Maadhimisho ya Siku ya Sheria: Spika Ndugai asema Bunge linajitahidi kuhakikisha kazi zake hazivuki mstari

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Spika Job Ndugai amesema Bunge la Tanzania linaahidi kutoa ushirikiano pale wanapohitajika akiongeza, watajitahidi kuhakikisha muhimili wa Mahakama unaheshimiwa ndani ya nje ya Bunge.

Ameeleza hayo leo katika maadhimisho ya Siku ya Sheria na miaka 100 ya Mahakama Kuu Jijini Dodoma, ambapo miongoni mwa masuala mengine amesema, jukumu la Mahakama kutoa Haki ni zito na linahitaji hofu ya Mungu.

Aidha, amesema kuna mashauri mengi yanayoshughulikiwa na Viongozi wa chini bila kufika Mahakamani. Ameomba kundi hilo kusimamia na kuwatendea Haki Watanzania, akisisitiza adui mkubwa katika ngazi za chini ni Rushwa.
 
Muulize na wale Covid 19 wapo kwa mujibu wa sheria kifungu Cha ngapi?

Au ni wagombea binafisi?
 
Tunakushukuru sana Spika Ndugai kwa ujumbe wako huo murua kabisa.

Mbali ya mhimili wa Mahakama, pia kuna haja hata maeneo mengine ya utoaji haki uzingatie huo ushauli uliotolewa na Mh. Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mbali ya Mahakama kuna maeneo mengine kama TUME YA UTUMISHI WA UMMA ambapo mojawapo ya kazi zake ni kusikiliza na kutatua migogoro ya kazini, kati ya mwajiri na mwajiriwa.

Ni muhimu sana TUME YA UTUMISHI WA UMMA walijue hilo kwasababu ni mojawapo ya taasisi zinazosimamia na kutoa haki.

Kama ilivyoelezwa, TUME ijikite kutoa haki kwa kumtanguliza Mungu bila ya upendeleo wowote, maana inaaminika kuwa kumekuwa na kawaida ya waajiri kuirubuni au kushinikiza TUME ili kuwakandamiza watumishi walioko kwenye mgogoro na mwajiri wao.

Inasemekana kuwa kuna baadhi ya wajumbe wa TUME wamekuwa wakiwa-influence wajumbe wenzao ili kutoa uamuzi ambao ni biased kwa kumkandamiza mtumishi, na kuwa slow kushughulikia matatizo ya watumishi.

Asante,
 
Tutamlaumu Ndugai bure
Sio bunge wala mahakama
Kuna mtu fulani yeye Ndio kila kitu na amenukuliwa akisema 'mimi ukinishauri Ndio unaniharibia kabisa'
Anyways..
Sio Mitano tena ni milele kabisa
Nchi hii ni tajiri sana
Tupo Uchumi wa kati
Au nasema uongo ndugu zanguuuuu
Mnayajua mavieitee nyinyi!!!
Sisi tunatembelea mavieitee! 😎😎😎
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom