Mkurugenzi wa ulinzi na usalama wa CHADEMA Wilfred Lwakatare atafikishwa tena mahakamani leo
---------------------- Update:-
---------------------- Update:-
Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu imeshindwa kwa mara nyingine kumpa dhamana mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema Wilfred Lwakatare.
Hakimu anayesikiliza kesi hiyo amesema ameshindwa kutoa uamuzi kwa sababu alikuwa likizo na anaomba siku ya leo aitumie kwa kupitia maombi hayo ya dhamana.
Hakimu huyo amesema atatoa uamuzi wa ama kutoa dhamana ama kumnyima dhamana Lwakatare kesho saa 2 asubuhi.
Viwanja vya mahakama vilifurika umati mkubwa wa wafuasi wa Chadema ambao muda wote walikuwa wakiimba Peoples Power!