Maalim Seif Anaaminika?

jyfranca

JF-Expert Member
Oct 3, 2010
297
8
Upinzani si kupinga kila jambo - Seif

Thursday, 18 November 2010 19:53 newsroom



Na Esther Mvungi,Dodoma
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Seif Sharif Hamad, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF, amesema haina maana kwa chama cha siasa kupinga kila jambo. Amesema CUF kwa upande wa Tanzania Bara kinafanya kazi ya upinzani kwa ustaarabu na kuongeza: ìTutapinga kwa hoja na si kwa malumbano. Seif alisema hayo jana baada ya kuapishwa kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, katika sherehe zilizofanyika Ikulu Ndogo ya Chamwino. Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hoja inayotolewa na baadhi ya wananchi na vyama vya siasa kuwa, CUF si chama cha upinzani kwa kuwa kimo ndani ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
seif-sharif.jpg


Haina maana kama Zanzibar kuna maeleweno na upande wa pili wa Muungano iwe tofauti, tutafanya kazi zetu kistaarabu,î alisema Seif.
Alisema lengo la wote ni kuleta amani, hivyo CUF inataka yaliyotokea Zanzibar yahamie Bara.Seif alisema ni kweli kwa upande wa Zanzibar CUF si chama cha upinzani kwa kuwa kimo ndani ya serikali. CHADEMA imevitenga vyama vingine vya upinzani vya CUF, NCCR-Mageuzi na TLP katika kuunda kambi ya upinzani.Utengano kati ya vyama hivyo umekuwa ukijionyesha wazi bungeni, ambapo katika uchaguzi wa wajumbe wa Bunge la SADC-PF uliofanyika Jumanne wiki hii, wabunge wa CHADEMA walimdhihaki mgombea wa CUF.

Baada ya Injinia Mohammed Habib Mnyaa wa CUF kutangazwa mshindi katika kundi la vyama vya upinzani, wabunge wa CHADEMA walipiga kofi wakisema CCM, CCM.
 
Ingekua hajapewa Umakamu wa Rais angesema ivi? Ningemwamini Seif tuu iwapo angekubali matokeo 1995,2000 na 2005. Ila kwa mwaka huu kukubali kwake matokeo ni kwa kua kapewa ulaji. Seif hawezi kuwashambulia CHADEMA, kama CHADEMA nao wakipewa ulaji ndo tutajua kama Seif wapo wengi ila kwa sasa Seif katuangusha. Wote waliouawa kwa ajili ya kudai demokrasia Zanzibar walikua wanafanya ivyo kumpa Seif ulaji
 
huyu anapoongea hapo atakuwa na mkasi mfukoni! umakamu wa rais aliopewa kazi yake ni kufunga majengo mapya kwa kukata utepe

hana kingine kule zenj cha kufanya. yule makamu wa pili ndo jembe lenyewe lakini huyu hana kipya....

kaolewa na ccm kasahau kila kitu!!!!!!!!!
 
haya maridhiano yameimaliza CUF, kwishnee. sasa CUF huku bara lazima wajikombe kombe walau wapewe wizara moja. upinzani kwa kweli umebakia kwa CHADEMA tu. Kudhihirisha hayo jana wabunge wa UPINZANI WA KWELI walivyotoka tu nje ya ukumbi wa bunge basi wale wa UPINZANI B yaani CUF wakavamia vile viti vya mbele ili Mweshimiwa Rais awakumbuke wakati wa kuunda serikali.

Kumbukeni hawa hawa CUF wamempa ilani ya uchaguzi JK na kukubali matokeo wakati kulikuwa na kasoro nyingi mno. CUF kwisha kazi. CCM wameshawachakachua.
 
huyu kaka ni kichwa kweli mie namwamini sana lakini kwa hapa amechakachuliwa!anacheza na sisiem....walipoona wamemmaliza wakampa hiyo kazi butu
 
Ugali huooo! mzee sefu keshapiga lapa sanaaa lazima aseme kitu cha namna hiyo asije rudishwa kikijini, mnyamwezi ndiyo anatanga na njia hajui ni mpinzani au ni nini? CCM ni mabingwa wa kuchakachua mpaka chama cha CUF wamekichakachua? kilichobaki sasa ni kutajwa siku maalum kwa vyama vya CCM na CUF kuungana rasmi.
 
Upinzani si kupinga kila jambo - Seif

Thursday, 18 November 2010 19:53 newsroom



Na Esther Mvungi,Dodoma
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Seif Sharif Hamad, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF, amesema haina maana kwa chama cha siasa kupinga kila jambo. Amesema CUF kwa upande wa Tanzania Bara kinafanya kazi ya upinzani kwa ustaarabu na kuongeza: ìTutapinga kwa hoja na si kwa malumbano. Seif alisema hayo jana baada ya kuapishwa kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, katika sherehe zilizofanyika Ikulu Ndogo ya Chamwino. Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hoja inayotolewa na baadhi ya wananchi na vyama vya siasa kuwa, CUF si chama cha upinzani kwa kuwa kimo ndani ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
seif-sharif.jpg


Haina maana kama Zanzibar kuna maeleweno na upande wa pili wa Muungano iwe tofauti, tutafanya kazi zetu kistaarabu,î alisema Seif.
Alisema lengo la wote ni kuleta amani, hivyo CUF inataka yaliyotokea Zanzibar yahamie Bara.Seif alisema ni kweli kwa upande wa Zanzibar CUF si chama cha upinzani kwa kuwa kimo ndani ya serikali. CHADEMA imevitenga vyama vingine vya upinzani vya CUF, NCCR-Mageuzi na TLP katika kuunda kambi ya upinzani.Utengano kati ya vyama hivyo umekuwa ukijionyesha wazi bungeni, ambapo katika uchaguzi wa wajumbe wa Bunge la SADC-PF uliofanyika Jumanne wiki hii, wabunge wa CHADEMA walimdhihaki mgombea wa CUF.

Baada ya Injinia Mohammed Habib Mnyaa wa CUF kutangazwa mshindi katika kundi la vyama vya upinzani, wabunge wa CHADEMA walipiga kofi wakisema CCM, CCM.

Kupinga kwa hoja na kulumbana tofauti yake ni nini? Kwani kwenye malumbano huwa hakuna hoja? Yeye ndio kaishiwa hoja mpaka ameungana na CCM: ametimiza ule usemi "If you fail to conquer your enemy, join him/ her". Kwenye picha hii ndio anapinga kwa hoja sio?

DSC_1991.JPG
 
Wakati ndio utakaowafunza wale wote wanaowaona CUF wajinga na hatua wanazochukua sasa ni kushindwa!. Katika kazi yeyote unatakiwa uangalie marejeo ya kazi kama hiyo au inayofanana na hiyo ili ujifunze kutoka hapo. Bado Maalim Seif ni mtu anayeaminiwa na Wazanzibar kwa hatua aliyoifikisha Zanzibar. Kupambana na CCM (Majambazi, wauwaji, mafisadi,...) lazima ieleweke sio kitu rahisi, na hatua zifuatwe, tunaamini CUF haitakufa kwa hatua yao ya kukubali kupoteza ushindi wao na kuunda serikali ya umoja na CCM. Au memesahau kuwa CUF walishasusia vikao vya baraza la wawakilishi na mwisho wawakilishi wote wakafukuzwa kazi? na uchaguzi wa wawakilishi ukafanywa upya na CCM wakajaza mapengo?
"time will tell..."
 
Kupinga kwa hoja na kulumbana tofauti yake ni nini? Kwani kwenye malumbano huwa hakuna hoja? Yeye ndio kaishiwa hoja mpaka ameungana na CCM: ametimiza ule usemi "If you fail to conquer your enemy, join him/ her". Kwenye picha hii ndio anapinga kwa hoja sio?

DSC_1991.JPG

Naona Pinda aliwaletea kiwingu tu hapa maana pwani mtindo mmoja
 
Upinzani si kupinga kila jambo - Seif

Thursday, 18 November 2010 19:53 newsroom



Na Esther Mvungi,Dodoma
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Seif Sharif Hamad, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF, amesema haina maana kwa chama cha siasa kupinga kila jambo. Amesema CUF kwa upande wa Tanzania Bara kinafanya kazi ya upinzani kwa ustaarabu na kuongeza: ìTutapinga kwa hoja na si kwa malumbano. Seif alisema hayo jana baada ya kuapishwa kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, katika sherehe zilizofanyika Ikulu Ndogo ya Chamwino. Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hoja inayotolewa na baadhi ya wananchi na vyama vya siasa kuwa, CUF si chama cha upinzani kwa kuwa kimo ndani ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
seif-sharif.jpg


Haina maana kama Zanzibar kuna maeleweno na upande wa pili wa Muungano iwe tofauti, tutafanya kazi zetu kistaarabu,î alisema Seif.
Alisema lengo la wote ni kuleta amani, hivyo CUF inataka yaliyotokea Zanzibar yahamie Bara.Seif alisema ni kweli kwa upande wa Zanzibar CUF si chama cha upinzani kwa kuwa kimo ndani ya serikali. CHADEMA imevitenga vyama vingine vya upinzani vya CUF, NCCR-Mageuzi na TLP katika kuunda kambi ya upinzani.Utengano kati ya vyama hivyo umekuwa ukijionyesha wazi bungeni, ambapo katika uchaguzi wa wajumbe wa Bunge la SADC-PF uliofanyika Jumanne wiki hii, wabunge wa CHADEMA walimdhihaki mgombea wa CUF.

Baada ya Injinia Mohammed Habib Mnyaa wa CUF kutangazwa mshindi katika kundi la vyama vya upinzani, wabunge wa CHADEMA walipiga kofi wakisema CCM, CCM.
Hakuna mtu mbinafsi kama Seif. Ni hatari kushinda wasaliti. Yeye siku zote ametanguliza maslahi yake. Alimsaliti Mzee Aboud Jumbe mwaka 1984 katika kile kilichoitwa kuchafuka kwa hali ya hewa ya siasa Zanzibar. Alipokosa kuchaguliwa kugombea uraisi Zanzibar mwaka 1985 alifanya kampeni za chini chini dhidi ya Abdul Wakili. Marehemu Wakili akampa uwaziri kiongozi. Lakini kufikia Januari 1988 kumchimba kwake Wakili kulisababisha afukuzwe nafasi hiyo na CCM. Baada ya hapo akawekwa ndani aliyemtoa ndani ni Lamwai kupitia Mahakama ya Rufaa. Lakini ni Mahakama anayoipinga kwamba inaingilia mambo ya Zanzibar.

Katika mazungumzo ya muafaka ya kwanza alipigania kurudishiwa mafao yake ya Uwaziri Kiongozi. Je, imewahi kutokea mtu aliyefukuzwa kazi akapewa mafao? Hiyo ni kwa Seifu. Ni lazima watu tumpinge kwa nguvu zote na kuanika unafiki wake bila woga wowote ule.
 
huyu kaka ni kichwa kweli mie namwamini sana lakini kwa hapa amechakachuliwa!anacheza na sisiem....walipoona wamemmaliza wakampa hiyo kazi butu

JAmani naomba kuuliza, kwa kuwa Seif ni CUF na kesha lamba Dume, je Lipumba naye inakuwaje? inavyoonekana huu muafaka umegusa pia hata jamhuri ya muungano kama nilivyoshuhudia bungeni mbunge mmoja wa CUF akijitoa kwenye kinyanganyiro cha unaibu spika akidai kuna muafaka wa CUF na CCM, Je LIPUMBA naye itakuwaje?
 
Kupinga kwa hoja na kulumbana tofauti yake ni nini? Kwani kwenye malumbano huwa hakuna hoja? Yeye ndio kaishiwa hoja mpaka ameungana na CCM: ametimiza ule usemi "If you fail to conquer your enemy, join him/ her". Kwenye picha hii ndio anapinga kwa hoja sio?

DSC_1991.JPG
Hii picha inatoa somo kubwa sana, Wazanzibar 4, wabara 2. Zanzibar ni kama wilaya 1 ya Dar es salaam na ina makamu wawili wa Rais, Rais wake na ina makamu wa Rais wa Muungano, hapa wanajipa madaraka tuu, hakuna cha kuongoza wala nini. Mwone Seif alivyotulia, raha tupu, waliokua wanambeba sasa wanazidi kuumia. Tusubiri tuu 2015
 
CUF wamesahau mapambano waliyopitia kwa vile sasa hivi kuna shibe ya muda,ndio maana utaona wanapingana sana na chadema ni wivu na kigeugeu tu.Cheo alichopewa Seif ni kanyaboya tu hana makali yoyote kama ataridhika na kula pepo ndio usaliti mkubwa sana na ndio mwelekeo anaotuonyesha sasa hivyo CCM na CUF huoni tofauti na ndio kumezwa kwa CUF.Chadema waendelee kupigana kwani wanaeleweka wanachopigania asiyeelewa kataka kutokuelewa au wanawabeza kwa sababu za kisiasa tu.Nchi hii inahitaji ukombozi wa kweli,anayeweza kwa sasa ni Chadema
 
Maalim wewe umejiunga na CCM, si ni nyie Cuf mliokuwa mnaitwa magaidi ama sio nyie?!! leo hii wewe umegeuka unasema kutoka nje sio ustarabu loh! yaani nyie CUF ni wanafiki wakubwa sana. mlikua mnataka madaraka basi.

Kwa taarifa hicho cheo ni sanaa tu wewe makamu wa kwanza huna lolote zaidi ya magari na posho za serikali basi. huwezi kumwajibisha mtu kazi wala huna uamuzi wowote nini kifanyike ama kisifanyike katika serikali hiyo. soma vizuri katiba uone nguvu ziko kwa makamu wa pili.
 
....Ndugu zanguni naomba 2we waelewa,naona fikra zetu,akili zetu zimetawaliwa na ushabiki tuu,inaelekea nyinyi ndugu zetu si wa-Tanzania wenye kupenda amani na utulivu.Maalim Seif Anaaminika tena sana,hakuna mwana siasa yoyote wa kipindi hichi anaoweza kumfikia Maalim Seif ktk harakati za siasa ya vyama vingi,aliosema Maalim na yale maoni aliotoa Mh. Hamad Rashid pale Dodoma ni ya kweli kabisa kua Chama cha Chadema kuna mambo jifunzeni kwa wenzenu CUF,chadema wasikurupuke tu.Cha ajabu na kushangaza Chama cha Chadema kina viongozi shupavu,makini yaani hawana mfano,kiasi ambacho hata leo kwenye vyombo vya habari tumemsikia naibu katibu mkuu wa chadema akikiri ndani ya nafsi yake kua kwa maadili yetu ya Ki-Tanzania haikua sahihi wala heshima kwa waheshimiwa wabunge wa chadema kutoka ukumbini wakati Mh Rais alipoanza kuhutubia.Lkn yote kwa yote Jamani hebu tumpeni Maalim Sief haki yake,tusijaribu kumbeza,tujaribu kua na utamaduni wa kukubali ukweli ingawa UNAUMA
 
Maalim Seif siku zote anachotaka madaraka, angekua muungwana asingekataa uchaguzi 95,200,2005 na kama asingepewa cheo angekubali cheo?
 
[h=2]Ukweli kUhusu Mgogoro wa Seif na Hamad Rashid CUF[/h]
Nimefuatilia makoa mkuu ya CUF nikagundua kuwa hali ni tete kwani kuna makundi Moja ni la Hamadi Rashid na Jingine ni la Maalim Seif Na kwamba makosa aliyofanya Seifu yamewagusa wengi na hapana Shaka kwamba ameanza kuyarekebisha!!!

Moja ya Mambo ambayo yamekuwa kero kubwa ni suala la pesa ambapo Mgao wa pesa za operations za Makao makuu zilikuwa hazipo Wakati kule Pemba wanatanua kwa kutumia fedha za serikali.

Julius Mtatilo aliwahi kuongea na gazeti la Sema Usikike akaelezea ukata wa fedha ambapo analazimika kutumia fedha zake Mwenyewe kwa ajili ya shughuri za Chama !!!

Mtatilo aliwahi kulalamika kwamba Ruzuku imechelewa lakini ukweli ni kwamba hata Ruzuku hiyo ilipotolewa ilikuwa haipelekwi Wilayani kama sheria inavyotaka!!

Mtu wa karibu na ofisi ya Uhasibu anasema Juzi tu baada ya Hamadi Rashidi kuelezea nia ya kugombea nafasi ya Katibu Mkuu ndipo Maalimu Seif akaamuru pesa zipelekwe kwenye Wilaya 1oo na kila Wilaya imepelekewa 300,000/= katika awamu ya kwanza na Fungu lililotengwa ni Tshs 180m kwa miezi 6.

Baadhi ya maofisa wa makao Makuu CUF wanalalamika kuwa ni kwa nini fedha zote hizo zilikuwa hazipelekwi mpaka watu walalamike??

Mjumbe Mmoja wa Baraza kuu kutoka Pemba anasema Maalimu Seif anatafuta njia za kumufukuza Hamad Rashid na jana aliitisha kikao cha siri Pemba na kufanya njama za kuandaa kashifa za Hamad Rashid lakini Watu waliokinyume na sef Pemba wakafichua uovu huo!!!

Mpaka sasa Cuf kimekuwa chama cha kuwindana!!!
Maalimu hataki Uchaguzi ufanyike na sasa anataka atoe urithi jambo ambalo halikubaliki!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom