Mtoa taarifa aliyepo Morogoro ambaye juzi alinijuza kuwepo taarifa ya kujiuzulu katibu wa mkoa huo na mie kuitoa kama tetesi JF na baadae kuthibitika. Sasa amenijulisha kuwepo mpango wa kumng'oa Mh. Suzana Kiwanga (MB viti maalumu) kwenye nafasi ya Mkoa wa Morogoro.
Wajumbe kutoka wilaya za mkoa huo watakutana Sept 03 mwaka huu kupanga safu ya uongozi ngazi ya mkoa chini ya usimamizi wa Dr. Slaa ili kuimarisha uongozi mkoani hapo ili moto uliowashwa na M4C usipoe mpaka 2015. Wajumbe wa wilaya za Kilombero na Manispaa ya Morogoro wanadaiwa kuwashawishi wajumbe toka wilaya nyingine ili wamtose M/kiti huyo.
Tuhuma zinazoelekezwa kwake ni pamoja na;
Mtoa taarifa ambaye yupo kwenye msafara wa M4C mkoani Morogoro anaeleza kuwa M/kiti huyo wa mkoa anahaha ni namna gani amwingie Dr. Slaa ili amshawishi azipe pengo tu la katibu wake aliyejiuzuru.
Tayari kuna vijana wasome wanahaha kuziwania nafasi hizo za ngazi ya mkoa na tayari wanapiga kampeni za chinichini.
Wajumbe kutoka wilaya za mkoa huo watakutana Sept 03 mwaka huu kupanga safu ya uongozi ngazi ya mkoa chini ya usimamizi wa Dr. Slaa ili kuimarisha uongozi mkoani hapo ili moto uliowashwa na M4C usipoe mpaka 2015. Wajumbe wa wilaya za Kilombero na Manispaa ya Morogoro wanadaiwa kuwashawishi wajumbe toka wilaya nyingine ili wamtose M/kiti huyo.
Tuhuma zinazoelekezwa kwake ni pamoja na;
- Anaendesha chama mkoa kwa simu kwani makazi yake ni Kinondoni DSM na huonekana Morogoro tu kama kuna ugeni wa Kitaifa au vikao vya chama.Na kukwamisha shughuli za chama za kila siku.
- Siyo mtu wa kujitoa kwa mali kukijenga chama pamoja na kupata ubunge. Kwa mfano;Mkoa hauna ofisi hata M4C imewalazimu kazi zao kupanga Mt. Uluguru Hotel. Mkoa na wialaya wamepanga kachumba kadogo mno tena kachumba kalikotengenezwa na wanachama wa kawaida.Hajaleta gari yake hata moja kwenye oparesheni inayoendelea, hata yeye anadadia gari ya Dr. Slaa.
- Anadaiwa kuwa mwanasiasa za kutengeneza makundi kwenye chama, anatuhumiwa kuvuruga uongozi wa chama wilaya ya Kilombero enzi za uhai wa Marehemu Regia Mtema kipenzi cha wana Kilombero na sasa anavuruga mkoa mzima. Haoni ghalama anapotaka kumwangamiza mwenzake. Kwa mfano aliwahi kuwasafirisha wajumbe toka Kilombero wakati wa uhai wa marehemu Regia agenda ikiwa kutaka kuwatosa wajumbe wa kamati tendaji wilaya waliokuwa wakimuunga mkono marehemu.
- Anadaiwa amekwamisha kupatikana kadi za kutosha wilayani, kwenye kata mpaka matawini. Kwani anatuhumiwa kununua kadi sh 300/= zote zinazotengwa kwa mkoa wa Morogoro na kuanza kuziuza mwenyewe kwenye mikutano kwa sh. 1500/=bila kuwasilisha mgawo wa mauzo hayo kwenye wilaya, kata na matawini hata kwenye oparesheni M4C yuko busy kuuza kadi.
- Anadaiwa kuwa na uelewa mdogo ambao hauendani ya kasi ya chama hiki kwa sasa.
Mtoa taarifa ambaye yupo kwenye msafara wa M4C mkoani Morogoro anaeleza kuwa M/kiti huyo wa mkoa anahaha ni namna gani amwingie Dr. Slaa ili amshawishi azipe pengo tu la katibu wake aliyejiuzuru.
Tayari kuna vijana wasome wanahaha kuziwania nafasi hizo za ngazi ya mkoa na tayari wanapiga kampeni za chinichini.