Maalim Seif: Hotuba ya Rais imesahau mambo muhimu ikiwemo Tume ya Uchaguzi na Haki za Binadamu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
0816dd82a447e302707a8ade65d49af8


Mwenyekiti wa chama cha ACT-Wazalendo Maalim Seif Hamad amesema amesikitishwa na hotuba ya kufungwa kwa Bunge la 11 iliyotolewana Rais John Magufuli leo Juni 16,2020 kwakua aliacha mambo ya msingi ambayo yanaliliwa na wananchi wa Tanzania

Akizungumza na wa mkutano wa chama cha ACT-Wazalendo mkoani Tanga, Maalim Seif amesema Rais ameongea vitu vingi lakini amesahau maswala ya msingi kama demokrasia, haki za binadamu pamoja na swala zima la tume huru ya uchaguzi

“Nimeisikia hotuba ya Rais John Magufuli ya kulifunga Bunge leo Juni 16, 2020 nasikitika sana amekwepa kuyazungumzia mambo matatu muhimu yanayolikumba Taifa letu Demokrasia na Haki za Binadamu, Tume Huru ya Uchaguzi na Uchumi imara kwa kila Mtanzania.” amesema

Ikumbukwe kuwa mapema leo Juni 16, 2020 Rais Magufuli alihutubia bunge la jamhuri ya Muungano kwa mara ya mwisho ikiwa ni kiashirilia cha kufikia ukomo kwa wabunge wote na kufungua njia za kuanza kwa uchaguzi wa madiwani , wabunge na rais mapema mwenzi Oktoba 2020
 
Seif Sharif Hamad anajitambua sana, ni mwanasiasa mkomavu haswa.
 
Hajasahau, bali hataki tume huru ya uchaguzi, maana anajua atapata tabu ya kupata % ya kura anazotaka kutangazwa mshindi.
 
Akishika nayeye madaraka atazungumzia hayo.. maana uanda ule kwa marekani wanademokrasia kiasi kwamba raia wanaachia makalio wazi kama njia ya kumtukana rais..!
 
Wabongo hatukosi nongwa saiv tumehamia kwenye tume huru
Ukiona kinazungumzwa ujue kina umuhimu wake.

NB. Mara zote mwamzi wa mechi ana nafasi kubwa Sana katika kuamua mchezo. Hivyo anapaswa kuwa mtu asiyetiliwa shaka. Maamzi yake yakitiliwa shaka, anaweza kuleta Taharuki.

So kuzungumza kuhusu Tume kipindi kama hiki si nongwa, bali kujaribu kuutafuta ukweli kama Refa anazo sifa za kuchezesha mechi kwa weledi, bila kuegemea kwa home team (CCM FC).

Aidha, kumbuka kwamba, Maalim ni muathirika wa Jecha-aliyejifanya kocha mchezaji wa CCM FC na kuipa ushindi kupitia bao la mkono.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom