Elections 2010 Maalim Seif Makamu wa Rais Zanzibar

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Taarifa zilizotufikia zimeeleza kwamba, Rais wa Zanzibar, Dr Ali Mohamed Shein amemteua Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais, na Balozi Seif Idd kuwa Makamu wa Pili wa Rais.

============
Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu 39 (1),(2) na (3) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohammed Shein amemteua Mhe. Seif Sharif Hamad kuwa Makamo wa Kwaza wa Rais.

Taarifa fupi kutoka Ikulu ya Zanzibar kwa waandishi wa Habari, Dk Shein pia ametumia uwezo wake kwa mujibu wa kifungu 39(1),(2) na (6) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Kumteua Mhe. Balozi Seif Ali Iddi kuwa Makamo wa Pili wa Rais.

Uteuzi wa balozi Iddi ambao umeanza tarehe 09 Novemba, 2010 haukutarajiwa hasa baada ya kushinda kiti cha ubunge jimbo la Kitope kwa ticket ya CCM. Kabla ya kuteuliwa Seif Iddi alikuwa naibu waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa.
 
Seif ndie Raisi wa Zanzibar ,kwa wamjuao Shein wanamjua ni mtu wa aina gani so far Maalim Seif ni mwanasiasa aliekomaa ukilinganisha na Dr Shein ,kama ilikuwa ni game ya Chess ,CCM walikula queen na hapo ndipo CUF wakaweka Checkmate ,angalieni na tazameni ni namna gani Chess inachezwa na ndivyo ilivyokuwa kwa maalim Seif na Matokeo. Let us see,si hasha Dr Shein ikawa hata ofisini haendi kila kitu akamkabidhi makamo wake wa kwanza.
 
Mwiba, Muafaka unamtaka makamu wa pili wa Raisi kuwa ndiyo makamu mtendaji, makamu wa kwanza yupo yupo tu, na infact Raisi akitaka kumdismiss, anamdismiss tu.
 
Thubutu!ccm wajanja ww,katiba(fake)inasema makam wa pili ndio kiongzi wa serkli bungen na ndio anayekaimu pindi rais akisafiri,task ya huyu wa kwanza labda kufungua warsha,kongamano nk...anyway nae wacha afaidi kodi za maskini
 
Seif ndie Raisi wa Zanzibar ,kwa wamjuao Shein wanamjua ni mtu wa aina gani so far Maalim Seif ni mwanasiasa aliekomaa ukilinganisha na Dr Shein ,kama ilikuwa ni game ya Chess ,CCM walikula queen na hapo ndipo CUF wakaweka Checkmate ,angalieni na tazameni ni namna gani Chess inachezwa na ndivyo ilivyokuwa kwa maalim Seif na Matokeo. Let us see,si hasha Dr Shein ikawa hata ofisini haendi kila kitu akamkabidhi makamo wake wa kwanza.

Unanikumbusha mambo ya Kagame na Rais wake wakati huo akiwa Vice-President. He was more Powerful.
 
Amemteua au katiba ndiyo inasema hivyo kuwa mshindi wa pili ni lazima awe makamu wa kwanza wa rais. Huyo balozi ni nani by the way?????????
 
Unanikumbusha mambo ya Kagame na Rais wake wakati huo akiwa Vice-President. He was more Powerful.

Yes ,kumbe inawezekana na ndivyo hivyo itakavyokuwa ,Shein hana choyo ni mtu hodari sana sana ,na yeye kama Raisi anaweza kabisa akatumia tiketi yake hiyo ,serikali zetu hazifuati chochote ,just zinakwenda kiamri kama vile jeshini ,alie na cheo kikuu ndie wa kufuatwa.
 
Maalim Seif ndio kashapotezwa kisiasa.
2015 CUF watamsimamisha mtu mwingine ambaye sio maarufu na watamwagwa vibaya sana.
Hapo hakutokuwa na feva ya kuteuliwa makamu kutoka CUF coz CCM itakuwa imeshinda kihalali.
 
Ni wachache sana waliolielewa hili Game la CCM, Sheria ya Serikali ya umoja wa kitaifa, sio ya kudumu ni ya mpito tu na ndio maana haijapelekwa kwenye ngazi ya katiba mama ya Tanzania. Utaratibu huu unatumika pale siasa zinapokuwa tete ili kuweka mambo sawa na baadae huondolewa na mfumo wa kawaida hurudishwa pindi hali ya kisiasa inapoonekana imekuwa shwari.

Hali ya kisiasa inawezaje kuwa shwari?

1 Kiongozi alokuwa anasababisha huo utete kupoteza uwezo wa kisiasa au
2 Kufariki dunia au
3 Moja ya vyama shindani kuwa na uwezo wa kushinda kwa kishindo na hivyo kuunda serikali ya chama kimoja.

Sasa ukiangalia Siasa za ZNZ Maalim Seif ndio alikuwa tatizo kwa CCM, maana anachoamini yeye na wanaCUF nao wanaamini hicho hicho. Maalim amekuwa kama Mungu mtu ndani ya CUF. CCM wakatumia akili kuwa kama tutafanikiwa kumdhibiti Maalim basi CUF ZNZ kwishney.

Tizama akili hii ya CCM, Rais CCM, makamu wa pili ambae ndie kama waziri kiongozi CCM, na ndie anakaimu Urais pindi Rais akiwa hayupo. Wawakilishi wa CCM ni wengi kuliko wa CUF hivyo wanaweza kupitisha chochote watakachopenda. CUF watapewa wizara chache na bajeti zao zitaangaliwa kwa macho yote so hakuna hata chembe ya Ofisadi utakaowezekana kwenye wizara zao wakati huo huo utendaji wao utahakikishwa unakuwa under perfomance na hivyo kila mtu ataamini chini ya CUF nchi haitatawalika.

Uchaguzi mwingine uje niambie kama kuna CUF atakaepita.
 
Hii sasa ni kama Russia, Shein ni Medvedev na Maalim Seif Sharif Hamad ni Putin! Ndie atakayeongoza nchi ya Zanzibar!
 
Sasa nyie watanganyika muna khofu gani wakati shein mumemteua nyie na huyo balozi seif idi pia ni kibaraka wenu hapana jipya hapo mutaendelea tu kuitawala zanzibar.

Ama kuhusu cuf mwaka 2015 wanaweza kumsimamisha juma duni na akashinda kwa kishindo.
 
Ni wachache sana waliolielewa hili Game la CCM, Sheria ya Serikali ya umoja wa kitaifa, sio ya kudumu ni ya mpito tu na ndio maana haijapelekwa kwenye ngazi ya katiba mama ya Tanzania. Utaratibu huu unatumika pale siasa zinapokuwa tete ili kuweka mambo sawa na baadae huondolewa na mfumo wa kawaida hurudishwa pindi hali ya kisiasa inapoonekana imekuwa shwari.

Hali ya kisiasa inawezaje kuwa shwari?

1 Kiongozi alokuwa anasababisha huo utete kupoteza uwezo wa kisiasa au
2 Kufariki dunia au
3 Moja ya vyama shindani kuwa na uwezo wa kushinda kwa kishindo na hivyo kuunda serikali ya chama kimoja.

Sasa ukiangalia Siasa za ZNZ Maalim Seif ndio alikuwa tatizo kwa CCM, maana anachoamini yeye na wanaCUF nao wanaamini hicho hicho. Maalim amekuwa kama Mungu mtu ndani ya CUF. CCM wakatumia akili kuwa kama tutafanikiwa kumdhibiti Maalim basi CUF ZNZ kwishney.

Tizama akili hii ya CCM, Rais CCM, makamu wa pili ambae ndie kama waziri kiongozi CCM, na ndie anakaimu Urais pindi Rais akiwa hayupo. Wawakilishi wa CCM ni wengi kuliko wa CUF hivyo wanaweza kupitisha chochote watakachopenda. CUF watapewa wizara chache na bajeti zao zitaangaliwa kwa macho yote so hakuna hata chembe ya Ofisadi utakaowezekana kwenye wizara zao wakati huo huo utendaji wao utahakikishwa unakuwa under perfomance na hivyo kila mtu ataamini chini ya CUF nchi haitatawalika.

Uchaguzi mwingine uje niambie kama kuna CUF atakaepita.

cuf wanajua siasa wewe,cuf ina vichwa makinisasana naniwajanja kuliko unavyofikiria wewe,cuf hawakuanza siasa jana walajuzi kama chamachenu flani mlichokishabikia na kimebwagwa na ccm vibaya,subiri uone mambo ya cuf kaka,mwenye wifu wajinyonge,wazanzibari lao 1 watajenga nchiyao watatuacha cc wadanganyika kwenye mataa tukishangaa,subiri uione zenj yenye neema inayokuja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom