Maalim Seif amsifu Rais Karume kwa mafanikio

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Maalim Seif amsifu Rais Karume kwa mafanikio

Habari Zinazoshabihiana


Na Ali Suleiman, Zanzibar

KATIBU Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, amesema suluhisho la matatizo ya Zanzibar ni wananchi kumaliza tofauti zao na kuweka pembeni chuki na uhasama.

Maalim Seif alisema hayo juzi katika ukumbi wa Baraza la Idd katika Jamat-Khan mjini hapa, alipozungumza na wananchi na wafuasi wa chama hicho.

"Wazanzibari kama kweli tunahitaji umoja na utulivu, basi kwanza tunatakiwa kuondosha tofauti za kisiasa...chuki na uhasama, zisipewe nafasi kutawala nyoyo zetu," alisema Maalim Seif.

Alisema yamekuwapo mafanikio makubwa katika kipindi cha Serikali ya Rais Amani Abeid Karume, ambapo wafadhili wamerudisha misaada yao na hiyo yote ni matokeo ya kuwapo mshikamano.

Alisema wapo watu hawataki kubadilika na wanaamini, kwamba chuki na fitina ndiyo njia pekee ya kufanikiwa na kutekeleza matakwa yao.

Maalim, Seif alieleza kufurahishwa kwake na kuwapo chakula katika kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, hali ambayo inaonekana wazi wakulima kujitahidi katika kilimo.

Alisifu wakulima wa kisiwa cha Pemba kwa kuzalisha chakula kwa wingi na ziada yake kutumika Unguja na mikoa mengine ya Tanzania Bara.

"Wakulima katika kisiwa cha Unguja, wanatakiwa kuimarisha shughuli za kilimo ili kufikia malengo ya kujitosheleza kwa chakula, kama ilivyo kwa upande wa Pemba," alisema Maalim Seif.

Katika Mwezi wa Ramadhan, chakula zikiwamo ndizi na muhogo, kilifurika kwa wingi Unguja kutoka Pemba.


source majira
 
damn pipo, hata kutoa props pale mnapohitaji hamuwezi kufanya hivyo, kazi kutoa lawama ! mpeni props karume bana !

Hongera karume jr !
 
Alisema yamekuwapo mafanikio makubwa katika kipindi cha Serikali ya Rais Amani Abeid Karume, ambapo wafadhili wamerudisha misaada yao na hiyo yote ni matokeo ya kuwapo mshikamano.

Huyu jamaa naona safari yake ya kurejea sisiemu inawadia. Anyway, anaruhusiwa, katiba inamruhusu.
 
jembe liitwe jembe, na pauri liitwe pauro na kijiko kiitwe kijikop, karume kajitahidi sana.

na ntafurahi zaidi kabla hajaondoka kuweza kuweka misingi ya kuwepo serikali ya kitaifa hapo zenji, basi hatutamsahau maisha
 
lakini watu binadamu hawataki kukubali hilo kwamba jamaa kafanya vizuri, unajua viongozi wetu wanapofanya vizuri wengine hujisikia vibaya maana kazi yao ni always kuona failures katika serikali yetu !

Hongera karume !
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom