Maajabu ya UKIMWI: Mume anao, mke na watoto hawana

DM MOWO

Senior Member
Oct 3, 2017
135
95
Nimekuwa nikifatilia mijadala ya UKIMWI humu kwa muda mrefu na haya ninayotaka kuyasema humu yalishasemwa na mimi nimeyashuhudia siku chache zilizopita kwa majirani zangu.

Jirani yangu huyu aliugua sana na kulazwa, Dokta akaamuru aje na mke wake na watoto wote wapimwe (hapa nahisi alikuwa na mashaka ya ugonjwa).Wakafanyiwa vipimo wote ndio jamaa kugundulika ana VVU tayari, mke na watoto wakawa wapo salama wakaenda hadi hopitali ya mkoa majibu yakawa vilevile. Basi, mme akaendelea na matibabu na kupata nafuu na sasa hivi anaendelea na dozi.

Sasa navyoandika hapa ndoa ilishavunjika familia ya mwanamke ilimlazimisha aachane na jamaa asije akamwambukiza na mwanamke akafanya hivyo. Jamaa alipata maumivu mara mbili akataka ajiue kilichomsaidia ushauri mzuri kutoka kwa marafiki.

Swali. Je, inakuwaje wanandoa mmojawapo ameathirika na nwingine yupo salama? Huu ugonjwa una maswali mengi bila majibu.

Karibu wadau kwa hoja zenu.

MAONI YA WADAU:
Hapa ndipo penye mkanganyiko wa ajabu kuhuhu UKIMWI. Theory zinazoletwa na akina kimsboy na Deception ndiyo zinapata nguvu nakuonekana UKIMWI is Just a Myth tuloletewa na wazungu.

Kipimo kinapima uwepo wa Kinga (sijui ndiyo Serology) Mwilini na sio uwepo wa Virus, kwamba kinga zikipungua ndiyo mtu anaukimwi wakati hata Mgonjwa TB kinga pia zinapungua.

Inamaana hapo Baba alikua anaumwa so kinga lazima zipungue na kipimo lazima kitasoma positive, mke na watoto hawaumwi ndio maana walikua negative.

Kuna Msemo niliupata unasema
USIENDE KUPIMA UKIMWI WAKATI UNAUMWA HATA KAMA NI MAFUA
 
Hiyo inatokea mara nyingi tu japo sijui sababu ni nini?
Muathirika anapokuwa na good adherence mara nyingi hupelekea kuwa suppressed na hivyo uwezekano wa kuambukiza wengine kuwa mdogo sana au kutokuwepo kabisa kwa njia ya kujamiiana
 
Hii pia ilitokea kwa uncle wangu alipimwa akakutwa na VVU, ila alikataa kutumia ARV.

Mke wake hakumuacha waliendelea kugegedana kama kawaida. Miaka saba baadae mjomba alifariki na kwa miaka yote vipimo vilikuwa vinaonyesha kaathirika.

Lakini mkewe na watoto wake wawili hawana ngoma mpaka leo.

Kuna watu wana bahati sana.
 
Hii pia ilitokea kwa uncle wangu alipimwa akakutwa na VVU, ila alikataa kutumia ARV.

Mke wake hakumuacha waliendelea kugegedana kama kawaida.Miaka saba baadae mjomba alifariki na kwa miaka yote vipimo vilikuwa vinaonyesha kaathirika.

Lakini mkewe na watoto wake wawili hawana ngoma mpaka leo.Kuna watu wana bahati sana.
Mtu yoyote mwenye damu group A+ hapati ukimwi, hiyo damu ina cell Fulani ambazo ni kinga pekeee kwa magonjwa makubwa Kama ukimwi na mengneyo
 
mimi kuna moja ndio sijaielewa mpaka leo, mama ni HIV negative amezaa mtoto ambaye ni HIV positive,mume ni HIV positive. Ndoa ilivunjika baada ya majibu hayo,baba akaachiwa mtoto amlee na sasa hivi mtoto ni mkubwa approximately ten years.
 
DM MOWO, UKIMWI haumpati mtu mwenye damu group A+ watu wenye group hilo wana kinga maalum zinazozuia magonjwa makubwa Kama UKIMWI kumpata mtu, ila watu hao hupata magonjwa madogo madogo kirahisi mno
 
Hapa ndipo penye mkanganyiko wa ajabu kuhuhu UKIMWI. Theory zinazoletwa na akina kimsboy na Deception ndo zinapata nguvu nakuonekana UKIMWI is Just a Myth tuloletewa na wazungu.

Kipimo kinapima uwepo wa Kinga (sijui ndo Serology) Mwilini na sio uwepo wa Virus, kwamba kinga zikipungua ndo mtu anaukimwi wakati hata Mgonjwa TB kinga pia zinapungua.

Inamaana hapo Baba alikua anaumwa so kinga lazima zipungue na kipimo lazima kitasoma positive, mke na watoto hawaumwi ndo maana walikua negative.

Kuna Msemo niliupata unasema
USIENDE KUPIMA UKIMWI WAKATI UNAUMWA HATA KAMA NI MAFUA
 
Tudadavulie basi ili tupate maarifa ndiyo maana nikaleta uzi hapa ili tujue zaidi kutoka kwenu nyie wataalamu.
Mkuu heshima kwako, hiyo hali huwa inatokea na hakuna cha ajabu, kitaalam hao wanaitwa DISCORDANT COUPLES, zipo sababu ( theories ) za kisayansi za kwa nini hali hiyo hutokea
 
Kiziwanda chema,
Mkuu unaonekana knowledge yako kuhusu antibodies na antigen iko mbali sana na bado unacomment kuhusu hivyo vitu bila kujua unapotosha watu.

Kupungua kinga mwilini haimaanishi ukipima HIV unakuwa +ve.. maana hata mtu akiwa na mimba kinga inapungua kidogo lakini hawi HIV +ve...

Kwenye kipimo cha HIV wnaangalia antibondies ambazo ni specific kwa HIV tu... yaani mtu akiwa na hao virusi mwilini cell zake zinatoa hio antibody ambayo ni specific tu kwa HIV na hio antibody haiwezi kutolewa in response to infection yoyote ile tofauti na HIV....

Kuhusu kukaa na na mke au mume bila kupata hilo ni somo la siku nyingine
 
Back
Top Bottom