Ustaadh
JF-Expert Member
- Oct 25, 2009
- 413
- 19
- Amekuwa anapigania 'haki na usawa' katika visiwa vya Zanzibar kwa miongo kadhaa.
- Keshakumbana na misukosuko kadhaa katika upiganaji wake
- Amekuwa anadai kila mara kuwa serikali ya CCM huwa inamuibia kura na yeye huwa ndiye mshindi halali katika chaguzi zote zilizopita isipokuwa wa mwaka huu.
- Amevumilia mengi na sasa kakubali kuwa na mashirikiano na CCM ili kuimarisha amani na mshikamano visiwani.
- Kuna wanaomkubali kwa 'ushujaa' wake na kuna wanaombeza kwa 'unafiki' wake.
- Vyovote iwavyo kasababisha mabadiliko visiwani......"kwa kiasi fulani" tunaweza kumfananisha na Mzee Nelson Mandela ingawa kwa mbali saaaana. Wewe unaonaje?