MWITONGO MAARIFA
JF-Expert Member
- Aug 11, 2018
- 276
- 1,428
Kijana Lusinde ameeleza kuwa chama Cha Mapinduzi kimekuwa kikizuia wananchi wa maeneo yaliyowachagua wapinzani kupelekewa miradi ya maendeleo kwa lengo la kuwafanya wananchi wakasirike na kuacha kuwachagua viongozi wa upinzani. Ameyasema hayo kwenye kampeni za Ubunge ukonga na kuongeza kuwa katika majimbo ya wapinzani wapo Watanzania lakini wanapaswa kujutia maamuzi na ya kuchagua upinzani na uchaguzi mwingine wachague CCM.
Ameendelea kusema kuwa wao ndani ya chama ukaa kwenye vikao na kusikiliza hoja za mawaziri na pale inapoletwa hoja ya kuwapelekea maendeleo wananchi waliokatika majimbo ya upinzani waziri husika uelekezwa kuhamishia miradi hiyo kwa majimbo ya chama tawala.
Kuhusu wabunge wa upinzania kuchachama Bungeni, amesema kuwa chama utoa maelekezo kwa Spika kwamba Mbunge yeyote wa upinzani anayebainika kujenga hoja na kupingana na matakwa ya chama tawala lazima atolewe ndani ya Bunge.
Swali langu kwa uongozi wa Bunge, kauli hizi kwao hawaoni Kama zinaondoa kabisa tafsiri ya Bunge na kubakia kuwa chombo au taasisi ya chama Tawala?Ni wakati gani muhimili huu unakuwa independent kama umekuwa ukiingiliwa na kufanya maamuzi kwa matakwa ya watu wachache ambao kwao chama ndio kipaombele na siyo Watanzania?
Haya yanatamkwa hadharani kwa sababu viongozi wa muhimili huu wameshindwa kabisa kutenganisha Bunge na itikadi zao za vyama na nilitegemea suala kama la Lusinde likemewe na watu wote wakiwemo viongozi wa Bunge lakini Hadi Sasa kimya.
Ngoma ikivuma Sana inakaribia kupasuka, CCM inaona ufahari kwa haya yanayotokea lakini kisiasa wanajichimbia kaburi maana haki ikipokonywa kwa wananchi itapokonywa pia kwa viongozi wa siasa na hivyo wanaoishi Kama malaika leo kesho wataishi kwa kusaga meno. It's just a matter of time and if you don't believe ask Sumaye, Lowasa, Mwigulu, Nape, Mrema, Marando, Mwandosya, Mwapachu, Msalimie seif etc, Waliamini kuhusu CCM lakini baadaye CCM iliwakataa na waliporudi kwa wananchi wanaumizwa na mfumo walioutengeza wao.
Ameendelea kusema kuwa wao ndani ya chama ukaa kwenye vikao na kusikiliza hoja za mawaziri na pale inapoletwa hoja ya kuwapelekea maendeleo wananchi waliokatika majimbo ya upinzani waziri husika uelekezwa kuhamishia miradi hiyo kwa majimbo ya chama tawala.
Kuhusu wabunge wa upinzania kuchachama Bungeni, amesema kuwa chama utoa maelekezo kwa Spika kwamba Mbunge yeyote wa upinzani anayebainika kujenga hoja na kupingana na matakwa ya chama tawala lazima atolewe ndani ya Bunge.
Swali langu kwa uongozi wa Bunge, kauli hizi kwao hawaoni Kama zinaondoa kabisa tafsiri ya Bunge na kubakia kuwa chombo au taasisi ya chama Tawala?Ni wakati gani muhimili huu unakuwa independent kama umekuwa ukiingiliwa na kufanya maamuzi kwa matakwa ya watu wachache ambao kwao chama ndio kipaombele na siyo Watanzania?
Haya yanatamkwa hadharani kwa sababu viongozi wa muhimili huu wameshindwa kabisa kutenganisha Bunge na itikadi zao za vyama na nilitegemea suala kama la Lusinde likemewe na watu wote wakiwemo viongozi wa Bunge lakini Hadi Sasa kimya.
Ngoma ikivuma Sana inakaribia kupasuka, CCM inaona ufahari kwa haya yanayotokea lakini kisiasa wanajichimbia kaburi maana haki ikipokonywa kwa wananchi itapokonywa pia kwa viongozi wa siasa na hivyo wanaoishi Kama malaika leo kesho wataishi kwa kusaga meno. It's just a matter of time and if you don't believe ask Sumaye, Lowasa, Mwigulu, Nape, Mrema, Marando, Mwandosya, Mwapachu, Msalimie seif etc, Waliamini kuhusu CCM lakini baadaye CCM iliwakataa na waliporudi kwa wananchi wanaumizwa na mfumo walioutengeza wao.