Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Heri ya X MASS wakazi wa Mji mzuri Morogoro, mji msafi unaovutia na kupendeza katika maeneo mengi. Tatizo kuna baadhi ya watu wanaochafua sifa ya mji huo. Nyakati za mchana ni wastaarabu wa hali ya juu. Lakini usiku wanaubadili mji na kuwa wa watu wasioaminika hata kidogo. Wezi, vibaka, na wadokozi hawalali, usiku kucha wanapita hapa na pale kwa ajili ya mawindo. Makahaba nao wanafanya kazi yao ipasavyo. Kuanzia Kahumba katikati ya mji mpaka Makuti stendi kubwa ya mabasi. Jinsi tulivyochapwa kamera zetu za kupigia picha katika gest moja pale Msamvu. Ni kama kiini macho hivi, Amakweli Morogoro mji kasoro bahari.