Maalim Seif amakinike na Zitto

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,632
697,606
Yaliyokwisha tokea yametokea... Yaliyokwisha jiri yamejiri.... Sasa vumbi linaelekea kutulia japo ni kama kuna chokochoko mpya inatafutwa na hapa hatafutwi mwingine bali Maalim Seif aliyekuwa katibu mkuu wa CUF.. Hatafutwi Zitto bali wafuasi waaminifu wanayemfuata Maalim Seif popote... ACT-Wazalendo ni self styled political party.... Kwenye siasa za Tanzania hakina impact kubwa zaidi ya mwenyekiti wake anayetoa matamko ya mara kwa mara....!
CUF ni mziki mwingine kabisa ni next level na kwenye siasa za Tanzania CUF ina impact kubwa sana....
Impacts za hivi vyama viwili vya siasa inaletwa na viongozi wake.. Seif ni mkongwe wa siasa za ccm na upinzani...Amewahi kuwa mpaka Waziri kiongozi, amekaa kizuizini kwa kesi ya uhaini....kesi isiyo na dhamama... Dhamira mtazamo, maono na maamuzi yake viko wazi sana... Ama dhamira moja na uamuzi mmoja... Na akiamua ameamua HATETEREKI na ndio maana anaaminika na wafuasi wake.... Amepitia kash kash nyingi za kisiasa, mafanikio na kuanguka pia.. Lakini hajawahi kuyumba wala kuyumbishwa.... Ni jasiri hata kwa hulka...

Zitto kidogo ni tofauti kabisa na Maalim... Hupenda kujijenga binafsi... Hana misimamamo thabiti na ni mwepesi kuyumbishwa ana kununuliwa... Safari yake kisiasa kwa miaka michache imekuwa na tongotongo nyingi lakini kubwa ni pale alipotaka kukihujumu chama chake kilichomlea na kuishia kufukuzwa kisha akajiundia chama kingine kilichotumika vibaya wakati wa uchaguzi mkuu 2015 huku mfaidikaji mkuu akiwa ni yeye mwenyewe
Leo hii Maalim yuko chama cha Zitto ACT, hayuko CHADEMA imekuwa faraja ya wengi kwa yeye kutokwenda huko...yangesemwa mengi... Lakini pia asingetosha kwa nafasi za chini... Pengine kuna mkakati wa baadae wa kuja kuunganisha nguvu.... ACT iliyokuwa inapumulia mashine mara ghafla umepata uhai mpya... Ujio wa Seif umekuja na Tsunami ya wanachama.... Sidhani kama likitokea na kutokea Zitto akaondoka ACT impact itakuwa kubwa kama vile Maalim kwa sababu zozote zile akaamua tena kuhama chama.....

Maalim ni mkongwe na anazijua fitina za aina zote hivyo anaweza kumdhibiti Zitto anayependa kusikika yeye tu na kuwa juu ya mamlaka yote.... Zitto hana impact kubwa kwa wanachama wake na hata serikalini lakini Maalim anayo tena ya kutisha....
Pamoja na umahiri wa uchambuzi wa mambo mbali mbali na uwezo wa kujenga hoja lakini ni mwepesi kwenye misimamo na hachelewi kugeuka akiona mambo ni magumu ama kuna faida atapata....
Hivyo basi siasa zijazo ndani ya ACT zitategemea uguswaji wa serikali, ushiriki wake na yatakayotokea kati ya Maalim na Zitto na wanachama wao


Jr
 
Mwaka huu mamangi mtataga yai la MBUNI .........!!

Yaani ninyi mtu yeyote akijaribu kuwaamini hata kwa bahati mbaya anakata tamaa.
Utanirekebisha kama nitakosea. Kama umetumia tribe card ku comment nikwambie tu. Hao unao waita mamangi ni wamesha ji establish kimaisha.. so wana source nyingi sana za kuingizanpesa. Hawategemei siasa.
Ila kama hujatumia triba card basi nimekosea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee hebu nikumbushe katika wale watatu kumbe M1 alikuwa nani vile?

Jr
Usitulet3 porojo za kimangi utafikiri vmezaliwa juzi.

Kwa taarifa yako Zitto kaanza active politics 2010 hata JF ilikuwepo, hakuna mtoto wa kudanganywa humu.

Mwambieni Kubenea aanze kazi yake kwenye vhjarida vyake, maana haviwezi kufungiwa kwa kum-deal Zitto.
 
Impact Ya ACT utaiona baada ya uchaguzi mkuu Pale CHADEMA itakapopoteza majimbo karibia yote na ACT itakapozoa majimbo mengi kupitia Zanzibar ,
 
Usitulet3 porojo za kimangi utafikiri vmezaliwa juzi.

Kwa taarifa yako Zitto kaanza active politics 2010 hata JF ilikuwepo, hakuna mtoto wa kudanganywa humu.

Mwambieni Kubenea aanze kazi yake kwenye vhjarida vyake, maana haviwezi kufungiwa kwa kum-deal Zitto.
Kwahiyo wewe unaona 2010 ni zamani sana? Wahed kweli wewe

Jr
 
Back
Top Bottom