Maafisa wa UN waliofukuzwa Ethiopia waondoka

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Maafisa saba wa mashirika ya Umoja wa mataifa ya kibinadamu waliofukuzwa nchini Ethiopia hawako tena nchini humo, Umoja wa mataifa umesema Jumatatu.

Msemaji wa Umoja wa mataifa Farhan Haq amesema “ waliondolewa nchini humo ili kuhakikisha usalama wao”.

Alhamisi, serikali ya waziri mkuu Abiy Ahmed iliwapa saa 72 maafisa hao wawe wameondoka Ethiopia. Serikali ilidai walikuwa wanaingilia masuala ya ndani ya nchi, na kuongeza tuhuma nyingine dhidi yao, ikiwemo kupeleka misaada na vifaa vya mawasiliano ya simu kwa waasi wa Tigray People’s Liberation Front ( TPLF).

Alhamisi, katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Antonio Guterres alielezea mshtuko wake, wakati wa taarifa hiyo, na Ijumaa alizungumza moja kwa moja na Abiy.

Maafisa waliyofukuzwa ni pamoja na naibu mkuu wa Umoja wa mataifa wa masuala ya misaada ya kibinadamu, naibu mratibu wa misaada ya kibinadamu, na mwakilishi wa shirika la Umoja wa mataifa linalohudumia watoto ( UNICEF).

Umoja huo umesema kwamba, Ethiopia haina msingi wa kisheria wa kufukuza wafanyakazi wake.

Chanzo: VOA Swahili
 
Maafisa saba wa mashirika ya Umoja wa mataifa ya kibinadamu waliofukuzwa nchini Ethiopia hawako tena nchini humo, Umoja wa mataifa umesema Jumatatu.

Msemaji wa Umoja wa mataifa Farhan Haq amesema “ waliondolewa nchini humo ili kuhakikisha usalama wao”.

Alhamisi, serikali ya waziri mkuu Abiy Ahmed iliwapa saa 72 maafisa hao wawe wameondoka Ethiopia. Serikali ilidai walikuwa wanaingilia masuala ya ndani ya nchi, na kuongeza tuhuma nyingine dhidi yao, ikiwemo kupeleka misaada na vifaa vya mawasiliano ya simu kwa waasi wa Tigray People’s Liberation Front ( TPLF).

Alhamisi, katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Antonio Guterres alielezea mshtuko wake, wakati wa taarifa hiyo, na Ijumaa alizungumza moja kwa moja na Abiy.

Maafisa waliyofukuzwa ni pamoja na naibu mkuu wa Umoja wa mataifa wa masuala ya misaada ya kibinadamu, naibu mratibu wa misaada ya kibinadamu, na mwakilishi wa shirika la Umoja wa mataifa linalohudumia watoto ( UNICEF).

Umoja huo umesema kwamba, Ethiopia haina msingi wa kisheria wa kufukuza wafanyakazi wake.

Chanzo: VOA Swahili
Duh, watu hawaelewi😂
 
Back
Top Bottom