M4C inachangisha kwa ajili ya nini; kiasi gani kimepatikana hadi hivi sasa...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Haya maswali yanatakiwa pia kujibiwa kwa kadiri harakati za M4C zinavyozidi kupamba moto. Ni muhimu kuyajibu ili kuonesha uwajibikaji, uwazi, na umakini.

a. M4C inachangisha fedha kwa ajili ya nini?
b. Kiasi gani cha fedha kinachokusanywa kinabakia katika maeneo husika (Mwanza in this case; kanda ya ziwa) - it has to be by percentage.
c. Hadi harakati hizi zilipoanza ni kiasi gani kimepatikana na kiasi gani kimeshatumika kufikia lengo la (a)?
d. Nani anasimamia fedha za M4C?
E. Nani anayesimamia project nzima ya M4C na anawajibika kwanini akiongozwa na utaratibu gani?

Binafsi najitolea kuchangia kidogo: Tsh. 100,000/= kuendeleza harakati!

Wale wengine wa hapa ambao nao wanataka kupledge please do with me... how much u want to give for M4C. Napendekeza CDM iteue mtu wa kucoordinate michango ya watakaotoa kutoka kwenye mitandao.
 
Napendekeza CDM iteue mtu wa kucoordinate michango ya watakaotoa kutoka kwenye mitandao.

Sema wewe labda watakusikia. Omutwale nimewahi kuwapa huu ushauri moja kwa moja na katika uzi wako hapa https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...amoto-kuu-za-chadema-ni-nini.html#post4898476

Niliandika:
Pili, CDM haijavuna vilivyo kutoka Uwezo wa DIGITAL MEDIA. Inapaswa kuanzisha mara moja kitengo-mtengamano (Integrated Unit) cha DIGITAL MEDIA chini ya Kurugenzi ya Habari. Kazi za Kitengo hiki ni pamoja na:

  • Kukusanya, kutathmini na kufanyia kazi maoni yanayotolewa na Sincere Online Community.
  • Kuwakilisha chama, kutoa mtazamo na mrejesho kwenye mijadala ya mitandao ya Kijamii (Makene anajitahidi lakini anaweza kufanya vizuri zaidi ili kuvunja rekodi ya Marehemu Regia Mtema)
  • Kukusanya michango ya fedha-mtandao na mali toka ndani na nje ya nchi.

Kitengo hiki kiwe na Graphics Designers wazuri wa ku-catch na ku-spiral blunders za wapinzani wa CDM in a Art-form

Kwa haraka huo ndiyo ushauri wangu kwa CDM
 
Maswali mazuri lakini mepesi na mengine tayari majibu yake yanajulikana hata kabla ya kuulizwa. Kwa mfano hilo swali la kwanza, la pili, la tatu na lile la nne.

Asante Mzee Mwanakijiji kwa kuchangia mabadiliko, utayari wako wa kuchangia kunathibitisha pasi na shaka kuwa somonla M4C limekuingia na umeelewa, hivyo tayari umejibu sehemu kubwa sana ya maswali yako yote manne. Hongera Mzee kwa kuwa sehemu ya mabadiliko. Wengine wengi watakufuata na kuchukua mfano wako, hasa wale ambao bado wanasema 'nitachangia kesho, nitachangia kesho'.
 
Ilikuweka takwimu sawa ngoja tusubiri walioko jikoni waje na taarifa kamili....
 
Asante Mzee Mwanakijiji kwa kuchangia mabadiliko, utayari wako wa kuchangia kunathibitisha pasi na shaka kuwa somonla M4C limekuingia na umeelewa, hivyo tayari umejibu sehemu kubwa sana ya maswali yako yote manne. Hongera Mzee kwa kuwa sehemu ya mabadiliko. Wengine wengi watakufuata na kuchukua mfano wako, hasa wale ambao bado wanasema 'nitachangia kesho, nitachangia kesho'.

Somo limeniingia mimi? unajua somo liliandikwa wapi? Kama unajua majibu ya maswali hayo hapo juu yaweke tu si kupuuzia.
 
Mzee Mwanakijiji
Maswali ya kototo we mzee, hivi inamana bado hujui fedha za M4C huwa zinatumikaje kama sio kuuza sura humu ukidhan ni FB? Msitake kuaminisha umma kwamba michango ya M4C ni kwa ajili ya watu wachache pia unauliza ni nani anasimamia fedha za M4C inamna CDM haina mhasibu au kazi za wakina Antony Komu pale makao makuu?
Pumba zenu hizi na akili kama za green guards zipelekeni huko huko magambani na CUF.
 
Last edited by a moderator:
Jana nimeulizwa swali kama hili hii ni michango ya watu tunatakiwa kuwa nayo transparency tusifiche kitu imepatika sh tano tuonyeshe hiyo sh tano imetumika vipi ili kesho tupata sh kumi.

Mimi nadhani wale wa arusha pale ilikofanyika wangetupa hesabu walikusanya sh ngapi zikatumika sh ngapi + pale dar serena ambapo ahadi na fedha tasilimu zilikua milioni 500 lengo likua bilioni 5 je zilifikiwa je hawa wa dar wana plan gani tena kufikisha hiyo amount kabla mwaka haujaisha.

Mimi nafikiri tufanye kitu fulani hivi mimi nahuzunika nilikosa na dar masomo yalinibana lakini kidogo sasa niko free sasa kiongozi yoyote wa dar wakishatupa mahesabu ya pesa zilizopatikana tuje na kitu kingine matembezi ya amani.

Let say kushikiri matembezi hayo utalipia sio chini ya 20000 tu target watu 5000 wa daressalaam nina uhakika tutawapata kama tutaanza matangazo mapema mpaka kwenye social media viongozi wote washiriki mimi nitakua bega kwa bega hapa tuna uhakika wa kupata 1 bilioni ili kufikia lengo la bilioni 5.

Hayo matembezi mfano wa wilaya ya kinondoni yanaongozwa na mdee na mnyika,mnyika anachukua watu wote wa kimara huku kuelekea jangwani,mdee anaongoza kutokea kawe kupitia hadi jangwani,na sehemu nyingine itakavyopangwa.

Hii itasaidia nini tunapohitimisha baadae kwenye mkutano mkubwa watu wataku inspired to contribute more wengi wataelewa vizuri lengo la m4c,tutakitangaza chama dar yote maana kila kona kutakua na matembezi kuelekea jangwani,tunakata ngebe za ccm rasmi,

Pili pale jangwani kuwe na hotuba nzito itayolezea chadema tuko tayari sasa kuongoza nchi tuna uwezo.

Sasa tunawezaje kuwapata hao watu 5000 maandalizi yaanze leo matembezi yawe mwezi 3 tuseme wanachama wenye mapenzi ya kweli ya chadema wana miezi 3 kuweka 20000 ya matembezi kusaidia movement ya m4c,mtu atakua na siku 90 kila siku anaweza kuweka 200 kwa miezi 3 akaweza pata ticket na ingependezwa wote tuwe ndani ya tshirt za m4c.

Naomba kuwasilisha na mikoa mingine waige hii idea tunapoita watu hotel fulani tunaonyesha kuna tabaka fulani tunalitenga hapana tufanye matembezi tena tukifanya na mikoa mingine matembezi ndo chama kitambulika mapema sana.

All the best kwa jioni ya leo

Fred kavishe
 
Mzee Mwanakijiji
Maswali ya kototo we mzee, hivi inamana bado hujui fedha za M4C huwa zinatumikaje kama sio kuuza sura humu ukidhan ni FB? Msitake kuaminisha umma kwamba michango ya M4C ni kwa ajili ya watu wachache pia unauliza ni nani anasimamia fedha za M4C inamna CDM haina mhasibu au kazi za wakina Antony Komu pale makao makuu?
Pumba zenu hizi na akili kama za green guards zipelekeni huko huko magambani na CUF.

Unafikiri umezungumza kitu cha akili; kichwa kama sambusa ya kuokota.
 
Haya maswali yanatakiwa pia kujibiwa kwa kadiri harakati za M4C zinavyozidi kupamba moto. Ni muhimu kuyajibu ili kuonesha uwajibikaji, uwazi, na umakini.

a. M4C inachangisha fedha kwa ajili ya nini?
b. Kiasi gani cha fedha kinachokusanywa kinabakia katika maeneo husika (Mwanza in this case; kanda ya ziwa) - it has to be by percentage.
c. Hadi harakati hizi zilipoanza ni kiasi gani kimepatikana na kiasi gani kimeshatumika kufikia lengo la (a)?
d. Nani anasimamia fedha za M4C?

Binafsi najitolea kuchangia kidogo: Tsh. 100,000/= kuendeleza harakati!

Wale wengine wa hapa ambao nao wanataka kupledge please do with me... how much u want to give for M4C. Napendekeza CDM iteue mtu wa kucoordinate michango ya watakaotoa kutoka kwenye mitandao.

Wewe unaleta swali hili hapa JF? subiri ban tu.maswali kama haya hapa jf elekeza kwa CCM siyo CDM!
 
Jana nimeulizwa swali kama hili hii ni michango ya watu tunatakiwa kuwa nayo transparency tusifiche kitu imepatika sh tano tuonyeshe hiyo sh tano imetumika vipi ili kesho tupata sh kumi.

Mimi nadhani wale wa arusha pale ilikofanyika wangetupa hesabu walikusanya sh ngapi zikatumika sh ngapi + pale dar serena ambapo ahadi na fedha tasilimu zilikua milioni 500 lengo likua bilioni 5 je zilifikiwa je hawa wa dar wana plan gani tena kufikisha hiyo amount kabla mwaka haujaisha.

Mimi nafikiri tufanye kitu fulani hivi mimi nahuzunika nilikosa na dar masomo yalinibana lakini kidogo sasa niko free sasa kiongozi yoyote wa dar wakishatupa mahesabu ya pesa zilizopatikana tuje na kitu kingine matembezi ya amani.

Let say kushikiri matembezi hayo utalipia sio chini ya 20000 tu target watu 5000 wa daressalaam nina uhakika tutawapata kama tutaanza matangazo mapema mpaka kwenye social media viongozi wote washiriki mimi nitakua bega kwa bega hapa tuna uhakika wa kupata 1 bilioni ili kufikia lengo la bilioni 5.

Hayo matembezi mfano wa wilaya ya kinondoni yanaongozwa na mdee na mnyika,mnyika anachukua watu wote wa kimara huku kuelekea jangwani,mdee anaongoza kutokea kawe kupitia hadi jangwani,na sehemu nyingine itakavyopangwa.

Hii itasaidia nini tunapohitimisha baadae kwenye mkutano mkubwa watu wataku inspired to contribute more wengi wataelewa vizuri lengo la m4c,tutakitangaza chama dar yote maana kila kona kutakua na matembezi kuelekea jangwani,tunakata ngebe za ccm rasmi,

Pili pale jangwani kuwe na hotuba nzito itayolezea chadema tuko tayari sasa kuongoza nchi tuna uwezo.

Sasa tunawezaje kuwapata hao watu 5000 maandalizi yaanze leo matembezi yawe mwezi 3 tuseme wanachama wenye mapenzi ya kweli ya chadema wana miezi 3 kuweka 20000 ya matembezi kusaidia movement ya m4c,mtu atakua na siku 90 kila siku anaweza kuweka 200 kwa miezi 3 akaweza pata ticket na ingependezwa wote tuwe ndani ya tshirt za m4c.

Naomba kuwasilisha na mikoa mingine waige hii idea tunapoita watu hotel fulani tunaonyesha kuna tabaka fulani tunalitenga hapana tufanye matembezi tena tukifanya na mikoa mingine matembezi ndo chama kitambulika mapema sana.

All the best kwa jioni ya leo

Fred kavishe
Mkuu nimekitafuta kitufe cha like nimekikosa. Nakupa LIKE KUBWA!
 
Mzee Mwanakijiji
Maswali ya kototo we mzee, hivi inamana bado hujui fedha za M4C huwa zinatumikaje kama sio kuuza sura humu ukidhan ni FB? Msitake kuaminisha umma kwamba michango ya M4C ni kwa ajili ya watu wachache pia unauliza ni nani anasimamia fedha za M4C inamna CDM haina mhasibu au kazi za wakina Antony Komu pale makao makuu?
Pumba zenu hizi na akili kama za green guards zipelekeni huko huko magambani na CUF.
Punguza povu,Mzee Mwanakijiji hajauliza report ya mapato na matumizi ya chama elezea uelewa wako wa michango ya M4C kama unafahamu una unalolihafamu piga kimya.
 
Ngoja tuone kama utapata majibu,Mimi niliishauliza hapa, JF watueleze wameishakusanya shillingi ngapi kwenye omba omba yao nikatukanwa, yaani unamuomba mtu pesa kwa kunyenyekea akiishakupa hautaki kumuambia alikupa shilingi ngapi.Pesa Bwana!!Haya mi ntachangia elfu TZS 50,000 ntafanye sasa.
 
Hili swali limekaa kishambenga shambenga, kwani huyu muuliza swali hapajui CHADEMA makao makuu? alishakwenda kuhitaji hizi details akanyimwa? au ndio anataka kuamsha Hisia kuwa hela hizi ni kwa ajili ya akina Mbowe and CO? Kweli mtoa mada una mapenzi mema na CHADEMA?
 
Back
Top Bottom