HUKO Niger, sio Nigeria kama watangazaji fulani Tanzania wasiojua jiografia wanavyokosea kuna dada mmoja kaishtaki serikali yake kwa kushindwa kumlinda.
Ninauliza, je, kwa hapa Tanzania haiwezekani ndugu zangu Maalibino mkaishataki serikali yetu kwa kushindwa kuwalinda. Hebu waoneni wanasheria wawashauri!
Msikubali kufanyiwa usanii wa kucheza mpira wakati wa jua huku nyie hamuwaoni au kushibishwa na hotuba nzuri ambazo ukiamkia asubuhi yake tayari mwenzenu mwingine kamalizwa.
Maana serikali yenyewe na wizara yenyewe ilivyokaa ni kwamba inalichukulia jambo hili kama ni uahalifu wa kawaida. La, hasha. Hilo hata kwa kipofu na kiziwi wanajua sio sawa. Huu ni uhalifu wa aina yake na unataka dhamira na mkakati maalum wa kushughulikia.
Nyie msipokuwa mstari wa mbele katika hili niaminini hamtafika popote. Na serikali yenyewe ndio hii? Na viongozi wenyewe ndio hawa? Labda iwe maajabu!
Watu wa ofisini na tai na viyoyozi toka lini wakawa wa msaada wa raia wa kawaida?
Hakikisheni mnakuwa mstari wa mbele ili mauaji ya ALBINO yasienee pembe nyingine za Kiafrika. Mnajua tena kwa umasikini wetu kuna mamilioni ya wajinga wanaoamini wanaweza kutajirika kwa nguvu za kishirikina bila kutumia akili na maarifa.
Wastaafu wa EAC acheni kulala barabarani tafuteni NGOs na taasisi nyingine za kisheria kupeleka dhuluma mliyofanyiwa na serikali toka ile ya awamu ya 1 hadi ya 4 ili washughulikiwe na mahakama na vyombo vya sheria vya kimataifa.
Mahakama za kimataifa haziwashughulikii tu viongozi wezi na wauaji bali pia hata serikai na viongozi wanaowadhulumu watu wao. Watakwenda wapi na wao kwa utegemezi ndio namba moja!
Walimu, madaktari na manesi tafuteni wataalamu wa masuala ya mishahara na haki za wafanyakazi toka ILO na kwingineko na kuishtaki serikali kwa kuwanyonya kutokana na mishahara isiyofika hata tarehe tano ya mwezi.
Ninauliza, je, kwa hapa Tanzania haiwezekani ndugu zangu Maalibino mkaishataki serikali yetu kwa kushindwa kuwalinda. Hebu waoneni wanasheria wawashauri!
Msikubali kufanyiwa usanii wa kucheza mpira wakati wa jua huku nyie hamuwaoni au kushibishwa na hotuba nzuri ambazo ukiamkia asubuhi yake tayari mwenzenu mwingine kamalizwa.
Maana serikali yenyewe na wizara yenyewe ilivyokaa ni kwamba inalichukulia jambo hili kama ni uahalifu wa kawaida. La, hasha. Hilo hata kwa kipofu na kiziwi wanajua sio sawa. Huu ni uhalifu wa aina yake na unataka dhamira na mkakati maalum wa kushughulikia.
Nyie msipokuwa mstari wa mbele katika hili niaminini hamtafika popote. Na serikali yenyewe ndio hii? Na viongozi wenyewe ndio hawa? Labda iwe maajabu!
Watu wa ofisini na tai na viyoyozi toka lini wakawa wa msaada wa raia wa kawaida?
Hakikisheni mnakuwa mstari wa mbele ili mauaji ya ALBINO yasienee pembe nyingine za Kiafrika. Mnajua tena kwa umasikini wetu kuna mamilioni ya wajinga wanaoamini wanaweza kutajirika kwa nguvu za kishirikina bila kutumia akili na maarifa.
Wastaafu wa EAC acheni kulala barabarani tafuteni NGOs na taasisi nyingine za kisheria kupeleka dhuluma mliyofanyiwa na serikali toka ile ya awamu ya 1 hadi ya 4 ili washughulikiwe na mahakama na vyombo vya sheria vya kimataifa.
Mahakama za kimataifa haziwashughulikii tu viongozi wezi na wauaji bali pia hata serikai na viongozi wanaowadhulumu watu wao. Watakwenda wapi na wao kwa utegemezi ndio namba moja!
Walimu, madaktari na manesi tafuteni wataalamu wa masuala ya mishahara na haki za wafanyakazi toka ILO na kwingineko na kuishtaki serikali kwa kuwanyonya kutokana na mishahara isiyofika hata tarehe tano ya mwezi.