M4c - arusha: Live - join the chain event - from snow crest hotel

chadema mkoa wa Arusha wamenunua vifaa vya matangazo na sasa harambe ya kuchangia kununua canter inaanza katibu wa chadema katoa mil 1...
 
Lema anasema kama watu wahali ya kati hawatashituka miaka mitano ijayo watauwawa magetini kwao kwani hali ya nchi ni mbaya sana polisi na makambuni ya ulinzi hayataweza kuzuia uwizi..
 
anasema anawapenda sana masela wake kwani kila kunapokuwa na maandamano ya kudai haki huwa hawamwangushi tofauti na watu wa kati kwani huwa kazi yao kuchungulia madirishani na kupiga simu sasa ombi lake ni wao kukiwezesha chama..
 
nasari anatoa mil 2 kwa mchango wa kununua gari la kubebea vifaa vya matangazo..
 
kwa mwendo huu chadema kinachukua nchi ccm ongezeni wahuni wa kupambana na chadema leo nilichokiona na kukisikia nina kila sababu ya kusema chadema ni tumaini jipya kwa Arusha mikutano itakuwa inafanyika mpaka mtoto aliyoko tumboni ajue anani anatetea majambazi na majangiri na nani anatetea wananchi..
 
Wafanya kwa ajili ya nini? Hii M4C inatakiwa isitishwe hadi mambo fulani yatengenezwe.

Kukusanya michango bila mrejesho wa matumizi na mapato ya michango inaashiria ufisadi, CHADEMA badilikeni haya mambo yataendelea kuwachafua na wabaya wenu watatumia hii kama propaganda, mnashindwa nini kutangaza matumizi ya fedha mnazokusanya?
 
Mzee Mwanakijiji mkutano huu wa leo umekuwa na mafanikio makubwa sana ambayo kwangu mimi ni kitu cha kuigwa na mikoa mingine ilikuelekea ukombozi wa taifa hili ikumbukwe mkutano huu ulikuwa wa wana Arusha tumefanikiwa kulipia vifaa vya matangazo mil 14.6 nitaweka picha ya vifaa hivyo pia katika mpango wa kununua gari litakalokuwa linabeba vifaa hivyo tumechanga mil 27.5 kama ahadi ambazo ndani ya mwezi huu zitalipwa na cash ni mil 1.2 ndugu zangu wapenda mabdiliko tujitoe kukichagia chama tuko vitani..
 
Last edited by a moderator:
ccm ni adui zaidi ya idd Amin na wote tunajua tulivyojitoa kumuondoa Idd Amin hivyo basi watanzania tujitoe kwa hali na mali kukisaidia chama chetu cha CHADEMA ili walioko msitari wa mbele wazidi kusonga mbele msisikilize propaganda za wapuuzi nape na kundi lake wanaotengeneza mazigira kuwa kuna pesa inaliwa tuwaamini viongozi wetukwani hata hivyo kua wa kaguzi wa serikali hukikagua chama chetu
 
Kukusanya michango bila mrejesho wa matumizi na mapato ya michango inaashiria ufisadi, CHADEMA badilikeni haya mambo yataendelea kuwachafua na wabaya wenu watatumia hii kama propaganda, mnashindwa nini kutangaza matumizi ya fedha mnazokusanya?

kama wewe ni mwanachama na mfatiliaji utakuwa unajua mapato ya M4C na nikukumbushetu vyamavyote vya siasaukguliwa cag ni ccm akiona dosai tapayuka masaburi yatamuwasha..swali dogo ccm huwa wanatangaza kama wanavyofanya cdm..
 
Napenda kuchukua nafasi hii kukipogeza chama cha demokrasia na maendeleo kwa kuwa wazi kwenye mapato na matumizi ni wakati sasa umefika wa chama cha majagili kuiga kuliko kuendelea kufanya siri..
 
kama wewe ni mwanachama na mfatiliaji utakuwa unajua mapato ya M4C na nikukumbushetu vyamavyote vya siasaukguliwa cag ni ccm akiona dosai tapayuka masaburi yatamuwasha..swali dogo ccm huwa wanatangaza kama wanavyofanya cdm..

Naomba uweke taarifa yoyote ya CAG kuhusu ukaguzi wa fedha za vyama vya siasa, na hata kama atakagua Mamlaka yake yapo kwa fedha za ruzuku inayotoka serikalini, hii ni kwa mujibu wa sheria ya ukaguzi wa Umma na sheria ya Vyama vya siasa na sio michango ya gold crest, Dar, Arusha na kwenye mikutano ya hadhara, Hoja yangu na ya wadau wengi ni kuhusu fedha za michango ya Wananchi, wengi wetu tunapenda mabadiliko ya Nchi yetu ila tusifanywe vipofu kushindwa kuhoji vitu vya msingi, CHADEMA waoneshe na kutenda kwa mifano , binafsi sikubaliani na hizi changisha changisha kama maelezo ya matumizi hayatolewi na huku watu wanapiga kelele kila kukicha.
 
mkuu PhD kama wewe ni gamba unanafasi nzuri zaidi kupata ripoti ya CAG hata hivyo chadema hutagaza pesa wanazopata kwanapochangiwa na tunaofatilia mambo tunajua pesa kiasi gani kina hitajika ukilinganisha na pesa tunayopata...niliwahi kusafiri na viongozi kwenye M4C niliona tabu wanazozipata..
 
Last edited by a moderator:
mkuu PhD kama wewe ni gamba unanafasi nzuri zaidi kupata ripoti ya CAG hata hivyo chadema hutagaza pesa wanazopata kwanapochangiwa na tunaofatilia mambo tunajua pesa kiasi gani kina hitajika ukilinganisha na pesa tunayopata...niliwahi kusafiri na viongozi kwenye M4C niliona tabu wanazozipata..

Mkuu yegella, mie Mwananchi wa kawaida kabisa tena nisiyekuwa muumini wa chama chochote cha siasa, ila naamini katika ujenzi wa Taifa imara lenye kuzingatia misingi ya utawala bora na haki, naunga mkono mwanasiasa yeyote mwenye maadili na anayeweka maslahi ya Taifa mbele bila kuzingatia chama chake.Suala la kutoa taarifa za michango ni nyenzo ya kuimarisha uwajibikaji, kama Taifa tupo hapa tulipo kwa kukosa uwajibikaji, hivyo basi kwa yeyote mwenye nia ya kuisaidia Tanzania kupiga hatua lazima asemee uwazi , uwajibikaji na kuchukua hatua panapostahili hatua na kwa wakati muafaka
 
mkuu PhD nimekusoma lakini kama nilivyosema awali kuwa chadema imekuwa ikitangaza mapato na matumizi..
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: PhD
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom