Lwakatare aomba Bukoba wapunguziwe kodi vifaa vya ujenzi, Magufuli amjibu ajenge kiwanda awapunguzie

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
Mbunge wa Bukoba Wilfred Lwakatare kwenye mkutano wa Magufuli na Bukoba aliomba Bukoba wapunguziwe vifaa vya ujenzi kama bati na simenti kwa kuwa serikali haiwezi kumjengea kila mwananchi nyumba

Akitolea mfano Kikwete kuwapa fidia ya ng'ombe wafugaji waliopatwa na janga la Ukame walipewa ng'ombe na Nyerere alivyofanya kwa CDA dodoma kwa kuwapa msaada wa kodi

Magufuli alimjibu kwa kumpa changamoto ya kujenga kiwanda Kyelwa wauze mabati hata kwa 1,000 kwa sababu kuna madini ya bati Kyelwa na sio mabati ya kutoka Dar na China na ni ya wafanyabiashara.

 
Hii nchi baada miaka michache ijayo itaendelea sana. Tutajielewa na kutafuta njia nyingine za kujikomboa. Tatizo wananchi wakichoka wakaamua kushindana kwa nguvu, tutaishia pabaya.

Nakubali shida na dhiki no waalimu wazuri sana, lakini viongozi wetu wakumbuke wanaongoza wananchi
 
Mbunge wa Bukoba Wilfred Lwakatare kwenye mkutano wa Magufuli na Bukoba aliomba Bukoba wapunguziwe vifaa vya ujenzi kama bati na simenti kwa kuwa serikali haiwezi kumjengea kila mwananchi nyumba
Akitolea mfano Kikwete kuwapa fidia ya ng'ombe wafugaji waliopatwa na fidia ya ng'ombe na Nyerere alivyofanya kwa CDA dodoma kwa kuwapa msaada wa kodi

Magufuli alimjibu kwa kumpa changamoto ya kujenga kiwanda Kyelwa wauze mabati hata kwa 1,000 kwa sababu kuna madini ya bati Kyelwa na sio mabati ya kutoka Dar na China na ni ya wafanyabiashara.


Kamjibu VIZURI SANA akili ya VYA BURE SI KWA ZAMA HIZI.......kwenye hili acheni UNAFIKI
 
Huyu rwakatale anamuogopa sana magu. Yan viongozi wamekuwa makondoo kweli. Cheki linavyojikanyaga . Rwakatare ungea kama mwanaume bhna kwani magu anakuzidi nini?
 
Magufuli ni mwiba kwa waliodumaa akili ufipa kila siku ni kulialia tu wapewe msaada, lakini Magufuli ni nuru kwa wanaotaka changamoto mpya na kijikwamua kimaisha.
Mmepewa vyeo mnaharisha tu sasa hivi.ngoja awatimue akili zitawakaa sawa.
 
Akiwa IKULU anasema yeye ndio amezunguka nchi nzima anajua Shida za WANANCHI MASIKINI na ndio waliompigia kura Kwaio SERIKALI YAKE NI YA MASIKINI.

Akiwa kwa hao MASIKINI anawaambia MWAAFA. Hakuna MSAADA kila MTU ABEBE MSALABA WAKE.

Sijui ni Masikini wapi huwa ana wazungumzia.
 
Haaaa kama vile napata kipicha fulani jinsi magufuri anavyomjibu Lwakatare kwa karibu kabisaa,
Huyu jamaa sijui ana roho ya chuma..!!???
Hivi hili tetemeko lingetokea huko kwao angemjibu hivyo..!!??
Nyie waropokaji huwa mjaaa tuu humu jf uzuri nimeangalia marudio ya hotuba hii pale itv alimjibu vizuri sana tena sana...............alimwambia waziri wa viwanda na Mbunge watafute mwekezaji kule kuna madini ya bati wakimpata wataweza kupanga bei lakini ni vigumu kutegemea mabati kutoka dar yapunguzwe bei unayo taka wewe ni vigumu sana watu wanafanya biashara...
 
Magufuli ni mwiba kwa waliodumaa akili ufipa kila siku ni kulialia tu wapewe msaada, lakini Magufuli ni nuru kwa wanaotaka changamoto mpya na kijikwamua kimaisha.

Hivi mkuu huwezi jibu uzi wowote bila kumtaja Lowasa au chadema ?

Kazi unayo! Iga hata mfano wa kada mwezip Pohamba
 
Nyie waropokaji huwa mjaaa tuu humu jf uzuri nimeangalia marudio ya hotuba hii pale itv alimjibu vizuri sana tena sana...............alimwambia waziri wa viwanda na Mbunge watafute mwekezaji kule kuna madini ya bati wakimpata wataweza kupanga bei lakini ni vigumu kutegemea mabati kutoka dar yapunguzwe bei unayo taka wewe ni vigumu sana watu wanafanya biashara...
Nyie Leo hii akipunguza kodi ya hivyo vifaa mtakuwa wa kwanza kushangilia hapa jukwaani,!
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom