Ma-First Lady wa Afrika na dhana ya ukoloni mamboleo.... a.k.a. Utandawizi

MwanaHaki

R I P
Oct 17, 2006
2,401
705
Alipokuwapo Mama Maria Nyerere enzi zake Ikulu, kazi yake ilikuwa ni moja tu. Kulea watoto na kumsaidia mumewe. Basi.

Akafuata Mama Sitti Mwinyi, naye alifanya hivyo hivyo.

Tatizo lilianza pale walipokuja hawa "wasomi", akianzia Anna Mkapa. Ikaanzishwa dhana ya First Lady. Ikabuniwa EOTF. Kazi kwa kwenda mbele... kila 'misaada' ya wafadhili ilipokuja ilipitia EOTF, ukiritimba fulani ukajengeka pale....

Kwa Mwalimu Salma Kikwete (Ualimu si kazi ya kustaafu...), mambo ni yale yale na WAMA.

Sasa tujiulize...

Hii dhana ya First Lady inamsaidia nani haswa? Kwa nini tuwe na "Mama wa Kwanza", kama wataalam wa Kiswahili walivyodadavua....

Kisha, tujiulize zaidi...

Hizo NGO za hawa ma-First Lady (tukianzia Tanzania) zinawasaidia nani haswa, ikizingatiwa kwamba wanapoondoka Ikulu wanaondoka nazo, na wakiwa Ikulu wanatumia rasilmali za Taifa... majengo ya ofisi, magari ya Ikulu, pesa za walipakodi, n.k.

Ma-First Lady wa Afrika wana taasisi yao, inaitwa OAFLA - Organisation of African First Ladies (Home | Organization of African First Ladies against HIV/AIDS).

Huu utandawazi wa kuiga kila kitu cha MZUNGU unatupeleka pabaya. Iko siku wananchi - wenye nchi - watadai haki zao... iko siku!

./Mwana wa Haki
 
kwa bongo first lady mama mkapa alikuwa mbunifu zaidi na ameset trend wote wanaofuata wanaiga..muda si mrefuu tutaona madhara ya kuiga bila kuwa na passion na uwezo nachoo..

EOTF mpaka sasa imefanya kazi nzuri kuwanyanyua akina mama wajasiriamali nchini..
 
kwa mujibu wa protokoli za diplomasia ( na maybe usalama wa taifa), first lady anatakiwa kupatiwa ulinzi masaa 24 na hivyo kuweka ugumu kwa hawa ma first lady kuendelea na shughuli walizokuwa nazo kabla ya kuukwaa u first lady.

mama hawa ambao wamekuwa wakifanya kazi day in day out ( na pengine kuwa na kipato kuliko cha waume zao na kuendesha familia wakati mwengine) hawangependa kukaa tu nyumbani kwa kuwa MUMEWE amepata cheo.

ndio nafikiri wanajikuta wakianzisha hizi NGO angalau ziwashughulishe kidogo
 
Labda wanaziitaji hizo NGO kuondoa stress; si unajua hadi kufuli a.k.a chupi za waume zao zinafuliwa na usalama wa taifa.
atafanya nini sasa!!?.

Na walio wengi mawazo hayo ya kuanzisha NGO huwa si yao; kuna wajanja ujipendekeza na kuwatumia.
 
Labda wanaziitaji hizo NGO kuondoa stress; si unajua hadi kufuli a.k.a chupi za waume zao zinafuliwa na usalama wa taifa.
atafanya nini sasa!!?.

Mkuu,

hivi kuna uhusiano kati ya neno "dope" na "doup"?
 
Alipokuwapo Mama Maria Nyerere enzi zake Ikulu, kazi yake ilikuwa ni moja tu. Kulea watoto na kumsaidia mumewe. Basi.

Akafuata Mama Sitti Mwinyi, naye alifanya hivyo hivyo.

Tatizo lilianza pale walipokuja hawa "wasomi", akianzia Anna Mkapa. Ikaanzishwa dhana ya First Lady. Ikabuniwa EOTF. Kazi kwa kwenda mbele... kila 'misaada' ya wafadhili ilipokuja ilipitia EOTF, ukiritimba fulani ukajengeka pale....

Kwa Mwalimu Salma Kikwete (Ualimu si kazi ya kustaafu...), mambo ni yale yale na WAMA.

Sasa tujiulize...

Hii dhana ya First Lady inamsaidia nani haswa? Kwa nini tuwe na "Mama wa Kwanza", kama wataalam wa Kiswahili walivyodadavua....

Kisha, tujiulize zaidi...

Hizo NGO za hawa ma-First Lady (tukianzia Tanzania) zinawasaidia nani haswa, ikizingatiwa kwamba wanapoondoka Ikulu wanaondoka nazo, na wakiwa Ikulu wanatumia rasilmali za Taifa... majengo ya ofisi, magari ya Ikulu, pesa za walipakodi, n.k.

Ma-First Lady wa Afrika wana taasisi yao, inaitwa OAFLA - Organisation of African First Ladies (Home | Organization of African First Ladies against HIV/AIDS).

Huu utandawazi wa kuiga kila kitu cha MZUNGU unatupeleka pabaya. Iko siku wananchi - wenye nchi - watadai haki zao... iko siku!

./Mwana wa Haki
Mwanahaki,
Umesahau Mama Sitti ndiye aliyekuwa mjasiriamali wa kwanza Ikulu. Huyu ndiye aliyetuuzia bia za Stella Artois na majenereta ya umeme.
Nilitaka tu kuliweka hilo sawa.
 
kwa bongo first lady mama mkapa alikuwa mbunifu zaidi na ameset trend wote wanaofuata wanaiga..muda si mrefuu tutaona madhara ya kuiga bila kuwa na passion na uwezo nachoo..

EOTF mpaka sasa imefanya kazi nzuri kuwanyanyua akina mama wajasiriamali nchini..
Mkuu wangu Mama Mkapa hakuset trend yoyote kaikuta EOTF na kaweza kuitumia kwa manufaa yake zaidi.She is a business woman haya maswala ya First Lady yameangukia mguuni kwake akiwa pekee na goli wazi hakuna hata goolkeeper.. akatufunga kwa kisigino.
 
Mwanahaki,
Umesahau Mama Sitti ndiye aliyekuwa mjasiriamali wa kwanza Ikulu. Huyu ndiye aliyetuuzia bia za Stella Artois na majenereta ya umeme.
Nilitaka tu kuliweka hilo sawa.


Alikwenda mbali zaidi kwani kulikuwa na tetesi kuwa ana plots 1000 hapa Dar!:pray:
 
Mkuu wangu Mama Mkapa hakuset trend yoyote kaikuta EOTF na kaweza kuitumia kwa manufaa yake zaidi.She is a business woman haya maswala ya First Lady yameangukia mguuni kwake akiwa pekee na goli wazi hakuna hata goolkeeper.. akatufunga kwa kisigino.

I love JF!:lock1:
 
hivi mbona wake au waume wa mabalozi hawataki kufanya kazi maana wanawakilisha nchi sasa hawa kwann wanafanya kazi lakini???
 
Back
Top Bottom