Maafisa wa Kampuni ya TOTAL watembelea bandari ya Dar

REDEEMER.

JF-Expert Member
Feb 22, 2015
8,925
14,880
Maofisa wa ngazi ya Juu kutoka Kampuni ya mafuta TOTAL wametembelea Bandari ya Dar es Salaam kuangalia miundombinu ya Bandari hasa hali ya njia za reli TRC na maeneo ya kuhudumia meli. TOTAL itatumia Bandari ya Dar kuingiza vifaa vya mradi wa bomba la mafuta wa Tanzania -Uganda.
IMG_20190223_124443.jpg


IMG_20190223_124437.jpg

IMG_20190223_124448.jpg
 
cha ajabu ni bomba refu kuliko yote duniani la mafuta la kupashwa moto (heated) linajengwa, na zaidi ya aslimia 75 litakuwa Tanzania
Atajua saa ngapi kama Lissu hajampotosha? Hawa wapo programmed na pumba kama MIGA tofauti na hapo hakuna walijualo
 
ushauri: mizigo midogo inayoweza kupitia Tanga ipitie Tanga kuinua na shughuli za uchumi upande huo pia
Ni kweli, saivi wameshaanza na shehena ya mafuta yote ya kaskazini lazima yapite Tanga, naona TPA ipo kwenye utekelezaji wa bandari kavu Arusha na reli ya kaskazini nayo inafufuliwa mpaka 2020 mizigo itaanza kushuka kwa wingi Tanga na lengo ni kuliteka mpaka soko la Kenya kusini.
 
Wale wapinga kila kitu lazima wakutukane, hivyo kaa mkao wa kupokea mitusi ya namna tofauti toka kwa hao vijana wa Lissu
 
ushauri: mizigo midogo inayoweza kupitia Tanga ipitie Tanga kuinua na shughuli za uchumi upande huo pia
Waligoma kuupitisha mzigo tanga maana garama zinaongezeka kwasababu ya double handling, hii nimara ya pili sasa wanakuja kuikagua hiyo port yetu huyo Mr Guy Heisbourg mwenye viatu vya brown na miwani nyeusi ni mtata sana anajua hayo maswala ya usafirishaji wa mafuta sana duniani, akisema kitu kifanyike ni lazima kifanyike mkienda nae tofauti basi kila kitu kina simama.watakagua zaidi ya mara tano au sita hapo bandarini.
 
NASEMAJE wenye wivu wajinyonge.
VIVA JPM govt.
Badala ya kusema viva jpm ungeeleza faida za hilo bomba kupita nchini hapo utaanza tupiana maneno na waupande wapili, mara nyingi tujikite kwenye hoja mkuu itasaidia kuleta uwelewesho kwa wengine, kunasiku mtu mmoja alileta mjadala hapa kwamba huo mradi umeyeyuka nilipo mjibu alielewa na tukawa sawa,soma niliandika nini mara ya kwanza hapo juu kuna mabo mengi sana ktk huu mradi sio lele mama ni mradi amabao unachangamoto nyingi sana ktk utekelezaji wake sasa niwangapi wanajua hilo?
 
Back
Top Bottom