Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,728
- 2,256
Siyo siri, kwa sasa hivi CCM inavuna kile Katibu wake Mkuu alichopanda.
Luteni Makamba, Katibu Mkuu wa CCM amekifikisha chama katika wakati mgumu pengine kuliko wakati wowote tangu kuzaliwa kwake mwaka 1977.
Wengi tulio wana CCM tulijiuliza ina kuwaje huyu jamaa wa cheo kidogo jeshini angeweza kuhimili asasi hii kubwa ya kisiasa.
Lazima tukumbuke kuwa kwanza Luteni ni cheo ambacho ni cha platoon commander, luteni anaongoza watu si zaidi ya 12.
Makamba kielimu hayuko juu sana , hivyo basi hata kwa uzoefu yeye si strategist, siyo political thinker, wala si administrator wa kutumainiwa.
Madudu yaliyojitokeza wakati wa uchaguzi ni ya kutia aibu kwa chama kikongwe kama CCM.
Siyo siri vile vile kuwa kwa kukosa usomi katika CCM,chama hakina sera wala dira inayoeleweka, hivyo basi chama kinaondokewa kwa wingi na vijana hasa wa rika la chini.
It is no longer mass party.
CHADEMA , chama kidogo sana , kimeweza kwa ustadi mkubwa kuamsha hisia za vijana wengi , na kuonekana kama tegemeo la wanyonge.
Wengi wetu tulivutiwa na slogan ya Ari mya,Nguvu mpya na Kasi mpya.This unfortunately was hot air which did not feature in any plans or strategies.
Makamba amekumbatia makundi fulani ambayo ni dhahiri hayana mvuto kwa jamii-na kundi hilo ni kundi la mafisadi.
Sura ya chama inaanza kujigeuza kuwa ni kundi la watu wa aina fulani.Siyo siri kuwa Lowassa, Rostam,Chenge na wengine wa mlengo huo ndio wanaoua sura ya chama katika jamii.
Siasa huwa haina mahakama, mahakama yake ni wananchi.
Ni wazi vile vile JK amegutuka, ingawaje hatujui kama amechelewa au la. Matukio ya Uchaguzi mkuu na uteuzi wake wa baraza la mawaziri ni kielelezo tosha juu ya kugutuka huko.
Ni juu ya mwenyekiti wa CCM kuchukua uamuzi mzito kabla 2015 kukiokoa chama.
But well, what the heck!!
Hata Mwalimu alisema CCM si mama yangu!
But it is sad to see a good party machinnery go to waste.
Makamba , kaburi la CCM!