Bill
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 8,278
- 8,493
Nimekuwa nikijiuliza kila mara niingiapo UBT (Ubungo Bus Terminal) alfajiri hadi saa 1 hivi asubuhi na kukuta msongamano mkubwa wa Mabasi yaendayo mikoani, magari madogo ya wasindikizaji, Taxi, abiria na wasindikizaji wao bila kuwasahau Madereva, Makonda, wapiga debe na hata wafanyakazi mbalimbali wa UBT na mabasi. Swali ninalojiuliza ni hili, " Je siku moto ukiwaka hapa stendi kuanzia majira ya saa 11:30 hadi 12 hivi asubuhi nini kitatokea?" Hakika ni maafa makubwa.
Ni maafa makubwa kwa nini? Hii stendi ina Milango 3 ya kuingilia na kutokea kwa mabasi na magari. Milango ya abiria ndio hivyo tena inakuruhusu kuingia tu lakini wakati wa kutoka unatumia kimlango kimoja. Katika Mazingira haya unategemea utawezaje kuokoa watu pamoja na mabasi/magari kwa uharaka kwa kutumia hii milango iliyopo?
Nashawishika kuamini kwamba hawa wasimamizi wetu (Serikali), kama ilivyowahi kutokea huko Mwanza na Bukoba (MV-Bukoba) na sasa Zanzibar (MV - Spice), ni wazembe.
Ukifika Ubungo pale, ile asubuhi, ni lazima utaogopa. Hivi kweli hii serikali yetu inawatu wanaotafiti (identify), kutathmini (assessment) na kutafuta namna ya kudhibiti (Manage) majanga/hatari hizi (Risks) kabla hazijatokea? Haingii akili kuona unasubiri kwanza maisha na mali za watu ziteketee ndio uuende tume. Kwa nini msifanye tafiti mapema hasa katika maeneo yanayogusa maisha ya watu kama vile maeneo ya usafiri, mikusanyiko ya watu na mkachukua hatua mapema, basi kama sio kuzuia majanga basi iwe kupunguza athari zitokanazo na majanga haya.
Ubungo Bus Terminal ni janga lingine linalosubiriwa kutokea (Mungu apishe mbali) na hatari kubwa ni kwamba mabasi na baadhi ya abiria hasa wazee na watoto, walemavu na wagonjwa hawataweza kujiokoa.
Tusisubiri kila kitu kukielekeza kwa Mungu tikidai ni mitihani yake wakati ni Uzembe wetu tena tena uliowazi. Chukueni hatua......
Ni maafa makubwa kwa nini? Hii stendi ina Milango 3 ya kuingilia na kutokea kwa mabasi na magari. Milango ya abiria ndio hivyo tena inakuruhusu kuingia tu lakini wakati wa kutoka unatumia kimlango kimoja. Katika Mazingira haya unategemea utawezaje kuokoa watu pamoja na mabasi/magari kwa uharaka kwa kutumia hii milango iliyopo?
Nashawishika kuamini kwamba hawa wasimamizi wetu (Serikali), kama ilivyowahi kutokea huko Mwanza na Bukoba (MV-Bukoba) na sasa Zanzibar (MV - Spice), ni wazembe.
Ukifika Ubungo pale, ile asubuhi, ni lazima utaogopa. Hivi kweli hii serikali yetu inawatu wanaotafiti (identify), kutathmini (assessment) na kutafuta namna ya kudhibiti (Manage) majanga/hatari hizi (Risks) kabla hazijatokea? Haingii akili kuona unasubiri kwanza maisha na mali za watu ziteketee ndio uuende tume. Kwa nini msifanye tafiti mapema hasa katika maeneo yanayogusa maisha ya watu kama vile maeneo ya usafiri, mikusanyiko ya watu na mkachukua hatua mapema, basi kama sio kuzuia majanga basi iwe kupunguza athari zitokanazo na majanga haya.
Ubungo Bus Terminal ni janga lingine linalosubiriwa kutokea (Mungu apishe mbali) na hatari kubwa ni kwamba mabasi na baadhi ya abiria hasa wazee na watoto, walemavu na wagonjwa hawataweza kujiokoa.
Tusisubiri kila kitu kukielekeza kwa Mungu tikidai ni mitihani yake wakati ni Uzembe wetu tena tena uliowazi. Chukueni hatua......