Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,802
- 11,961
Habari wana jf, maalim seif ameongea na waandishi wa habari na kuzungumzia suala la Membe huku akimtolea maneno makali sana.
Nimeshindwa kushangaa, leo hii maalim seif unasema Membe katumwa? Mbona siku ya kumpitisha pale chamani kuwa mgombea uraisi ulimsifia sana? Membe unalo la kujifunza, pole sana
===
MGOMBEA urais wa chama cha ACT Wazalendo visiwani Zanzibar ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, ameeleza kusikitishwa kwake na tamko la jana la mgombea urais wa Tanzania kupitia chama hicho, Bernard Membe, kuwa yeye ni mgombea halali wa urais, hivyo ataipeperusha bendera ya chama na ana uhakika atashinda.
Akifafanua Kuhusu suala hili, Maalim Seif amesema “Nasikitika sana kwa aliyoyazungumza Membe jana. ACT-Wazalendo kupitia mkutano mkuu wa Taifa tuliamua tunataka mabadiliko katika nchi yetu. Mkutano mkuu ukabariki tushirikiane na vyama makini kuiondoa CCM madarakani. Membe alipokuja tulimwambia uamuzi wa mkutano mkuu ni tushirikiane na vyama vingine. Tukamuuliza tukiamua kushirikiana utakubali, akasema “Naam.” Tulipoona kampeni zetu zimesuasua, tukaamua, na Membe akiwepo, tumuunge mkono Tundu Lissu.”
Ameongeza kuwa, “Mgombea wetu Bernard Membe haonekani. Ni afadhali mzee wa ubwabwa Hashim Rungwe anaonekana. Kamati ya uongozi kwa kauli moja pamoja na Membe tulikubaliana tumuunge mkono Tundu Lissu. Sio kwamba hatumpendi Membe. Mimi nam-challenge, afanye hizo kampeni zake tuone hizo kampeni ziko wapi. Nia yake ni kutaka kuwachanganya Watanzania.”
Kuhusu kuwapo kwa mpasuko ndani ya Chama cha ACT Wazalendo, Maalim Seif amesisitiza kuwa “Hakuna mpasuko ndani ya ACT-Wazalendo. Membe anataka iaminike hivyo, lakini hakuna. Chama kimefanya uamuzi, wewe unaenda kinyume. Tukuelewe vipi? Si umeletwa ACT kwa mission (shughuli) maalum.”
PIA SOMA
= > Uchaguzi 2020 - Bernard Membe: Watanzania mkae macho na mkae chonjo. Nafunga bao la Ushindi dakika ya 89 kwenye Uchaguzi huu 2020
Nimeshindwa kushangaa, leo hii maalim seif unasema Membe katumwa? Mbona siku ya kumpitisha pale chamani kuwa mgombea uraisi ulimsifia sana? Membe unalo la kujifunza, pole sana
===
MGOMBEA urais wa chama cha ACT Wazalendo visiwani Zanzibar ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, ameeleza kusikitishwa kwake na tamko la jana la mgombea urais wa Tanzania kupitia chama hicho, Bernard Membe, kuwa yeye ni mgombea halali wa urais, hivyo ataipeperusha bendera ya chama na ana uhakika atashinda.
Akifafanua Kuhusu suala hili, Maalim Seif amesema “Nasikitika sana kwa aliyoyazungumza Membe jana. ACT-Wazalendo kupitia mkutano mkuu wa Taifa tuliamua tunataka mabadiliko katika nchi yetu. Mkutano mkuu ukabariki tushirikiane na vyama makini kuiondoa CCM madarakani. Membe alipokuja tulimwambia uamuzi wa mkutano mkuu ni tushirikiane na vyama vingine. Tukamuuliza tukiamua kushirikiana utakubali, akasema “Naam.” Tulipoona kampeni zetu zimesuasua, tukaamua, na Membe akiwepo, tumuunge mkono Tundu Lissu.”
Ameongeza kuwa, “Mgombea wetu Bernard Membe haonekani. Ni afadhali mzee wa ubwabwa Hashim Rungwe anaonekana. Kamati ya uongozi kwa kauli moja pamoja na Membe tulikubaliana tumuunge mkono Tundu Lissu. Sio kwamba hatumpendi Membe. Mimi nam-challenge, afanye hizo kampeni zake tuone hizo kampeni ziko wapi. Nia yake ni kutaka kuwachanganya Watanzania.”
Kuhusu kuwapo kwa mpasuko ndani ya Chama cha ACT Wazalendo, Maalim Seif amesisitiza kuwa “Hakuna mpasuko ndani ya ACT-Wazalendo. Membe anataka iaminike hivyo, lakini hakuna. Chama kimefanya uamuzi, wewe unaenda kinyume. Tukuelewe vipi? Si umeletwa ACT kwa mission (shughuli) maalum.”
PIA SOMA
= > Uchaguzi 2020 - Bernard Membe: Watanzania mkae macho na mkae chonjo. Nafunga bao la Ushindi dakika ya 89 kwenye Uchaguzi huu 2020