Fundi Madirisha
Senior Member
- Jun 30, 2020
- 184
- 986
Ninakishangaa sana chama ambacho ndicho kinatakiwa kua kinara katika kutii katiba ya nchi lakini kinafumbia na kukumbatia mambo ya ajabu kabisa.
Ni uvunjaji wa sheria na katiba ya nchi kuona kiongozi wa chama cha siasa tena mwenyekiti wa Wilaya kabisa bado ni mtumishi wa umma tena ni mkuu wa idara ya serikali. Hii siyo sawa na tunapaswa kukemea tabia kama hizi
Ndugu Ayubu Maandazi almaarufu kama Maandazi, mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Magu mkoani Mwanza ni mratibu Elimu kata anaendelea kupokea mshahara wa serikali huku ni kiongozi wa chama. Mtumishi wa aina hii atenda haki lini kwa watumishi wenzake wasiokua wana CCM?Je, katiba inaruhusu upuuzi kama huu?
Mtu unapokua kiongozi wa chama cha siasa unapaswa kua mtumishi wa umma? Huu siyo wizi ni kitu gani?
Tunaomba na kuvisihi vyombo vyetu vya kisheria kufuatilia jambo hili, nchi hii ni ya wote na hakuna aliye juu ya katiba.
Ni uvunjaji wa sheria na katiba ya nchi kuona kiongozi wa chama cha siasa tena mwenyekiti wa Wilaya kabisa bado ni mtumishi wa umma tena ni mkuu wa idara ya serikali. Hii siyo sawa na tunapaswa kukemea tabia kama hizi
Ndugu Ayubu Maandazi almaarufu kama Maandazi, mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Magu mkoani Mwanza ni mratibu Elimu kata anaendelea kupokea mshahara wa serikali huku ni kiongozi wa chama. Mtumishi wa aina hii atenda haki lini kwa watumishi wenzake wasiokua wana CCM?Je, katiba inaruhusu upuuzi kama huu?
Mtu unapokua kiongozi wa chama cha siasa unapaswa kua mtumishi wa umma? Huu siyo wizi ni kitu gani?
Tunaomba na kuvisihi vyombo vyetu vya kisheria kufuatilia jambo hili, nchi hii ni ya wote na hakuna aliye juu ya katiba.