Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Lwakatare: Siwezi kuwa mzururaji wa vyama vya siasa
na Mobin Sarya
MJUMBE wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi (CUF), ambaye alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilfred Lwakatare, amesema hawezi kudhalilisha utu wake kwa kugeuka mzururaji kwenye vyama vya siasa.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano jana kuhusiana na uvumi uliozagaa kwamba ameakiasi chama hicho na anakusudia kukihama baada ya kuenguliwa nafasi yake ya unaibu Katibu Mkuu, Lwatare alisema atakuwa amewasaliti wapiga kura wake kwa kufanya hivyo.
Siwezi kujidhalilisha kiasi hicho, nitakuwa nimewasaliti wafuasi wangu pamoja na wajumbe wa CUF nchi nzima walionichagua kwa kishindo katika uchaguzi uliopita kuwa mjumbe wa Baraza kuu, nikapata kura nyingi kuliko mjumbe yeyote nikifuatiwa na Juma Haji Duni, alisema Lwakatare.
Alisema kwa matokeo hayo yanadhihirisha wazi jinsi anavyokubalika na kupendwa ndani ya chama hicho, ingawa Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba amemuacha katika uteuzi wa nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Bara kama alivyofanya kwa Juma Haji Duni.
Hata hivyo, alisema hawezi kujua sababu iliyosababisha asiteuliwe kwenye nafasi hiyo tena, ingawa anaamini mwenyekiti wake ameamua kutumia uwezo wake kikatiba na kumchagua, Joran Bashange kutoka Morogoro.
Lwakatare alisema anachojivunia ni kwamba wananchi wa Jimbo la Bukoba ndio mtaji wa kisiasa, wala hilo la kuachwa haliwezi kumsumbua ingawa wajumbe wengi kutoka mikoani wamekuwa wakihoji kwanini ameachwa
________________________
The real leader nilisema hapa kuwa mtu asibabaike na ukubwa wa Chama, jambo muhimu ni kule anakotoka ikiwa wananchi wanaimani na wewe hata ukiwa mfagia ofisi basi watakuunga mkono tu, ndio nikasema wale wa wafuasi wa Sultani CCM ikiwa kweli wanajiamini kuwa ni watetezi wa wananchi hata wasione tabu kumhama Sultani CCM na kujiunga Chama kingine chochote kile kubaki na Sultani CCM ni kubaki na damu ya kifisadi rangi ya kifisadi na kabila la kifisadi na mambu ya kifisadi, majumuisho ni kuwa ukihama huko kama ulipokuwa CCM ulipata kura 999 basi ukihamia upinzani utapata 1000 ,imani ya wananchi kwako itazidi na kuona kuwa ni kweli upo kwa kutetea maslahi yao na kuupinga udhalim kwa Tanzania nzima ,ila kubakia kwa Sultani CCM ni kutafuta ugonjwa wa moyo na sindikizo la damu.
Huu ni wakati muwafaka wa kuihama CCM usingojee mpaka Sultani amekutafutia mgombea mbadala ikifikia hapo basi ujue ndio mwanzo wa kupigwa buti na haitokubalika kurukia chama kingine na wananchi wakakukubali ,huu ndio msimu mzuri wa kuhamia Chama kingine ili kutunza wapiga kura wako ambao wamechoshwa na siasa zisizo na faida na sera za Sultani CCM zisizo tekelezeka.
Mlioko kwa Sultani CCM upepo wa mabadiliko unaitembelea Tanzania na kuanguka kwa Sultani CCM kunanyemelea kwa kasi kubwa sana isivyotegemewa ,huwezi kuamini ikiwa unajipa moyo kuwa kwa sasa CCM haiwezi kuondoka madarakani huko ni kujidanganya kukubwa ambako hujawahi kujidanganya toka uzaliwe ,ndio maana yake una macho lakini huoni una masikio lakini husikii ndio katika nyinyi mnaong'ang;ania kubakia na CCM ,mkiamini kuwa CCM ndio iliyowafikisha hapo na kuwacha kuwaamini wananchi ambao ndio waliowapa kura ,nakuhakikishieni kuwa ikiwa umewaamini wananchi wako unaweza kwenda Chama chochote kile na ukahama nao na wakakupa kura zako ni hatari kubakia kwa Sultani CCM kwani wananchi walio wengi hawana imani nae au imani imewatoka ,wewe waliokuchagua na kukufikisha bungeni huna unalowafanyia ,kauli zako na kuunga mkono kwako huko bungeni si kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi wa kijijini kwako au WaTanzania kwa ujumla bali unatumiaka na Wafuasi waliokusdi nguvu kuwavushia miradi yao ya utapeli ,au uongo ?
Wewe unadai kujengewa barabara kwa wapiga kura wako,unadai kujengewa zahanati kwa wapiga kura wako unadai kila unachoona kitakuonyesha kuwa wewe upo bungeni kwa kuwaletea maendeleo ,toka uhamie hapo hujafanikiwa hata kuwapelekea kiwembe cha kujinyolea kutoka serikalini kama ni faida ya wewe kuwepo hapo ,hivi wananchi hao wakuchague kwa jambo gani ,umepiga makelele kuwadaia lakini hakuna hata moja lililotekelezwa miradi yote inayopitishwa huwa ni miradi hewa kwa wananchi na miradi faida binafsi kwa wengine ,hama Chama cha Sultani CCM kwa kuwaridhisha wananchi wako ,ni bora uwepo upinzani utaisabika ni mkweli kuliko kubaki kwa mtawala CCM utakuwa unapoteza wapiga kura wako na kuwapa fursa ya kuhamia kwengine maana kama waliokupigia kura 2005 ni 100 ukirudi utawakuta wamebaki 50 tena wagonjwa wahoi bintaaban huna la kuwambia jipya ukipiga kampeni za kuwafurahisha 25 watakuona muongo mkbwa kama wewe hakuna utabakiza 25 hawa ni ndugu na jamaa zako wa karibu watabaki wakuchune wakikumaliza wataondoka atabaki mkeo na watoto ambao hawajafikia hata umri wa kupiga kura lazima uulize kama lile shamba la pamba lipo maana toka upate ubunge hujaonekana hujui hata moja.
Weka kando yote kama hujaamka basi amka na mapema mkakati wa Sultani CCM ni kupandikiza wenzao hadi huko vijijini baada ya kuona kuwa kuna hatari ya ule mtindo wa kupandikiza ukubwani kuwa na mvutano na kuwagawa mapande hivyo wanahakikisha huko huko kijijini mtu wao mvivu anapita. Wewe uliekuwa unaonekana kidomodomo unawekwa kando na mapema njia na mipango wenyewe mnaijua hivyo hama Chama na mapema kwani kuwemo CCM ni kutafuta lawama na wanachi.
na Mobin Sarya
MJUMBE wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi (CUF), ambaye alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilfred Lwakatare, amesema hawezi kudhalilisha utu wake kwa kugeuka mzururaji kwenye vyama vya siasa.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano jana kuhusiana na uvumi uliozagaa kwamba ameakiasi chama hicho na anakusudia kukihama baada ya kuenguliwa nafasi yake ya unaibu Katibu Mkuu, Lwatare alisema atakuwa amewasaliti wapiga kura wake kwa kufanya hivyo.
Siwezi kujidhalilisha kiasi hicho, nitakuwa nimewasaliti wafuasi wangu pamoja na wajumbe wa CUF nchi nzima walionichagua kwa kishindo katika uchaguzi uliopita kuwa mjumbe wa Baraza kuu, nikapata kura nyingi kuliko mjumbe yeyote nikifuatiwa na Juma Haji Duni, alisema Lwakatare.
Alisema kwa matokeo hayo yanadhihirisha wazi jinsi anavyokubalika na kupendwa ndani ya chama hicho, ingawa Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba amemuacha katika uteuzi wa nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Bara kama alivyofanya kwa Juma Haji Duni.
Hata hivyo, alisema hawezi kujua sababu iliyosababisha asiteuliwe kwenye nafasi hiyo tena, ingawa anaamini mwenyekiti wake ameamua kutumia uwezo wake kikatiba na kumchagua, Joran Bashange kutoka Morogoro.
Lwakatare alisema anachojivunia ni kwamba wananchi wa Jimbo la Bukoba ndio mtaji wa kisiasa, wala hilo la kuachwa haliwezi kumsumbua ingawa wajumbe wengi kutoka mikoani wamekuwa wakihoji kwanini ameachwa
________________________
The real leader nilisema hapa kuwa mtu asibabaike na ukubwa wa Chama, jambo muhimu ni kule anakotoka ikiwa wananchi wanaimani na wewe hata ukiwa mfagia ofisi basi watakuunga mkono tu, ndio nikasema wale wa wafuasi wa Sultani CCM ikiwa kweli wanajiamini kuwa ni watetezi wa wananchi hata wasione tabu kumhama Sultani CCM na kujiunga Chama kingine chochote kile kubaki na Sultani CCM ni kubaki na damu ya kifisadi rangi ya kifisadi na kabila la kifisadi na mambu ya kifisadi, majumuisho ni kuwa ukihama huko kama ulipokuwa CCM ulipata kura 999 basi ukihamia upinzani utapata 1000 ,imani ya wananchi kwako itazidi na kuona kuwa ni kweli upo kwa kutetea maslahi yao na kuupinga udhalim kwa Tanzania nzima ,ila kubakia kwa Sultani CCM ni kutafuta ugonjwa wa moyo na sindikizo la damu.
Huu ni wakati muwafaka wa kuihama CCM usingojee mpaka Sultani amekutafutia mgombea mbadala ikifikia hapo basi ujue ndio mwanzo wa kupigwa buti na haitokubalika kurukia chama kingine na wananchi wakakukubali ,huu ndio msimu mzuri wa kuhamia Chama kingine ili kutunza wapiga kura wako ambao wamechoshwa na siasa zisizo na faida na sera za Sultani CCM zisizo tekelezeka.
Mlioko kwa Sultani CCM upepo wa mabadiliko unaitembelea Tanzania na kuanguka kwa Sultani CCM kunanyemelea kwa kasi kubwa sana isivyotegemewa ,huwezi kuamini ikiwa unajipa moyo kuwa kwa sasa CCM haiwezi kuondoka madarakani huko ni kujidanganya kukubwa ambako hujawahi kujidanganya toka uzaliwe ,ndio maana yake una macho lakini huoni una masikio lakini husikii ndio katika nyinyi mnaong'ang;ania kubakia na CCM ,mkiamini kuwa CCM ndio iliyowafikisha hapo na kuwacha kuwaamini wananchi ambao ndio waliowapa kura ,nakuhakikishieni kuwa ikiwa umewaamini wananchi wako unaweza kwenda Chama chochote kile na ukahama nao na wakakupa kura zako ni hatari kubakia kwa Sultani CCM kwani wananchi walio wengi hawana imani nae au imani imewatoka ,wewe waliokuchagua na kukufikisha bungeni huna unalowafanyia ,kauli zako na kuunga mkono kwako huko bungeni si kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi wa kijijini kwako au WaTanzania kwa ujumla bali unatumiaka na Wafuasi waliokusdi nguvu kuwavushia miradi yao ya utapeli ,au uongo ?
Wewe unadai kujengewa barabara kwa wapiga kura wako,unadai kujengewa zahanati kwa wapiga kura wako unadai kila unachoona kitakuonyesha kuwa wewe upo bungeni kwa kuwaletea maendeleo ,toka uhamie hapo hujafanikiwa hata kuwapelekea kiwembe cha kujinyolea kutoka serikalini kama ni faida ya wewe kuwepo hapo ,hivi wananchi hao wakuchague kwa jambo gani ,umepiga makelele kuwadaia lakini hakuna hata moja lililotekelezwa miradi yote inayopitishwa huwa ni miradi hewa kwa wananchi na miradi faida binafsi kwa wengine ,hama Chama cha Sultani CCM kwa kuwaridhisha wananchi wako ,ni bora uwepo upinzani utaisabika ni mkweli kuliko kubaki kwa mtawala CCM utakuwa unapoteza wapiga kura wako na kuwapa fursa ya kuhamia kwengine maana kama waliokupigia kura 2005 ni 100 ukirudi utawakuta wamebaki 50 tena wagonjwa wahoi bintaaban huna la kuwambia jipya ukipiga kampeni za kuwafurahisha 25 watakuona muongo mkbwa kama wewe hakuna utabakiza 25 hawa ni ndugu na jamaa zako wa karibu watabaki wakuchune wakikumaliza wataondoka atabaki mkeo na watoto ambao hawajafikia hata umri wa kupiga kura lazima uulize kama lile shamba la pamba lipo maana toka upate ubunge hujaonekana hujui hata moja.
Weka kando yote kama hujaamka basi amka na mapema mkakati wa Sultani CCM ni kupandikiza wenzao hadi huko vijijini baada ya kuona kuwa kuna hatari ya ule mtindo wa kupandikiza ukubwani kuwa na mvutano na kuwagawa mapande hivyo wanahakikisha huko huko kijijini mtu wao mvivu anapita. Wewe uliekuwa unaonekana kidomodomo unawekwa kando na mapema njia na mipango wenyewe mnaijua hivyo hama Chama na mapema kwani kuwemo CCM ni kutafuta lawama na wanachi.