MP CHACHANDU
JF-Expert Member
- Dec 4, 2016
- 875
- 615
Ni kweli kwamba maafisa utumishi wote wa serikali ya awamu hii ya tano wanafanya kazi chini ya kiwango kwa hofu ya kufukuzwa kazi hivyo kuzifanya taasisi za serikali kushindwa kufanya kazi zilizokusudiwa mfano kwenye taasisi nyingi za serikali kumekuwepo na ukosefu wa vifaa na rasimali watu lakini hawa maafisa utumishi wanaogopa kupeleka matatizo hayo ngazi za juu za serikali kwa hofu ya kwamba watafukuzwa kazi wakipeleka matatizo hivyo kusababisha sisi wananchi tuumie na kushindwa kupata huduma bora.
Pili watumishi wa umma amepatwa na matatizo mbalimbali mfano kusimamishiwa mishahara bila kosa ,kushindwa kulipwa malimbikizo yao ,kushindwa kupandishwa vyeo nk lakini maafisa utumishi wamekuwa wakikwepa kutatua changamoto hizi kwa kuhofia kutumbuliwa na viongozi wa ngazi za juu.
Tatu, maafisa utumishi wa mahakama zote Tanzania ndiyo wanahofu kuzidi idara zote za utumishi wa umma nchini mfano ,waliwaajiri vijana 485 mwezi June 2016 na kuwapa mikataba yote ya kazi na kuanza kazi na waliwalipa mpaka na pesa za kujikimu lakini wakawarudisha nyumbani ili kupisha zoezi LA uhakiki wa watumishi hewa uhakiki umeisha hata hao vijana hawajarudishwa kazini maafisa utumishi wa mahakama nchini wanaogopa kuwarudisha waajiriwa hawa wao maafisa utumishi wa mahakama wanaogopa kutumbuliwa .
Pili watumishi wa umma amepatwa na matatizo mbalimbali mfano kusimamishiwa mishahara bila kosa ,kushindwa kulipwa malimbikizo yao ,kushindwa kupandishwa vyeo nk lakini maafisa utumishi wamekuwa wakikwepa kutatua changamoto hizi kwa kuhofia kutumbuliwa na viongozi wa ngazi za juu.
Tatu, maafisa utumishi wa mahakama zote Tanzania ndiyo wanahofu kuzidi idara zote za utumishi wa umma nchini mfano ,waliwaajiri vijana 485 mwezi June 2016 na kuwapa mikataba yote ya kazi na kuanza kazi na waliwalipa mpaka na pesa za kujikimu lakini wakawarudisha nyumbani ili kupisha zoezi LA uhakiki wa watumishi hewa uhakiki umeisha hata hao vijana hawajarudishwa kazini maafisa utumishi wa mahakama nchini wanaogopa kuwarudisha waajiriwa hawa wao maafisa utumishi wa mahakama wanaogopa kutumbuliwa .