MAakungwi! Watoa Masomo! Walimu wa Mapenzi Ni Upotoshaji wa Jamii na Kujiingizia Kipato Isivo Halali

lara 1

JF-Expert Member
Jun 10, 2012
15,700
29,111
IGWEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mwenzangu imekuwa fashion siku kusikia eti mtu kaibuka tu nae mfundaji! Au sijui mama mchungaji anatoa somo mambo ya ndoa au jinsi ya kupata mchumba afu mnalipa! Au kitchen party mnamlipa mtu aje afunde! Au mtu anaitisha semina watu mnatoa hela ukajifunze kukaa na mumeo! Khaaaaaaaaaa!

Mume wako mwenyewe kuishi nae akufundishe mtu ambae hata hamjui! Si bora ukajifunze kwa mamkwe aliemlea! Khaaaaaa! Mimi haya mambo sikubaliani nayo kabisaaaaaaaa! Tena hata kwenye kitchen party naendaga mda wa kula na kucheza mziki baaaaaaaaaaaaaas! Mimi sikubaliani kabisaaaa na mambo yenu kwa sababu nzito zifuatazo!

1. Wanaume Sio Universal!!!!!!!!!!! Hakuna jambo linafanya kazi kwa wanaume wote. Wanaume hawafanani asilani kila mtu hulka yake. Wewe mke/GF ndo unajua maruhani ya mwenzio uzuri sasa kupoteza mda mtu hamjui huyo bwana wala uzaifu wake atakufundisha lipi usilolijua! Logically tu haileti picha! Unaweza kukuta mumeo mzungu kama Baba Lara 1, chakula chochote anajilia tu, Hata haulizi kapika nani, maadam akute chakula baaaas! hana makuu, kama mboga ndogo anawaachieni watoto mle, sasa kule unafundishwa Mumeo umtengeee Mipaja, wewe na wanao mle miguu, vikwapa na shingo! Si kunyanyasa watoto huko. Yeye anashinda nyumbani wewe umekaa strong room bank huko siku nzima anakubrainwash uwahi kupika! Badala kama nguvu unazo uende chuo evening ujiendeleze mjikwamue, eti uwahi kupika??????? Haingii akilini mtu amjue mumeo na lipi litamfaa mumeo kuliko wewe unaelala nae na kuamka nae!!!!!!!!!!

2.Autheticity ya huyo Mwalimu!!!!!!!!! Mtu kaamka tu kaamua kuanzia leo nafunda! Hakuna chuo wala qualifications za kupima uwezo wa huyo ticha! Mostly unakuta mtu tu, hata elimu yake sio kivile, hana biashara ya kueleweka, ndo kujiingizia kipato anafunda!!!!!!! Mimi siku Mama Salma Kikwete akisema anafunda nawahije coz uwezo wake nimeuona!!!!!!!! Hata akiwa na ndoa anawazuga ya furaha nyie mnauhakika gani kama ya furaha kweli sio maigizo! Ukute ndoa yenyewe ya kumlamba mumewe miguuu! Mjini hapa!!!!!!!!!!! Na kama she is as good as she claims kwanini hayo mambo asimfanyie mumewe amfungulie biashara za maana na kumnunulia prado aache kukauka kooo? Mi upendo usikuwa na indicators za kupima siuaminigi kabisaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!

3. Hamna Jipya!!!!!!!!!! The old boring staffs alizoniambia bibi yangu (R.I.P) Usafi, Utiii, Ukarimu, blah blah blah! Alianza bibi mpaka mjukuuu! Jipya hakunaga! Bora hata nikamsikize mtu aniambie kuna design mpyaa ya machjo imeingia inaitwa I phone 6 it will be more interesting!!!!!!!!!

My take girls you know your man better n your man knows you, na mpaka amekupenda it means you are perfect for him, sasa kutaka kuperfect world standards ndo mnajiletea mgongano! Dont let people you dont know dictate to you how to live with your man!

Even men like you to be yourself cause it more fan, ukisahfuzu mafundisho you become a Cold Bi.tch who is never wrong and always watching out standards are adhered!!!!!!!!!

MJINI HAPA!!!!!!!!!!! MJINI CHUO KIKUUU!!!!!!!!!!!!

Neo langu sio sheria au tamko la kikatiba!!!!!!! Feel free to agree to disagree!!!!!!!!!!! Its a free country after all!!!!!!!!
 
Kumbukumbu zangu, zinaniambia you used to shabikia makungwi na chicken parties.......
Hongera kwa kukua, naona wewe umeelewa zaidi kwanini mwanzoni mwa mwaka nikasema .......Sikwambii.......
 
Wanaoniboa ni mashosti wanaotumika kuchangisha! Eti ujeee, ni nzuri sijui kufanyajekufanyaje. Majambazi woote hao kina aunt sadaka sijui sadati.

Wanatafuta a lousy venue.
Kiingilio 30,000x400= 12,000,000
Msosi kama wakitoa 400x10,000 =4,000,000
Kupamba hardly 300,000
Dj na mziki hardly 300,000
Kama kuna drinks za kunyunyizia hata wakitumia milioni moja!

Faida= 7,000,000 na ushee kwa siku na masaa tu.

Wizi mtupu. Mie hata nikiwa kwenye kitchen party kamati hayo maujinga ya kumuita mama victor anaambia watu wafanye douching na huku daktari kakataza, afu mnampa laki 3 huwa nagoma. Bora tununue food processor hapo, eboo.

Bora umewastukia aisee. Wanawake hawana outing na hapo wanaenda kuonyesha nguo zao za vitenge tu hamna lolote.
 
Kumbukumbu zangu, zinaniambia you used to shabikia makungwi na chicken parties.......
Hongera kwa kukua, naona wewe umeelewa zaidi kwanini mwanzoni mwa mwaka nikasema .......Sikwambii.......

Ujue kuna elimu mbili hapa unachanganya!

Kuna elimu ya uwanja wa fundi seremala hio hata uniamshe saa tisa usiku naishabikia!!!!!!!!!! Hio kitu kama hujafundishwa hutokaaa ukijue hata kuwa kutafakari kwa kina au intuition zako binafsi! Kama chejo la Iphone 6 s hujalisikia ama kuliona huwezi kulijua kwa critical thinking!!!!!!!!

Kuna elimu ya mahusiano na jinsi ya kuishi na mtu ndo naipinga kabisaaaaaaaaaaaa! Mtu unatakiwa uishi nae jinsi alivo hakuna standards!
 
Wanaoniboa ni mashosti wanaotumika kuchangisha! Eti ujeee, ni nzuri sijui kufanyajekufanyaje. Majambazi woote hao kina aunt sadaka sijui sadati.

Wanatafuta a lousy venue.
Kiingilio 30,000x400= 12,000,000
Msosi kama wakitoa 400x10,000 =4,000,000
Kupamba hardly 300,000
Dj na mziki hardly 300,000
Kama kuna drinks za kunyunyizia hata wakitumia milioni moja!

Faida= 7,000,000 na ushee kwa siku na masaa tu.

Wizi mtupu. Mie hata nikiwa kwenye kitchen party kamati hayo maujinga ya kumuita mama victor anaambia watu wafanye douching na huku daktari kakataza, afu mnampa laki 3 huwa nagoma. Bora tununue food processor hapo, eboo.

Bora umewastukia aisee. Wanawake hawana outing na hapo wanaenda kuonyesha nguo zao za vitenge tu hamna lolote.

Hahahaaaaaaaaa! Muandaaji Dinner mwenyewe hana mume! (Utazania mie nnaemsema mwenzangu ninae!!!!! LOL! Its such an ironic world)

Mama victor yule mda si mda atatajirika! MJINI MIPANGO!!!!!!!!!1

Hahahaaaaaaaa! @ Food processor!!!!!!!! Mi siku hizi naona bora hata mtu afanye Bridal Shower @ Obay huko ndo mambo yao siku hizi! Kama ile ya Made Kimei ilinogaje (Niliiona kwenye picha tu wajameni!)
 
296127_586209294743841_603893296_n.jpg
 
the issue is kila mtu anafikiri jinsi ya kupata kipato halali, sasa huangalia soko liko wapi kwa wingi. by 2000 wafundaji walikuwa juu sana i do remember mama Terry ilikuwa kumpata bila kuwa 150000 haji kumfunda mwali wenu.

istoshe huko chalizne kulikuwa kuna mama mdogo, yeye allikuwa anafunda wali ndani kwa siku 7 na alikuwa kwa miez 3 anaandaa somo kwa kila mtu mke aliyetaka kwenda, mnafunzwa ya ndani.

but kwasasa haya mambo yamekuwa ya kawaida sana manake hata mombasa raha ukiingia unafundwa vya ndani vyote. hayo ya mtu kusema ukumbini sijui kitchen party galla yamekuwa hayana jipya tena. jambo pekee ambalo mie huwa nalikubali ni mafunisho ya ujasiriamali ambayo watu hupokea kwenye haya mafundisho kama tu yatakuwa na kipengele cha ujasiriamali.
 
eheheee hadi shoga bilali nae kungwi........sijui huwa anafunda nini ?
600615_586206598077444_1258805405_n.jpg
 
Kungwi au wengine wamuita somo,ni mtu muhimu sana,na mara nyingi anakuwa ni mtu wa kwenye ukoo wenu,unawekwa ndani,si chini ya mwezi mmoja kwa mfano kabila tetu sisi,na mara nyingi huyu kungwi anakuwa na upendo nawe wa dhati,na ni mtu mzima na ambaye yupo kwenye ndoa kwa muda mrefu,wangu mie sikumlipa hata shs kumi,ila siku natoka saba,mama,dada zangu,walimpatia zawadi na mimi pia kumshukuru,nami nilikuwa sioni umuhimu wake hivyo hivyo,coz mwanaume nimeshadate nae kwa muda mrefu,nkajiona kama nimefuzu na ndoa kwangu nimteremko,aisee nilifundishwa mambo mengi,na kwa kuyapractise hayo alonifundisha,ndoa yangu imesimama imara,namshukuru mungu.I see no matter how much is ur exposure n education,sijui uzungu,usidharau makungwi,otherwise kama haupo tayari kwa ndoa yako kudumu,na divorce kwako sio issue coz huoni dhambi kuwa mzinzi.ila tu wengi siku hizi hii kitu wanaifanyia biashara,na wale wasiojua maana halisi ya kufundwa na kungwi wanamwaga tu pesa zao.na hii kitu si ya kugfundishwa siku moja tu kwenye k party,hapo kuna mashosti,wengine hata wachumba au waume,hawana.hawapaswi kujua ulofundishwa na kungwi wako,ni siri yenu.hizo dharau ndo maana mtu anaolewa siku mbili,kaona mkato wa chumba,halafu anaachika.wanawake wa kileo tuache ujuaji wa kimagharibi,otherwise ndoa zitakuwa kama za kina JLo marekani.ukipenda chukua,ukiona ngumu kumeza iache.mimi imenisaidia sana,na ninampenda na kumheshimu sana kungwi wangu.
 
Kwa nini asifanyiwe? Aache kununuliwa led lcd ya inchi 64 juu ya nini? Na masufuria non-stick? Maznat aliolewa chuo cha pili na mume wa mtu na akafanyiwa kitchen party lol. Chezeiya mjini?
Hivi na wewe dada utafanyiwa kitchen paty.
 
He he he, mie nilistuka tangu nazaliwa kwenye hili. Wizi mtupu

Kuanzia sijui kufunda, kuchezwa na kurushwa rushwa is not my type kabisa.

Najua nina vingine vizuri vya kufidia kuliko pangaboi ku bed.
 
Kongosho uje nikufunde kwi kwi kwi
kuna mtu ana group la kufunda fb, unalipa kiingilio teh. Sijui nilipe nikashuhudie?
 
Last edited by a moderator:
Kama hela zinakujaa nlipie pop corn tu pale mliman city
Anayefunda mwenyewe ana mabwaba mia kidogo, sasa akufunde nini?

Kongosho uje nikufunde kwi kwi kwi
kuna mtu ana group la kufunda fb, unalipa kiingilio teh. Sijui nilipe nikashuhudie?
 
Last edited by a moderator:
Mjini mipango shosti. Afu unajua bank inakukopesha hela ya kununua fortuner ama nissan patrol. Haikukopeshi wese. Lazma ugangamale atii! Unatuma kwa mpesa wanakuadd. Afu huwa nahisi ni Smile yule, sijui kwa nini!
hahahahah! wtt wa kileo mnatabu kweli
sasa anafundia mtandaoni??
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom