MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Alipokuwapo Mama Maria Nyerere enzi zake Ikulu, kazi yake ilikuwa ni moja tu. Kulea watoto na kumsaidia mumewe. Basi.
Akafuata Mama Sitti Mwinyi, naye alifanya hivyo hivyo.
Tatizo lilianza pale walipokuja hawa "wasomi", akianzia Anna Mkapa. Ikaanzishwa dhana ya First Lady. Ikabuniwa EOTF. Kazi kwa kwenda mbele... kila 'misaada' ya wafadhili ilipokuja ilipitia EOTF, ukiritimba fulani ukajengeka pale....
Kwa Mwalimu Salma Kikwete (Ualimu si kazi ya kustaafu...), mambo ni yale yale na WAMA.
Sasa tujiulize...
Hii dhana ya First Lady inamsaidia nani haswa? Kwa nini tuwe na "Mama wa Kwanza", kama wataalam wa Kiswahili walivyodadavua....
Kisha, tujiulize zaidi...
Hizo NGO za hawa ma-First Lady (tukianzia Tanzania) zinawasaidia nani haswa, ikizingatiwa kwamba wanapoondoka Ikulu wanaondoka nazo, na wakiwa Ikulu wanatumia rasilmali za Taifa... majengo ya ofisi, magari ya Ikulu, pesa za walipakodi, n.k.
Ma-First Lady wa Afrika wana taasisi yao, inaitwa OAFLA - Organisation of African First Ladies (Home | Organization of African First Ladies against HIV/AIDS).
Huu utandawazi wa kuiga kila kitu cha MZUNGU unatupeleka pabaya. Iko siku wananchi - wenye nchi - watadai haki zao... iko siku!
./Mwana wa Haki
Akafuata Mama Sitti Mwinyi, naye alifanya hivyo hivyo.
Tatizo lilianza pale walipokuja hawa "wasomi", akianzia Anna Mkapa. Ikaanzishwa dhana ya First Lady. Ikabuniwa EOTF. Kazi kwa kwenda mbele... kila 'misaada' ya wafadhili ilipokuja ilipitia EOTF, ukiritimba fulani ukajengeka pale....
Kwa Mwalimu Salma Kikwete (Ualimu si kazi ya kustaafu...), mambo ni yale yale na WAMA.
Sasa tujiulize...
Hii dhana ya First Lady inamsaidia nani haswa? Kwa nini tuwe na "Mama wa Kwanza", kama wataalam wa Kiswahili walivyodadavua....
Kisha, tujiulize zaidi...
Hizo NGO za hawa ma-First Lady (tukianzia Tanzania) zinawasaidia nani haswa, ikizingatiwa kwamba wanapoondoka Ikulu wanaondoka nazo, na wakiwa Ikulu wanatumia rasilmali za Taifa... majengo ya ofisi, magari ya Ikulu, pesa za walipakodi, n.k.
Ma-First Lady wa Afrika wana taasisi yao, inaitwa OAFLA - Organisation of African First Ladies (Home | Organization of African First Ladies against HIV/AIDS).
Huu utandawazi wa kuiga kila kitu cha MZUNGU unatupeleka pabaya. Iko siku wananchi - wenye nchi - watadai haki zao... iko siku!
./Mwana wa Haki