Maalim Seif akiri kuwepo kwa ubaguzi wa ajira Visiwani Zanzibar unaosababishwa na tofauti za kisiasa

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,499
9,279
Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, ameeleza kuanzishwa kwa mfumo mpya wa ajira ikiwa ni hatua za kutibu ubaguzi wa ajira visiwani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Amekiri kuwepo kwa ubaguzi wa ajira kwa baadhi ya Wazanzibari, unaotokana na misingi ya tofauti za kisiasa na kwamba, tatizo hilo linakwenda kupatiwa ufumbuzi.

“… kulikuwa na changamoto katika taasisi za kiserikali katika kuajiri, sasa serikali itaanzisha mfumo rasmi wa kimtandao kwa kuomba ajira na sio kama zamani,” amesema Maalim Seif wakati wa ziara yake kisiwani Pemba jana Jumatano tarehe 6 Januari 2021.

Kwenye ziara hiyo, Maalim Seif amesema, wananchi hususan vijana, wanatarajiwa kunufaika na uwekezaji ambao uko njia kufanyika katika uvuvi.

“Kuna uwekezaji unaotarajiwa kufanyika katika sekta ya samaki, uwekezaji huu utawanufaisha hususani vijana,” amesema.

Maalim Seif ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, anaendelea na ziara yake Pemba akikutana na viongozi mbalimbali wa serikali, chama chake na wakuu wa taasisi.
 
Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, ameeleza kuanzishwa kwa mfumo mpya wa ajira ikiwa ni hatua za kutibu ubaguzi wa ajira visiwani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Amekiri kuwepo kwa ubaguzi wa ajira kwa baadhi ya Wazanzibari, unaotokana na misingi ya tofauti za kisiasa na kwamba, tatizo hilo linakwenda kupatiwa ufumbuzi.

“… kulikuwa na changamoto katika taasisi za kiserikali katika kuajiri, sasa serikali itaanzisha mfumo rasmi wa kimtandao kwa kuomba ajira na sio kama zamani,” amesema Maalim Seif wakati wa ziara yake kisiwani Pemba jana Jumatano tarehe 6 Januari 2021.

Kwenye ziara hiyo, Maalim Seif amesema, wananchi hususan vijana, wanatarajiwa kunufaika na uwekezaji ambao uko njia kufanyika katika uvuvi.

“Kuna uwekezaji unaotarajiwa kufanyika katika sekta ya samaki, uwekezaji huu utawanufaisha hususani vijana,” amesema.

Maalim Seif ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, anaendelea na ziara yake Pemba akikutana na viongozi mbalimbali wa serikali, chama chake na wakuu wa taasisi.
Maalim is another stupid power monger politician ever in Zanzibar!
 
Alikuwa kwenye madaraka kipindi cha mwaka 2010-2015, kwa nini hakuona umuhimu wa kushughulika nalo?
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Naona umekazia upande wa kisiasa na kidin bado Sana kma kupanga nyumba kaz kwa christian
 
Maalim is another stupid power monger politician ever in Zanzibar!
Hilo neno waache waseme wazanzibari wenyewe sio wewe Mtanganyika, kwanini munawashwa na pilipili musioila?
Ndio mana Watanganyika munafeli sana Tundu Lissu yuko ulaya anawaongoza kwa clip za Yotube
 
Hilo neno waache waseme wazanzibari wenyewe sio wewe Mtanganyika, kwanini munawashwa na pilipili musioila?
Ndio mana Watanganyika munafeli sana Tundu Lissu yuko ulaya anawaongoza kwa clip za Yotube
Ungeweza kuwa na hoja ila hapo mwishoni umekosea. Revolutionaries wengi tu wameongoza mapambano wakiwa mbali na homeland. Hta kina Mohammed Badie walianzisha vuguvugu la misri akiwa bado Marekani.

Hta Kagame alisuka mipango ya kupindua Rwanda akiwa Marekani, Kabila alikua Tz, Wamba Dia Wamba alitoa command akiwa mikocheni alafu unaongelea clip za youtube?

Huyo Maalim wenu alipoporwa uchaguzi hakwenda kwa mnaoita mabeberu kudai haki yake? Ila Leo mwenzenu akiondoka for security concerns mnaanza kejeli.

Siku Maalim anadondoka kwa uzee, nakuapia hapa ndio mwisho wa ACT.
 
Ungeweza kuwa na hoja ila hapo mwishoni umekosea. Revolutionaries wengi tu wameongoza mapambano wakiwa mbali na homeland. Hta kina Mohammed Badie walianzisha vuguvugu la misri akiwa bado Marekani.

Hta Kagame alisuka mipango ya kupindua Rwanda akiwa Marekani, Kabila alikua Tz, Wamba Dia Wamba alitoa command akiwa mikocheni alafu unaongelea clip za youtube?

Huyo Maalim wenu alipoporwa uchaguzi hakwenda kwa mnaoita mabeberu kudai haki yake? Ila Leo mwenzenu akiondoka for security concerns mnaanza kejeli.

Siku Maalim anadondoka kwa uzee, nakuapia hapa ndio mwisho wa ACT.
Maalim baada ya kuporwa uchaguzi amekuja na plan "B" kuwasaidia wazanzibar waliokwisha kukata tamaa kutokana na ubaguzi uliokithiri, watu kuumizwa kwenye haki zao za msingi, maendeleo ya kibaguzi yaliyokubuhu u-unguja na u-pemba sasa kama yote haya watayamaliza na Hussen Mwinyi hiyo stupidity ya maalim seif itakuwa wapi na yeye lengo lake siku zote ilikuwa ni kuiongoza Zanzibar kwa usawa?

Kama unaamini Tundu Lissu atawakomboa watanganyika kupitia youtube kwa sababu ya vuguvugu la misri na mpiango ya kagame kupindua akiwa Marekani nk ntakuwa na hamu sana kuja kuona hilo likitokea kwa nchi kama Tanzania. Lissu alisema uchaguzi unafuatiliwa kwa ukaribu na mataifa lakini baada kuporwa hatukuona impact, alisema hatakubali kuibiwa uchaguzi hatukuona impact, alikimbilia ubalozi wa ujerumani akidai mtu atakayemuua kampigia simu hatukuona impact yoyote lakini mwisho aliitisha maandamano hakuna aliyetoka.

security concerns iko wapi? Yeye Tundu Lissu alisema hatarudi Tanzania kwa sababu hajahakikishiwa ulinzi mbona alikuja hivyo hivyo hakujali security concerns? au lengo lake ilikuwa ni Urais tu kufa au kupona?

Kisiasa Tanzania bara lazima mukubali muko nyuma sana yaani zaidi ya sana na wasiwasi wangu sasaiv itawabidi muanze upya., maalim lazima atakuwa ni Genius mtarudi kwake kujifunza siasa again.
 
Maalim baada ya kuporwa uchaguzi amekuja na plan "B" kuwasaidia wazanzibar waliokwisha kukata tamaa kutokana na ubaguzi uliokithiri, watu kuumizwa kwenye haki zao za msingi, maendeleo ya kibaguzi yaliyokubuhu u-unguja na u-pemba sasa kama yote haya watayamaliza na Hussen Mwinyi hiyo stupidity ya maalim seif itakuwa wapi na yeye lengo lake siku zote ilikuwa ni kuiongoza Zanzibar kwa usawa?
Ambacho huelewi ni kwamba CHADEMA ni taasisi sio ACT ambayo Maalim ndio kila kitu no wonder CHADEMA haijawahi rudia mgombea Urais na still kimekuwa main opposition all times. So whether Lissu is here or not, 2025 moto ni uleule na wewe unajua hilo ndio maana mkamuacha membe mkamsupport Lissu.

Maalim aliapa hatowahi kuingia serikali inayonuka damu je kma alijua anahitaji kuponya wapemba ni kivp asingewaponya 2010-15? Kivp asusie 2016-2020 alafu ndio useme kaja na strategy mpya? Hakuna strategy mpya wakati unarudia upuuzi ule ule wa kusurrender kwa CCM kma ilivokua 2010.

Otherwise Maalim ndio ACT siku akistaafu chama kitapasuka kama ilivyokua CUF. Time will tell na mtarudi hapa kuitana wasaliti.
 
Kwanini wasiongee hao wapemba wenyewe au unawasemea? Tanganyika achen ufala
Tanganyika lazima wacomment sababu zenji ni koloni letu. Hamuoni Rais alichaguliwa Dodoma nyie mkaletewa jina tu, mlivyogoma mkapigwa virungu na mkakubali nusu mkate.

Upinzani Tanzania ni CHADEMA wao wakiteleza tu ndio tusahau kabisa CCM kutoka madarakani.
 
Ambacho huelewi ni kwamba CHADEMA ni taasisi sio ACT ambayo Maalim ndio kila kitu no wonder CHADEMA haijawahi rudia mgombea Urais na still kimekuwa main opposition all times. So whether Lissu is here or not, 2025 moto ni uleule na wewe unajua hilo ndio maana mkamuacha membe mkamsupport Lissu.

Maalim aliapa hatowahi kuingia serikali inayonuka damu je kma alijua anahitaji kuponya wapemba ni kivp asingewaponya 2010-15? Kivp asusie 2016-2020 alafu ndio useme kaja na strategy mpya? Hakuna strategy mpya wakati unarudia upuuzi ule ule wa kusurrender kwa CCM kma ilivokua 2010.

Otherwise Maalim ndio ACT siku akistaafu chama kitapasuka kama ilivyokua CUF. Time will tell na mtarudi hapa kuitana wasaliti.
Kwanini Tundu Lissu baada ya kufika belgium alimtaka rais Magufuli kuunda serikali yenye kuleta umoja na mashirikiano ili kuwaponya Watanganyika? Ilhali anajua fika uchaguzi uliporwa na kunuka damu na alikuwa mgombea urais aliyeshuhudia unyama huo? kwanini alisarender kiasi hiki

Sasa kama ameachwa Membe akasapotiwa Lissu mbona Chadema walimuacha Said Issa mgombea Urais wa chadema Zanzibar wakamuunga mkono Maalim seif mi nadhan hapa huna hoja ya msingi, sijui kila uchaguzi mnabadilisha mgombea hii sio hoja hapa nadhan wewe ni mgeni sana kwenye siasa za Zanzibar, Kule zanzibar maalim seif ndio chaguo lao ikibidi maalim kustaafu siasa ni suala linalohitaji dakika 1 tu Maalim seif au uongozi useme sasa mchagueni mtu fulani kuwa rais wenu.,

Kwani ilihitaji miaka mingapi kule Zanzibar baada CUF kuuliwa watu kuunga mkono ACT? few minutes tu Maalim aliposema sasa tupo ACT asubuhi Wazanzibari woote waliamka wakiwa ni ACT hiyo ndio Zanzibar mkuu., lazma uelewe hivyo.

Chadema bado ni wageni sana kwenye hizi siasa maalim seif alipoingia SUK ana mambo mengi ametegemea na insh Allah ni suala la muda tu mutakuja kumuunga mkono, Chadema sasa mtaanzia wapi chama kina mpasuko wa nguvu , Lema yupo canada hawez kurud, Lissu yupo ulaya, hawa waliopo nusu wanaunga mkono CCM nusu hawajulikani., mpaka kuja kufikia mupate hiyo strong Institution itachukua muda sana ndio mana nimekwambia Chadema itabidi ianze siasa Mwanzo. Mwanzo kabisa
 
Tanganyika lazima wacomment sababu zenji ni koloni letu. Hamuoni Rais alichaguliwa Dodoma nyie mkaletewa jina tu, mlivyogoma mkapigwa virungu na mkakubali nusu mkate.

Upinzani Tanzania ni CHADEMA wao wakiteleza tu ndio tusahau kabisa CCM kutoka madarakani.
Muulize Tundu Lissu ilibidi amuamkie Maalim Seif Shikamoo..,

Siasa za vyama vingi vinaanza hakukua na Chadema wala mavi ya nini ni Maalim seif pekee aliweza kuunda chama cha CUF na akatengeneza strong opposition kule zanzibar ndio baadae na Tanganyika mkaja mkaamka.,
 
Hilo neno waache waseme wazanzibari wenyewe sio wewe Mtanganyika, kwanini munawashwa na pilipili musioila?
Ndio mana Watanganyika munafeli sana Tundu Lissu yuko ulaya anawaongoza kwa clip za Yotube
Pamoja na "MATAGA" wa marekani kuandamana wakitaka bwana "TRUMP" asalie madarakani pamoja na kushindwa, ila hujasikia IGP wakule akisema watapigwa kipigo cha mbwa koko, makamo wa raisi Mike Pence yani mama Samia Suluhu Wakule kasema "MATAGA" hao wanaiaibisha MAREKANI.
Ccm na vibaraka wenu mna la kujifunza.
 
Tanganyika lazima wacomment sababu zenji ni koloni letu. Hamuoni Rais alichaguliwa Dodoma nyie mkaletewa jina tu, mlivyogoma mkapigwa virungu na mkakubali nusu mkate.

Upinzani Tanzania ni CHADEMA wao wakiteleza tu ndio tusahau kabisa CCM kutoka madarakani.
Wateleze Mara ngapii?? Bado mna matumaii na CHADEMA... you are hopeless
 
Wataongelea wapi labda?
Acheni ukiritimba wa kuwapangia wazanzibari cha kufanya.,

Kiongozi wa kwanza wa kambi rasmi ya upinzani bungeni alitokea Pemba tena mwanamke kupitia chama cha Wananchi CUF Bibi Fatma Maghimbi uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi Tanzania., Chadema mlikuwa wapi?? Acheni kuwaongelea wapemba na wazanzibar hamuwawez
 
Acheni ukiritimba wa kuwapangia wazanzibari cha kufanya.,

Kiongozi wa kwanza wa kambi rasmi ya upinzani bungeni alitokea Pemba tena mwanamke kupitia chama cha Wananchi CUF Bibi Fatma Maghimbi uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi Tanzania., Chadema mlikuwa wapi?? Acheni kuwaongelea wapemba na wazanzibar hamuwawez

Hoja yako ni nini hapa? Na cdm imeingiaje hapa?
 
Kwanini Tundu Lissu baada ya kufika belgium alimtaka rais Magufuli kuunda serikali yenye kuleta umoja na mashirikiano ili kuwaponya Watanganyika? Ilhali anajua fika uchaguzi uliporwa na kunuka damu na alikuwa mgombea urais aliyeshuhudia unyama huo? kwanini alisarender kiasi hiki

Sasa kama ameachwa Membe akasapotiwa Lissu mbona Chadema walimuacha Said Issa mgombea Urais wa chadema Zanzibar wakamuunga mkono Maalim seif mi nadhan hapa huna hoja ya msingi, sijui kila uchaguzi mnabadilisha mgombea hii sio hoja hapa nadhan wewe ni mgeni sana kwenye siasa za Zanzibar, Kule zanzibar maalim seif ndio chaguo lao ikibidi maalim kustaafu siasa ni suala linalohitaji dakika 1 tu Maalim seif au uongozi useme sasa mchagueni mtu fulani kuwa rais wenu.,

Kwani ilihitaji miaka mingapi kule Zanzibar baada CUF kuuliwa watu kuunga mkono ACT? few minutes tu Maalim aliposema sasa tupo ACT asubuhi Wazanzibari woote waliamka wakiwa ni ACT hiyo ndio Zanzibar mkuu., lazma uelewe hivyo.

Chadema bado ni wageni sana kwenye hizi siasa maalim seif alipoingia SUK ana mambo mengi ametegemea na insh Allah ni suala la muda tu mutakuja kumuunga mkono, Chadema sasa mtaanzia wapi chama kina mpasuko wa nguvu , Lema yupo canada hawez kurud, Lissu yupo ulaya, hawa waliopo nusu wanaunga mkono CCM nusu hawajulikani., mpaka kuja kufikia mupate hiyo strong Institution itachukua muda sana ndio mana nimekwambia Chadema itabidi ianze siasa Mwanzo. Mwanzo kabisa
Nachojaribu kukueleza ni Kwamba zinapokuja siasa za Tanzania CHADEMA ndio main opposition na ACT ipo reduced to the isles alone. Niambie chama gani ambacho walau kina wanachama/mashabiki kila mkoa zaidi ya CHADEMA? So taasisi kama hiyo huwezi sema inamtegemea Lissu kwenye struggle unlike CUF/ACT sio taasisi zinatembelea nguvu ya mtu mmoja tu ndio maana nasema leo Maalim akidondoka chama kimekufa.... Mark my words.

2. Unadhani succession itakuwaje? Jussa amuachie Mazrui? Ama Bimani amuachie Himid? ACT kama ingeweza kuenea nchi nzima ndio mngekua taasisi imara ila kwa mlivyo scattered mara Pemba, kusini alafu Ujiji sidhani kama mtafika kokote so kubali kataa CHADEMA is way ahead of your party na huu ni ukweli mchungu. Hata CUF iliwazidi influence kusini na defection hazikua nyingi tofauti na mlivyotarajia.

3.Unasema Maalim ameingia SUK kuna mategemeo alikua nayo. Ndio tunahoji kwanini hakuyatekeleza 2010-15 alipokua SUK ndio aje afanikiwe leo? Kama SUK ilifeli kufikia 2015 nini kinakufanya uamini mpaka 2025 mtakua intact? Hamuwezi rudia kitu kile kile ambacho kilifeli mkiamini sahvi kuna mabadiliko. Its insanity mkuu

4. Unadai kuna mpasuko CHADEMA, ni upi huo? Mbona kamati kuu unanimously waliwafuta uanachama na mpaka sasa sijaona opposition yoyote ya maamuzi kutoka kwa baraza!!? Embu tusaidia mgogoro gani huo, and to make records straight hao kina Halima walisema bado ni CHADEMA na hawaendi CCM so at least mpaka sasa bado ni opposition hayo ya kuwa ni CCM ni subjective.

NB: Lissu kumdrop Issa ni strategic tu sababu alihitaji kura za zenji from ACT lakini alijua fika bara atazoa za kutosha kuzidi Membe. So ni kheri asacrifice mkoa wenye kura laki 3 kuliko Bara kwenye kura million 28!! Otherwise nisaidie strategy gani mlitumia kupisha kura 28m za Urais ili mgombee kwenye kura 3 pekee? Then unakuja hapa kudai mna strategy? Hamkujua Membe ni pandikizi? Funny
 
Back
Top Bottom