Kweli kabisa mkuu. Mishahara ikipanda tu bidhaa na huduma zitapanda bei maisha yatakuwa magumu sana kwa wapigakura. Chondechonde Rais Samia usipandishe mishahara hata kwa senti moja mama yetu mpendwa.Mshahara unatosha. Akipandisha vitu vitspanda
Hiyo fedha iliyofujwa na wahuni wachache kwanini haiwanufaishi watumishi?
Huu uchawi sasaMshahara unatosha. Akipandisha vitu vitspanda
Wanaofuja fedha nao ni wazalendo kwa kuwa fedha wanazofuja zinaongeza mzunguko wa fedha mtaani hivyo kuwanufaisha wapigakura. Wafujaji wanapaswa kupongezwa kwa kitendo hiki cha uzalendo.Hiyo fedha iliyofujwa na wahuni wachache kwanini haiwanufaishi watumishi?
Kwakuwa mnakula za ufisadi hapo kwenu sio?Mshahara unatosha. Akipandisha vitu vitspanda
DidomaHizi sherehe zinafanyikia wapi kitaifa
DodomaHii mei mosi kitaifa inafanyika wapi?
Ni kufurahi kwa kwenda mbele.Wahenga walisema usiku wa deni haukawii kukucha. Leo wafanyakazi wa Tanzania wanaungana na wafanyakazi kutoka pembe zote za dunia kuadhimisha siku ya wafanyakazi, maarufu kama Mei Mosi. Mtakumbuka mwaka jana Rais wa Tanzania Hon Samia Suluhu Hassan aliaahidi kuwaongezea mishahara wafanyakazi siku ya leo tarehe 1/5/2022 kama alivyonukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari.
Leo ndio leo, asemaye kesho ni muwongo! Leo lazima mbivu na mbichi zijulikane. Lakini pamoja na ahadi hiyo ambayo Rais aliitoa kwa uhakika, wafanyakazi wajiandae kwa jibu lolote la kukera litakalotolewa siku ya leo kwani mvumilivu hula mbivu. Waendelee tu kuvumilia huku wakila mtori kwa kuwa nyama ziko chini. Unapokula mtori hupaswi kuwa na wasiwasi kwani baada ya kumaliza mtori utazikuta nyama tele chini ya bakuli.
Hata hivyo, habari zinazojipenyeza ni kuwa huenda vita ya Ukraine na Urusi ikachangia mama Samia kutokuwaongezea wafanyakazi mishahara kwa sababu vita hii imeangusha uchumi wa nchi zote duniani, ikiwemo Tanzania kama anavyotupenyezea taarifa mdau huyu hapa chini
Uhakika: Jinsi Vita ya Urusi na Ukraine Itakavyokwamisha Upandishaji wa Mishahara ya Wafanyakazi
Tuendelee kufuatilia nini kitakachotokea siku hii ya leo kwani ni siku mbayo ama wafanyakazi watalia au watatoka na kicheko. Stay tuned!
Vitu vimepanda maradufu,je ni miaka mingapi mishahara haijaongezwa?Mshahara unatosha. Akipandisha vitu vitspanda
Kuna ukweli katika hiyo kauli yako?Kwa sasa kipaumbele ni msoga unit na urojo family wafanyakazi tuendelee kuumia. Hii nchi aisee
Mama urojo ametoka mamtoni alikokua anaponda kuku kwa mrija kwa week mbili akivunja record ya ziara ya bata mamtoni tangu kupapa uhuru, je unataka ushahidi gani kupinga ukweli ni zamu ya team urojoKuna ukweli katika hiyo kauli yako?
Ndio maana niliwapa tahadhari mapema kuhusu hili jambo lakini wengine wakaishia kunibagaza na kuniona bazazi. kiko wapi sasa?Vitu vimepanda maradufu,je ni miaka mingapi mishahara haijaongezwa?
Nashauri hizi nyongeza za mishahara zitungiwe sheria na kanuni isiwe hisani ya wanasiasa hasa Rais.
Na sahivi atakuwa anajiandaa kusafiri tenaMama urojo ametoka mamtoni alikokua anaponda kuku kwa mrija kwa week mbili akivunja record ya ziara ya bata mamtoni tangu kupapa uhuru, je unataka ushahidi gani kupinga ukweli ni zamu ya team urojo
Tetete kwa hiyo kaupiga mwingi?Mbona hakupandisha lakini tayari bidhaa zilishapanda mapema sana, tena hata kabla ya vita vya Ukraine na Russia
Hivi huwa mnafikiri kabla ya kuongea au ilimradi tu nanyi mmeonekana hapa JF
Heri aghairi kabisa au kupunguza bajeti ya gharama yoyote ile kati ya vipaumbele mojawapo kiuwekezaji 2022/23, kuliko kuvunja rekodi ya UNAFKI kwa kuahidi watu kupandisha mishahara kisha kutopandisha.
Ni mwaka wa 7 sasa mishahara haijapandishwa huku hali mitaani kiuchumi ikiwa tete kabisa.
Natumai Mama ataupiga mwingi, ili CHAWA tuje tuzagae hapa JF kusifia hata visivyostahili kusifiwa, sababu ongezeko la mishahara kwa wafanyakazi siyo hisani bali ni haki yao kisheria, duniani kote