Luteni Generali wa Jeshi la Rwanda, Jaques Musemakweli auawa kwa kulishwa sumu

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
2,205
4,695
Ni habari ya kushtua sana ya kifo cha Jasusi mbobezi.

Taarifa kutoka vyanzo vya kuaminika zinathibitisha kuwa Jaques Musemakweli Lt Jenerali wa Jeshi la Ulinzi Rwanda amefariki huku sumu ikihusishwa na kifo chake.

Mwendazake aliwahi kuongoza Idara nyeti ya ujasusi almaarufu Directorate of Military Intelligence (DMI), Mkuu wa Kikosi cha Ulinzi wa Rais na Mkuu wa Utawala Jeshini.

Kabla ya kifo chake alihudumu katika nafasi ya Inspector General wa Jeshi la Rwanda

Taarifa za uhakika zinaeleza Mwendazake alikuwa mtu wa karibu sana na Rais Kagame hadi umauti unamkuta.

Kifo chake kimemshtua sana Rais Kagame aliyeagiza uchunguzi (Autopsy) ufanywe mara moja

Serikali ya Rwanda imetoa taarifa kuthibitisha kifo chake.

Luteni Generali huyo alifariki Februari 12, 2021 majira ya saa 1:30 AM kwa saa za Rwanda.

Ukaribu wa mwendazake na Rais Kagame inadaiwa ulileta chuki dhidi yake kutoka kwa baadhi ya Majenerali wa nchi.

Source: Vyanzo mbalimbali kutoka Rwanda + Jeshi la Rwanda
 
Imenikumbusha jasusi mbobezi Bernard Kamilius Membe ambaye alishindwa kufanya kampeni hata kewenye kata yake alipokuja kwa mbwembwe nyingi kuutaka urais. Alikuwa domp zegge.
 
PK kiboko...

Miaka fulani kulikuwa na mwanaharakati mmoja dhidi ya serikali yake kule California. Jamaa alikuwa paranoid tu kila saa anajisemea wanataka kuniua, wanataka kuniua. Baada ya muda kweli akafa baada ya kunywa kahawa nyumbani kwake (alikuwa anaishi peke yake) na baada ya uchunguzi ikagundulika kuwa alipewa sumu. PK is real.
 
Rwanda bado haijatulia na haitakaa itulie chini ya mkono wa chuma wa PK. Jamaa ana mbinu nyingi sana za kudili na wale wote anaowaona kua watakua tishio kwake hapo mbeleni.

Hii ni dalili mbaya kwa utawala wa PK
Rwanda ni ndugu zetu na marafiki zetu wa kuaminika
 
Imenikumbusha jasusi mbobezi Bernard Kamilius Membe ambaye alishindwa kufanya kampeni hata kewenye kata yake alipokuja kwa mbwembwe nyingi kuutaka urais. Alikuwa domp zegge.
Ukistaajabu ya Membe utayaona ya Hassy Kitine, yeye alitoka kuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa (cheo kinachokaliwa kwa sasa na Ndg. Diwani Athuman) lakini alishindwa Ubunge Iringa tena mbele ya Mgombea wa Upinzani. Aliishia tu kulalamika kuwa aliibiwa kura.
 
PK kiboko...

Miaka fulani kulikuwa na mwanaharakati mmoja dhidi ya serikali yake kule California. Jamaa alikuwa paranoid tu kila saa anajisemea wanataka kuniua, wanataka kuniua...baada ya muda kweli akafa baada ya kunywa kahawa nyumbani kwake (alikuwa anaishi peke yake) na baada ya uchunguzi ikagundulika kuwa alipewa sumu. PK is real.

Duuuh
 
PK kiboko...

Miaka fulani kulikuwa na mwanaharakati mmoja dhidi ya serikali yake kule California. Jamaa alikuwa paranoid tu kila saa anajisemea wanataka kuniua, wanataka kuniua...baada ya muda kweli akafa baada ya kunywa kahawa nyumbani kwake (alikuwa anaishi peke yake) na baada ya uchunguzi ikagundulika kuwa alipewa sumu. PK is real....
Watu wanashindwa kuelewa PK was a former field operative. real spy. Zile skills hazizeeki. He still has it and probably anazitumia against wale anao waona ni wapinzani wake.
 
Toka ulimwengu ulipoumbwa,wanadamu wenye mamlaka juu ya wenzao hasa kisiasa na usalama huwezi kuingilia anga zao wakakuangalia tu lazima tu ufe ,haina budi upotee tu utafanyaje sasa , kifo kinakuhusu kabisa ijapokuwa njia za kuondoka ni tofauti..kuna kazi nyingine watu wazisikie tu zikitajwa lakini mhusika kama hajajiandaa vizuri lazima apotee.

Wakati mwingine huna hatia kabisa lakini pia inabidi uondoke tu kwa ajili ya kuepusha hofu nyingine kwa watu au mamlaka. Watu wa usalama ambao siyo sahihi wajiandae kisaikolojia, kazi ambayo ukiishi kama James bond wa kwenye movie wala hufiki mbali..
 
Back
Top Bottom