufuka, najua wapemba hata Abesi Aman karume mnamchukia sema kusema hadharan mnashindwa kwa kuwa mtakosa Nchi mkisema Abeid mnabaki kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa, kwa habari hii ndo utajua kuwa wapemba ndo wanaopinga muungano sababu muungano unawalinda watu wa Unguja wakati wao wanakiu ya kuitwaa zanzibar, wapemba wamejaa visasi katka nafsi zao hawataridhika mpaka Nchi washike wao sio Shein mpemba mwenye itikadi za kibara na kiunguja, ndomana ukichunguza kwa makini utajua Uhamsho ni kilio cha upemba utagundua CUF ndo Uhamsho nao CUF 98 ni wapemba na ndo wanaililia zanzibar kuliko pemba yao.Nyerere hakuwafanya muwe masikini umasikini mmeutaka wenyewe, ina maana bila muungano kipindi hicho Seif na Jumbe wangesomesha wapi watu vyuo vikuu???? Waliowatawala Zanzibar hawakuweka kipaumbele Elimu bali waliwapa Elimu ya Dini na si kuwapa Elimu zote mbili, wakawafundisha mambo ya kishenzi kama ushoga na ubaguzi na nyie wapemba mlisahau wenzenu wazanzibar na kujifanya warabu ni baba zenu na kuzana nao hicho ndo kinachowaumiza wazanzibar wakikumbuka ivyo basi wanaona heri Muungano udumu maana nyie ni wabinafsi hakika, kama mliwatenga wazanzibar na kujiita nyie warabu je mkipewa nchi si mtaifanya iwe ya warabu??
 
Mbona na yeye amemeza ndoano ya UMAKAMU WA PILI WA ZNZ. Hana kitu naye ni samaki tu!
 
mh kaka mbn 2015 mbali hatujui hata kama dunia inausha dec 21 ushaanza kumtafutia kura nway inaonekana wengi wanaotumia Jf ni wabara nakushauri ungeprint vipeperushi kama mnavyofanyaga ukavigawa Tanzania visiwani......there will always be one Tanzania where all right will be shared equally mnavong'an'ania kujitenga westerners wanachekelea coz wanajua ndo itakua rahisi kwako kutawala ebu amkeni basi na nyie hao viongozi wachache wanaosema tutengane wana uchu wa madaraka na vibaraka wa westerners ohooo chukulieni mfano Libya uoni walikuja kusupport upande gani? sasa hvi Libya iko wapi? so maswala ya kuanza kujadili viongozi nani mzuri nani mbaya si wakati wake besides unaeza onekana hata unafanya treason kwa viongozi wengine you guys have to be extra carefully.....Peace guys one Tanzania... forever relatives
 
Alifukuzwa CCM na kutiwa ndani kwa kosa la uhaini. CCM walitumia vyombo vyote vya habari kupoteza kisiasa maalim huku Maalim akitumia sana BBC na DW kupitia watangazaji akina Ali Saleh na Salim Said Salim

Alianzisha Nkama huru huku wanachama wake wakipatikana kwa kujificha. Mara waarabu, watajesha Utumwa na Zanzibar itakuwa kama Rwanda. Waliokuwa wakimuunga Mkono maalim seif wakipoteza kazi na maslahi yao ndani ya chama. Vyombo vya USALAMA walikuwa na moja kuhakikisha Hakuna Nkama huru, hakuna Cuf kuimarika

SASA HIVI: NI MAKAMO WA KWANZA WA RAIS. analindwa..
 
Kwa kauli yake Nyerere alikuwa akiumia kichwa sana na kukosa usingizi kutokana na kuwepo kwa nchi iitwayo Zanzibar pembeni ya nchi yake ya Tanganyika. Alitamka wazi wazi kwamba alitamani Zanzibar aididimize katika Bahari ya Hindi kama angeweza. Hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kulitekeleza hilo bila shaka lakini ambacho Nyerere alikusudia ni kuiondoa Zanzibar katika ramani ya dunia na aidhibiti kwa kuiweka ndani ya viganja vya mikono yake, ndani ya mamlaka yake, amri yake, uendeshaji wake, aipe atakacho na ainyime atakacho. Nyerere alianzisha vyema mradi wake huu kwa kulitumia vuguvugu la ukabila katika zama za kupigania uhuru lililoanzishwa na wakoloni kwa kulifanya mtaji wa kuwasambaratisha wazanzibari na kuwagawa mafungu ili azma yake itimie.

Nyerere alilichukua kundi moja la wazanzibari na kulipa maarifa ya Pan Africanism kwamba kila mwenye ngozi nyeusi na mwenye asili yake kutokea bara ndie muafrika wa kweli, mzawa na mwenye haki za kiafrika zitokanazo na ardhi ya Afrika, kinyume chake na mwengine yeyote ni mgeni Afrika na ni mgeni hivyo hivyo kwa Zanzibar ambayo ni sehemu ya Afrika. Alilihamasisha kundi hilo kuwadharau na kuwaona wenzao kuwa hawana sifa ya kuwa wazanzibari. Kupitia fitna hizo wazanzibari wakachinjana na kuuana mara kadhaa wenyewe kwa wenyewe, wazawa wa visiwa hivi (badala ya wakoloni wao) katika zama za kupigania uhuru na mapinduzi ya 1964.

Nyerere alikamilisha mradi wake wa kuiweka Zanzibar katika mikono yake kupitia muungano wa kijanja wa 1964. Kupitia muungano huo Nyerere aliyajengea rasmi misingi ya kisheria isiyo na mipaka na hojiwa mamlaka yake ya kuidhibiti Zanzibar. Hivyo basi enzi ya wazanzibari kunyanyasika kupitia kitanzi cha muungano ikaanzia hapo. Uimara wa muungano ulitegemea sana migawanyiko ya wazanzibari. Utawala wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tokea mwaka 1964 ulijaribu kwa nguvu zote kumzuia kila mtu mwenye mwenye asili ya kisiwa cha Pemba kushika nyadhifa za juu za serikali hiyo kwa shutma kwamba eti wapemba wananasibika na wapinga mapinduzi ya 1964. Nyerere alihakikisha anailinda na kuisimamia kwa nguvu zake zote misimamo hii ya wanamapinduzi ili aweze kujenga ridhaa ya mamlaka yake kwa Zanzibar kwa watawala wanamapinduzi wa Zanzibar.

Firauni alifanya vituko vingi duniani vya kufuru hadi kufikia kujiita Mungu. Mungu alimpelekea habari Firauni kwamba atazaliwa mtoto wa kiume ambae atakua nabii na ataleta nuru na ukombozi kwa watu wa Israel. Baada ya kupata habari hizo Firauni hakuruhusu uhai wa mtoto yoyote wa kiume aliyezaliwa akifahamu kwamba ndie adui kwa utawala wake. Aliweza kuwaangamiza watoto wachanga wote wa kiume waliozaliwa ili kuunusuru utawala wake. Jambo la kushangaza ni jinsi Nabii Mussa (mtoto wa kiume) alivyolelewa na kukulia ndani ya kasri ya Firauni. Hii ni kwa sababu Nabii Mussa ni rehma kutoka kwa Mungu, hivyo Firauni na wasaidizi wake hawakuwa na uwezo wa kumuangamiza. Nabii Mussa alikuwa yuko chini ya nusura ya Mungu ambayo bila shaka inashinda nguvu za wote ambao wangetamani kumdhuru.

Maalim Seif hakuwahi kutamani kuwa mwanasiasa wala kuwa kiongozi tokea utoto wake, ujana wake na hata alipokuwa mwanafunzi ijapokuwa kipaji cha uongozi kilionekana kwake mapema mno. Hakuwahi kuwaza kama angekuwa kiongozi siku moja. Hii ina maana uongozi haikuwa tunu yake wala ndoto yake. Tunaweza kusema uongozi kwa Maalim Seif ni rehma kwa wazanzibari kutoka kwa Mungu ili aje awakomboe kutokana na utawala uliojengewa misingi imara kwa muda mrefu ya ubaguzi, chuki, farka, unyanyasaji, ukandamizaji na maonevu kadhaa wa kadhaa. Maalim Seif ameletwa kuja kuwaunganisha wazanzibari waliogawanywa tokea miaka ya 1950 na kuwafanya waonane kwamba wao ni ndugu wa damu. Maalim Seif amekuja kuwaunganisha wazanzibari kudai nchi yao iliyopotea kupitia mungano wa 1964 na kuirejesha ndani ya mamlaka yao ili waweze kujiamulia mambo yao yote kijamii, kisiasa na kiuchumi na hivyo wapate kuifaidi keki ya taifa lao tukufu.

Hivyo basi majemedari wa mapinduzi hawakuweza kuizuia rehema ya Mungu na hivyo hawakuwa na nguvu za kuiepusha rehma ya Mungu isimpeleke Maalim Seif ikulu ya serikali yenye misingi ya kimapinduzi. Katika makala hii tutaeleza japo kwa ufupi jinsi umuhimu wa Maalim Seif ulivyo kwa wazanzibari. Viongozi wote wengine wanazuka, wanakuwa maarufu na kupotea lakini sivyo kwa Maalim Seif ambae nyota yake inazidi kung'ara kila siku zikienda. Jambo hili linawatahayarisha na kuwaiaibisha wale wenye mawazo ya akina Borafya wanaodhani ipo siku wanaweza wakamtusi Maali Seif akatukanika, wakamfedhehi akafedheheka, wakamkejeli akakejelika na wakamdharau akadharaulika.

Katika mwaka 1975 Maalim Seif akiwa katika kazi yake ya uwalimu hapo katika chuo cha uwalimu Beit raas (sasa SUZA) alipokea taarifa kwamba anahitajika na Rais Aboud Jumbe. Alishangaa sana kusikia wito wa Rais kwani hakutarajia kabisa kama angejulikana au kuhitajika na Rais siku moja. Baada ya kuwasili ikulu, Rais Aboud Jumbe alimwambia Maalim Seif kwamba kuanzia siku hiyo atafanya kazi katika ofisi yake kama katibu msaidizi maalum (special assistant) wa Rais. Hivyo ndivo rehema ya Mungu ilivyomfikisha Maalim Seif ikulu ya Zanzibar ndani ya zama za revolutionary justice. Hakuota, hakuwaza, hakujisogeza wala hakuomba.
Katika mwaka 1977 Rais Aboud Jumbe aliamua kufanya mabadiliko ya baraza la mapinduzi. Kupitia mabadiliko hayo alimtangaza Maalim Seif pamoja na wenzake kuwa ni mawaziri wapya wateule wa SMZ yeye akiwa ni waziri wa elimu. Kufuatia mabadiliko hayo serikali ya Aboud Jumbe ikapata nuru. Ilitoa unafuu mkubwa kwa wananchi ukilinganisha na utawala wa Karume uliotangulia. Baada ya mapinduzi wanafunzi hawakuweza kuendelea na maomo kwa mujibu wauwezo wao wa kupasi mitihani bali ilikuwa kwa kuzingatia makabila ya baba zao. Utaratibu uliotumika uliruhusu waafrika asilimia themanini (80%), waarabu asilimia kumi na tano (15%), wahindi asilimia nne (4%) na wakomoro asilimia moja (1%) kuendelea na masomo. Baada ya kuwa waziri Maalim Seif alimshauri Jumbe kuubadilisha utaratibu huo na badala yake wanafunzi wachaguliwekuendelea na masomo kwa uwezo wao wa kupasi mitihani na sio makabila yao. Jumbe na Seif walifanikiwa kufanya hivyo japokuwa walipambana na upinzani mkali wa Seif Bakari na Natepe (Burgess 2009).

Sambamba na hili Maalim Seif alifanya jitihada ya kuwatafutia wanafunzi wa kizanzibari nafasi maalum za kujiunga na chuo kikuu cha Dar-es-Salaam hata kama kiwango chao cha kufaulu kilikuwa chini ukilinganisha na wanafunzi wa Tanzania bara kwa sababu kwamba Zanzibar inatoa kiwango kidogo cha wanafunzi wanaokwenda katika elimu ya juu ukilinganisha na Tanzania bara na kwa kuzingatia kwamba elimu ya juu ni suala la muungano. Maalim Seif pia alimshauri Jumbe nafasi za elimu ya juu baina ya wanafunzi wa Pemba na Unguja iwe kwa uwiano wa asilimia 40 - Pemba na asilimia 60 – Unguja. Kabla ya hapo kulikuwa na kiwango kikubwa cha ubaguzi katika kuchagua wanafunzi wa kujiunga na vyuo vikuu baina ya Unguja na Pemba kukiwa na upendeleo mkubwa kwa kisiwa cha Unguja ili kujenga chuki baina ya watu wa Unguja na Pemba. Hata hivyo kutokana na asilimia kubwa (60) ya nafasi za Unguja, wanafunzi kutoka Unguja hawakuweza kujaza nafasi zao na hivyo nafasi hizo kukamilishwa na wanafunzi kutoka Pemba (Burgess 2009).

Baada ya Rais Aboud Jumbe kulazimishwa kujiuzulu, Rais mpya Ali Hassan Mwinyi aliingia madarakani. Mwinyi alimteua Maalim Seif kuwa waziri kiongozi wa serikali yake. Chini ya ushauri mzuri wa Maalim Seif Zanzibar ilizidi kupata neema katika Utawala wa Mwinyi. Zanzibar ilirudisha matumizi ya paspoti ili kudhibiti uingiaji holela wa watu na hivyo basi mambo mengi ya udhia kama vile ujambazi, uhalifu, madawa ya kulevya na maradhi ya kuambukiza yaliweza kudhibitiwa. Upigaji watu kiholela na kuwaweka ndani mambo ambayo yalikuwa yakifanywa na Youth League katika awamu zilizotangulia yaliondoshwa. Serikali mpya pia ikawashawishi vijana kusoma na kupatiwa nafasi za masomo nje ya nchi. Halkadhalika vijana wasomi wakashawishiwa kuomba nafasi za uongozi serikali bila ya kuzingatia makabila ya baba zao au mahusiano ya baba zao na u-hizbu, u-Afro au ukomred kabla ilivyokuwa kabla (Burgess 2009). Halkadhalika Mwinyi na Maalim Seif walianzisha katiba mpya ya mwaka 1984 iliyoruhusu utawala wa sheria na mipaka ya madaraka kwa mihimili ya dola ambayo iliandikwa na mwanasheria mkuu wa serikali wa wakati huo ambe ni waziri wa katiba na sheria wa sasa, Abuu Bakar Khamis Bakar. Pia walianzisha mfumo mpya wa mahakama za kisheria na kufutilia mbali mahakama za wananchi zilizoanzishwa na Karume ambazo zilikuwa zikiendeshwa kinyume na misingi ya sheria na haki. Haki za binaadamu katika katiba ya Zanzibar zililingana zaidi na zile za umoja wa mataifa kuliko zile zilizokuwemo katika katiba ya Jamhuri ya muungano.

Kwa kweli serikali ya Mwinyi na Maalim Seif pamoja na kudumu kwa muda mfupi sana iliweza kuleta mabadiliko mengi. Mabadiliko mengine yalikuwa ni pamoja na uhuru wa wananchi kutoa maoni yao. Mambo mengi ambayo kwa njia moja au nyingine yalionekana kuwa ni ya kubana haki za raia ambayo yalikuja mara baada ya Mapinduzi yalibadilishwa katika wakati huo. Vizuizi vingi vya kufaidi uhuru na haki za kiraia viliondolewa. Vyombo vya habari vya Serikali vilitakiwa kuanzisha vipindi maalum vya kuwapa nafasi wananchi kutoa maoni yao juu ya uendeshaji wa nchi yao. Vipindi kama ‘Zanzibar ni Njema' katika Radio ya Zanzibar na ‘Jicho' katika Televisheni ya Zanzibar (TVZ) vilivyotoa fursa kwa Wazanzibari kutoa maoni yao kuhusu uendeshaji na utendaji wa Serikali yao vilianzishwa katika kipindi hicho.

Lakini kubwa zaidi katika utawala wa Mwinyi na Maalim Seif ilikuwa ni kuruhusiwa biashara huria, yaani ‘Trade Liberalisation' hatua ambayo ilipelekea ghafla kubadilika kwa hali za maisha ya watu na kuimarika kwa uchumi na pato la taifa. Jambo hili lilimchukiza sana Nyerere kwani ni kinyume na siasa yake ya ujamaa lakini Mwinyi na Seif walimjibu Nyerere kuwa "tunataka kuuimarisha ujamaa kwa kutumia mfumo huria". Majibu hayo yalimpoza Nyerere. Uhaba mkubwa wa chakula uliokuwepo kabla ulimalizika na umasikini ukapungua makali yake kwa kiwango kikubwa. Wafanya biashara kutoka nchi za jirani kama Kenya na Tanzania bara wakawa wanakuja Zanzibar kutafuta bidhaa. Maisha ya watu yakaboreka na neema kutanda. Hapo ndipo Mwinyi alipozaa msemo wake maarufu, Zanzibar ni njema atakae aje na baadae msemo huu ukawa miongoni mwa maneno ya hekima.


Baada ya kifo cha Edward Sokoine, Nyerere alimteua Salim Ahmed Salim kuwa waziri mkuu mpya. Hivyo basi Salim Ahmed Salim kwa upande wa Jamhuri ya muungano alitarajiwa sana kuwa mrithi wa kiti cha urais baada ya kustaafu Nyerere. Kwa upande wa Zanzibar nako Maalim Seif alitarajiwa sana kurithi kiti cha urais baada ya Mwinyi kumaliza muda wake. Upepo huo wa lisiasa haukuwa ukiwapungia vyema wanamapinduzi wa Zanzibar. Hivyo basi wanamapinduzi hawakupendelea mabadiliko hayo kutokea na walifanya kila wawezalo kuubalisha upepo huo wa kisiasa ili Salim Ahmed Salim kwa upande wa Jamhuri ya Muungano na Maalim Seif kwa upande wa Zanzibar wasiweze kuwa marais wanaofuatia. Kosa la Maalim Seif lilikuwa ni upemba wake wakati Salim Ahmed alikuwa na makosa matatu. Kosa la kwanza ni uarabu, kosa la pili ni upemba kama Maalim Seif na kosa la tatu ni mwanachama wa zamani wa ZNP. Ijapokuwa Nyerere na Mwinyi walimuona Salim ndiye anaefaa zaidi kuwa raisi wa Jamhuri ya muungano lakini alipigwa vita na wanamapinduzi.

Nyerere kwa kuwatii wanamapinduzi akasitisha azma ya kumteua Salim na badala yake kumteua Mwinyi kuwa rais Mpya wa Jamhuri ya muungano. Kwa upande wa Zanzibar majina matatu ya Idri Abdul-wakil, Maalim Seif na Salmin Amour ndio yaliojadiliwa na NEC kuteua mmoja wao kuwa rais mpya baada ya Mwinyi kupelekwa katika kiti cha urais wa Jamhuri ya Muungano. Mzee Idris alikuwa wa mwanzo kuomba jina lake liondoshwe kutokana na uzee. Maalim Seif alikuwa kijana na alijulikana zaidi katika chama, katika NEC na wananchi wa Unguja na Pemba hivyo kulikuwa na kila aina ya uwezekano wa kushinda kura nyingi kulinganisha na Idris Abdul-wakil. NEC ilishangazwa sana kutangazwa ushindi wa Idris Abdulwakil. Hapana shaka wanamapinduzi waliingilia kati suala hilo na kumfanya Nyerere kuchakachua matokeo ya kura ili kumpinga Maalim Seif na Kumpitisha Idris. Hapa ndipo wakati mgumu kwa siasa za Zanzibar baada ya kuzaliwa CCM ulipoanza. Wazanzibari hawakufurahia Mwinyi kupelekwa bara wala hawakufurahishwa na uteuzi wa Idris na kuachwa Maalim Seif kwa kuwa Idris hakujulikana vyema na wazanzibari. Takriban asilimia 80 ya wananchi wa Pemba na asilimia 63 ya wanachi wa Mkoa wa Mjini maghrib Unguja walimpigia Idris kura ya "hapana" na hivyo kuzua mtafaruku mkubwa wa kisiasa. Baada ya wimbi la kukataliwa Idris kutanda Zanzibar na hivyo siasa za CCM kuwa ngumu mno Nyerere alimshauri Idris kumteua Maalim Seif kuwa waziri kiongozi.

Hata uteuzi huo wa waziri kiongozi haukuwafurahisha wanamapinduzi. Wao walitaka waziri kiongozi awe Salmin Amour. Hivyo basi wakazidisha na kuendeleza chuki na vita vyao dhidi ya Maalim Seif. Kila aina ya shutma na visingizio wakavitoa ili kumpotezea umaarufu Maalim Seif ndani ya chama na ndani ya Serikali. Moja ya shutma zilizowahi kutolewa ni kuwadharau, kuwavunjia heshima na kuwadhalilisha wanamapinduzi, akina Seif Bakari. Shutma nyengine ni kutaka kurejesha usultani Zanzibar. Katika kipindi hichi kuliimarika mahusiano ya kidiplomasia baina ya Zanzibar na falme za kiarabu. Wanamapinduzi wakatumia fursa hiyo kutoa shutma kwamba Maalim Seif ana mipango wa kurejedisha utawala wa kisultani Zanzibar. Katika ziara moja ya Maalim Seif nchini Oman katika jitihada zake za kuiletea neema Zanzibar, Sultan Qabous alisema wazi kwamba ana kila sababu ya kuisaidia Zanzibar kwa kiwango kikubwa kwa kuwa ni wasomi wa kizanzibari ndio walioijenga Oman bila ya serikali ya Oman kuchangia chochote katika elimu zao (Burgess 2009). Maalim Seif na Qabous kupitia ziara hiyo waliahidiana mambo mengi ya maendeleo kwa Zanzibar kama vile ujenzi wa viwanja vya ndege, kutanua miradi ya maji na ujenzi wa barabara. Ahadi zote hizo zilibezwa, kupuuzwa na kuzuiliwa utekelezaji wake na wanamapinduzi.

Tuhuma nyengine dhidi ya Maalim Seif ni kuwapendelea wapemba. Maalim Seif alituhumiwa kuwapendelea wapemba kwa ushauri wake wa mgao wa huduma na mipango ya maendeleo kwa asilimia 60- Unguja na 40 – Pemba. Baada ya tuhuma kadhaa wa kadhaa kushindikana kutumika kama sababu na visingizio vya kumtoa Maalim Seif katika wadhifa wake ikatumika shutuma ya kufanya upinzani ndani ya chama. Kupokonywa Maalim Seif uwaziri kiongozi kukawadia na habari zikazagaa kila upande. Mrithi wa nafasi Maalim Seif iliamuliwa kuwa Dr Omar Ali Juma ili kuwatuliza wapemba baada ya kitendo cha kutolea Maalim Seif. Hata hivyo Dr Omar aliposikia habari hizo haraka alifiki kwa Maalim Seif na kumwambia kwamba kuna habari kwamba unataka kutolewakatika nafasi yako na baadae nafasi nipewe mimi lakini mimi sitokubali nikijua ni kuwagawa wazanzibari na kujenga fitna. Tarehe 18 Januari mwaka 1988 Seif Sharif akapokonywa wadhifa wa uwaziri kiongozi na Dr Omar Ali Juma akachaguliwa kuwa waziri mkuu mpya huku Dr Omar Ali Juma akifurahia na wala hakukataa kama alivyoahidi kabla.

Baada ya kitendo cha Maalim Seif kufukuzwa Zanzibar haikuwa shuwari. Mengi yalizungumzwa, chama cha CCM kulaaniwa na kukataliwa, Nyerere kuonekana ndie anaewagawa wazanzibari na Muungano kushutumiwa. Matukio hayo yalimkera sana Nyerere na ndipo alipolazimika kumfukuza Maalim Seif kabisa katika chama ili akose jukwaa la kufanyia siasa. Kikao cha NEC kilichofuatia kilijadili tuhuma dhidi ya Maalim Seif na wenzake saba tuhuma dhidi ya Seif na wote walitakiwa kujiuzulu nafasi zao katika chama ambapo baada ya wote kugoma kufanya hivyo Nyerere akatamka mbele ya wajumbe wa NEC "kama mmegoma kujiuzulu kwa nafasi niliyonayo nimekufukuzeni nyote katika chama". Maalim seif na wenzake walifukuzwa katika chama siku ya mwezi 27 Ramadhani, kwa mujibu wa waislamu ni usiku wenye uwezekano mkubwa wa kupatikana lailatul-qadr.

Baada ya Maalim Seif kutolewa serikalini na kufukuzwa katika chama wazanzibari wakaghadhibika mno. Watu makundi kwa makundi wakarudisha kadi za chama na wengine kuzichana. Wengine walitengeneza sanamu za Nyerere hususan huko Pemba na kuziharibu hadharani kuonyesha hasira zao. Mara tu Maalim Seif alipowasili kisiwani Pemba kutokea Dodoma makundi kwa makundi ya watu walikuwa wakikusanyika wakiwa na hamu na shauku ya kuzungumza nae. Nchi ilipooza na siasa za chama cha mapinduzi Zanzibar zikakwama. Nyerere akahisi kwamba hata kuwa nje ya chama na serikali Maalim Seif ataendelea kuwa tishio kwa nchi na chama hivyo tuhuma kadhaa zikabuniwa ili kumtia gerezani. Serikali ilijaribu kwanza kutaka kumshtaki Maalim Seif kwa madai kuiba nyaraka za serikali lakini baada ya kushindwa kuthibitisha walimshtaki kwa kosa la kuitisha mikutano haramu. Seif alifungwa jela kwa kipindi cha miezi 30 kuanzia mwezi wa Mei 1989 hadi mwezi wa Novemba mwaka 1991. Jitihada mbali mbali zikachukuliwa za kidiplomasia, shirika la Amnesty International na wasomi kudai Seif Sharif atolewe jela. Baada ya hapo akatolewa pamoja na masharti na vikwazo vingi. Pamoja na yote hayo bado Maalim Seif aliapa kutimiza ahadi yake ya kuwatetea wazanzibari kama alivyoahidi.........itaendlea
 

Attachments

  • AHMED AIR PORT 7.bmp
    1.3 MB · Views: 87
  • AHMED AIR PORT 6.bmp
    1.3 MB · Views: 80
imeandikwa na ahmed omar khamis


  • akina borafya ni simba walioshindwa kula nyama mbugani watakula buchani?


kwa kauli yake nyerere alikuwa akiumia kichwa sana na kukosa usingizi kutokana na kuwepo kwa nchi iitwayo zanzibar pembeni ya nchi yake ya tanganyika. Alitamka wazi wazi kwamba alitamani zanzibar aididimize katika bahari ya hindi kama angeweza. Hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kulitekeleza hilo bila shaka lakini ambacho nyerere alikusudia ni kuiondoa zanzibar katika ramani ya dunia na aidhibiti kwa kuiweka ndani ya viganja vya mikono yake, ndani ya mamlaka yake, amri yake, uendeshaji wake, aipe atakacho na ainyime atakacho. Nyerere alianzisha vyema mradi wake huu kwa kulitumia vuguvugu la ukabila katika zama za kupigania uhuru lililoanzishwa na wakoloni kwa kulifanya mtaji wa kuwasambaratisha wazanzibari na kuwagawa mafungu ili azma yake itimie.

Nyerere alilichukua kundi moja la wazanzibari na kulipa maarifa ya pan africanism kwamba kila mwenye ngozi nyeusi na mwenye asili yake kutokea bara ndie muafrika wa kweli, mzawa na mwenye haki za kiafrika zitokanazo na ardhi ya afrika, kinyume chake na mwengine yeyote ni mgeni afrika na ni mgeni hivyo hivyo kwa zanzibar ambayo ni sehemu ya afrika. Alilihamasisha kundi hilo kuwadharau na kuwaona wenzao kuwa hawana sifa ya kuwa wazanzibari. Kupitia fitna hizo wazanzibari wakachinjana na kuuana mara kadhaa wenyewe kwa wenyewe, wazawa wa visiwa hivi (badala ya wakoloni wao) katika zama za kupigania uhuru na mapinduzi ya 1964.

Nyerere alikamilisha mradi wake wa kuiweka zanzibar katika mikono yake kupitia muungano wa kijanja wa 1964. Kupitia muungano huo nyerere aliyajengea rasmi misingi ya kisheria isiyo na mipaka na hojiwa mamlaka yake ya kuidhibiti zanzibar. Hivyo basi enzi ya wazanzibari kunyanyasika kupitia kitanzi cha muungano ikaanzia hapo. Uimara wa muungano ulitegemea sana migawanyiko ya wazanzibari. Utawala wa serikali ya mapinduzi ya zanzibar tokea mwaka 1964 ulijaribu kwa nguvu zote kumzuia kila mtu mwenye mwenye asili ya kisiwa cha pemba kushika nyadhifa za juu za serikali hiyo kwa shutma kwamba eti wapemba wananasibika na wapinga mapinduzi ya 1964. Nyerere alihakikisha anailinda na kuisimamia kwa nguvu zake zote misimamo hii ya wanamapinduzi ili aweze kujenga ridhaa ya mamlaka yake kwa zanzibar kwa watawala wanamapinduzi wa zanzibar.

Firauni alifanya vituko vingi duniani vya kufuru hadi kufikia kujiita mungu. Mungu alimpelekea habari firauni kwamba atazaliwa mtoto wa kiume ambae atakua nabii na ataleta nuru na ukombozi kwa watu wa israel. Baada ya kupata habari hizo firauni hakuruhusu uhai wa mtoto yoyote wa kiume aliyezaliwa akifahamu kwamba ndie adui kwa utawala wake. Aliweza kuwaangamiza watoto wachanga wote wa kiume waliozaliwa ili kuunusuru utawala wake. Jambo la kushangaza ni jinsi nabii mussa (mtoto wa kiume) alivyolelewa na kukulia ndani ya kasri ya firauni. Hii ni kwa sababu nabii mussa ni rehma kutoka kwa mungu, hivyo firauni na wasaidizi wake hawakuwa na uwezo wa kumuangamiza. Nabii mussa alikuwa yuko chini ya nusura ya mungu ambayo bila shaka inashinda nguvu za wote ambao wangetamani kumdhuru.

Maalim seif hakuwahi kutamani kuwa mwanasiasa wala kuwa kiongozi tokea utoto wake, ujana wake na hata alipokuwa mwanafunzi ijapokuwa kipaji cha uongozi kilionekana kwake mapema mno. Hakuwahi kuwaza kama angekuwa kiongozi siku moja. Hii ina maana uongozi haikuwa tunu yake wala ndoto yake. Tunaweza kusema uongozi kwa maalim seif ni rehma kwa wazanzibari kutoka kwa mungu ili aje awakomboe kutokana na utawala uliojengewa misingi imara kwa muda mrefu ya ubaguzi, chuki, farka, unyanyasaji, ukandamizaji na maonevu kadhaa wa kadhaa. Maalim seif ameletwa kuja kuwaunganisha wazanzibari waliogawanywa tokea miaka ya 1950 na kuwafanya waonane kwamba wao ni ndugu wa damu. Maalim seif amekuja kuwaunganisha wazanzibari kudai nchi yao iliyopotea kupitia mungano wa 1964 na kuirejesha ndani ya mamlaka yao ili waweze kujiamulia mambo yao yote kijamii, kisiasa na kiuchumi na hivyo wapate kuifaidi keki ya taifa lao tukufu.

Hivyo basi majemedari wa mapinduzi hawakuweza kuizuia rehema ya mungu na hivyo hawakuwa na nguvu za kuiepusha rehma ya mungu isimpeleke maalim seif ikulu ya serikali yenye misingi ya kimapinduzi. Katika makala hii tutaeleza japo kwa ufupi jinsi umuhimu wa maalim seif ulivyo kwa wazanzibari. Viongozi wote wengine wanazuka, wanakuwa maarufu na kupotea lakini sivyo kwa maalim seif ambae nyota yake inazidi kung'ara kila siku zikienda. Jambo hili linawatahayarisha na kuwaiaibisha wale wenye mawazo ya akina borafya wanaodhani ipo siku wanaweza wakamtusi maali seif akatukanika, wakamfedhehi akafedheheka, wakamkejeli akakejelika na wakamdharau akadharaulika.

Katika mwaka 1975 maalim seif akiwa katika kazi yake ya uwalimu hapo katika chuo cha uwalimu beit raas (sasa suza) alipokea taarifa kwamba anahitajika na rais aboud jumbe. Alishangaa sana kusikia wito wa rais kwani hakutarajia kabisa kama angejulikana au kuhitajika na rais siku moja. Baada ya kuwasili ikulu, rais aboud jumbe alimwambia maalim seif kwamba kuanzia siku hiyo atafanya kazi katika ofisi yake kama katibu msaidizi maalum (special assistant) wa rais. Hivyo ndivo rehema ya mungu ilivyomfikisha maalim seif ikulu ya zanzibar ndani ya zama za revolutionary justice. Hakuota, hakuwaza, hakujisogeza wala hakuomba.

Katika mwaka 1977 rais aboud jumbe aliamua kufanya mabadiliko ya baraza la mapinduzi. Kupitia mabadiliko hayo alimtangaza maalim seif pamoja na wenzake kuwa ni mawaziri wapya wateule wa smz yeye akiwa ni waziri wa elimu. Kufuatia mabadiliko hayo serikali ya aboud jumbe ikapata nuru. Ilitoa unafuu mkubwa kwa wananchi ukilinganisha na utawala wa karume uliotangulia. Baada ya mapinduzi wanafunzi hawakuweza kuendelea na maomo kwa mujibu wauwezo wao wa kupasi mitihani bali ilikuwa kwa kuzingatia makabila ya baba zao. Utaratibu uliotumika uliruhusu waafrika asilimia themanini (80%), waarabu asilimia kumi na tano (15%), wahindi asilimia nne (4%) na wakomoro asilimia moja (1%) kuendelea na masomo. Baada ya kuwa waziri maalim seif alimshauri jumbe kuubadilisha utaratibu huo na badala yake wanafunzi wachaguliwekuendelea na masomo kwa uwezo wao wa kupasi mitihani na sio makabila yao. Jumbe na seif walifanikiwa kufanya hivyo japokuwa walipambana na upinzani mkali wa seif bakari na natepe (burgess 2009).

Sambamba na hili maalim seif alifanya jitihada ya kuwatafutia wanafunzi wa kizanzibari nafasi maalum za kujiunga na chuo kikuu cha dar-es-salaam hata kama kiwango chao cha kufaulu kilikuwa chini ukilinganisha na wanafunzi wa tanzania bara kwa sababu kwamba zanzibar inatoa kiwango kidogo cha wanafunzi wanaokwenda katika elimu ya juu ukilinganisha na tanzania bara na kwa kuzingatia kwamba elimu ya juu ni suala la muungano. Maalim seif pia alimshauri jumbe nafasi za elimu ya juu baina ya wanafunzi wa pemba na unguja iwe kwa uwiano wa asilimia 40 – pemba na asilimia 60 – unguja. Kabla ya hapo kulikuwa na kiwango kikubwa cha ubaguzi katika kuchagua wanafunzi wa kujiunga na vyuo vikuu baina ya unguja na pemba kukiwa na upendeleo mkubwa kwa kisiwa cha unguja ili kujenga chuki baina ya watu wa unguja na pemba. Hata hivyo kutokana na asilimia kubwa (60) ya nafasi za unguja, wanafunzi kutoka unguja hawakuweza kujaza nafasi zao na hivyo nafasi hizo kukamilishwa na wanafunzi kutoka pemba (burgess 2009).

maalim-seif-564x423.jpg

makamo wa kwanza wa rais wa zanzibar na katibu mkuu wa cuf, malim seif sharif hamad

baada ya rais aboud jumbe kulazimishwa kujiuzulu, rais mpya ali hassan mwinyi aliingia madarakani. Mwinyi alimteua maalim seif kuwa waziri kiongozi wa serikali yake. Chini ya ushauri mzuri wa maalim seif zanzibar ilizidi kupata neema katika utawala wa mwinyi. Zanzibar ilirudisha matumizi ya paspoti ili kudhibiti uingiaji holela wa watu na hivyo basi mambo mengi ya udhia kama vile ujambazi, uhalifu, madawa ya kulevya na maradhi ya kuambukiza yaliweza kudhibitiwa. Upigaji watu kiholela na kuwaweka ndani mambo ambayo yalikuwa yakifanywa na youth league katika awamu zilizotangulia yaliondoshwa. Serikali mpya pia ikawashawishi vijana kusoma na kupatiwa nafasi za masomo nje ya nchi. Halkadhalika vijana wasomi wakashawishiwa kuomba nafasi za uongozi serikali bila ya kuzingatia makabila ya baba zao au mahusiano ya baba zao na u-hizbu, u-afro au ukomred kabla ilivyokuwa kabla (burgess 2009). Halkadhalika mwinyi na maalim seif walianzisha katiba mpya ya mwaka 1984 iliyoruhusu utawala wa sheria na mipaka ya madaraka kwa mihimili ya dola ambayo iliandikwa na mwanasheria mkuu wa serikali wa wakati huo ambe ni waziri wa katiba na sheria wa sasa, abuu bakar khamis bakar. Pia walianzisha mfumo mpya wa mahakama za kisheria na kufutilia mbali mahakama za wananchi zilizoanzishwa na karume ambazo zilikuwa zikiendeshwa kinyume na misingi ya sheria na haki. Haki za binaadamu katika katiba ya zanzibar zililingana zaidi na zile za umoja wa mataifa kuliko zile zilizokuwemo katika katiba ya jamhuri ya muungano.

Kwa kweli serikali ya mwinyi na maalim seif pamoja na kudumu kwa muda mfupi sana iliweza kuleta mabadiliko mengi. Mabadiliko mengine yalikuwa ni pamoja na uhuru wa wananchi kutoa maoni yao. Mambo mengi ambayo kwa njia moja au nyingine yalionekana kuwa ni ya kubana haki za raia ambayo yalikuja mara baada ya mapinduzi yalibadilishwa katika wakati huo. Vizuizi vingi vya kufaidi uhuru na haki za kiraia viliondolewa. Vyombo vya habari vya serikali vilitakiwa kuanzisha vipindi maalum vya kuwapa nafasi wananchi kutoa maoni yao juu ya uendeshaji wa nchi yao. Vipindi kama ‘zanzibar ni njema' katika radio ya zanzibar na ‘jicho' katika televisheni ya zanzibar (tvz) vilivyotoa fursa kwa wazanzibari kutoa maoni yao kuhusu uendeshaji na utendaji wa serikali yao vilianzishwa katika kipindi hicho.

Lakini kubwa zaidi katika utawala wa mwinyi na maalim seif ilikuwa ni kuruhusiwa biashara huria, yaani ‘trade liberalisation' hatua ambayo ilipelekea ghafla kubadilika kwa hali za maisha ya watu na kuimarika kwa uchumi na pato la taifa. Jambo hili lilimchukiza sana nyerere kwani ni kinyume na siasa yake ya ujamaa lakini mwinyi na seif walimjibu nyerere kuwa "tunataka kuuimarisha ujamaa kwa kutumia mfumo huria". Majibu hayo yalimpoza nyerere. Uhaba mkubwa wa chakula uliokuwepo kabla ulimalizika na umasikini ukapungua makali yake kwa kiwango kikubwa. Wafanya biashara kutoka nchi za jirani kama kenya na tanzania bara wakawa wanakuja zanzibar kutafuta bidhaa. Maisha ya watu yakaboreka na neema kutanda. Hapo ndipo mwinyi alipozaa msemo wake maarufu, zanzibar ni njema atakae aje na baadae msemo huu ukawa miongoni mwa maneno ya hekima.

Baada ya kifo cha edward sokoine, nyerere alimteua salim ahmed salim kuwa waziri mkuu mpya. Hivyo basi salim ahmed salim kwa upande wa jamhuri ya muungano alitarajiwa sana kuwa mrithi wa kiti cha urais baada ya kustaafu nyerere. Kwa upande wa zanzibar nako maalim seif alitarajiwa sana kurithi kiti cha urais baada ya mwinyi kumaliza muda wake. Upepo huo wa lisiasa haukuwa ukiwapungia vyema wanamapinduzi wa zanzibar. Hivyo basi wanamapinduzi hawakupendelea mabadiliko hayo kutokea na walifanya kila wawezalo kuubalisha upepo huo wa kisiasa ili salim ahmed salim kwa upande wa jamhuri ya muungano na maalim seif kwa upande wa zanzibar wasiweze kuwa marais wanaofuatia. Kosa la maalim seif lilikuwa ni upemba wake wakati salim ahmed alikuwa na makosa matatu. Kosa la kwanza ni uarabu, kosa la pili ni upemba kama maalim seif na kosa la tatu ni mwanachama wa zamani wa znp. Ijapokuwa nyerere na mwinyi walimuona salim ndiye anaefaa zaidi kuwa raisi wa jamhuri ya muungano lakini alipigwa vita na wanamapinduzi.

Nyerere kwa kuwatii wanamapinduzi akasitisha azma ya kumteua salim na badala yake kumteua mwinyi kuwa rais mpya wa jamhuri ya muungano. Kwa upande wa zanzibar majina matatu ya idri abdul-wakil, maalim seif na salmin amour ndio yaliojadiliwa na nec kuteua mmoja wao kuwa rais mpya baada ya mwinyi kupelekwa katika kiti cha urais wa jamhuri ya muungano. Mzee idris alikuwa wa mwanzo kuomba jina lake liondoshwe kutokana na uzee. Maalim seif alikuwa kijana na alijulikana zaidi katika chama, katika nec na wananchi wa unguja na pemba hivyo kulikuwa na kila aina ya uwezekano wa kushinda kura nyingi kulinganisha na idris abdul-wakil. Nec ilishangazwa sana kutangazwa ushindi wa idris abdulwakil. Hapana shaka wanamapinduzi waliingilia kati suala hilo na kumfanya nyerere kuchakachua matokeo ya kura ili kumpinga maalim seif na kumpitisha idris. Hapa ndipo wakati mgumu kwa siasa za zanzibar baada ya kuzaliwa ccm ulipoanza. Wazanzibari hawakufurahia mwinyi kupelekwa bara wala hawakufurahishwa na uteuzi wa idris na kuachwa maalim seif kwa kuwa idris hakujulikana vyema na wazanzibari. Takriban asilimia 80 ya wananchi wa pemba na asilimia 63 ya wanachi wa mkoa wa mjini maghrib unguja walimpigia idris kura ya "hapana" na hivyo kuzua mtafaruku mkubwa wa kisiasa. Baada ya wimbi la kukataliwa idris kutanda zanzibar na hivyo siasa za ccm kuwa ngumu mno nyerere alimshauri idris kumteua maalim seif kuwa waziri kiongozi.

Hata uteuzi huo wa waziri kiongozi haukuwafurahisha wanamapinduzi. Wao walitaka waziri kiongozi awe salmin amour. Hivyo basi wakazidisha na kuendeleza chuki na vita vyao dhidi ya maalim seif. Kila aina ya shutma na visingizio wakavitoa ili kumpotezea umaarufu maalim seif ndani ya chama na ndani ya serikali. Moja ya shutma zilizowahi kutolewa ni kuwadharau, kuwavunjia heshima na kuwadhalilisha wanamapinduzi, akina seif bakari. Shutma nyengine ni kutaka kurejesha usultani zanzibar. Katika kipindi hichi kuliimarika mahusiano ya kidiplomasia baina ya zanzibar na falme za kiarabu. Wanamapinduzi wakatumia fursa hiyo kutoa shutma kwamba maalim seif ana mipango wa kurejedisha utawala wa kisultani zanzibar. Katika ziara moja ya maalim seif nchini oman katika jitihada zake za kuiletea neema zanzibar, sultan qabous alisema wazi kwamba ana kila sababu ya kuisaidia zanzibar kwa kiwango kikubwa kwa kuwa ni wasomi wa kizanzibari ndio walioijenga oman bila ya serikali ya oman kuchangia chochote katika elimu zao (burgess 2009). Maalim seif na qabous kupitia ziara hiyo waliahidiana mambo mengi ya maendeleo kwa zanzibar kama vile ujenzi wa viwanja vya ndege, kutanua miradi ya maji na ujenzi wa barabara. Ahadi zote hizo zilibezwa, kupuuzwa na kuzuiliwa utekelezaji wake na wanamapinduzi.

Tuhuma nyengine dhidi ya maalim seif ni kuwapendelea wapemba. Maalim seif alituhumiwa kuwapendelea wapemba kwa ushauri wake wa mgao wa huduma na mipango ya maendeleo kwa asilimia 60- unguja na 40 – pemba. Baada ya tuhuma kadhaa wa kadhaa kushindikana kutumika kama sababu na visingizio vya kumtoa maalim seif katika wadhifa wake ikatumika shutuma ya kufanya upinzani ndani ya chama. Kupokonywa maalim seif uwaziri kiongozi kukawadia na habari zikazagaa kila upande. Mrithi wa nafasi maalim seif iliamuliwa kuwa dr omar ali juma ili kuwatuliza wapemba baada ya kitendo cha kutolea maalim seif. Hata hivyo dr omar aliposikia habari hizo haraka alifiki kwa maalim seif na kumwambia kwamba kuna habari kwamba unataka kutolewakatika nafasi yako na baadae nafasi nipewe mimi lakini mimi sitokubali nikijua ni kuwagawa wazanzibari na kujenga fitna. Tarehe 18 januari mwaka 1988 seif sharif akapokonywa wadhifa wa uwaziri kiongozi na dr omar ali juma akachaguliwa kuwa waziri mkuu mpya huku dr omar ali juma akifurahia na wala hakukataa kama alivyoahidi kabla.

Baada ya kitendo cha maalim seif kufukuzwa zanzibar haikuwa shuwari. Mengi yalizungumzwa, chama cha ccm kulaaniwa na kukataliwa, nyerere kuonekana ndie anaewagawa wazanzibari na muungano kushutumiwa. Matukio hayo yalimkera sana nyerere na ndipo alipolazimika kumfukuza maalim seif kabisa katika chama ili akose jukwaa la kufanyia siasa. Kikao cha nec kilichofuatia kilijadili tuhuma dhidi ya maalim seif na wenzake saba tuhuma dhidi ya seif na wote walitakiwa kujiuzulu nafasi zao katika chama ambapo baada ya wote kugoma kufanya hivyo nyerere akatamka mbele ya wajumbe wa nec "kama mmegoma kujiuzulu kwa nafasi niliyonayo nimekufukuzeni nyote katika chama". Maalim seif na wenzake walifukuzwa katika chama siku ya mwezi 27 ramadhani, kwa mujibu wa waislamu ni usiku wenye uwezekano mkubwa wa kupatikana lailatul-qadr.

baada ya maalim seif kutolewa serikalini na kufukuzwa katika chama wazanzibari wakaghadhibika mno. Watu makundi kwa makundi wakarudisha kadi za chama na wengine kuzichana. Wengine walitengeneza sanamu za nyerere hususan huko pemba na kuziharibu hadharani kuonyesha hasira zao. Mara tu maalim seif alipowasili kisiwani pemba kutokea dodoma makundi kwa makundi ya watu walikuwa wakikusanyika wakiwa na hamu na shauku ya kuzungumza nae. Nchi ilipooza na siasa za chama cha mapinduzi zanzibar zikakwama. Nyerere akahisi kwamba hata kuwa nje ya chama na serikali maalim seif ataendelea kuwa tishio kwa nchi na chama hivyo tuhuma kadhaa zikabuniwa ili kumtia gerezani. Serikali ilijaribu kwanza kutaka kumshtaki maalim seif kwa madai kuiba nyaraka za serikali lakini baada ya kushindwa kuthibitisha walimshtaki kwa kosa la kuitisha mikutano haramu. Seif alifungwa jela kwa kipindi cha miezi 30 kuanzia mwezi wa mei 1989 hadi mwezi wa novemba mwaka 1991. Jitihada mbali mbali zikachukuliwa za kidiplomasia, shirika la amnesty international na wasomi kudai seif sharif atolewe jela. Baada ya hapo akatolewa pamoja na masharti na vikwazo vingi. Pamoja na yote hayo bado maalim seif aliapa kutimiza ahadi yake ya kuwatetea wazanzibari kama alivyoahidi.

….itaendelea


huuu wote.....uliouandika ni utumbo....

1.hivi unajua ndiye aliyefanya fitina mpaka muanzilishi wa cuf james mapalala kufukuzwa ndani ya chama kisa mkristo.....
2.hivi unamkumbuka yeye ndio chanzo cha aboud jumbe.......kupata matatizoo

3.hivi unajua jamaa anabagua sana wakristo hata serikali ya umoja wa kitaifa baraza la mawazili hakuna mkristooo

4.hivi unajua wakati maalim seif yupo ndani gerezani familia yake ilikuwa inalelewa na hamadi rashidy halafu badae anakuja kumtimuaa hamad baada ya kuomba hata nafasi ya ukatibu.....

Siipendi ccm....ila naichukia cuf..kwa ubaguzi wake...wa kidini ni heri kura yangu nipige ccm japo siipendi...maana hamna ubaguzi wa dini wala kabila.....
 
Imeandikwa na Ahmed Omar Khamis


  • Akina Borafya ni simba walioshindwa kula nyama mbugani watakula buchani?


Kwa kauli yake Nyerere alikuwa akiumia kichwa sana na kukosa usingizi kutokana na kuwepo kwa nchi iitwayo Zanzibar pembeni ya nchi yake ya Tanganyika. Alitamka wazi wazi kwamba alitamani Zanzibar aididimize katika Bahari ya Hindi kama angeweza. Hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kulitekeleza hilo bila shaka lakini ambacho Nyerere alikusudia ni kuiondoa Zanzibar katika ramani ya dunia na aidhibiti kwa kuiweka ndani ya viganja vya mikono yake, ndani ya mamlaka yake, amri yake, uendeshaji wake, aipe atakacho na ainyime atakacho. Nyerere alianzisha vyema mradi wake huu kwa kulitumia vuguvugu la ukabila katika zama za kupigania uhuru lililoanzishwa na wakoloni kwa kulifanya mtaji wa kuwasambaratisha wazanzibari na kuwagawa mafungu ili azma yake itimie.

mimi mtanganyika, hii thread inahusu zanzibari. hainihusu kabsaaaaaa. pelekeni huko baharini.
 
huuu wote.....uliouandika ni utumbo....

1.hivi unajua ndiye aliyefanya fitina mpaka muanzilishi wa cuf james mapalala kufukuzwa ndani ya chama kisa mkristo.....
2.hivi unamkumbuka yeye ndio chanzo cha aboud jumbe.......kupata matatizoo

3.hivi unajua jamaa anabagua sana wakristo hata serikali ya umoja wa kitaifa baraza la mawazili hakuna mkristooo

4.hivi unajua wakati maalim seif yupo ndani gerezani familia yake ilikuwa inalelewa na hamadi rashidy halafu badae anakuja kumtimuaa hamad baada ya kuomba hata nafasi ya ukatibu.....

Siipendi ccm....ila naichukia cuf..kwa ubaguzi wake...wa kidini ni heri kura yangu nipige ccm japo siipendi...maana hamna ubaguzi wa dini wala kabila.....
zanzibar kuweka waziri mkristo ni sawa na marekani au uingereza au vatican au italy kuweka waziri muislamu....
zanzibar hakuna wazanzibari wakristo kuna watanganyika wakristo..na wakuja wakristo ..
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom