Maalim Seif amkejeli Yusuf Makamba

Sokomoko

JF-Expert Member
Mar 29, 2008
1,915
127
Maalim Seif amkejeli Yusuf Makamba
Na Salma Said, Zanzibar


KATIBU Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad amesema anajisifia nafasi yake ya ukatibu mkuu katika chama chake kutokana na kuheshimiwa maamuzi yake tofauti na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yussuf Makamba, ambaye hana maamuzi katika chama chake.



Seif aliitoa kauli hiyo juzi katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Demokrasia Mkoa wa Mjini Magharibi alipokuwa akiwahutubia wanachama na wapenzi wa CUF baada ya maandamano makubwa ya kupinga maamuzi yaliotolewa na CCM kuhusiana na mazungumzo ya muafaka Visiwani Zanzibar baina ya vyama vyao.


"Mimi najisifu kuwa kweli ni katibu mkuu, ninaposema ninasikilizwa na maamuzi yangu yanaheshimiwa na viongozi wote lakini wewe Makamba kwa nini unakubali kuchezewa chezewa," alisema na kuongeza: "Ikiwa saini yako haina nguvu unaambiwa basi hata hicho cheo chako hakithaminiwi katika chama chako."


Kauli hiyo ya Maalim Seif ilikolezwa na bango lililokuwa limewekwa mbele ya mkutano likiwa limebeba ujumbe uliofanana na matamshi hayo ya katibu mkuu wa CUF kuhusu nafasi ya uu ya Katibu Mkuu wa CCM katika chama chake.


"Ikiwa Makamba wewe hujielewi ni nani basi Seif ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF)," alisema na kuongeza: "Kiongozi mzuri na mwenye upeo na mwenye kusikiliza na kusikilizwa na kuheshimiwa mawazo yake na yeye kuheshimu na wengine lakini sio kiongozi kudharauliwa na hata watu wa chini yake.



"Mimi hao kina Jussa, Hamad Rashid, wabunge na wengine ni wakubwa lakini wanaheshimu ninachozungumza. Inakuwaje wewe huheshimiwi?" alihoji Maalim Seif na kuwaambia

wanachama wake kwamba anakumbuka alipokuwa mwanachama wa CCM chini ya mwenyekiti wake, Mwalimu Julius Nyerere,

jinsi vikao vilivyoendeshwa na kuwa mwenyekiti alipotaka jambo hakuna aliyepinga.



Alisema leo hii ndani ya CCM kiongozi wake anapozungumza na kutoa maamuzi wanachama wanashindwa kuheshimu vikao na hakuna thamani ya kiongozi mkuu wa chama kama ilivyotokea kwa Rais jakaya Kikwete kuyumbishwa na vikao vyake.



"Nilikuwa CCM, najua mwenyekiti akitaka jambo, lakini leo Kikwete anayumbishwa na wahafidhina wachache eti kwa kisingizio cha kulinda Mapinduzi. Ni hoja za kibumbavu kabisa," alisema Maalim Seif.



Seif alisema viongozi wa Serikali ya Zanzibar wana hoja za kitoto za kwamba atakapoingia madarakani huenda akawafunika serikali nzima kutokana na rekodi yake ya utendaji kazi.

Source: Mwananchi




Makamba hajiamini sio kwamakusudi ila nikweli cheo chake ni kikubwa yaani hakiwezi. Huku nyuma watu walipiga sana kelel kuwa Makamba hauwezi ukatu mkuu wa CCM lakini tuliona jinsi alivyo wachekesha kina Kikwete mbele ya NEC wakati wakiteuliwa kina Msekwa. Kwa kuwa Mwenyekiti wao ni mtu wa kupenda kucheka cheka naona ndio maana amemweka mchekeshaji mhe mgosi wa ndima Yusuph Makamba. Hawa watu wanafanya hivi kwakuwa hapo serious na masuala ya nchi. Kucheka na vichekesho ni moja ya sanaa na wao ni wasanii. Mpo hapo wanaCUF?
 
Chama Cha Mapinduzi kimejenga chini ya katiba yake na miongozo, na sio chama cha mtu mmoja ama wawili.

Kazi ya Katibu Mkuu ilikuwa ni kuchukua yale yote toka kwenye mikutano ya muafaka na kuyapeleka katika kikao kinachohusika na maamuzi ya chama. Kikao hicho ni Halmshauri Kuu ya Chama.

Kimsingi ametekeleza wajibu wake vizuri na anastahili pongezi kwa hilo. CUF inajulikana kwa kutokua na mfumo wa kichama, kipo kipo kama genge la kihuni. Na Maalimu Seif aliliona hilo mapema ndio maana hata akaamua kuachana na cheo cha Makamu mwenyekiti wa CUF, ili mradi aweze kukiburuza chama kwa kigezo cha ukatibu Mkuu...
 
Zanzibar CCM ina nguvu kubwa kwenye mambo yanayohusu zanazibar ndo maana hata kabla ya mwafaka kuongelewa na CCM nilisema hakutakuwa na serikali ya mseto zanzibar hata siku moja, kuna mahafidhina ambao kwa matakwa yao kusingekuwa na kitu kinachoitwa upinzani zanzibar na hivyo hawawezi kukubali hoja yeyote kutoka upinzani.
CCM bara imeshika makali ndio maana hawawezi kuwaamulia mambo yanayohusu zanzibar unless wakubali kuwa CCM ni moja. lakini ninajua ni kwamba kuna CCM mbili zenye maamuzi sawa.
 
Chama Cha Mapinduzi kimejenga chini ya katiba yake na miongozo, na sio chama cha mtu mmoja ama wawili.

Kazi ya Katibu Mkuu ilikuwa ni kuchukua yale yote toka kwenye mikutano ya muafaka na kuyapeleka katika kikao kinachohusika na maamuzi ya chama. Kikao hicho ni Halmshauri Kuu ya Chama.

Kimsingi ametekeleza wajibu wake vizuri na anastahili pongezi kwa hilo. CUF inajulikana kwa kutokua na mfumo wa kichama, kipo kipo kama genge la kihuni. Na Maalimu Seif aliliona hilo mapema ndio maana hata akaamua kuachana na cheo cha Makamu mwenyekiti wa CUF, ili mradi aweze kukiburuza chama kwa kigezo cha ukatibu Mkuu...

..you are wrong and totally wrong. i once asked you the meaning of chama, na kama CUF ni chama cha magenge mbona hakijafutwa?
 
..you are wrong and totally wrong. i once asked you the meaning of chama, na kama CUF ni chama cha magenge mbona hakijafutwa?
CUF iliyosajiliwa katika ofisi ya vyama sio hii ambayo katibu wake Mkuu ni Maalim Seif...

Kila kitu kilichotakiwa wakati wa usajili kwa sasa vimewekwa kando, labda vitakuja tumika tena mara baada ya Seif kutoka katika chama hicho...
 
"Mimi najisifu kuwa kweli ni katibu mkuu, ninaposema ninasikilizwa na maamuzi yangu yanaheshimiwa na viongozi wote lakini...."

Kwa maneno mengine atakachoamua Maalim ndicho hicho hicho... Ni nini maana ya kuwa na chama ipawo uwamuzi ni wa mtu mmoja tu..?
Hii ni zaidi ya uhuni.
 
CUF iliyosajiliwa katika ofisi ya vyama sio hii ambayo katibu wake Mkuu ni Maalim Seif...

Kila kitu kilichotakiwa wakati wa usajili kwa sasa vimewekwa kando, labda vitakuja tumika tena mara baada ya Seif kutoka katika chama hicho...

Inaonekana kwako wewe kilichosajiliwa kwa ajili ya ccm ni ufisadi na wizi kama inavyofanyika sasa hivi. Hivi viongozi wa ccm wanapata faida gani wapemba wakiuwawa na polisi na jeshi kila baada ya chaguzi huko visiwani?
 
Kwa maneno mengine atakachoamua Maalim ndicho hicho hicho... Ni nini maana ya kuwa na chama ipawo uwamuzi ni wa mtu mmoja tu..?
Hii ni zaidi ya uhuni.

lakini wengi hawaoni hilo mzee ! na wakati ndio huu, kutolea wapinzani uchwara uvivu !
 
lakini wengi hawaoni hilo mzee ! na wakati ndio huu, kutolea wapinzani uchwara uvivu !

Tukisema mmetumwa nabisha! hivi CUF na CCM au CUF na CHADEMA au CCM na SAU kipi chama? na kipi genge la wahuni?wahujumu uchumi?wezi?waongo?na majina mengi mabaya? badilikeni mme elimishwa muelimishe sio mpotoshe!
 
Maalim Seif, I said and repeating that wewe ni Dikteta, na Kwa hakika nimekulinganisha na Marehemu Jonas Savimbi.

Unatoa mfano wa Nyerere nani asiyejua kwamba Nyerere alikuwa na Kaudikteta kake nako ndiko kalikoifikisha nchi hapa ilipo!!!

Kwa mfumo wa Vyama vyetu katibu mkuu si wa kuamua mambo kama ufanyavyo wewe~!!!
 
Inaonekana kwako wewe kilichosajiliwa kwa ajili ya ccm ni ufisadi na wizi kama inavyofanyika sasa hivi. Hivi viongozi wa ccm wanapata faida gani wapemba wakiuwawa na polisi na jeshi kila baada ya chaguzi huko visiwani?
Mdada Taratibu, maana hata hao Chadema kuna wakati uburuzwa vilevile na hii inaondoa maana halisi ya chama na maamuzi yake. Rudi kwenye mada hii na uelewe ni nini kinazungumzwa hapa.

Hao Wapemba wasingepuuza amri halali ya serikali yasingewakuta hayo. Kumbuka kuwa wao walianza fujo hizo kwa kuvamia vituo vya polisi na kupora silaha. Sasa watu wa aina hiyo utawaitaje?
 
Mdada Taratibu, maana hata hao Chadema kuna wakati uburuzwa vilevile na hii inaondoa maana halisi ya chama na maamuzi yake. Rudi kwenye mada hii na uelewe ni nini kinazungumzwa hapa.

Hao Wapemba wasingepuuza amri halali ya serikali yasingewakuta hayo. Kumbuka kuwa wao walianza fujo hizo kwa kuvamia vituo vya polisi na kupora silaha. Sasa watu wa aina hiyo utawaitaje?

Nimeuliza swali kuwa ccm wanafurahia nini kuona damu ya wapemba ikimwagika?
 
Nimeuliza swali kuwa ccm wanafurahia nini kuona damu ya wapemba ikimwagika?

Naona unasoma mbio mbio, jibu nimeshakupa na ni hili hapa: "Hao Wapemba wasingepuuza amri halali ya serikali yasingewakuta hayo. Kumbuka kuwa wao walianza fujo hizo kwa kuvamia vituo vya polisi na kupora silaha. Sasa watu wa aina hiyo utawaitaje?"
 
Mdada Taratibu, maana hata hao Chadema kuna wakati uburuzwa vilevile na hii inaondoa maana halisi ya chama na maamuzi yake. Rudi kwenye mada hii na uelewe ni nini kinazungumzwa hapa.

Hao Wapemba wasingepuuza amri halali ya serikali yasingewakuta hayo. Kumbuka kuwa wao walianza fujo hizo kwa kuvamia vituo vya polisi na kupora silaha. Sasa watu wa aina hiyo utawaitaje?

Kaka Amri nyingine sio Halali hata kama zimetolewa na serikali, amri ya kuua raia hata kama imetolewa na nani si halali ndo maana tunaangaika ili kufuta adhabu ya kifo kwa maana sio halali, mbona CCM wenyewe wanalijua hili kuwa amri nyingine si halali soma thread ya watu wa Tabata Dampo utagundua kuwa hata wao wanakubali kuwa amri nyingine si halali.
 
Naona unasoma mbio mbio, jibu nimeshakupa na ni hili hapa: "Hao Wapemba wasingepuuza amri halali ya serikali yasingewakuta hayo. Kumbuka kuwa wao walianza fujo hizo kwa kuvamia vituo vya polisi na kupora silaha. Sasa watu wa aina hiyo utawaitaje?"

Picha zilizoonyeshwa kwenye TV nyumbani zilionyesha raia wasio na hatia wakipigwa risasi na kufa. Hawakuwa na silaha wala chochote chenye mfano huu. Katika hili tafuta sababu nyingine kwa nini ccm wanafurahia damu ya wapemba kumwagika?
 
Kaka Amri nyingine sio Halali hata kama zimetolewa na serikali, amri ya kuua raia hata kama imetolewa na nani si halali ndo maana tunaangaika ili kufuta adhabu ya kifo kwa maana sio halali, mbona CCM wenyewe wanalijua hili kuwa amri nyingine si halali soma thread ya watu wa Tabata Dampo utagundua kuwa hata wao wanakubali kuwa amri nyingine si halali.
Kamanda,
Tatizo la Tabata sio sawa kabisa na yale yaliyotokea huko Zenj. Hapa naona tukumbushane juu ya uhuni wa CUF tokea kuanza kwa mfumo huu wa vyama vingi. Wamekuwa wakitoa amri mbalimbali kwa wanachama wao zenye nia ya kuhatarisha maisha ya watu wengine. Hii ikiwa ni pamoja na kuwaambia wanachama wao kupigana na polisi. Inapofika hatua kama hii unategemea nini kifanyike?

Tabata kilichokosewa ni kutofuata taratibu za kisheria ikiwa ni pamoja na kutolewa notisi kwa wahusika ambayo inawapa muda ya kuvunja nyumba zao au kujitetea kwa nini nyumba hizo zisivunjwe katika muda uliotolewa katika notisi. Ndio maana uvunjaji ule haukuwa halali.
 
Kamanda,
Tatizo la Tabata sio sawa kabisa na yale yaliyotokea huko Zenj. Hapa naona tukumbushane juu ya uhuni wa CUF tokea kuanza kwa mfumo huu wa vyama vingi. Wamekuwa wakitoa amri mbalimbali kwa wanachama wao zenye nia ya kuhatarisha maisha ya watu wengine. Hii ikiwa ni pamoja na kuwaambia wanachama wao kupigana na polisi. Inapofika hatua kama hii unategemea nini kifanyike?

Tabata kilichokosewa ni kutofuata taratibu za kisheria ikiwa ni pamoja na kutolewa notisi kwa wahusika ambayo inawapa muda ya kuvunja nyumba zao au kujitetea kwa nini nyumba hizo zisivunjwe katika muda uliotolewa katika notisi. Ndio maana uvunjaji ule haukuwa halali.

Kibunango wewe kweli kiboko! Yale mauaji ya 2001 unadai yalitokana na wapemba kukaidi amri ya halali ya serikali?Serikali ipi wakati ZNZ hakuna Serikali tangu 1995?Amri halali hutolewa na Serikali halali Serikali iliyopo madarakani ZNZ (Zanzibar Nzuri Zamani) sio Serikali halali. Wao wenyewe wanasema kuwa "msipo tuchagua tunachukua tunaweka waaa" Mhe Karume alishawahi kusema "hata msipo nipigia kura kura yangu na ya shadya inatosha kunirudisha ikulu" hizo ndio siasa za Zanzibar yaani ukisikia Mapinduzi Daima ndio hayo wanashinda wengine wengine kazi yao kupindua.
 
Kibunango wewe kweli kiboko! Yale mauaji ya 2001 unadai yalitokana na wapemba kukaidi amri ya halali ya serikali?Serikali ipi wakati ZNZ hakuna Serikali tangu 1995?Amri halali hutolewa na Serikali halali Serikali iliyopo madarakani ZNZ (Zanzibar Nzuri Zamani) sio Serikali halali. Wao wenyewe wanasema kuwa "msipo tuchagua tunachukua tunaweka waaa" Mhe Karume alishawahi kusema "hata msipo nipigia kura kura yangu na ya shadya inatosha kunirudisha ikulu" hizo ndio siasa za Zanzibar yaani ukisikia Mapinduzi Daima ndio hayo wanashinda wengine wengine kazi yao kupindua.
Kimsingi umekubali kuwa unaposhindwa kutii amri halali ya Polisi unajua nini kinafuata na mbaya zaidi pale unapovamia kituo cha polisi najua fika kuwa unafahamu kuwa na polisi watajihami. Zaidi naona unaleta zile hadithi za kwenye Bar'za za kahawa na Masikani.
 
Kimsingi umekubali kuwa unaposhindwa kutii amri halali ya Polisi unajua nini kinafuata na mbaya zaidi pale unapovamia kituo cha polisi najua fika kuwa unafahamu kuwa na polisi watajihami. Zaidi naona unaleta zile hadithi za kwenye Bar'za za kahawa na Masikani.

Police haruhusiwi kuua eti kwa sababu ujafuata amri yake ndo maana tuna polisi wanashitakiwa iwapo mhalifu anafia mikononi mwake, haki ya binadamu kwanza kabla ya yote, hivi unaweza kueleza kwanini walizuiwa kuandama siku ile mbona juzi wameruhusiwa na hakuna fujo iliyotokea, sometimes wanakuwa provoked, sijawahi kukaa visiwani lakini maisha ya kule ni jino kwa jino na jicho kwa jicho no maana wanaamua kuandamana wapeni ruhusa.

Mwalimu aliiambia serikali ya mwinyi wakati wanazuia watu kumbeba Mchungaji mwitikira "Mwacheni abebwe kama anataka kubebwa kama maiti" thats what happened na walipomwacha hakuna watu walijotokeza kumbeba
 
Kwa maneno mengine atakachoamua Maalim ndicho hicho hicho... Ni nini maana ya kuwa na chama ipawo uwamuzi ni wa mtu mmoja tu..?
Hii ni zaidi ya uhuni.

read between the lines man!!A leader is the person with authority and in that case si kila kitu kinaamuliwa na wanachama wote, hiyo itakuwa ni baraza la wapiga soga,a leader is the one to provide the ones led with visions ndo maana Shariff akatamka maneno hayo, however democracy inafuata kwenye certain issues ambazo zinahitaji executive decisions! unanikumbusha mambo ya Simba na Yanga, wanachama wake wanavyofikiri kuwa watakuwa involved kwenye kila kitu hata jambo dogo tu!! Trust your leader and use democracy appropriately. Makamba ni clown of the CCM, we kumbuka watu kama Kawawa au Kolimba walipokuwa makatibu wakuu walivyokuwa wanaheshimika!!!Makamba ni kama muuza kahawa tu wa pale Ilala! Ni kioja, shule muhimu to some extent wajameni
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom