kidunula1
JF-Expert Member
- Apr 2, 2016
- 6,299
- 6,321
Salam wadau humu,
Daaa jumamosi iliyopita nilistaajabu sana huku. Yaani kuna Dada alifariki mwezi Wa saba tukahudhuria msiba,nikaaga ule mwili kwa kuuona kwa macho yangu halafu juzi akaonekana huku akiwa hai ila aliyevurugika Akili. Yaani kijiji kizima watu walikuwa kama wapo msibani mana kila kona habari zilikuwa ni huyo Dada na hadi sasa huku habari ni hizohizo na watu wanaendelea kumiminika nyumbani kwao na huyo Dada ili kumuona utadhani ni kipindi kile kule Loliondo. Niliwaza sana.
Kabla ya kifo chake huyo Dada alikuwa na magunia ya mpunga kama 80 hivi, na ng'ombe kadhaa, kajumba kake na kiwanja pamoja na cherehani vitu ambavyo vyote viliuzwa na ndugu Mara tu baada ya kifo chake. Na aliporudi hyo juzi vitu pekee alivyoweza kuwauliza watu wakamuelewa ni hayo magunia yake ya mpunga, ng'ombe na cherehani yake.
Sura ya huyo Dada tangu arudi imekuwa ikibadilika badilika, Mara awe mweusi Mara awe maji ya kunde. Na haongei tena kiluga anaongea kiswahili kilichonyooka. Polisi walikuja wakamcheki wakawauliza ndugu waliodai huyo kiumbe ndiye ndugu yao alozikwa mwezi Wa saba. Ndugu hao walidai sura ya ndugu yao imebadilika kwa kiasi Fulani ila alama zote za mwilini zilifanya waamini yule ni ndugu yao. Baada ya hapo polisi walimuhojihoji huyo Dada japo hawakupata ushirikiano vema mana dishi lilionekana kuyumba kisha wakaondoka na kuwaachia ndugu huyo ndugu yao
Wataalamu Wa haya mambo kama wapo humu watufafanulie vizuri mazingira ya namna hii huwa ni nini hasa na inawezekanaje?
Jambo hili limetokea Wilaya ya Kwimba ktk kijiji cha Sanga.
Daaa jumamosi iliyopita nilistaajabu sana huku. Yaani kuna Dada alifariki mwezi Wa saba tukahudhuria msiba,nikaaga ule mwili kwa kuuona kwa macho yangu halafu juzi akaonekana huku akiwa hai ila aliyevurugika Akili. Yaani kijiji kizima watu walikuwa kama wapo msibani mana kila kona habari zilikuwa ni huyo Dada na hadi sasa huku habari ni hizohizo na watu wanaendelea kumiminika nyumbani kwao na huyo Dada ili kumuona utadhani ni kipindi kile kule Loliondo. Niliwaza sana.
Kabla ya kifo chake huyo Dada alikuwa na magunia ya mpunga kama 80 hivi, na ng'ombe kadhaa, kajumba kake na kiwanja pamoja na cherehani vitu ambavyo vyote viliuzwa na ndugu Mara tu baada ya kifo chake. Na aliporudi hyo juzi vitu pekee alivyoweza kuwauliza watu wakamuelewa ni hayo magunia yake ya mpunga, ng'ombe na cherehani yake.
Sura ya huyo Dada tangu arudi imekuwa ikibadilika badilika, Mara awe mweusi Mara awe maji ya kunde. Na haongei tena kiluga anaongea kiswahili kilichonyooka. Polisi walikuja wakamcheki wakawauliza ndugu waliodai huyo kiumbe ndiye ndugu yao alozikwa mwezi Wa saba. Ndugu hao walidai sura ya ndugu yao imebadilika kwa kiasi Fulani ila alama zote za mwilini zilifanya waamini yule ni ndugu yao. Baada ya hapo polisi walimuhojihoji huyo Dada japo hawakupata ushirikiano vema mana dishi lilionekana kuyumba kisha wakaondoka na kuwaachia ndugu huyo ndugu yao
Wataalamu Wa haya mambo kama wapo humu watufafanulie vizuri mazingira ya namna hii huwa ni nini hasa na inawezekanaje?
Jambo hili limetokea Wilaya ya Kwimba ktk kijiji cha Sanga.