beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Zanzibar inaadhimisha miaka 57 ya Mapinduzi leo na baadhi ya masuala aliyozungumzia Rais Hussein Mwinyi katika hotuba yake ni kama ifuatavyo:
Dkt. Hussein Mwinyi amesema Zanzibar inapaswa kuleta Mapinduzi katika sekta ya Uvuvi ili wavuvi waweze kuvua kwa zana za kisasa, na rasilimali za Bahari kuu ziweze kuwanufaisha Wazanzibari.
Kuhusu sekta ya Kilimo, Rais Mwinyi amesema ni lazima kuwe na Mapinduzi ili Wakulima wapate kuongeza tija, kuinua mazao ya Karafuu na Mwani, na vilevile kuondoa utegemezi wa Chakula kutoka nje.
Akizungumzia Sheria na Taasisi, Dkt. Mwinyi amesema Mapinduzi ni muhimu ili kumuwezesha Mzanzibari mwenye #Biashara kufanya shughuli zake bila vikwazo.
Aidha, amesema Mapinduzi yanahitajika kwenye Utumishi wa Umma kujenga Uwajibikaji, kuboresha huduma pamoja na maslahi ya Watumishi wa Umma.
Amesisitiza kuwa, Mapinduzi hayo yanawezekana ikiwa Uchumi utafunguliwa kwa kuweka mazingira mazuri ya ukuaji na Makusanyo ya Kodi yakiongezeka.
Dkt. Hussein Mwinyi amesema Zanzibar inapaswa kuleta Mapinduzi katika sekta ya Uvuvi ili wavuvi waweze kuvua kwa zana za kisasa, na rasilimali za Bahari kuu ziweze kuwanufaisha Wazanzibari.
Kuhusu sekta ya Kilimo, Rais Mwinyi amesema ni lazima kuwe na Mapinduzi ili Wakulima wapate kuongeza tija, kuinua mazao ya Karafuu na Mwani, na vilevile kuondoa utegemezi wa Chakula kutoka nje.
Akizungumzia Sheria na Taasisi, Dkt. Mwinyi amesema Mapinduzi ni muhimu ili kumuwezesha Mzanzibari mwenye #Biashara kufanya shughuli zake bila vikwazo.
Aidha, amesema Mapinduzi yanahitajika kwenye Utumishi wa Umma kujenga Uwajibikaji, kuboresha huduma pamoja na maslahi ya Watumishi wa Umma.
Amesisitiza kuwa, Mapinduzi hayo yanawezekana ikiwa Uchumi utafunguliwa kwa kuweka mazingira mazuri ya ukuaji na Makusanyo ya Kodi yakiongezeka.