Maajabu ya awamu ya tano, hakuna ajira mpya, wametoa watumishi hewa, hakuna nyongeza ya mishahara, lakini kila mwaka bajeti ya mishahara inapaa

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Mwezi March mwaka 2014 serikali ilitumia Bilioni 375.9 kulipa mishahara kwa watumishi (Salaries and wages). Kumbuka kipindi hicho kulikua na watumishi hewa, kulikua na watu wanalipwa mishahara miwili miwili, kulikua na nyongeza ya mishahara, na watumishi wapya waliajiriwa kila mwaka.

Kipindi kama hicho (mwezi March) Mwaka 2018 serikali ilitumia Bilioni 527.4 kulipa mishahara. Kipindi kama hicho mwaka huu, serikali imetumia Bilioni 557.6 kulipa mishahara. Hizi ni takwimu rasmi kama zilivyotolewa na Wizara ya Fedha na Mipango. Yani gharama ya kulipa mishahara imekua ikiongezeka mwaka hadi mwaka licha ya kuondolewa wafanyakazi hewa na dili nyingine feki.

Kwa wale wachumi daraja la kwanza, hii inawezekanaje? Yani unaondoa wafanyakazi hewa, unazuia nyongeza ya mishahara, unazuia ajira mpya lakini gharama ya kulipa mishahara inazidi kuongezek. JK aliwezaje kuwa na wafanyakazi hewa na wote wakalipwa, akaweka nyongeza ya mishahara kila mwaka kwa watumishi wote hadi wale hewa, na akaweza kuajiri maelfu kila mwaka kwa gharama ndogo? Who can explain this Economic paradox?

By G malisa
FB_IMG_1565965477126.jpg
 
CCM ni ile ile!!!

Hapo waulize wameajiri watumishi wangapi ku-justify hilo ongezeko la mishahara kama watakupa jibu la kuingia akilini.
 
Itakuwa ajira nyingi na pesa nyingi zimeenda katika vyombo vya usalama. Mfano majeshi yote yameongozewa maslahi mengi tu.
 
Kuna tabaka linaishi kama Malaika maumivu yapo kwa sisi huku wafagia uwanja kulipishwa Ultrasound walipishaji wanaishi kama wapo angan ila kila jambo lina mwisho
 
Kabla ya uhakiki Jiwe alisema serikali ilikuwa ikilipa wafanyakazi zaidi ya bilion 700 baada ya kuondoa watumishi hewa serikali ilianza kulipa b500 na ushee. Arafu mwezi wa saba mwaka huo 2014 JK aliongeza mshahara na kuongeza ajira mpya na Mwaka 2015 JK aliajiri tena wafanyakazi wengine na pia ulipofika mwezi wa saba aliongeza mshahara
 
Watanzania tuna nidhamu ya woga na hatuna ushirikiano ndio chanzo cha kuzaliwa huyu malaika mkuu!!
 
Niseme tumemwachia. Na yeye kishajua kuwa watanzania ni waoga. Hawawezi kihoji ndio maana kapitia hapo anatawala.
Tatizo a tz. Wanafki wengi
Watanzania tuna nidhamu ya woga na hatuna ushirikiano ndio chanzo cha kuzaliwa huyu malaika mkuu!!
 
Mwezi March mwaka 2014 serikali ilitumia Bilioni 375.9 kulipa mishahara kwa watumishi (Salaries and wages). Kumbuka kipindi hicho kulikua na watumishi hewa, kulikua na watu wanalipwa mishahara miwili miwili, kulikua na nyongeza ya mishahara, na watumishi wapya waliajiriwa kila mwaka.

Kipindi kama hicho (mwezi March) Mwaka 2018 serikali ilitumia Bilioni 527.4 kulipa mishahara. Kipindi kama hicho mwaka huu, serikali imetumia Bilioni 557.6 kulipa mishahara. Hizi ni takwimu rasmi kama zilivyotolewa na Wizara ya Fedha na Mipango. Yani gharama ya kulipa mishahara imekua ikiongezeka mwaka hadi mwaka licha ya kuondolewa wafanyakazi hewa na dili nyingine feki.

Kwa wale wachumi daraja la kwanza, hii inawezekanaje? Yani unaondoa wafanyakazi hewa, unazuia nyongeza ya mishahara, unazuia ajira mpya lakini gharama ya kulipa mishahara inazidi kuongezek. JK aliwezaje kuwa na wafanyakazi hewa na wote wakalipwa, akaweka nyongeza ya mishahara kila mwaka kwa watumishi wote hadi wale hewa, na akaweza kuajiri maelfu kila mwaka kwa gharama ndogo? Who can explain this Economic paradox?

By G malisaView attachment 1182924
Hali hiyo hutokana na kwamba kuna wafanyakazi wengi wamejiendeleza na masomo,sasa unakuta kama mtu alikuwa analipwa mshahara wa kidato cha nne anarekebishiwa anakuwa analipwa wa diploma au degree.
Kwa hali hiyo lazima gharama iongezeke hivyo tusiangalie upande mmoja mmoja u have to think beyond the perspective!
 
Back
Top Bottom